Hili ndilo kundi la wanadini wenye uwezo mkubwa kuliko wasioamini dini na wanadini wengine

Hili ndilo kundi la wanadini wenye uwezo mkubwa kuliko wasioamini dini na wanadini wengine

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Kuna propaganda kubwa zinaendelea duniani na JF za kuwaponda wanaoamini dini, na kuwaona wanaopuuza mambo ya imani kuwa ni majiniasi. Hii ni kweli kwa aina flani ya wanadini na sio sahihi kabiss kwa kundi kubwa la wanadini pia.

Dini namaanisha watu wanaoamini kuhusu uwepo wa Mungu na nguvu zake.


Kundi kubwa la wanadini wamefungwa kwenye kifungashio cha maelekezo ya wanadamu. Viongozi wamewapiga pin wasimuone huyo Mungu bila kupitia wao.

Wamebuni nadharia na siasa nyingi za kuwadunisha waumini ili wawatawale. Waumini waliokubali kuwa chini ya mifumo hii unaweza kuwaambia wafanye chochote wakafanya. Hii imepelekea watu wasio na dini kutumia watu hawa na viongozi wao kama rejea ya ujinga wa dini na wanadini hao.

Kiukweli kundi letu sisi tunaoamini na kufundisha uwezo wa Mungu kwa mtu mmojammoja ni mkubwa kuliko kiongozi wa kisiasa na kidini, kuliko mqgonjwa na shida. Tunahamasisha mwanadamu hapaswi kuwa chini ya mwanadamu mwenzake kiroho kwa ujanja wowote ule.

Tunawaaminisha kuwa sentensi za Mungu ni kubwa na zina uwezo mkubwa kuliko hata vinu vya nuclear vya NK. Tunaokataza watu wasiwe na best friend yoyote duniani kabla ya kumfanya Yesu/Mungu kuwa rafiki/msiri na mwezeshaji mkuu wa maisha binafsi.

Tunaohamasisha mwanadamu mwenye roho mtakatifu anauwezo mkubwa kiakili na kinguvu kuliko mchawi, mganga, majini, majambazi etc. Na hawa wanatakiwa kumuogopa na kutetemeka sio yeye kuwaogopa huyu ndiye mtu mwenye akili na nguvu zote duniani.

Ni hayo tu.

Mtumishi
Matunduizi
 
  • Thanks
Reactions: I M
nakuunga mkono kwamba, binadamu asilazimishwe kuwasiliana na Mungu kupitia mtu fulani
na hili ndo fundisho la biblia na la mitume

Yn 14:6​

Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Sema kuna njia nyingine zimebuniwa. Njia ni moja tu yaani Yesu
kuna njia za uongo zimebubniwa mfano, tunatakiwa kupitishia maombi yetu kwa Bikra Maria au padri au askosfu au Papa(pope)
pia uongo upo kwamba hadi watu fulani FULANI watuombee
 
"I have too much respect for the idea of God to hold him responsible for such an absurd WORLD. "
 
"I have too much respect for the idea of God to hold him responsible for such an absurd WORLD. "
 
"I have too much respect for the idea of God to hold him responsible for such an absurd WORLD. "
 
Back
Top Bottom