Hili swali linanitatiza sana, kuna utaratibu wowote wa mwanajeshi kuacha kazi, pale anapotakiwa kwenda vitani?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Nimejaribu kufikiria hivyo, baada ya kuona picha za wanajeshi walio-uwawa huko kwenye vita ya Ukraine na Urusi.

Naona vijana wameangamia, huku wakiwa wameacha tegemezi, watoto, wake n.k; huku wanaofanya maamuzi wakiwa ofisini wakipulizwa viyoyozi.

Inawezekana, wakuu? Uhai kwanza, mengine baadaye.​
 
Kwahiyo MWANAJESHI akiwa hivyo kuwa akiona vita aache kwenda we utalindwa na Nani Na pia unataka turudi utumwani tumilikiwe na taifa x namana adui akija kwako atamfanya mke wako anavyotaka watoto wako na Mali zako pamoja na ww mwenyew
 
Kwahiyo MWANAJESHI akiwa hivyo kuwa akiona vita aache kwenda we utalindwa na Nani Na pia unataka turudi utumwani tumilikiwe na taifa x namana adui akija kwako atamfanya mke wako anavyotaka watoto wako na Mali zako pamoja na ww mwenyew
Kwa hiyo uko tayari, mtu mwingine apotee, ili wewe uendelee kufurahia maisha?
 
Hii dunia unahitaji akili sana iwapo haupo kwenye kundi la watawala. Whoever created system ya binadamu ya discpline walikuwa na akili kubwa sana sababu tungeuana mpaka tuishe. Imagine kiongozi wako anayepata kila kitu na watoto wapo salama anatoa amri uache familia na watoto wako uende ukapigane nchi nyingine au kulinda amani halafu yeye ndo anapewa sifa kuwa ni jemedari amiri jeshi mkuu.
 
Umefikiria point kubwa mkuu.....[emoji123][emoji123][emoji23][emoji23]
 
Inahitaji umakini mkubwa katika kufikiria
 
Kwanza ujue mwanajeshi si raia ila raia anaweza kuwa mwanajeshi na si kila raia anaweza kufuzu kuwa mwanajeshi. Inachukua mafunzo ya kipekee sana kumbadirisha raia kuwa mwanajeshi. Swali lako umeuliza kiraia ndiomana unashangaa inakuwaje amri inapotoka wanajeshi wanatii bila kupinga.
Just know that It takes special trainings to turn a civilian to be a SOLDIER and once a soldier will always be a soldier.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…