ile ardhi tunasema ni ya waisrael sio kwasababu waliuziwa au kulowea pale, ni kwasababu Mungu aliwapa kama urithi wa vizazi vyao vyote, ndio maana wengi wapo Marekani, wapo nchi nzuri za ulaya ambako kuna maisha bora kuliko israel, lakini wanarudi Israel kwa sababu Biblia (Torah) inavyo vifungu vinavyoonyesha aliwapa wao iwe ya kwao. ni wanadamu pekee ambao Mungu mwenyewe aliyeumba dunia hii aliwapa specific area kuwa mali yao.
ushahidi upo, makaburi ya wafalme wao yapo hadi leo, makaburi ya ibrahim, Daudi, suleiman, na wengi sana yapo. pia hekalu ambalo suleiman alilijenga na ambalo lilikuwepo hata kipindi cha Yesu mabaki yake yapo hadi leo, pale kwenye weiling wall (ukuta wa kilio), ila wakati wa crusades waislam/ottoman waliwapiga wakristo wakavunja hekalu hilo na kujenga ule msikiti. ule msikiti haujajengwa na muhamad saw, ila hekalu ambalo Yesu aliabudi yaani lile lilijenga miaka 40 akawaambia atalivunja ajenge kwa siku 3 lipo hadi leo ndio pale wanaendaga kugusa matofali na kulia lia. ila huo msikini hata haukuwepo kipindi cha muhamad hivyo wapalestina au niseme waislam hakuna chochote wanakidai pale.