Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tofauti Wao wanazichukulia kama ngano tu za entertainment.Hata wao zipo ndo maana Hadi movies wanaziectia.
Sisi huwa tunaishia kwenye kusimulia tu
Wanaishi nazo lakini mfano sikukuu za Halloween nkTofauti Wao wanazichukulia kama ngano tu za entertainment.
Sisi tunaziamini mpaka tunapeleka Sadaka/kafara au kuuana kabisa kisa hizi story
Alikua harmonize huyo. Si umesema alikua anavuta sigara huku akakohoaNiaje waungwana,
Hiki kisa, au tukio lilintokea miaka mingi kidogo. Enzi zile za kwenda kuangalia movie katika vibanda vya video. Sasa siku hiyo nilienda kuangalia video katika banda moja nililokuwa napenda kwenda kuangalia.
Banda hilo lilikuwa maeneo ya Manzese Midizini kwa mama fulan jina kapuni, na mimi home ni maeneo ya Magomeni mikumi jijini Dar es salaam.
Njia yangu kubwa kutoka home hadi Midizini, ilikuwa kagera kimamba, nakatiza daraja la mbao, napandisha pale Mburahati Mianzini, napasua Makaburi ya Mburahati kwa jongo hadi midizini. Na kurudi i was doing the same thing kwa kufuata njia ile ile niliyokuja nayo.
Ratiba yangu kwa siku ilikuwa ni shule kwanza, nlipotoka shule, nlielekea mazoezini (mpirani), baada ya kutoka mpirani ndo nikawa naenda sasa kujipoza vibandani kumuangalia Dharmendra, Amita Bachan, Rambo, Anord, Bruce Lee nk.
Ratiba yangu ya mwisho baada ya kutoka huko katika banda la video, ilikuwa ni kwenda katika maskani yetu fulan ambayo ni ya uncle wangu kujifunza mchezo wa karate. Uncle ndo alikuwa masta wetu. Hivyo nilijiamini sana kwamba hakuna kitu au mjinga yeyote anaeweza kunifanyia ushen.z.i mbele yangu. Karate na ngumi ni michezo ambayo humfanya mchezaji ajiamini sana, kwamba anaweza kupambana na mtu yoyote, mahali popote na kwa muda wowote.
Basi bwana siku hiyo nimemaliza kumuangalia Dharmendra mida ya usiku, nakumbuka ilikuwa movie fulan inaitwa LOHA. Tukatoka kila mtu akawa anaelekea kwao. Mimi nikawa natambaa mdogo mdogo kuelekea home.
Nilivyofika katika makaburi ya mburahati kwa jongo kama kawaida yangu, nikageuka nyuma kuangalia huku na huko, sikuona mtu ananifuata nikaendelea na safari yangu.
Sasa nimesogea sogea hadi katikati ya makaburi, kwa mbele nikaona kitu kama mbuzi mweupe, lakini kilichonishangaza na kunitia hofu ni kwamba yule mbuzi alikuwa kama vile amekaa kwenye kitu anavuta sigara, nikafikicha macho kama vile siamini ninachokiona.
Nikaendelea kusogea taratibu ili nihakikishe kuwa ninachokiona ni chenyewe au.
Kusogea nikasikia mbuzi anakohoa, ikabidi nigeuke ili nitoke nduki maana niliona pale hata karate zangu haziwezi kunisaidia.
Sasa wakati nageuka nikaona nyuma yangu kuna kundi la watu wamebeba jeneza wanakuja upande wangu halafu juu ya jeneza kuna mtu kakaa na yeye anavuta fegi, halafu kila jamaa wakipiga hatua, yeye anajamba.
Nikaona nyuma hakufai bora huku huku nilipotaka kupakimbia. Nikageuka na kuanza kutoka nduki kuelekea kwa mbuzi anaevuta sigara. Ghafla nikaona na mbuzi na yeye anatoka nduki na sigara yake.
Akili ikanijia nikaacha kukimbia ule upande anakimbilia mbuzi, nikaelelea upande wangu.
Breki ya kwanza ikawa Magomeni Mapipa, yani sikumbuki hata mikumi home nilipapita saa ngapi, au kule Mapipa nilifika fikaje fikaje.
Nikarudi nyumbani salama. Toka siku hiyo sikurudi tena kwenda video usiku, na ukawa mwisho wa kuendekeza movie.
Ni nani mwngine ambae ashawahi kukumbana na songombingo la aina hiyo?
Aisee it was scary
Una uhakika hao waliokuwa mango garden walikuwa ni twanga pepeta kweliNilikuwa nandesha BAISKERI Saa 5 usiku nipo kasi bonde la mkwajuni natoka magomeni naitafuta MWANANYAMALA
Mbele wakapita watu wamebeba jeneza
Nikakumbuka story za VIJIWENI
nikasema hapa sifungi brake nitakufa Kwa ajari mbaya nikapita katikati ya mazishi
sielewi ilikuwaje ila kuja kushituka nipo VIJANA SOCIAL HALL
MANGO GARDEN walikuwa TWANGAPEPETA nikaenda kucheza muziki
Sasa hizo Halloween si ni kama michezo tu for fun kuombana pipi.Wanaishi nazo lakini mfano sikukuu za Halloween nk
Kitambo hiyo, mzee shutigansia ndani hiyo it was good days my boss πππMusape na musape sandakalawe na musapeView attachment 2874815View attachment 2874819