Hili la mbunge baraza la wawakilishi kuwadharau samaki aina ya Kambale na Sato wa ziwa Victoria lisipite pasipo mjadala. Linatoa picha mbaya

Jamani kama taifa tuna kazi ya kufanya kweli kweli.

Wakati viongozi wakuu wa wizara zinazo husika na muungano wakiumiza vichwa kuimarisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar bado kuna wabunge wanaharibu juhudi hizo.

Sikikizeni hapo ili kwa umoja wetu tunajadili.

Your browser is not able to display this video.
 
Hajui kwamba raisi wake amesign blue economy na Mzungu hao changu, kolekole atawasikia tu mtaletewa kambale kwa kwenda mbele.

Kolekole ni wa Mzungu na Mchina meli kubwa za uvuvi za EU zinavua kila kitu mpaka watoto wa samaki wameruhusiwa, Magufuli (RIP) angekuwepo mngekula hao kolekole na changu, ila kwa sasa zoeeni tu kambale mpaka mshike adabu!
 
Kashalipwa posho yake
 
"......sitaki kumbuka zamani.....",

Huu mstari upo kwenye wimbo fulani wa komando Jide nadhani.
 


Wao hawahitaji Kambale na Sato samaki wa "ajabu ajabu" wao samaki wao ni Changu, kolekole, Nguru, Tasi.

Kambale na Sato hawana soko huko kwao hivyo serikali haina haja ya kutumia Bln of money kuzalisha samaki hao kwani hawatapata soko huko.

Hayo ni maoni yake kama mbunge/muwakilishi wa Wananchi wa huko, shida ni pale anapowaita Kambale na Sato samaki wa "ajabu ajabu" utadhani kwamba anaweza kuumba hata gamba moja tu la Sato!!--- ana kiburi sana huyo.
 
Nenda kalale chato
 
Ubaguzi ni kitu kibaya sana
Sio wabaguzi! Na hasa ukiangalia suala zima la kambale hapa kisiwani.

Ufugaji na uuzaji wa kambale bado ni kitu kigeni sana, na kwa wenyeji ambao hawajawaji kuvuka bahari ni jambo linalowastua sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…