Hili la watu kula supu ya ngozi ya ng'ombe/mbuzi lina usalama kiasi gani?

Hili la watu kula supu ya ngozi ya ng'ombe/mbuzi lina usalama kiasi gani?

Tulizoea bidhaa kama ngozi ya ng'ombe ikitumika katika utengenezaji wa bidhaa mbalimbali kama vile mikanda, Mabegi nk.

Nna mwezi mzima na zaidi naweka oda ya ngozi ya ng'ombe kwa ajili ya kuchemshia mbwa nakosa nashindwa kujua kwanini.

Basi Ikabidi nimuulize huyo muuza bucha kwanini zimekuwa adimu hivyo au soko la Nje ya nchi limekuwa kubwa

Jibu alilonipa sikuamini kwani aliniambia ya Kuwa oda nyingi zinachukuliwa kwa ajili ya kwenda kutengenezea supu ya kuuza na wachache hubeba majumbani kwa matumizi ya nyama ya kula Wao.
Wateja wengi wa supu hiyo ni wale wa hali ya chini na walevi wa Pombe za bei rahisi na matatap kutokana na kutoweza kumudu gharama za kununua nyama au supu ya nyingine tuzijuazo

Wanachofanya ni kuchoma /kuunguza yale manyoa yote na baada ya hapo hubandika jikoni tayari kwa kuchemsha supu hiyo.

Bado sijajua kama ulaji wa aina hiyo ya supu ya ngozi una madhara kiafya kwa walaji hao au ni sawa tu. Na mtu anaekula nyama.

Supu hiyo imekuwa ikiuzwa kibakuli kwa. Sh 500.

Naahidi kuja na Picha na tukio hili nimejionea mwenyewe hapa Kilimanjaro

Hili la watu kula supu ya ngozi ya ng'ombe /mbuzi linasababishwa na ugumu wa maisha.​

Unakuta mtu kapata Kvant jana anaamka asubuhi ni mchovu na sna buku mfukoni. The next ni supu ya ngozi siku ipite​

 
Ndo mana makongoro yanaitwa kongoro na sio ngozi, hapa naongelea mtu kula ngozi na sio kongoro,
Kongoro lina nyama na mafuta flani hivo ndani yake isitoshe pia ni tiba kwa watu wa miguu inayouma
Kweli nimeamini weye ndiye mwenye hiyo id.Kwa hiyo kongolo halina ngozi?😂😂😂😂
 
Ugumu wa maisha ndio chanzo cha watu kula ngozi na sehemu za siri za wanyama mfano pum*** za mbuzi na ng'ombe zimekuwa maarufu, watu wanagegeda kwa fuji. Turudi kwenye mada. Kazi mojawapo ya ngozi ni kutoa uchafu mwili kwa njia ya jasho. Sumu za mwili pia hutolewa kwa njia ya jasho ingawa zinaweza kutolewa kwa njia nyingine. Hivyo kula ngozi ni sehemu ya kula sumu za mwili wa huyo mnyama
Asante, naona wengi wao hawaelewi hili, ngozi ilivo ngumu inatumika kutengeneza bags na mikanda sasa sijui kongoro linatumika kutengeneza bidhaa gani
 
Mimi kitaa chetu tulikuwa tukipata hata kwa mia tatu kabla ya kupandishwa kuwa jero na watu wanakuwa nyomi kwenye supu

Nb: Imeniuma sana kuhusisha hiyo kitu na walevi wa mataputapu wkt mtaani hii kitu ni pendwa kwa rika .
 

Hili la watu kula supu ya ngozi ya ng'ombe /mbuzi linasababishwa na ugumu wa maisha.​

Unakuta mtu kapata Kvant jana anaamka asubuhi ni mchovu na sna buku mfukoni. The next ni supu ya ngozi siku ipite​

Supu ya ngozi kibakuli 500
 
Asante, naona wengi wao hawaelewi hili, ngozi ilivo ngumu inatumika kutengeneza bags na mikanda sasa sijui kongoro linatumika kutengeneza bidhaa gani
Kongoro nyama ni ndogo sana , asilimia kubwa ni ngozi, mfupa na uboho, ila kitamu zaidi ni ngozi na uboho, ngozi ya ngumu ndio maana kongoro linachemshwa mda mrefu ili ngozi iive
 
Back
Top Bottom