Ni kosa la jinai kwa raia wa Tanzania kumiliki silaha ama risasi bila kufuata taratibu na sheria za umiliki wa silaha za Tanzania, ikiwa ni pamoja na kutengeneza zana hizo.
Hata hivyo kwa kadiri ya bandiko lako ndugu, ni wazi kuwa neno ama jina la jambazi si geni kwako. Na kwamba, athari na matokeo ya kazi za majambazi ndani ya jamii yetu, unazifahamu vyema. Na Kwamba jambazi siku zote, ni mwenye kusudi la kuharibu na kuihalifu sheria za nchi.
Hata hivyo imetokea bahati nzuri kwa jeshi letu la polisi, kwamba siku zote wamekuwa ni wenye kuhakikisha uhalifu na matukio ya ujambazi yanatoweka kabisa ndani ya jamii zetu. Na kama inavyofahamika kuwa rais wa JMT pia ni amiri jeshi mkuu wa mjeshi ya ulinzi na usalama, kwamba ni jukumu lake kuhakikisha taifa li katika usalama kwa kiasi cha kutosha.
Kama ambavyo inafahamika katika sheria za kiutendaji wa jeshi la polisi, kwamba utii wa sheria bila shuruti ndio jambo la msingi kwa kila mtu. Kwamba sheria ni mvunjifu wa sheria basi ni dhahiri kuwa shurutii itakufaa sana kwa wakati huo. Kwa hiyo shuruti haina kusudi la kuua isipokuwa kwa mharifu mwenyewe; yeye ndiye mwenye kuchagua ni shuruti ya aina gani ambayo itawapasa jeshi la polisi limpatie kwa wakati huo: Kwa maana haiwezekani kwa mharifu kutaka kujaribu kupoteza uhai wa mtu kwa makusudi kabisa, na kwa wakati mmoja mharifu huyo anapewa amri ya kusitisha zoezi hilo naye akakahidi: Hivyo jeshi la polisi likaendelea kumbembeleza mharifu huyo. Jambo hilo hliwezekani hata kidogi, kwa maana kufanya hivyo ni kuendelea kuhatarisha uhai wa watu wengine wengi.
Ifahamike kuwa utii wa sheria bila shuruti ndio wajibu ambao kila mtu anapaswa azingatie. Na kwamba kushindwa kutii sheria ni kuikaribia shuruti kwa hiari. Na kwa wakati mmoja kwa kadiri unavyo hatarisha uhai wa wengine ndivyo unavyoongeza ukubwa wa shuruti.
Si sawa kuua na hivyo ndivyo ilivyo, kwani si sawa kuipotosha sheria: Isipokuwa kuitii sheria. Na hiyo ndiyo tiba kwa jambazi kuuawa na polisi, na siyo kinyume chake