Hili la kufungwa barabara limekaaje? Kwa namna hali ilivyokuwa leo kwenye usafiri maeneo ya Posta na Kivukoni mpaka ifike hiyo tarehe 30 tutakuwa hoi

Hili la kufungwa barabara limekaaje? Kwa namna hali ilivyokuwa leo kwenye usafiri maeneo ya Posta na Kivukoni mpaka ifike hiyo tarehe 30 tutakuwa hoi

Hivi kule kwenye mazishi yz Elizabeth UK walikojazwa kwenye bus hawakujifunza jambo?
 
Nje ya bara la Africa; hivi wengine huko duniani nao huaga wanafunga barabara kama huku kwetu? Mfano, mkutano wa marais/nchi za G7 or G8 na wenyewe wanafungaga barabara kama hivi? Kwanini viongozi wa Africa hawanaga imani na wananchi wao? Wanawaibia sana or what? Ingekua enzi za Magufuli nina hakika hu mkutano ungepelekwa Dodoma na sio Dar.
Masikini wakazi wa Kigamboni
labda Arusha.

Dodoma haina uwezo wa kuhost hao wakubwa
 
akili zao zimeishia kwenye kufunga barabara tu, hawana utashi mwingine hao
 
Kwani kabla ya bodaboda na bajaj tulisafiri vipi hapa mjini? Bodaboda na bajaj katikati ya jiji ni uchafu wafanye huduma zao nje ya city centre.
Na support asilimia. Hakunaga mji ulioendelea duniani ukiwa na bodaboda na bajaji kama usafiri wa umma.
Lawama zote ni kwa serikali kuingiza siasa kwwnye mambo ya msingi.

Mfumo wa BRT ndo ufanye kazi kwenye main roads...wakishindwa kuleta mabasi watafute watu binafsi wasafirishe abiria.

Huku wakija na mipango wa city light rails, trams,metros nk. We have to think big. Uwezo tunao.

Kama wanasema Riziki, riziki zipo tu...sidhani kuna mtu anapenda kuwa Bodaboda au dereva bajaji
 
Sasa muwape taarifa ma gabachori tusipoenda kazini wasipige
Shabaniiii mbona huji peleka watoto shulee
 
Hata wakifunga wana options nyingi ingawa huu upuuzi hamna. Si uliona mazishi ya Lizzy hawa wanaofunga njia leo walipakiwa kwenye daladala na walitulia tuliiii.
Hivi lile daladala walilopakiwa, if I'm not mistaken, hata dereva hawakupewaga; walijitafuta wenyewe from airport hadi mitaa ya ushuani. Wanashindwa nini kufanya hivo wakiwa kwao as well? I mean, hapa nyumbani tungeboresha zaidi; tafuta Youtong moja la maana, au Makpolo halafu kamamda 1 ana drive hilo with full of ulinzi na escort ya maana, tukio linakua la mara moja then wananchi wanendelea na shughuli zao, wakitaka kutoka, zoezi linafanyika hivo hivo, I think lisaa limoja tu lingekua linatosha
 
K
Hivi lile daladala walilopakiwa, if I'm not mistaken, hata dereva hawakupewaga; walijitafuta wenyewe from airport hadi mitaa ya ushuani. Wanashindwa nini kufanya hivo wakiwa kwao as well? I mean, hapa nyumbani tungeboresha zaidi; tafuta Youtong moja la maana, au Makpolo halafu kamamda 1 ana drive hilo with full of ulinzi na escort ya maana, tukio linakua la mara moja then wananchi wanendelea na shughuli zao, wakitaka kutoka, zoezi linafanyika hivo hivo, I think lisaa limoja tu lingekua linatosha
Kila kitu kiliandaliwa na mwenyeji wao.
 
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam imetangaza kuwa Barabara tisa Jijini Dar es Salaam, zimefungwa kwa siku sita kuanzia leo Januari 25 hadi Januari 30, 2025 ili kupisha misafara ya viongozi wanaokuja kutoka nchi mbalimbali kuhudhuria mkutano wa Nishati Afrika.

Taarifa ya Polisi iliyotolewa leo Jumamosi Januari 25,2025 na Kamanda Kanda Maalumu ya Polisi Dar es Salaam, Jumanne Muliro, imesema Mkutano huo utakaofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Januari 27 hadi Januari 28, 2025, unatarajiwa kuhudhuriwa na zaidi ya marais 25 na mawaziri 60 kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambapo pia bajaji na bodaboba hazitaruhusiwa kuingia katikati ya Jiji katika kipindi chote ambacho mkutano huo utakuwa ukifanyika.

Barabara zitakazofungwa ni pamoja na Barabara ya Nyerere kutokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwenda katikati ya Jiji, Barabara ya Sokoine, Kivukoni na Lithuli kuanzia taa za Gerezani kwenda Hoteli ya Johari Rotana, Hyatt Regency hadi Ikulu; Barabara ya Ohio kutokea Kivukoni kwenda Hoteli ya Serena na Barabara ya Ghana kutokea barabara ya Ohio kwenda Hoteli ya Onomo

Zingine ni Barabara ya Bibi Titi kutokea makutano ya barabara za Ohio na Ally Hassan Mwinyi kwenda Hoteli ya Crowne; Barabara ya Azikiwe kwenda Hoteli ya Four Points, Hoteli ya Golden Tulip City Center na Hoteli ya Holiday Inn; Barabara ya Morogoro kutokea Sokoine kwenda Hoteli ya Tiffany No. 1; Barabara ya Makunganya kutokea Azikiwe kwenda Hoteli ya Tiffany No. 2 na Barabara ya Garden kutokea barabara ya Lithuli kwenda Hoteli ya Southern Sun pamoja na Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa JNICC.
Mkuu hufungwa kwa muda tu, pale msafara wa viongozi wanapotaka kupita, na ni kwa wale wenye vyombo vya moto na baiskeli tu, kwa watembea kwa miguu huruhusiwa kuendelea na shughuli zao kama kawaida, baada ya msafara kupita na askari wa usalama barabarani kujiridhisha kuwa hakuna ratiba nyingine ya msafara wa viongozi basi barabara hufunguliwa mara moja kuendelea na shughuli za kiuchumi, nimeona kwa macho yangu hapa Keko mataa, msafara unapita Nyerere road kutoka Nyerere Air port na kupita barabara ya kati ya mwendokasi kuelekea IKUL.U haupiti juu ya (fly over) daraja.
 
Back
Top Bottom