Hili la Ukosefu wa Ajira tatizo lilianzia hapa kwenye D2, wazazi tuwaambie vijana ukweli, vyuo vya ovyo ovyo elimu ovyo!

Hili la Ukosefu wa Ajira tatizo lilianzia hapa kwenye D2, wazazi tuwaambie vijana ukweli, vyuo vya ovyo ovyo elimu ovyo!

Ndugu wazazi wenzangu wasalamu,

Kuna jambo nataka niwaeleze, na hii ni pamoja na vijana wenzangu, wanaopata maisha ya tabu kwenda kusoma miaka zaid ya 18 kutegemea ndoto ambazo hazitimii.

Nitaeleza kidogo:
Hapo zamani kidogo, chini ya miaka ya 2000s ilikuwa ni lazima mtoto afaulu Darasa la nne ndio aendelee na masomo ya Darasa la 5 hadi la saba, kuanzia miaka ya 2000 hivi, hali ikabadilika, wakasema wote waendelee, watu kimya...

Hadi kufikia mwaka 2002, kwa "waliobahatika" kuendelea na secondari FORM 11 ilikuwa lazima upate wastani wa ngalao alama 30, nao ukafutwa, awali ilikuwa 21, yani angalao D flat,

Kuendelea secondary, yani form 3 had 4, ilikuwa ni kaz sana kupata Div 1, ili ufaulu kias hicho lazima uwe mtu smart sana yani sana, yani sana, saivi yani Single Digits kawaida sana.

Kipindi hicho Kupata Div ONE au TWO, lazima uwe umepata D hesabu, otherwise huwezi pata DIV 1 ukiwa na F ya hesabu, kwa sasa hivi mambo ni tofauti kabisa, hata uwe na F ngap wewe ni Kijiti tu
Hiyo haikuishia hapo, ikaja kwenda Chuo, kuna wanasiasa wanataka vyuo vikuu viwe kila wanapotoka

Kuna chuo kikuu kinajenga matawi kila mkoa na wilaya
Kuna chuo kikuu kina tawi Kizumbi, Simiyu, Msata, Dodoma, na maeneo mengine mengi tu kutaja machache,

Coz zinazofundishwa huko ni zile zile, Laws, Accounting, BAs, Education, Business Admins, Compyuta etc.

Kuna wimbi la vyuo vya elimu ya afya ya D2, yani ukiwa na D2 za biology na Chemistry , una chance ya kuwa mfamasia au Daktari....

Ili kusoma chuo kikuu zamani, kupata coz ilibidi ufaulu wa hali ya juu sana, kuna kipindi UDSM ilikuwa kupata Laws lazima upate Div 1 ya 3 au 4 mwisho, sikuizi hata E 2 NA D1 Unasoma Laws,

Zamani bila form 6 au Cheti kisafi cha Dip huwez kwenda Chuo kikuu, sikuizi ni D4 TU, zinatosha.

Turudi kwenye vyuo vyenyewe,

Zamani ilikuwa ukifaulu kwa daraja zuri la 2, au tatu unapangiwa vyuo, kama chuo cha maji, Arusha Tech, Dip ya Afya nk.

Sasa hivi ni mwendo wa D4 tu, na wengine wameacha kutoa elimu ya ufundi wanatoa Degree.. yani ni mwendo wa kufyatua tu Bachela.

Coz kama IT, Computer Science and Engeneering, Forests, ects lazima uwe mwanafunzi mwenye mchepuo wa sayansi, na shule nyingi zilikuwa na maabara , sasa hivi mtu ana A ya chemistry hajawahi ona Spatula kwa macho, au hajawahi hata kufanya titration.


Chanzo ilikuwa ni moja,

Wanasiasa wengi waliona fahari kusifia ufaulu bila kujua madhara yake kwa taifa, jiulize kila mwaka ufaulu unaongezeka?? how is that?

Wanasiasa wengi wakaanza kujinasibisha na degree za uwongo nk..( ref Msemakweli)
Wengine na ma PHD ya kubumba hadi kwa viongozi wa dini... hadi wafanyabiashara,... jina DOKTA likabamba sana....

Matokeo yake;

AJIRA AJIRA AJIRA AJIRA>>>>>>>>>AJIRA 8000, mara Mil 8, Mara elf 5 Mara elfu Moja,

Utaajiri wote kwenye serikali ipi?

Nani afanye kazi zinazohitaji skills za kati kama ufundi.

Waliodhani wanasaidia wananchi wakawapoteza moja kwa moja, ikawa sasa shida imekuja kukaa kwa wazazi na vijana wao...tip LOAN BOARD... unasoma degree yako huko ya nini sijui, unawekewa deni MIl 28, hakuna kazi na deni linaongezeka kila siku, na huko tunakoenda lazima watapita na huko bank kujaribu ku recover bad loans.. ni suala la muda tu.


Wazazi hawataki kuelezewa ukweli au vijana wanapenda kujionesha wapo chuo kikuu hata kama ni kupoteza muda...

Fundi AC huwez muona hana kazi
Fundu bomba kila siku kazi
FUndi mchundo kazi za kutosha
Fundi Cherehani kila siku kazi
Fundi rangi kazi za kutosha
Fundi mechanics kazi za kumwaga.. nk nk..

FUNDI DEGREE AMELALA ANASUBIRIA MCHONGO NA KUPERUZI STATUS ZA WHATSUP NA INSTAGRAM. Twende kazi

Wengine wamekalia kusubiria kazi vyuoni, yani degree after degree.. hadi PHD with '0' experience...

Mwisho wa siku serikali inazidiwa na tatizo iliyotengeneza yenyewe........ degree na elimu zenye ufaulu unaoongezeka kila Mwaka....

To you Hon. Ndungai, you cant make real hustlers with this kind of generation come what may.

Sasa hivi mmekuja na mjadala wa kufuta kiingereza kimya kimya, mmeanza na Mahakamani ambapo ndio sehem lugha ya kingereza inatumiwa zaidi, tunawaangalia tu... tatizo liongezeke tuone nini kitatokea.

Disclaimer;
I'm not trying to control the state house neither Ministry of Education, just my few cents on the drama.
Ufundi ni low skill labour. Je wewe unashona suruali ngapi kwa mwaka ili unishawishi niwe fundi hapa mtaani?
 
Kwani hao waliosoma zamani waliunda ndege au gari?
Utaniaminishaje kuwa walihitimu vizuri wakati hawaja achieve cha maana zaidi ya ku implement/ issue office documents tu.
Mashirika mengi yaliflisiwa na watu waliosoma zamani .
Waliosoma zamani were very incompetent people, they were less informed and non innovative. Fuc#k the old school idea!!!
 
Inasikitisha sana.Kutokana na hali inayoendelea hapa nchini Ninashauri kiongozi mkuu wa serikali ajiuzulu ili kupisha kiongozi mwingine mwenye uwezo zaidi
 
.
20220312_080502.jpg
 
Ndugu wazazi wenzangu wasalamu,

Kuna jambo nataka niwaeleze, na hii ni pamoja na vijana wenzangu, wanaopata maisha ya tabu kwenda kusoma miaka zaid ya 18 kutegemea ndoto ambazo hazitimii.

Nitaeleza kidogo:
Hapo zamani kidogo, chini ya miaka ya 2000s ilikuwa ni lazima mtoto afaulu Darasa la nne ndio aendelee na masomo ya Darasa la 5 hadi la saba, kuanzia miaka ya 2000 hivi, hali ikabadilika, wakasema wote waendelee, watu kimya...

Hadi kufikia mwaka 2002, kwa "waliobahatika" kuendelea na secondari FORM 11 ilikuwa lazima upate wastani wa ngalao alama 30, nao ukafutwa, awali ilikuwa 21, yani angalao D flat,

Kuendelea secondary, yani form 3 had 4, ilikuwa ni kaz sana kupata Div 1, ili ufaulu kias hicho lazima uwe mtu smart sana yani sana, yani sana, saivi yani Single Digits kawaida sana.

Kipindi hicho Kupata Div ONE au TWO, lazima uwe umepata D hesabu, otherwise huwezi pata DIV 1 ukiwa na F ya hesabu, kwa sasa hivi mambo ni tofauti kabisa, hata uwe na F ngap wewe ni Kijiti tu
Hiyo haikuishia hapo, ikaja kwenda Chuo, kuna wanasiasa wanataka vyuo vikuu viwe kila wanapotoka

Kuna chuo kikuu kinajenga matawi kila mkoa na wilaya
Kuna chuo kikuu kina tawi Kizumbi, Simiyu, Msata, Dodoma, na maeneo mengine mengi tu kutaja machache,

Coz zinazofundishwa huko ni zile zile, Laws, Accounting, BAs, Education, Business Admins, Compyuta etc.

Kuna wimbi la vyuo vya elimu ya afya ya D2, yani ukiwa na D2 za biology na Chemistry , una chance ya kuwa mfamasia au Daktari....

Ili kusoma chuo kikuu zamani, kupata coz ilibidi ufaulu wa hali ya juu sana, kuna kipindi UDSM ilikuwa kupata Laws lazima upate Div 1 ya 3 au 4 mwisho, sikuizi hata E 2 NA D1 Unasoma Laws,

Zamani bila form 6 au Cheti kisafi cha Dip huwez kwenda Chuo kikuu, sikuizi ni D4 TU, zinatosha.

Turudi kwenye vyuo vyenyewe,

Zamani ilikuwa ukifaulu kwa daraja zuri la 2, au tatu unapangiwa vyuo, kama chuo cha maji, Arusha Tech, Dip ya Afya nk.

Sasa hivi ni mwendo wa D4 tu, na wengine wameacha kutoa elimu ya ufundi wanatoa Degree.. yani ni mwendo wa kufyatua tu Bachela.

Coz kama IT, Computer Science and Engeneering, Forests, ects lazima uwe mwanafunzi mwenye mchepuo wa sayansi, na shule nyingi zilikuwa na maabara , sasa hivi mtu ana A ya chemistry hajawahi ona Spatula kwa macho, au hajawahi hata kufanya titration.


Chanzo ilikuwa ni moja,

Wanasiasa wengi waliona fahari kusifia ufaulu bila kujua madhara yake kwa taifa, jiulize kila mwaka ufaulu unaongezeka?? how is that?

Wanasiasa wengi wakaanza kujinasibisha na degree za uwongo nk..( ref Msemakweli)
Wengine na ma PHD ya kubumba hadi kwa viongozi wa dini... hadi wafanyabiashara,... jina DOKTA likabamba sana....

Matokeo yake;

AJIRA AJIRA AJIRA AJIRA>>>>>>>>>AJIRA 8000, mara Mil 8, Mara elf 5 Mara elfu Moja,

Utaajiri wote kwenye serikali ipi?

Nani afanye kazi zinazohitaji skills za kati kama ufundi.

Waliodhani wanasaidia wananchi wakawapoteza moja kwa moja, ikawa sasa shida imekuja kukaa kwa wazazi na vijana wao...tip LOAN BOARD... unasoma degree yako huko ya nini sijui, unawekewa deni MIl 28, hakuna kazi na deni linaongezeka kila siku, na huko tunakoenda lazima watapita na huko bank kujaribu ku recover bad loans.. ni suala la muda tu.


Wazazi hawataki kuelezewa ukweli au vijana wanapenda kujionesha wapo chuo kikuu hata kama ni kupoteza muda...

Fundi AC huwez muona hana kazi
Fundu bomba kila siku kazi
FUndi mchundo kazi za kutosha
Fundi Cherehani kila siku kazi
Fundi rangi kazi za kutosha
Fundi mechanics kazi za kumwaga.. nk nk..

FUNDI DEGREE AMELALA ANASUBIRIA MCHONGO NA KUPERUZI STATUS ZA WHATSUP NA INSTAGRAM. Twende kazi

Wengine wamekalia kusubiria kazi vyuoni, yani degree after degree.. hadi PHD with '0' experience...

Mwisho wa siku serikali inazidiwa na tatizo iliyotengeneza yenyewe........ degree na elimu zenye ufaulu unaoongezeka kila Mwaka....

To you Hon. Ndungai, you cant make real hustlers with this kind of generation come what may.

Sasa hivi mmekuja na mjadala wa kufuta kiingereza kimya kimya, mmeanza na Mahakamani ambapo ndio sehem lugha ya kingereza inatumiwa zaidi, tunawaangalia tu... tatizo liongezeke tuone nini kitatokea.

Disclaimer;
I'm not trying to control the state house neither Ministry of Education, just my few cents on the drama.
Kipindi nasoma , kwa mawazo haya isingekuwa ajabu , mwalimu wangu kusema tukupigie makofi , Eko kaka natamani ningekuona hata sura nikupongeze ila ndio hivyo tena , tupo kwenye andaki ya "where we dare to talk openly " .

Natamani elimu ingepita kwanza mtaani kuwajulisha wazazi kuwa kwenda chuo sio uhakika wa ajira tena , maana wazazi wakishaona watoto wamepewa hela ya kujikimu basi wengi wao wanafikiri bila shaka ajira ni lazima , kutwa kucha kuwananga vijana waliohitimu na wapo nyumbani tu .

Poleni sana ndugu zangu wahitimu, embu kubali uhalisia wa muda wa sasa ili muendane na mtaa .
 
D2 maake kwanza apa nichekee😂😂😂😂 wew unataka D ngapi kwa mfano Elimu ya Tz ni complex kuliko ata za nchi za nje
 
Mkuu hiyo sio sababu wala nini Acha raia wawe na elimu shida ni serikali sio Degree nyingi Hebu nenda nchi zilizoendelea KAZI zinatafuta watu licha yakuwa nawasomi wengi viwanda vipo vingi , uwekezaji ndo usiseme ajira zinatafuta watu. SASA Tanzania yetu imekalia siasa tuu kipindi kile chamagu Mpaka wawekezaji wanakimbia Kwa Ujinga na uonevu Kwa wawekazaji hizo ajira zitatoka wapi.

Kama unavyoona Nchi inavyopambana kuongeza miundo mbinu ya barabara, madaraja , kuongeza njia zengine mbadala za usafiri kupunguza foleni na shida ya usafiri kutatua hayo matatizo ndivyo serikali pia inatakiwa kuwekeza zaidi katika viwanda, Miradi na masharti ya kuwekeza yawe nafuu kukabiliana na tatizo la ajira na sio kuweka vikwazo watu wasiwe naelimu.
 
Huu uzi ni madini sana ajabu watu hawataki vitu vya msingi. System ya elimu yetu na mtaala kwa ujumla inasikitisha sana na kadri siku zinavyosonga ndivyo inavyozidi kudorora.

Waliomaliza form four ndiyo tunawachukua siku hizi kufanya kazi za ndani, ufahamu wake huwezi mtofautisha na darasa la saba! Baadhi ya Graduate wa siku hizi ndio hawa wanaandika "tyu badala ya tu" "xaxa badala ya sasa"!! Unaongea nae unaona hata form 4 wa zamani alikuwa smart kuliko yeye!

Tuna safari ndefu na ya kusikitisha.
 
Mifumo hii ya elimu zetu tusitegemee kuwa na job creators bali watembeza bahasha kila kukicha. Hawa wachina, wahindi huko kwao wana home industries nyingi sana na hizo zimeajiri wengi pamoja na kutengeneza vitu mbalimbali na kuuza mpaka nje ya mipaka yao huku sie tunayo Sido kila mkoa lakini iko hoi bin taaban. Hawa wachina na Kanji bhai nowdays wanakuja huku kwetu na technology yao wengine hawana kabisa wanaanzisha projects kisha wanawapa vibarua wenye degree kwa ujira wa utumwa. Inasikitisha sana,kuwa mtumwa kwenye nchi yako mwenyewe yenye wingi wa maziwa na asali.
 
Mkuu hiyo sio sababu wala nini Acha raia wawe na elimu shida ni serikali sio Degree nyingi Hebu nenda nchi zilizoendelea KAZI zinatafuta watu licha yakuwa nawasomi wengi viwanda vipo vingi , uwekezaji ndo usiseme ajira zinatafuta watu. SASA Tanzania yetu imekalia siasa tuu kipindi kile chamagu Mpaka wawekezaji wanakimbia Kwa Ujinga na uonevu Kwa wawekazaji hizo ajira zitatoka wapi.

Kama unavyoona Nchi inavyopambana kuongeza miundo mbinu ya barabara, madaraja , kuongeza njia zengine mbadala za usafiri kupunguza foleni na shida ya usafiri kutatua hayo matatizo ndivyo serikali pia inatakiwa kuwekeza zaidi katika viwanda, Miradi na masharti ya kuwekeza yawe nafuu kukabiliana na tatizo la ajira na sio kuweka vikwazo watu wasiwe naelimu.
Yawezekana hujui maana ya elimu. Elimu sio degree wala vyeti.
 
Yawezekana hujui maana ya elimu. Elimu sio degree wala vyeti.
Hatujafika huko na usilazimishe tufike huko elimu zetu hazizai matunda na hazimuathiri MTU Kwa kumjengea misingi imara na uwezo wa kureason wala shida sio vikwazo Ila nimfumo wa elimu lakini usiseme elimu inaenda kutengeneza shida ya ajira.
 
Pa
Hapa kweli wa afrika tumepigwa na kitu kizeetoo kwa head.

#MaendeleoHayanaCham
Palamagamba alisoma PhD ujerumani. Nadhani alisoma kwa Kiingereza huko ujerumani.

Kimsingi ufundishaji kwa maana ya transfer of knowledge iko kwa kiwango cha chini. Hata somo la Kiswahili linafundishwa kwa kiwango cha chini.
Lawama zisielekezwe kwenye lugha tu
 
Hapa kweli wa afrika tumepigwa na kitu kizeetoo kwa head.

#MaendeleoHayanaChama
Nilipokuwa Shule ya Msingi nilikuwa natafsiri maswali ya Kiswahili kwa Kilugha.

Sekondari nilitafsiri Kiingereza kwa Kiswahili ndipo nirudi kujibu kwa Kiingereza.

Hata sasahivi nikiambiwa andaa mpango kazi kwa kiingereza. nitaanza kuhangaika kutafsiri.

Huyo jamaa katupiga sana na kitu chenye tani nyingi sana kichwani
 
Back
Top Bottom