Hili la Bandari, lawama hii iende kwa hayati Magufuli

Hili la Bandari, lawama hii iende kwa hayati Magufuli

Bado sehemu mbalimbali za nchi yetu zinaendelea kujadili kuhusu Uwekezaji wa DP-World. Mbaya zaidi, mitazamo inayotolewa sasa inajadiliwa kwa milengo ya kidini, jambo ambalo si la kawaida katika nchi yetu.

Ni nini mzizi wa haya yote?

Kisa kilianza Mwaka 2020, wakati wa Uchaguzi Mkuu. Ulikuwa ni moja kati ya chaguzi ambazo zilijawa na malalamiko mengi kutoka upinzani, uvunjifu wa sheria za uchaguzi na kupeleka Uchaguzi ule kugubikwa na ripoti chafu za Waangalizi wa ndani na nje.

Lakini kwa nini haya yote yalitokea?

Haya yote yalitokea ili kutimiza adhma ya aliyekuwa Rais wa wakati huo Hayati, Dkt. John Magufuli ya kutaka kutengeneza Bunge la Jamuhuri ya Muungano lenye wanachama wa chama chake tu (CCM). Hili linathibitishwa na kauli yake aliyoitoa Tarehe 22 Januari 2020, alisema;

“Haiwezekani Mkurugenzi nikuteue mimi, nikulipe mini mshahara na kukujazia mafuta kwenye gari halafu kwenye Uchaguzi utangaze kuwa Mpinzani ameshinda”

Kauli hii ndio leo hii imesababisha leo bunge letu kuwa ni Bunge la chama kimoja. Hivyo, maamuzi yote kufanywa kwa kuridhisha chama na viongozi wake wakuu, wakiwamo Rais wa Jamhuri ya Tanzania kama Mwenyekiti wa Chama hiko.

Je, hasara ya jambo hili ni nini?

Hapa kwenye hasara ndipo kwenye lawama, Magufuli alituachia Bunge lisilo na meno, Bunge ambalo lingekubali kila kitu kwa kuwa kimekubalika na Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa chama. Bunge linalopitisha hoja bila kuchunguza kwa kina.

SUALA LA BANDARI SI LA KUJADILIWA VIJIWENI NA KWENYE NYUMBA ZA IBADA.

Haya maoni ambayo watu wanayajadili, vipengele ambacho vinatia shaka kwenye Mkataba, vilipaswa kujadiliwa bungeni kwa sababu, Bunge ndicho chombo pekee chenye Mamlaka ya kuongoza mijadala hii ambayo imezua gumzo, si kuacha mambo haya kwenda mpaka kwenye nyumba za ibada.

Naamini ya kuwa; kuna kundi kubwa la Wabunge ambao wanaamka sasa hivi kutambua kumbe kuna baadhi ya vipengele katika Mkataba vinazua utata, ila walivyokuwa bungeni, kwa sababu ya “Mob Psychology” wakakubali tu bila kuvitathimini ili vinapofika mtaani wananchi waelewe kuwa Bunge lao limejadili kitu gani kupunguza uwezekano wa kuzuka kwa utata huku mitaani.

Matokeo yake, suala hili linajadiliwa kidini leo hii. Tupo kwenye hatari ya KUGAWANYIKA.

JE, CCM HUJALI MASLAHI YA CHAMA KULIKO NCHI WANAYOONGOZA?

Ni rahisi sana kwa mtu yeyote kujibu swali hili kwa jibu la NDIO. Kwa sababu kuu mbili;

  1. Hoja nilizojadili hapo juu, naamini Hayati Magufuli wakti wa uhai wake hakufikiria madhara ambayo nchi ingeweza kuyapata endapo Bunge litaundwa kwa chama chake tu kupitia kupora Uchaguzi mkuu. Lakini hapa ndipo tulipofikia.
  2. Leo, tarehe 27 Agosti, Rais amekasirishwa sana na amepoteza imani na Mkurugenzi na Mkuu wa wilaya ya Mtwara, kwa sababu ya kushindwa kusambaza kadi za CCM kwa wananchi ambao kwa madai yake wanasema ni Upinzani. Amesema“Siwezi kustahimili kadi za chama zinarudishwa, Mkuu wa wilaya yupo, DED yupo, namtimua leo, kadi za chama zinarudishwa na watu wanashida anaulizwa nini, ooh! Unajua kule wengi wapinzani, so what? Watanzania wale, sina imani na mkuu wa Wilaya aliyesababisha kadi zirudishwe
Inaonyesha dhahiri kuwa, Rais ameumizwa kuona chama kinakataliwa na baadhi ya watu, ila sikuona hatua kama hii ikichukuliwa kwenye ubadhilifu ulioandikwa kwenye ripoti ya CAG.

Makosa yale aliyofanya Hayati, ya kutanguliza chama kisha Taifa. Anayafanya aliyepo sasa. Muda utaongoea.



Mwl. Diwani.



Tafadhali 0acha kuleta ujinga wako hapa kila kitu unataka kumuunganisha JPm na mabo ya yasiyofaa.

Jenga hoja kuonesha udhaifu wa uongozi uliopo. Mbona mbunge wa Ngorongoro ameungana na wananchi wenzie kuwatetea lakini serikali hii wanamkamata. Mzungumzie kiongozi aliyeko madarakani ndio chanzo cha yote siyo JPM.

Angekuwepo JPM kwanza yeye mwenyewe mkataba huo ungeletwa kwake au kushauri nafikiri angefunguliwa mashitaka kwanza na hata huko bungeni mkataba huo usingepelekwa maana angeutupilia mbali. JPM alipenda sekta binafsi ya Tanzania ishirikiane na wawekezaji kwa nia ya kuwapa ujuzi, uzoefu na kujengewa uwezo kuendesha shughuli za kiuchumi ili kipato cha pesa za kigeni zinufaishe taifa badala ya sasa.
 
Bado sehemu mbalimbali za nchi yetu zinaendelea kujadili kuhusu Uwekezaji wa DP-World. Mbaya zaidi, mitazamo inayotolewa sasa inajadiliwa kwa milengo ya kidini, jambo ambalo si la kawaida katika nchi yetu.

Ni nini mzizi wa haya yote?

Kisa kilianza Mwaka 2020, wakati wa Uchaguzi Mkuu. Ulikuwa ni moja kati ya chaguzi ambazo zilijawa na malalamiko mengi kutoka upinzani, uvunjifu wa sheria za uchaguzi na kupeleka Uchaguzi ule kugubikwa na ripoti chafu za Waangalizi wa ndani na nje.

Lakini kwa nini haya yote yalitokea?

Haya yote yalitokea ili kutimiza adhma ya aliyekuwa Rais wa wakati huo Hayati, Dkt. John Magufuli ya kutaka kutengeneza Bunge la Jamuhuri ya Muungano lenye wanachama wa chama chake tu (CCM). Hili linathibitishwa na kauli yake aliyoitoa Tarehe 22 Januari 2020, alisema;

“Haiwezekani Mkurugenzi nikuteue mimi, nikulipe mini mshahara na kukujazia mafuta kwenye gari halafu kwenye Uchaguzi utangaze kuwa Mpinzani ameshinda”

Kauli hii ndio leo hii imesababisha leo bunge letu kuwa ni Bunge la chama kimoja. Hivyo, maamuzi yote kufanywa kwa kuridhisha chama na viongozi wake wakuu, wakiwamo Rais wa Jamhuri ya Tanzania kama Mwenyekiti wa Chama hiko.

Je, hasara ya jambo hili ni nini?

Hapa kwenye hasara ndipo kwenye lawama, Magufuli alituachia Bunge lisilo na meno, Bunge ambalo lingekubali kila kitu kwa kuwa kimekubalika na Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa chama. Bunge linalopitisha hoja bila kuchunguza kwa kina.

SUALA LA BANDARI SI LA KUJADILIWA VIJIWENI NA KWENYE NYUMBA ZA IBADA.

Haya maoni ambayo watu wanayajadili, vipengele ambacho vinatia shaka kwenye Mkataba, vilipaswa kujadiliwa bungeni kwa sababu, Bunge ndicho chombo pekee chenye Mamlaka ya kuongoza mijadala hii ambayo imezua gumzo, si kuacha mambo haya kwenda mpaka kwenye nyumba za ibada.

Naamini ya kuwa; kuna kundi kubwa la Wabunge ambao wanaamka sasa hivi kutambua kumbe kuna baadhi ya vipengele katika Mkataba vinazua utata, ila walivyokuwa bungeni, kwa sababu ya “Mob Psychology” wakakubali tu bila kuvitathimini ili vinapofika mtaani wananchi waelewe kuwa Bunge lao limejadili kitu gani kupunguza uwezekano wa kuzuka kwa utata huku mitaani.

Matokeo yake, suala hili linajadiliwa kidini leo hii. Tupo kwenye hatari ya KUGAWANYIKA.

JE, CCM HUJALI MASLAHI YA CHAMA KULIKO NCHI WANAYOONGOZA?

Ni rahisi sana kwa mtu yeyote kujibu swali hili kwa jibu la NDIO. Kwa sababu kuu mbili;

  1. Hoja nilizojadili hapo juu, naamini Hayati Magufuli wakti wa uhai wake hakufikiria madhara ambayo nchi ingeweza kuyapata endapo Bunge litaundwa kwa chama chake tu kupitia kupora Uchaguzi mkuu. Lakini hapa ndipo tulipofikia.
  2. Leo, tarehe 27 Agosti, Rais amekasirishwa sana na amepoteza imani na Mkurugenzi na Mkuu wa wilaya ya Mtwara, kwa sababu ya kushindwa kusambaza kadi za CCM kwa wananchi ambao kwa madai yake wanasema ni Upinzani. Amesema“Siwezi kustahimili kadi za chama zinarudishwa, Mkuu wa wilaya yupo, DED yupo, namtimua leo, kadi za chama zinarudishwa na watu wanashida anaulizwa nini, ooh! Unajua kule wengi wapinzani, so what? Watanzania wale, sina imani na mkuu wa Wilaya aliyesababisha kadi zirudishwe
Inaonyesha dhahiri kuwa, Rais ameumizwa kuona chama kinakataliwa na baadhi ya watu, ila sikuona hatua kama hii ikichukuliwa kwenye ubadhilifu ulioandikwa kwenye ripoti ya CAG.

Makosa yale aliyofanya Hayati, ya kutanguliza chama kisha Taifa. Anayafanya aliyepo sasa. Muda utaongoea.



Mwl. Diwani.



Mkuu Diwani, kwanza kabisa chukuwa maua yako. Miundombinu ya kisiasa anayoitumia SSH, muasisi wake ni JPM. Siyo kwamba Magufuli aliengua wapinzani tu, hata huko kwenye chama chake alipitisha watu aliowataka yeye bila kuzingatia maoni ya wanaccm wenzake waliyoyatoa kwenye sanduku la kura za maoni.Kwake yeye mtu mwenye uwezo wa kuhoji na kukosoa hakuwa sahii kwake bila kujali chama anachotoka. Nikupe mifano michache ambako kura za maoni zilisiginwa: Shinyanga mjini, Kawe, Mwibara, Mueza...na sehemu nyingine nyingi tu. Kosa hili ni kweli analistahili pamoja watu wake waliokuwa wakimzunguka. Tulipokuja kwenye uchaguzi yalikuwa ni maigizo tu na kuumiza wapinzani bila sababu ya msingi. Nakumbuka bila aibu Bashiru Ally akiwa Mwananchi Communication alitamka bayana kuwa vyombo vya dola vitatumika kuisaidia Serikali ya Magufuli ktk uchaguzi na kweli ndicho kilichotokea. Kwenye campaign jpm alienda mbali na kuhaidi watu vyeo serikalini hata kama hawakuchaguliwa kwenye huo uchaguzi. Ni bahati mbaya tu hapa nchini kwetu utawala wa Sheria ulishasiginwa lakini uchagu huo haukuwa uchaguzi bali ujambazi wa uchaguzi.

Kwa hali ilivyokuwa, si vibaya kabisa kwa wale wenye maoni kuwa, JPM alikuwa akiweka miundo mbinu ya kubadili katiba hili apewe mitano tena. Japo alikuwa akijikataza lakini mazingira tayari yalikuwa wazi. Kauli kama vile za spika wa wakati ule "atake hasitake", kauli za kina Nkamia nk vilikuwa ni viashiria tosha ya kile kilichokuwa kikipikwa. Zaidi ya hayo JPM hakutaka kukosolewa wala kuhojiwa kwa kile alichokuwa akikifanya, hasa vile vyenye maslahi yake binafsi. Kwa mantiki hiyo alichaguwa wabunge ambao yeye angeweza kuwamdu. Kwa miundo mbinu hiyo aliyoiasisi JPM serikali ya Samia inatumia weakness hiyohiyo kupitisha mambo yake. Kwa maana nyingine bunge aliisadii Serikali, badala yake limekuwa kama mzigo kwa serikali kwasababu wanalipwa bila kutimiza wajibu wao kama wabunge. Hii inadhibitishwa na kauli ya Kinana aliyoitoa hivi karibuni akiitaka nec ya CCM imutake Rais kuwaondoa mawaziri wavivu na kukemea bunge lisipitishe kila kitu kinacholetwa na serikali bila kuhoji.

Siyo swala la mkataba wa bandari tu ambao umepita ktk hili bunge na kuleta malalamiko mengi ktk jamii. Nakumbuka tozo za ajabuajabu zilipitishwa na hili bunge hadi mitandao ya kijamii na vyombo vya habari ndo viligeuka kuwa bunge. Ni bunge la Magufuli, Bashiru na Polepole.
 
Back
Top Bottom