Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

Nina

Wanabodi,

Wewe kama mwana JF, unapata an added advantage to be the first to know, ambapo leo katika tukio la maboresho ya jeshi la polisi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais, Dr. John Pombe Magufuli, ametoa kauli kwa kutumia fasihi, ambapo ameliamuru jeshi la polisi, kukabiliana na majambazi wenye silaha kwa "kuwanyang'anya silaha kwa kutumia mbinu za medani, (kivita) (MM) ambazo hutumiwa na majeshi wakati wa vita, ambapo kazi huwa ni moja tuu, kumteketeza adui!.

Amri hiyo kwa Jeshi la Polisi, inamaanisha, Polisi hawahitaji tena kuwakamata majambazi wanaotumia silaha, bali kukabiliana nao kwa kuwaua papo kwa papo, na polisi wataofanya mauaji hayo ya kuwauwa majambazi hayo papo kwa papo bila kuwapeleka mbele ya vyombo vya sheria, hawatafikishwa tena mahakamani, kama zamani, bali sasa watapandishwa vyeo!.

Agizo hilo limepokelewa kwa shangwe na makofi kwa kila aliyekuwe pale.

Rais huku akisema kwa msisitizo kwa kutumia fasihi ya "kuwanyanganya silaha", kwa vile majambazi wanatumia silaha, zenye risasi kufanya ujambazi, na jeshi la polisi nalo wanazo silaha zenye risasi, haoni kwa nini majambazi hayo yasinyang'anywe silaha zao!. Namna pekee ya kunyanganya silaha jambazi mwenye silaha, ni kumalizana nao, papo kwa papo!.

Sina shaka kabisa na nia ya dhati ya rais Magufuli, kutoa amri, hiyo, kufuatia nchi na wananchi kuchoshwa na vitendo vya ujambazi kuongezeka, hivyo majambazi wakijua kuwa wakikamatwa watauwawa right away, then, amri hii badala ya kupunguza ujambazi wa kutumia silaha, ndio kwanza utaongeza impunity kwa majambazi wanaotumia silaha, na wakati huo huo kuligeuza jeshi letu la polisi kugeuka Gestapo!.

Sio majambazi wote wanaotumia silaha, huzitumia silaha hizo kufanyia mauaji!, sio silaha zote zinazobebwa zinakuwa loaded!, wengine huzitumia kutishia tuu, lakini hawana nia ya kufanya mauaji, na kuna wengine hubeba silaha ambazo hazina risasi, na wengine hutumia toy pisto!,na majambazi wengine, hubeba silaha, na ziko loaded, lakini hawafanyi mauaji baada ya kupata walichotaka!, lakini kufuatia amri hii, hao majambazi wenye huruma na maisha ya watu, hawatakuwa na huruma tena, na kama polisi ndio kwanza wamekuwa licenced to kill kwa mtindo wa MM, then every encounter ya polisi na majambazi, tutegemee nothing, no justice but blood bath!.

Tanzania ni nchi ya kidemokasia inayofuata katiba yenye kuzingatia haki na utawala wa sheria!, amri kuu ya kwanza ya haki, ni "no one is condemned unheard", yaani hakuna mtu atakayehukumiwa bila kusikilizwa!. Amri hii ya rais, imewapa mamlaka polisi, sio tena kuchunguza, kukamata na kuwapeleke majambazi wanaotumia silaha, mbele ya sheria, bali sasa polisi hawana tena haja ya kukamata na kufanya uchunguzi, bali kukitokea tuu tukio la uhalifu wa kutumia silaha, polisi wamepewa mamlaka kuwa ni wachunguzi, prosecutors, mahakimu tena kwa kutoa "capital punishment", na hakuna tena haja ya kumsubiri rais kuzisaini hizo hati za capital punishment, bali, wao wenyewe kutumia MM, kuitekeleza adhabu ya kifo, na baada ya hapo kusubirria kupandishwa vyeo!. Just imagine mashindano ya kupanda vyeo miongoni mwa polisi wetu!.

Kama wanasheria wetu, hawatashitushwa na amri hii ya rais, nitaamini sasa Watanzania wameanza kumwelewa rais wetu, na ukiisha elewa, huna haja ya kuhoji!.

Angalizo: Sitetei vitendo vyovyote vya uhalifu wa aina yoyote, bali natetea utoaji wa haki!, hata jambazi anayetumia silaha, anastahili kutendewa haki!. Natolea mfano wa nchi mbili za Maekani na Uingeeza. Miaka ya nyuma nchi zote hizi zilikubwa na vitendo vingi vya mauaji. Uingeeza ikafuta adhabu ya kifo!, vitendo vya mauaji, vikapungua kwa kiasi kikubwa!. Maekani ikaendelea na adhabu ya kifo, vitendo vya mauaji bado vimeongezeka!.

Amri ya kuwaua majambazi papo kwa papo, haitapunguza ujambazi, bali itawafanya hao majambazi ndio kugeua wauwaji wakuu, kwa hoja za "ama zao, ama zetu" na kwenye tukio lolote la ujambazi wa kutumia silaha, polisi wakitokea, sasa sio tena kutuliza amani bali kufanya a blood bath!, hivyo polisi sasa pia watakuwa ni target ya majambazi!.

Kwetu sisi waandishi, ikitokea polisi wakakutana na gun mike, au boom mike, au hata kamera wakaiona ni kama sihaha!, kama ilivyotokea mwa Daudi Mwangosi!, askai mhusika, atapandishwa cheo!. Kama wale vija wa Zombe, sasa watawadiwa vyeo!.

Huko nyuma niliwahi kushauri, kama katiba ni kikwazo, rais Magufuli, aiweke pembeni katiba na badala yake atawale kwa kutumia 'presidential decrees' tuu!. Hivyo kwa amri hii ya polisi kuua majambazi papo kwa papo, kama mahakama ni kikwazo, pia anaweza kuiweka pembeni, na kuwatumia polisi kutoa hukumu za kifo cha papo kwa papo, tena hili litaokoa fedha nyingi sana, maana majaji wa mahakama zetu, wanahudumiwa kwa gharama kubwa sana!.

Wasiwasi wangu kwa amri kama hizi, sio ili kuokoa maisha ya majambazi wanaotumia silaha, au kuwaacha tuu majambazi wanaotumia silaha kuua, lakini wao kuuliwa tuinawatetea!, no!, wasiwasi wangu ni utekelezaji wa amri za aina hii, zisije kuwa kwa majambazi ni mwanzo tuu, baadae amri kama hizi za 'kinyemela' zikaelekezwa kwa makundi mengine, yanayoonekana ni kero!.

Mwaka 1976, kulifanyika mauaji ya wazee waliokuwa wakituhumiwa kuwa ni wachawi. Serikali kupitia waziri wa Mambo ya Ndani kipindi hicho, Ali Hassan Mwinyi Mwinyi, kupitia Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mwanza, chini ya RC Peter Kisumo, RSO, RPC, DSO, na OCD wakadhamiria kwa kauli moja kukomesha vitendo hivyo kwa hizo hizo MM alizoamrisha Magufuli zitumike!.

Katika Mahojiano, yaliyoendeshwa eneo la Kigoto, watuhumiwa wawili, Masanja Makula Mazengenuka, na Isaack Mwanamkoboko, walipoteza maisha!.

Mwalimu Nyerere alikasika sana, Waziri Mwinyi, IGP, Pundugu, Director wa TISS Mzena, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Kisumo, RSO, RPC, DSO na OCD wote wakastaafishwa kwa manufaa, na wengine kupandishwa kizimbani, ambapo wote walifungwa, isipokuwa mshtakiwa Mzee wangu, tena aliokoka kwa vile tuu alikuwa anatetewa na wakili Murtaza Lakha!.

Utendaji wa Jeshi la Polisi unaongozwa na kitu kinachoitwa Police General Ordes ambacho tumekirithi kutoka kwa Waingereza kama tulivyorithi sheria zetu mbalimbali, ambazo zina maelekezo yote ni kwenye mazingira gani polisi anaruhusiwa kutumia silaha kuwadhibiti wahalifu na kuna polisi maalum wa kazi hiyo wanaoitwa snipers au wadunguaji, ambao wana shabaha na uwezo wa kulenga maeneo rasmi ya kulenga ili kumdestabilize mhalifu kwa lengo la kumkamata lakini sio kwa lengo la kumua!. Agizo la jana la Rais Magufuli, ni kuwaelekeza polisi kuua tena kwa haraka bila kuchelewa, na sasa kwa kila mauaji ya polisi, polisi hao badala ya kupandishwa kizimbani, sasa watapandishwa vyeo!.

Japo lengo la agizo hilo la rais, amelitoa kwa dhamira njema,(in good faith), lakini utekelezaji wake, unaweza kuligeuza jeshi letu la polisi kugeuka Gestapo!, na hata Adofu alipoanza, alianza hivi hivi kwa kuwa a populist leader, anayeshangiliwa sana na umati wa watu!, ni baadae sana, ndipo watu wakaja kugundua, by that time, it was too little too late, wakaishia kujuta!, kwa upande wetu, chonde chonde twendeni taratibu jamani, tufungue macho mapema before it is too late, tusije kujuta!.

Jumamosi Njema.

Pasco
Rejea.
Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know ...
IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality
Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa .
Simshangai Pasco wa JF tu; hapana, nawashangaa waandishi wote wa ..

Nina wasiwasi kama umepitia jeshini kwani kama ungepitiaungejua maana ya Mbinu Za Medani! Sio kuua asilani!
 
kwa upande wetu, chonde chonde twendeni taratibu jamani, tufungue macho mapema before it is too late, tusije kujuta
13528875_10209925973126643_344507121337551544_n.jpg
 
  1. Ninamshangaa sana Mpemaanavyoshabikia majambazi nayeye nimojawao nn?? Badala ya kuleta haja maendeleo unakomaa na habari zamajambazi siku wakikutembeleautaelewa vizuri umuhimu wa kauli ya raisi.

    ReportEditDelete
    + QuoteReply
1101112131415



Tatizo lako ni moja,huna utulivu wa fikra,una fuatilia hoja jukwaani kwa jicho la kishabiki,ukiipitia na kukosa walau sentensi moja iliyomsifu "mtakatifu wa watakatifu" unapaniki.

Kimsingi hakuna anayepingana na nia njema ya Mh.John Pombe Joseph Magufuli,Rais wa JMT na Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama katika kukabiliana na vitendo vya kihalifu nchini,ulinzi na usalama wa Taifa ni jukumu la msingi la kila Mtanzania bila kujali nafasi yake.

Hofu yetu ni namna kiongozi wetu anavyotoa matamko na maelekezo kwa vyombo vyake,na hofu yetu si ya bahati mbaya,tuna kumbukumbu ya matukio ya mauwaji yenye picha ya kupambana na uhalifu,lakini baadae ikagundulika yalikuwa ni mauwaji ya Raia wema wasio na hatia.

Hili linaweza lisionekane kuwa Tatizo,lakini ikitokea kesho ukapoteza ndugu/jamaa yako kwa kuuliwa kinyama kwa kudhaniwa ni jambazi,ndipo utakapokumbuka kwa nini tulilipinga kwa nguvu zote Tamko hili linalowahimiza polisi wetu kutumia nguvu badala ya weledi katika kupambana na uhalifu na wahalifu.

Sitaki kutumia mifano inayoleta simanzi,lakini kifo cha Mh.Imran Kombe aliyeuwawa kikatili kwa kudhaniwa ni jambazi bado nakikumbuka na ni moja ya tukio la kinyama zaidi dhidi ya haki ya kuishi ambayo ni haki namba 1 kwa mwanadamu yeyote.Kumbuka kifo hakina Rufaa,ukifa umekufa,Imran Kombe aliuwawa kimakosa lakini uhai wake haukurudi,alikufa.

Unalikumbuka tukio la kusikitisha la vijana watatu wafanyabiashara wa madini toka Mahenge?Vijana hawa nao waliuliwa kimakosa kwa kudhaniwa ni majambazi,lakini baadae iligundulika kuwa ni Raia wema waliouliwa kimakosa,ni nani aliyekikatia kifo rufaa ili vijana wale warudishiwe uhai wao?Kifo hakina rufaa.

Pamoja na nia njema ya kupambana na uhalifu,kwa kupitia mifano hiyo michache,upo uwezekano wa jeshi letu kutenda makosa wawapo Katika utekelezaji wa amri ya mkuu wao yenye motisha ya kupandishwa vyeo.Ni vema jeshi letu ambalo kwa siku za hivi karibuni limebobea sana katika intelijensia ya kuzuia haki za kisiasa,lijikite sasa kukabiliana na changamoto za uhalifu nchini kwa kuwa na mbinu za kisasa za kiintelejensia zitakazowawezesha kuitambua Mipango ya kihalifu mapema na kuidhibiti,badala ya kujipangu kumrukia jambazi ili wapandishwe vyeo.
 
Massenberg, sasa naanza kuelewa kwanini Marais wastaafu hawakauki Ikulu.

Mkulu ataleta shida kubwa sana kwa haya matamko yake.
Inapaswa mtu awe anamkumbusha kuwa yeye ni Rais.
Ajue kuwa kutoa order zenye utata na ambazo hazitekelezeki kunashusha hadhi yake!

hatari..!
 
Wanabodi,
Usikute kifo cha Akwilina, ni utekelezaji wa agizo hili!. Yule polisi aliyefyatua risasi aliona jambazi fulani lenye silaha miongoni wa waandamanaji wale, na akalifyatulia risasi ili kulinyanganya silaha, lakini risasi hiyo ikapinda na kuingia kwenye dala dala ya kumpata yule malaika wa Mungu.

Hobo, tusiwalaumu sana vijana wa kamanda Sirro, as if tukio la kifo cha Akwilina lilipangwa, ni bahati mbaya tuu, na limetokea katika utekelezaji wa amri halali ya Amiri Jeshi Mkuu!.

Polisi hawakuanza leo matukio kama haya, hivyo hapa ni katika kukumbushana tuu, mambo kama haya yaliishatokea huko nyuma, yametokea sasa, na yatatokea tena!. Tutakumbushana!.
P
 
Wanabodi,
Usikute kifo cha Akwilina, ni utekelezaji wa agizo hili!. Yule polisi aliyefyatua risasi aliona jambazi fulani lenye silaha miongoni wa waandamanaji wale, na akalifyatulia risasi ili kulinyanganya silaha, lakini risasi hiyo ikapinda na kuingia kwenye dala dala ya kumpata yule malaika wa Mungu.

Hobo, tusiwalaumu sana vijana wa kamanda Sirro, as if tukio la kifo cha Akwilina lilipangwa, ni bahati mbaya tuu, na limetokea katika utekelezaji wa amri halali ya Amiri Jeshi Mkuu!.

Polisi hawakuanza leo matukio kama haya, hivyo hapa ni katika kukumbushana tuu, mambo kama haya yaliishatokea huko nyuma, yametokea sasa, na yatatokea tena!. Tutakumbushana!.
P
Mkuu tangu lini risasi ikapinda au kukata kona?kwa nini isingepinda na kumtwanga mkuu wake?kilichotokea ni uzembe na kufanya kazi kwa mazoea,au pia inaweza kuwa makusudi jeshi LA police halifai linatakiwa liundwe upya ili tupate watu timamu,
 
Baada ya Mhe. Zitto kushikiliwa na polisi kwa tuhuma za kulichafua jeshi la polisi, nafanya tuu rejea ya kuangazia usafi wa jeshi letu la polisi.
Tuungane kuombea Zitto atendewe haki, lakini pia tusiache kulitaka jeshi letu la polisi, wajitathmini
Paskali.
 
Leo tarehe 21 december kauli yako pale kurasini ya kuzuia askari kuwekwa ndani wakufanya kosa na kwamba polisi akiua apandishwe cheo apewe na cheti huku ukijinasibu kuwa polisi hawezi kumuonea mtu huo ni udikteta nikitumia vyema kigezo cha kuingilia mihimili mingine hapo umefeli.
•Labda mheshimiwa huwajui polisi hawa unaowasifu kama huamini zile silaha walizokuonyesha kuwa zimenyang'anywa kwa majambazi zingine n za zamani ila umelishwa matango poli
Mheshimiwa Amirijeshi mkuu Nchi hii hakuna aliyepo juu ya sheria(kwa mujibu wa katiba)
Hivyo ni vyema ujipime kwa kauli zako kwani zinaweza kuwaletea viburi watendaji wako mheshimiwa tafadhali nakuomba sana jirekebishe.

...







Kayasema hayo, tena hadharani?

Askari wamepewa liseni ya kuua yeyote 'anayetuhumiwa' kuwa jambazi?
Kutuhumiwa kuwa jambazi kipimo chake ni kipi? Hicho kipimo anacho askari pekee?

Jambazi mwenye silaha, au jambazi mkaba kabari n.k. wote hukumu zao ziwe ni kifo kwa mkono wa askari?
Mahakama, mahakimu na sheria zipo za nini kama askari wamepewa uamzi wa mwisho!

Huku ndiko kukosa busara na akili ya ubinaadam inayomwondolea heshima.

Ni mwendelezo wa mambo ambayo tayari tumeyashuhudia, askari kutowajibishwa kwa makosa wanayofanya. Aliyemuua mwanafunzi Akwilina ni mfano wa haya anayoyasemea sasa hivi kila mtu ajue.

Mwisho wake ni nini, askari akimuua mpizani wa serikali au yeye mwenyewe asisumbuliwe? Apandishwe cheo?






naunga mkono uboreshaji wa miundombinu
 
Wakuu habari za leo?
Nimemsikia Mh Rais wakati akizungumza na Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo yandani kuwa endapo askari polisi akifanikiwa kumuua mtuhumiwa wa ujambazi basi yeye hataki kusikia eti askari wake amewekwa mahabusu kwajili ya uchunguzi. Amemtaka IGP kumpandisha cheo na kumpatia zawadi zingine ikiwemo kumuongezea mshahara wake badala ya kumsweka rumande kwa uchunguzi.
Je ni sahihi kwa Mkuu wa nchi kutamka maneno yale tena hadharani??

Kila mara tumekuwa tukiwalalamikia Polisi kwa kuwabambikizia kesi raia vp kwa maneno yale kweli Mh Rais ni Mtetezi wa Wanyonge au ndiye kitanzi kwa Wanyonge??
 
Wakuu habari za leo?
Nimemsikia Mh Rais wakati akizungumza na Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo yandani kuwa endapo askari polisi akifanikiwa kumuua mtuhumiwa wa ujambazi basi yeye hataki kusikia eti askari wake amewekwa mahabusu kwajili ya uchunguzi. Amemtaka IGP kumpandisha cheo na kumpatia zawadi zingine ikiwemo kumuongezea mshahara wake badala ya kumsweka rumande kwa uchunguzi.
Je ni sahihi kwa Mkuu wa nchi kutamka maneno yale tena hadharani??

Kila mara tumekuwa tukiwalalamikia Polisi kwa kuwabambikizia kesi raia vp kwa maneno yale kweli Mh Rais ni Mtetezi wa Wanyonge au ndiye kitanzi kwa Wanyonge??
Huyu atapelekwa ICC, haya yanawekwa kwenye records!
 
Back
Top Bottom