Hiki kizazi mnaharibu sana Kiswahili "KUHEMEA" ndio maana yake nini?

weeh acha urongo wako. kiswahili hakina neno hilo. huo ni msemo wa kanda ya ziwa huko umeshaambiwa.
 
Kujumua
nimekutana nayo iringa ikiwa na maana amenunu kwa bei ndogo bei ya jumla kwa ajili ya kwenda kuuza kwa bei kubwa kidogo apate faida.(Kuchuuza/mchuuzi)KUJUMUA KWA maana ya mfanya biashara
Neno moja linaweza likawa na maana zaidi ya moja .
"Kujumua" ni neno la wafanyabiashara wanaonunua mali ya jumla na kuuza rejareja.
 
Hilo neno si la kizazi hiki, bali la kizazi kile. Ninakaribia miaka 40 na hilo neno nimekua nalisikia likiwa na maana ya kununua mahitaji ya nyumbani. Kizazi hiki wanasema 'shopping/kununua groceries'.
Kuhemea ni kula slope kwa mtu mwingine kwasababu huna uwezo wa kujitunza

SHOPPING SIO KUHEMEA
 
Hilo neno si la kizazi hiki, bali la kizazi kile. Ninakaribia miaka 40 na hilo neno nimekua nalisikia likiwa na maana ya kununua mahitaji ya nyumbani. Kizazi hiki wanasema 'shopping/kununua groceries'.
Nafikiri kuhemea linatumika na watu masikini zaidi/kipato cha chini.
 
Hilo neno si la kizazi hiki, bali la kizazi kile. Ninakaribia miaka 40 na hilo neno nimekua nalisikia likiwa na maana ya kununua mahitaji ya nyumbani. Kizazi hiki wanasema 'shopping/kununua groceries'.
Wakanda yaziwa hao
 
Hilo neno nalisikia sana kwa watu wa kanda ya ziwa,ila kwetu Nyanda za juu kusini sijawahi kusikia
 
wasukuma na waha ndio wanapenda kulitumia hili neno, mara ya kwanza kulisikia niliuliza mara mbili, mtu anakuambia ametoka kuhemea
 
Kuhemea = Shopping
Neno lisikupe shida maana lugha yetu inatengenezwa kwa njia ya kutohoa
 
Hebu wacha kujidhalilisha mwamba, hilo neno mbona lipo muda sana! Kiswahili sahihi kabisa hicho labda kama angesema "kuemea" ndiyo tungemjadili!
 
Anayeharibu kiswahili ni nyie mnaobadili maana ya maneno. Hili neno ni sawa according to TUKI
 
Hilo neno mara yangu ya kwanza kuliskia ni nilivyoenda kwa wasukuma , wanalitumia sana yan
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…