a sinner saved by Christ
JF-Expert Member
- Feb 19, 2017
- 611
- 993
KUDOWEA sehemu kubwa ya jamii wanatumia neno DOWEA wakimaanisha kuvizia kula chakula .Kwetu lilitumika mtoto akienda kuvizia chakula kwa majirani, utasikia anahemea kwa watu.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
KUDOWEA sehemu kubwa ya jamii wanatumia neno DOWEA wakimaanisha kuvizia kula chakula .Kwetu lilitumika mtoto akienda kuvizia chakula kwa majirani, utasikia anahemea kwa watu.
Kuchakura na kuhemea ni vitu tofauti.Kuku anachakura, sio anahemea.
Kujumua
nimekutana nayo iringa ikiwa na maana amenunu kwa bei ndogo bei ya jumla kwa ajili ya kwenda kuuza kwa bei kubwa kidogo apate faida.(Kuchuuza/mchuuzi)KUJUMUA KWA maana ya mfanya biashara
Neno moja linaweza likawa na maana zaidi ya moja .
Anataka kwenda "kupumulia" sokoni 🤣Sasa hapo hujaelewa nini kuhemea=kupumulia=kupoluteHilo neno lipo toka zamani ni nsamiati wa kusema natafuta kula, kama kuku anavyotafuta kula, anahemea.
Ndiyo maana nikasema huelewi unalozungumza. Omba ushauri haraka. Unaonekana uko nyuma ya wakati muda wote.najua neno boda boda limerasmishwa kwwnye kamusi za kiswahili na kingereza.
nimeweka kama mfano usio halisi ,kwa kuwa maneno mapya yaliyotungwa na bakita ,binafsi siyakumbuki kwa kuwa ni mageni na kwangu ni magumu kwa vile hatuyatumii katika jamii yetu kuwasiliana ni mapya.au hayajazoeleka na wengi wetu.
Kiasi kwamba ukilisikia kwa mara ya kwanza unapata linakupa ukakasi.Kana kwamba jamii nzima miaka yote mlikuwa mnakosea kutumia maneno mliyokuwa mkiyatumia na kuwasilina au hamuijui au hakuwahi kuijua lugha yenu wenyewe ya kiswahili ISIPOKUWA bakita pekee ndio wenye kujua lugha ya kiswahili.
Ndio maana nikashauri ingefaa,wanapotunga maneno ni vizuri kutumia yale yaliyozoeleka na yanayotumika na sehemu kubwa ya jamii katika kuwasiliana.
Jifunze kuwa mtu mwelevu (understanding). Usibishe tu ili kubisha. Hapa hakuna ushabiki wa Simba vs Yanga vs Kayoko.weeh acha urongo wako. kiswahili hakina neno hilo. huo ni msemo wa kanda ya ziwa huko umeshaambiwa.
Kiswahili cha Kanda ya Ziwa hicho. Kama ni mzaliwa wa Pwani au Kaskazini huwezi jua hicho kiswahili.Yaani nakutana na mfanyakazi wangu mmoja leo namuuliza ulikuwa wapi time niliyokuwa nakutafuta ananiambia boss nilitoka kuhemea nikamuuliza kuhemea ndio maana yake nini maana tayari kichwani nilishawaza mambo ya hovyo akaniambia kuhemea ni kwenda kununua mahitaji ya nyumbani yaani sikumuelewa hivi neno kuhemea ni kununua mahitaji ya nyumbani?
Mkuu Manjagata , kuhemea na kuemea ni maneno sahihi ya Kiswahili.Hebu wacha kujidhalilisha mwamba, hilo neno mbona lipo muda sana! Kiswahili sahihi kabisa hicho labda kama angesema "kuemea" ndiyo tungemjadili!
Ni neno sahihi la Kiswahili mkuu, licheki kwenye Kamusi.Mimi mwenyewe nimelisikia na kulizoea. Ni la miaka mingi. Oni Sigara na BAKITA yako tusaidie.
Nami ni wa hukohuko.Wakanda yaziwa hao
Inawezekana pia likabeba maana hiyo.Nafikiri kuhemea linatumika na watu masikini zaidi/kipato cha chini.
Hii maana uliyotoa hapo nadhani mmekuwa mnaitumia huko kwenu. Mimi ni mzaliwa wa Mwanza miaka ya 80. Tangu nikiwa mdogo, hilo neno lilikuwa linatumika kumaanisha kutafuta/kununua mahitaji ya nyumbani.Kuhemea ni kula slope kwa mtu mwingine kwasababu huna uwezo wa kujitunza
SHOPPING SIO KUHEMEA