Historia ya kweli ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda

Historia ya kweli ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda

NI MWENDELEZO WA HISTORIA YA KWELI YA MAUAJI YA KIMBARI YA RWANDA

Sehemu ya nne

Kabla ya mvua ni mawingu.! Je, kabla ya mawingu ni nini?

JUA KALI…

Katika mapambano yoyote yale mara nyingi ili kufikia lengo unapaswa kufanya mambo ya mzunguko mno kana kwamba unatoka nje ya lengo hilo lakini hatimaye uje kutimiza lengo hilo hilo.

Nitaomba kunena kwa mifano ya uhalisia…

Nimekuwa nikieleza mara kadhaa kwamba nimesoma masomo ya bibilia darasani kwa muda wa miaka sita. Nakumbuka nikiwa kijana wa sekondari mwalimu wangu wa somo la ‘Divinity’ tuliwahi kujadili nae sana kuhusu kisa cha wana wa Israel kutoka Misri kwenda Kanani. Mimi na wanafunzi wenzangu kwenye mjadala huo tulikuwa tunauliza ni kwa nini wana wa Israel watumie miaka arobaini kusafiri kutoka Misri kwenda Kanani wakati kiuhalisia kwa mwendo wa kutembea kwa miguu hata sasa kama utatembea utatumia kama siku tatu tu hivi kama utapita njia sahihi ambayo imekuwa inatumiwa na watu tangu mwanzoni mwa kizazi agano jipya (miaka ya 300 B.C na kuendelea mpaka sasa).

Tulilikoleza swali letu zaidi kwa kuongeza hoja ya kwamba wana wa Israel kama ambavyo tunasoma kwenye vitabu vitakatifu ni kwamba, katika safari yao hii mbele yao, juu angani kulikuwa na kama wingu au muda mwingine nguzo ya moto ambayo iliwa inawaongoza njia ya kupita. Tulijenga hoja kwamba nguzo hii ya moto na hilo wingu wingu lilikuwa lina wamiss lead kufuata muelekeo na njia ambayo siyo sahihi n hiki ndicho kiliwafanya wazunguke jangwani kwa miaka takribani arobaini ambapo kiuhalisia walipaswa kutumia siku tatu tu.

Tulijenga hoja kwamba, kama ambavyo tunasioma kwenye bibilia, yafaa kusema kwamba nguzo hiyo ya moto na wingu hilo vilikuwa ni vitu vya kimiujiza kutoka kwa Mwenyezi Mungu mwenyewe, sasa kwa nini Mwenyezi Mungu awaongoze watu wake kwenye njia ambayo si sahihi? Kutokana na ukaribui wa Misri na Israel hii ina maana kwamba kwa muda wa miaka arobaini ambayo wana wa Israel walikuwa wanarandaranda jangwani, ‘they were moving in circles’… walikuwa wanazunguruka milima tu kufuata wingu na nguzo ya moto. Yaani wanaweza wakapiata sehemu ‘A’ alafu mwakani wakapita tena pale pale bila kujua. Walikuwa hawaendi mbele, walikuwa wanazunguruka tu milima na majangwa. Tukauliza, kwa nini Mwenyezi Mungu awafanye namna hii ‘wateule’ hawa?

Mwalimu wetu huyu, nguli wa theolojia na masula ya ‘Uungu’ alitupatia majawabu kadhaa ambayo mengine yalikuwa yanatokana na tafasiri za kimantiki na mengine kutokana na tafasiri za kitheolojia. Mfano, alitueleza kwamba Mwenyezi Mungu hakutaka kizazi kilichotoka Misri kiingie kanani na badala yake alitaka watoto wao tu ndio waingie kanani. Kwa hiyo kwa miaka arobaini ile kizazi kile kilichotoka kanani chote kilipotea na kuibuka kizazi kipya cha watoto ambao walilzaliwa ndani ya miaka hiyo arobaini. Lakini pia alitueleza kwamba Mwenyezi Mungu alikuwa anataka kuwaonyesha wana wa Israel ukuu wake na miujiza yake… ndipo hapa alitupa mifano ya Mana kudondoka kutoka mbinguni, makundi ya ndege aina ya kware kudondoka ili Waisrael wachinje na kula baada ya kulalama kuwa wameikosa sana nyama… na mifano mingine mingi.

Mfalme Mutara III ambaye ana undugu wa kihistoria na baba yake Kagame, Mr. Geogratias

Lakini binafsi yangui jawabu ambalo lilinikosha zaidi lilikuwa ni nadharia aliyotupa mwanatheolojia huyu pamoja na mstari kwen ye biblia uliosema kuwa “..,nataka kuifundisha mikono yako kupigana vita..”

Kwamba Mwenyezi Mungu alikuwa anataka kuwafundisha Waisrael namna ya kupambana vita kabla hawajaingia kanani. Kwa hiyo kwa miaka hiyo arobaini waliyokuwa wanarandaranda jangwani walikutana na misuko suko mingi ya mapambano ya kivita ambayo iliwafanya wawe bora katika medani hizo za kivita. Hii ilikuja kuwasaidia pia pindi walipoingia Kanani ambako walikuta kuna taifa la watu ambao wanaishi hapo na walikuwa hodari kweli kweli katika vita. Mojawapo ya wapelelezi waliotumwa na Musa kwenda kuipeleleza kanani na wakazi wake, alieleza kuwa watu hao ni wenye miraba minne na hodari kweli kweli mpaka alifikia hatua ya kusema “…sisi ni kama panzi tu mbele yao..”

Lakini uzoefu wa miaka arobaini ya mapambano ya vita uliwawezesga Israel kuivamia kanani na kuua wakazi wake wote na kuifanya nchi yao, nchi yao ya ahadi, nchi yao ya maziwa na asali. Jawabu hili la mwanatheolojia yule ndilo ambalo lilinikosha zaidi.

Kwa nini nimeeleza haya yote…

Katika sehemu iliyopita nilieleza kuhusu vikundi vidogo vidogo vya wapiganaji wa kitusi waliopo kwenye kambi za wakimbizi ambavyo viliitwa ‘Inyezi’. Vikundi hivi mara kwa mara vilikuwa vinavamia Rwanda kwa majaribio ya kuipindua serikali lakini bila mafanikio yoyote kwa muda wa zaidi ya miaka thelathini.

Licha ya nia ‘njema’ ya vikundi hivi kutaka kuipindua serikali lakini katika picha kubwa zaidi vilikuwa vinaongeza tu mateso kwa Watusi wenzao ambao bado walikuwa wamebakia nchini Rwanda. Kwa sababu kila jaribio la mapinduzi lilipokuwa likifanywa na vikundi hivi vya Inyezi, serikali ya Rwanda yenye mlengo wa Kihutu iliwatia jela watusi waliopmo ndani ya nchi na kuua mamia wengine kwa lengo la kutuma ujumbe kwa Watusi wengine kwamba wanatakiwa ‘kuwa wapole’. Wasilete fyokofyoko zozote.

Lakini mateso ya Watusi yalipoongezeka chini ya Rais Juvenal Habyarimana, kulikuwa na ulazima wa jambo fulani kufanyika. Lakini wapo Watusi wenye kuona kwa jicho la tatu ambao walijua kabisa kwaba jambo hilo haliwezi kufanikishwa na vikundi vya Inyezi kutoka kwenye kambi za ukimbizi. Walifahamu fika kwamba jambo hilo linapaswa kuwa la kimkakati na utekelezaji wa weledi wa hali ya juu kabisa. Wanahitaji ‘kutoka nje ya lengo ili kutimiza lengo’. Wanahitaji ‘kurandaranda jangwani kwa miaka arobaini kabla ya kuingia kanani’. Wanahitaji kupotea jangwani ili wafike nyumbani.

Watusi hawa ambao walipata ‘maono’ haya niliwaeleza katika sehemu iliyopita, walikuwa ni Fred Rwigyema na Paul Kagame.

Nitaeleza nadharia hii ya krandaranda jangwani kwa miaka arobaini inashabihiana vipi na kilichofanywa na Kagame na mwenzake Rwigyema… lakini kabla hatujaenda huko nhebu tuwafahamu japo kwa uchache… paul Kgame na Fred Rwigyema ni akina nani?

Fred Gisa Rwigyema

Alipozaliwa jina ambalo alipewa na wazazi wake aliitwa Emmanuel Gisa, alizaliwa tarahe 10 April mwaka 1957 kijijini Mukiranza katika eneo maarufu la Gitamara kusini mwa Rwanda. Katika machafuko ya mwaka 1959 na 1960 ambayo pia yalimuondoa Mflame Kigeri na kukomesha utwala wa Kifalme wa Watusi, visa ambavyo nilivieleza katika sehemu iliyopita, Fred pamoja na familia yake walikimbia nchi ya Rwanda na kwenda Uganda kwenye kambi za wakimbizi.

Akiwa nchini Uganda na hasa alipokuwa sekondari alikutana na kuwa marafiki na Salim Saleh (jina halisia alipozaliwa aliitwa Caleb Akandwanaho) mdogo wake Rais Yoweri Museni. Wote wawili mwaka 1976 walipomaliza shule ya upili walisafiri mpaka hapa Tanzabnia kuungana na kaka yake Salim Saleh, yaani Bw. Yoweri Museveni ambaye alikuwa ameanzisha vugi vugu la FRONASA (Front For National Salvation). Vuguvugu hili ambalo mwanzoni lilianza kama kikundi tu cha wanaharakati ambao walikuwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam ambako Museveni alikuwa anasomea shahada yake ya uchumi na sayansi ya siasa. Lakini baadae harakati hizi zilipamba moto na kuzaliwa kikundi cha waasi wa FRONASA chini ya uongozi wa Yoweri Museveni ambacho mwanzoni kilikuwa na lengo kuu moja la kumuondoa madarakani Rais Dikteta wa Uganda kipindi hicho, Nduli Idd Amin Dadaa. Ndicho kikundi hiki ambacho Fred Rwigyema na Salim Saleh walikuja kujiunga nacho walipoingia Tanzania.

Baadae Fred na wenzake welipelekwa na Museveni nchini msumbiji katika harakati za wenzao wa FRELIMO, hii nitaeleza zaidi hapo baadae.

Paul Kagame

Paul Kagame amezaliwa kwenye kijiji kinachoitwa Tambwe pia maeneo ya kusini mwa Rwanda mwaka 1957, tarehe 23 October. Baba yake anayeitwa Deogratias familia yao ilikuwa na ukaribu sana na familia ya kifalme kipindi hicho Rwanda bado ikitambulika kama ‘Kingdom of Rwanda’. Pia Mr. Deogratia familia yao pia ilikuwa na undugu wa karibu na Mfalme Mutara III lakini baba yake Paul Kagame hakupendelea kutumikia mfumo wa kiserikali mfano labda kuwa afisa fulani wa serikali au mpambe wa mfalme, badala yake aligeukia masuala ya biashara ambayo alifanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Pia mama yake Paul Kagame, Asteria Rutagambwa, anatokea kwenye familia ya Malkia wa mwisho wa Rwanda, Rosalia Gicanda.

Baada ya machafuko ya mwaka 1959 na mwaka 1960 ambayo niliyaeleza kwenye sehemu zilizopita, ambayo yalisababisha maelfu ya Watusi kukimbia Rwanda, familia ya akina Paul Kagame nayo ilikuwa ni moja ya familia ambazo zilikimbilia kwenye kambi ya wakimbizi nchini Uganda. Ikumbukwe kwamba kipindi ambacho familia yao inakimblia Rwanda, Paul Kagame alikuwa ni mtoto wa miaka miwili tu. Kwa hiyo ni vizuri kukumbuka huko mbele tunavyoendelea na makala hii kwamba Paul Kagame amekulia nje ya Rwanda. Kwamba alirejea Rwanda walau kwenda kuugusa mchanga wa ardhi ya nchi yake tayari akiwa ni mtu mzima kabisa.

Walipofika Uganda yeye na familia yake waliishi katika kambi ya wakimbizi ya Nshungerezi iliyopo kaskazini mwa Uganda mkoa mdogo wa Toro. Ni mahala hapa kwenye kambi ya wakimbizi na kwenye hali hii ya utoto ndipo ambapo Paul Kagame na Fred Rwigyema walikutana na kuwa marafiki wa ‘kufa na kuzikana’.

Kagame alianza shule ya msingi kwenye shule maalumu ambayo ilijengwa karibia na kambi, maalumu kwa ajili ya watoto wa wakimbizi ‘kutoa tongotongo’ walau. Mwenyewe Paul Kgame anasema kwamba kitu kikubwa ambacho alijifunza kwenye shule hii ya wakimbizi ambacho anakithamini zaidi mpaka leo hii ilikuwa nikijua lugha ya Kingereza na pia kuweza kuelewa na kujichanganya (integrate) na tamaduni za Uganda.

Kutokana na kufanya vizuri sana darasani kushinda watoto wenzake wengine wa kikimbizi alipofikisha umri wa miaka tisa alihamishiwa kwenye mojawapo ya shule zenye heshima kubwa sana kipindi hicho ambayo ilikuwa inaitwa Rwengoro Primary School ambayo ilikuwa umbali wa kilomita zipatazo 16 kutoka kwenye kambi ya wakimbizi ambayo alikuwa anaishi na familia yake. lakini Licha ya umbali huu mkubwa kutoka kati ya shule anayosoma na kwenye kambi ya wakimbizi ambayo walikuwa wanaishi na familia yake, Paul Kagame alimaliza shule hii ya msingi kwa kupata alama za juu zaidi kuliko mwanafunzi yeyote yule kwenye Wilaya nzima.

Kutokana na kupata alama za juu kiasi hicho, Paul Kagame alipelekwa kwenye shule ya upili ambayo tunaweza kusema ndiyo ilikuwa bora zaidi nchini Uganda kwa kipindi hicho ambayo inaitwa Ntare School. Hii ndiyo shule ambayo pia hata Yoweri Museveni alisoma.

Mwanzoni masomo yake hapa shule ya Ntare yalienda vizuri sana, lakini muda si muda mambo yakaanza kubadilika.

Mwaka 1975 baba yake mzazi Kagame, Mr. Deogratias alifariki dunia tukio ambalo lilimuumiza moyo sana Kagame na kumpa msongo mkubwa wa mawazo. Lakini pia kabla ya kidonda cha kuondokewa na baba yake hakijapoana mwaka uliofuata rafiki yake kipenzi Fred Rwigyema aliondoka kwenda mahala kusikojulikana bila kumuaga yeyote yule. (nilieleza hapo juu kuwa mwaka huu ndio ambao Fred alijiunga na vuguvugu la FRONASA chini ya Yoweri Museveni… lakini hakuna ambaye alikuwa analijua hili kwa kipindi hicho).

Matukio haya makubwa mawili, baba yake kufariki na baadae rafiki yake kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha, kulimfanya Kagame awe kama vile ‘nusu amechanganyikiwa’. Ilikuwa karibia kila siku walimu shuleni kwake Ntare wanaletewa kesi ya Paul Kagame kupigana na wanafunzi wenzake. Alikuwa akimsikia mtu anatamka neno hata liwe dogo kiaisi gani lakini kama lina uelekeo la kuikosoa au kukashifu Rwanda basi atakuvaa na kuanza kurusha ngumi.

Mabadiliko yake haya hasi ya kitabia yalifanya maendeleo yake kitaalumu kushuka na pia walimu kuchoka utovu wake wa nidhamu na hatimaye kutimuliwa hapa Ntare School. Wazazi wake walipambana na akapata nafasi shule ya Old Kampala Secondary ambako alimalizia huko shule yake ya upili lakini akiwa na alama za chini kabisa kuliko ilivyo kawaida yake.

Baada ya kumaliza shule ya upili Paul Kagame alikuwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo. Alikuwa anajihisi kama vile amepotea na kupoteza dira ya maisha. He needed to find himself. Alikuwa anahitaji sababu ya kuendelea kuishi. Na si kuishi tu bali pia kuishi kwa kutimiza kusudi la yeye kuwepo duniani.

Paul Kagame alihitaji kuamsha tena hari na morari ndani yake. Na ndipo hapa ambapo alikata shauri ya kuitembelea nchi yake ya Rwanda kwa mara ya kwanza kabisa tangu alipoondoka akiwa na miaka miwili tu.

Hii ilikuwa ni mwaka 1977 ambapo Kagame alikata shauri ya kwenda Rwanda kwa mara ya kwanza maishani mwake. Safari yake hii ya Rwanda ndiyo ambayo iliamsha hari na morali ya kumjenga Kgame huyu ambaye tunaye siku hii ya leo. Nitarudi kueleza.

Itaendelea...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Oya mze baba unatu lostisha ,,unaquote VP Uzi mzima acha hizo pigo
 
Hizi stori za mauaji ya rwanda zinabadilikabadilika inategemea ni nani anayesimulia, ukiwasikiliza watu wa kambi ya kagame wana upande wao wa stori (nadhani ni kama huu ulioletwa hapa na mwandishi wa stori hii) lakini ukiwasikiliza wale wenzao wahutu nao wana stori zao juu ya hayohayo mauaji, yote kwa yote, siku zote washindi ndio wanaoandika historia "history is written by the victors - Winston Churchill"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NI MFULULIZO WA HISTORIA YA KWELI YA MAUAJI YA KIMBARI YA RWANDA

Sehemu ya tano.


Ni jambo la kusikitisha sana kwamba Historia yetu ambayo watoto wetu wanafundishwa mashuleni na kuandikwa kwenye vitabu imechujwa mno kiasi kwamba inakuwa kama ni hadithi tu za kusadikika.
Kwa mfano kama umebahatika kuijui historia ya ukweli kuhusu Vita ya Kagera kisha ukasoma 'version' ambazo zimeandikwa kwenye vitabu na kuaminishwa kwa umma, machozi yanaweza kukutoka.

Ubaya ni kwamba hata wale ambao wamebahatika kujua ukweli halisi wa matukio na vilivyo nyuma ya pazia hawawezi kuthubutu kutia mkono na kuandika kile ambacho wanakijua.

Ndio maana naamini ni busara hata kwangu pia niandike kwa sehemu kile ambacho historia zetu hakivisemi lakini pia ni muhimu kuandika kwa "ustaarabu" kwa faida ya pande zote.

Kutengenezwa kwa Jasusi Paul Kagame

Katika sehemu iliyopita nilieleza kwamba, Paul Kagame mwaka 1977 alitembelea nchi ya Rwanda ambapo hakuwahi kuikanyaga tangu alipokuwa mtoto wa miaka miwili tu. Paul Kagame alifanya safari hii kutokana na kukosa amani ndani ya moyo wake. Alikuwa anatafuta 'kusudi' lake la maisha. Katika kipindi hiki alikuwa amempoteza baba yake mzazi na pia rafiki yake kipenzi Fred Rwigyema alikuwa amepotelea kusikojulikana.

Kwa hiyo Paul Kagame alienda Rwanda kwa ajili ya 'soul searching'. Alikuwa anataka kupata hamasa kwenye roho yake ili aweze kujua kusudi la maisha yake.

Kutokana na historia ya familia yake kuwa na ushawishi kwa kiasi fulani (nilieleza kwamba baba yake ana undugu wa kiukoo na Mfalme Kigeli na mama yake ana undugu wa damu na Malkia wa mwisho wa Rwanda) kwa hiyo hizi safari zake za Rwanda alizifanya kwa siri kubwa pia ukizingatia kwamba serikali ilikuwa makini sana na watusi ambao wako nje ya Rwanda kama wakimbizi kutokana na harakati zao na kiu yao ya kutaka kuipindua serikali mara kwa mara.
Safari hii ilikuwa ya maana sana kwa Kagame na alijenga 'connection' ambazo zilikuja kumsaidia sana miaka ya baadae kwenye harakati zake.

Mwaka 1978 alifanya safari nyingine kwenda Rwanda na safari hii hakupitia mpaka wa Uganda bali aliingia kupitia Zaire (Congo). Kwa wiki kadhaa ambazo alikaa Kigali kwa siri kubwa, alitumia muda huo kuimarisha 'connection' ambazo alikuwa nazo na pia kusoma hali ya kisiasa na uimara wa serikali.

Safari hizi mbili ziliamsha hari kubwa mno katika nafsi ya Paul Kagame. Aliona kwa uhalisia kabisa mateso na manyanyaso ambayo watusi walikuwa wanapitia nchini Rwanda. Akajihisi kabisa kwamba alikuwa ana jukumu la kufanya kitu kuyamaliza mateso hayo.

Aliporejea nchini Uganda Kagame akageuka kama mwanaharakati hivi katika kambi za wakimbizi akihamasisha vijana wenzake kujizatiti na kuweka mipango ya kuikombia Rwanda.

Wakati huo huo, rafiki yake Fred Rwigyema ambaye alipotea bila yeyote kujua ni wapi alikuwa ameelekea… alikuwa nchini Tanzania katika kambi ya FRONASA chini ya uongozi wa Yoweri Musseveni ambao walikuwa wanaweka mikakati ya kumuondoka madarakani Dikteta Idd Amin.

Habari kuhusu kijana mahiri, mwanaharakati Paul Kagame zilimfikia Yoweri Musseveni na alitamani awe sehemu ya 'timu' yake.
Ndipo hapa ambapo Fred Rwigyema ambapo ndio kwanza alikuwa amerejea Tanzania kutoka msumbuji ambako alipelekwa na Musseveni kwenye mafunzo ya pamoja na wapiganaji FRELIMO juu ya vita za msituni…alitumwa kwenda nchini Uganda kwa ajili ya masuala kadhaa lakini mojawapo ilikuwa kumshawishi Paul Kagame kujiunga na wapiganaji wa Yoweri Musseveni walioko nchini Tanzania.

Sasa basi…

Kuna mahala mkoani Morogoro, sitapaja kwa jina au exactly sehemu gani… lakini ni nje ya mji kidogo kuna 'Espionage Farm' ya siri ambayo mwaka 1978 Paul Kagame na maafisa kadhaa wa kikundi cha FRONASA walikuwa recruited na kupata mafunzo ya Ujasusi na masuala ya Intelijensia.

Niseme kwamba Paul Kagame ni moja ya maafisa bora na hodari kabisa kuwahi kuzalishwa na Idara yetu Usalama wa Taifa.

Kagame amewahi kutumia kwenye 'high profile missions' kadhaa lakini kubwa zaidi ni ile ambayo aliongoza kikosi cha Intelijensia ya wapiganaji wa UNLA (Ugandan National Liberation Front) katika vita ya Kagera.

Tofauti na historia ilivyoandikwa kuhusu vita ya Kagera, lakini ukweli na uhalisia ni kwamba wapiganaji wa UNLA ambao walikuwa ni zaidi ya 20,000 walikuwa ni kiungo muhimu sana katika ushindi wa vita ya Kagera. Suala hili tutalizungumzia siku moja kama tukipata wasaa wa kuichambua vita ya Kagera.

Kuna kikao cha siri sana kilifanyika pale Moshi ambacho kinajulikana kana "Moshi Conference" ambacho kiliudhuliwa na watu adhimu kabisa wapatao 28 na mmoja wao alikiwa Paul Kagame.
Katika kipindi hiki, Rais ambaye alikuwa amepinduliwa na Amin na kukimbilia Tanzania, Bw. Milton Obote alikuwa na kikundi chake cha wapiganajia ambacho alikiita kwa jina la Kiswahili "KIKOSI MAALUM" ambacho makamanda wake walikuwa ni Tito Okello na David Oyite Ojok. Hawa nao pamoja na Obote mwenyewe walikuwepo kwenye kikao cha mjini Moshi.
Pia Yoweri Musseveni alikuwepo kuiwakilisha FRONASA. Pia walikuwepi wanaharakati wengine mashuhuri kama vile Akena p'Ojok, William Omaria, Ateka Ejalu, Godfrey Binaisa, Andrew Kayiira, Olara Otunnu pamoja na baadhi ya 'wakubwa' kutoka kwenye vyombo vya ulinzi vya nchi yetu ambao kwa sababu ya 'staha' sitaandika majina. Jumla walikuwa watu ishirini na wanane.

Kikao hiki kilizaa mpango mkakati wa kijeshi ambao ndio ulitumika kwenye vita ya Kagera na kumshinda Amin. Paul Kagame ndiye ambaye alibebeshwa mzigo wa mikakati ya Intelijensia ya kijeshi.

Octoba 1978 tukaingia vitani dhidi ya majeshi ya Amin. Licha ya swahiba wake Kanali Muammar Gaddafi kutuma wapiganaji 2,500 pamoja na silaha nzito za mivita na za kisasa kwa kipindi hichi kama vifaru aina ya T-54, T-55, magari ya kivita ya kisovieti aina ya BTR APC na Grad MRL pamoja na ndege za kivita aina ya MiG 21 na ndege hatari za kivita (supersonic bombers) aina ya Tu-22 kumsaidia Amin… ajabu ni kwamba licha ya majeshi ya amini kuwa imara kiasi hiki kwa maana ya vifaa vya kivita lakini mwanzoni mwa mwezi April 1979 tulimpiga Amin mpaka "Ikulu" na kumlazimu kukimbilia Libya kwa swahiba wake Gaddafi na baadae kukimbilia Saudi Arabia.

Siku moja kabla ya kutangaza kuisha kwa vita ya Kagera, yaani April 10 Tanzania tukamsimika Yusufu Lule kuwa Rais mpya wa Uganda. Yusufu Lule ameishi sana hapa Tanzania hasa baada ya Idd Amin kuingia madarakani.
Pamoja na hilo lakini akina Musseveni nao waliunda chombo chao cha kijeshi ambacho kiliitwa National Consultative Commission (NCC). Hiki kwa kiasi fulani ndio walikifanya kama chombo chenye maamuzi ya mwisho kuhusu nchi.

SILAHA NZITO ZA KIJESHI AMBAZO UGANDA ILIPOKEA KUTOKA KWA KANALI GADDAFI


Gari za kivita aina ya BTR APC

Miezi miwili tu baada ya majeshi ya Tanzania kumsimika Yusufu Lule kuwa Rais, kukaanza kutokea mvutano mkali kati ya NCC ya kina Musseveni na Rais Yusuf Lule. Mvutano huu ulikuwa ni juu ya mamlaka ya Rais ambayo NCC walimuona Lule kama anavuka mipaka yake. Lule naye kwa upande wake alikuwa anaonekana hataki nchi kuingozwa na jeshi (NCC).
Hatimaye tarehe 10 June mwaka huo 1979 NCC kwa ushawishi mkubwa wa Musseveni wakamuondoa madarakani Godfrey Binaisa kuwa Rais mpya wa Uganda.

Kimsingi Binaisa alikuwa kama 'kikaragosi' tu lakini kiuhalisia NCC ndio walikuwa wanaongoza nchi.

Lakini taratibu naye utamu wa madaraka ukaanza kumkolea.

Ikumbukwe kwamba katika kipindi hiki chote Milton Obote bado alikuwa nchini Tanzania hajarejea Uganda.
Kulianza kuzuka taarifa kwamba mnadhimu mkuu wa jeshi Brigedia Jenerali David Oyite Ojok ambaye kipindi cha vita ya Kagera alikuwa kamanda wa jeshhi ka pamoja la Tanzania na UNLA, alikuwa anafanya maandalizi ya kuhakikisha Obote anarejea Uganda.

Jeneralari Ojok anatokea eneo la kaskazini mwa Uganda kama ilivyo kwa Obote. Licha ya Ojok kuanza mikakati ya kumrudisha Uganda Obote lakini pia kwenye jeshi nyadhifa za juu zote alikuwa anahakikisha zinashikiliwa na watu wanaotoka ukanda wa kaskazini mwa nchi.

Harakati zote hizi Binaisi aliziona kama juhudi za kumuondoa madarakani ili kusafisha njia kwa Obote kurejea madarakani.

Mwezi May 1980 Rais Godfrey Binaisa alimuondoa Ojok kwenye cheo cha Mnadhimu mkuu wa jeshi.
Suala hili lilipingwa vikali na NCC na wakafikia hatua ya kumuondoa madarakani Rais Binaisa na kuunda tume maalumu ambayo waliita Presidential Commision ambayo ndiyo ilifanya kazi ya kuongoza nchi badala ya Rais.
Tume hii wanakamati wake walikuwa ni Museveni, Oyite Ojok, Okello na Muwanga.
Muwanga alipewa cheo cha uenyekiti wa tume japokuwa kiuhalisia wenye nguvu za ushawishi kwenye tume walikuwa ni Museveni na Ojok.

Baada ya hapa ndipo ambapo hasa umahiri wa Paul Kagame unaonekana. Ikumbukwe kwamba wakati yote haya yaliendelea Paul Kagame alikuwa na ushawishi mkubwa sana kwenye jeshi la Uganda kutokana na umahiri wake wa masuala ya Intelijensia. Kwa hiyo yeye ndiye ambaye alikuwa anawashauri ni nani anafaa kuwa Rais na nani hafai.

Baada tu ya nchi kuanza kuongozwa na Tume maalumu niliyoitaja hapo juu, Ojok akaanza tena mipango ya kumrejesha Milton Obote ndani ya Uganda. Ilikuwa wazi kwamba Ojok alikuwa anataka Obote ashike madaraka. Lakini watu wengi wa kabila la Baganda/Waganda walikuwa wanampinga Obete kwa kuwa yeye ndiye ambaye alimpindua Mfalme wao wa Baganda miaka kadhaa nyuma na kushika Urais kabla ya yeye pia kupinduliwa na Ids Amin. Kwa hiyo kulikiwa na mvutano kati ya watu wa maeneo ya kaskazini na kusini mwa Uganda.

Ndipo hapa ambapo Paul Kagame akaona fursa. Kwamba 'vita ya panzi, furaha ya kunguru'.
Yoweri Museveni yeye hatokei Kusini wala Kaskazini mwa Uganda… yeye amezaliwa na kukulia eneo la magharibi mwa nchi linalopakana na Rwanda sehemu inaitwa Ntungamo. (Hii ni moja ya sababu ya baadhi ya watu kuamini ana asili ya Kitusi).
Kwa hiyo huu ugomvi wa watu wa kaskazini na wa kusini haukuwa na mslahi nao kabisa. Ndipo hapa kwa kushauriana na Paul Kagame wakaanza michakato ya siri pembeni ya kujitenga na NCC na UNLA japokuwa Museveni alikuwa na ushawishi kwenye vyombo vyote hivyo.

Hatimaye mwaka 1980 Milton Obote alirejea Uganda na kushiriki kwenye uchaguzi mkuu mwaka huo na "kushinda". Matokeo ya uchaguzi yalipingwa vikali na watu wengi akiwemo Yoweri Museveni.

Ndipo hapa ambapo Yoweri Museveni, Pual Kagame na Fred Rwigyema pamoja na Waganda wengine thelathini na saba tu walianzisha kikundi chao cha kijeshi walichokiita National Resistance Army (NRA) lengo kuu likiwa ni kumuondoa madarakani Rais mpya Milton Obote.

Kikundi hiki kiliendesha mapigano ya msituni dhidi ya majesho ya serikali kwa karibia miaka sita.
Licha ya udogo wake kwa idadi ya watu (japo baadae waliongezeka kuzidi watu arobaini wa awali) lakini ufanisi wao kwenye kushambulia kwa uhodar na kulichosha jeshi la serikali ulikuwa wa hali ya juu. Miaka hii sita ya kupambana na majeshi ya serikali yalidhihirisha namna ambavyo Paul Kagame alikuwa ni nguli wa 'psychological warfare' ambayo pia ilikuja kudhihirika kipindi cha mauaji ya kimbari (tutaongelea zaidi tukifika hapo).

Katika kipindi hiki cha vita kwa masuala ya kijeshi Paul Kagame alikuwa mtu muhimu na mwenye kuheshimika zaidi na wapiganaji wa NRA kuzidi hata Museveni mwenyewe. Nyadhifa zao ndani ya NRA zilikuwa karibia kwenye usawa mmoja.

Kwa upande wa jeshi la serikali hali ilianza kuwa tete. Kukaanza kutokea mifarakano ya kikabila kati ya wenyewe kwa wenyewe. Kaskazini mwa Uganda kuna makabila makuu mawili, Walangi (kabila wanalotokea Obote na Ojok) na Waacholi (kabila la Tito Okello ambaye kwa kipindi hicho alikuwa kamanda wa jeshi).
Askari wengi wa miguu walikuwa ni Waacholi na ndio ambao walikuwa wanakufa zaidi kwenye vita hiyo dhidi ya NRA. Walangi wengi walikuwa ni maafisa wa jeshi na 'Special Forces'. Kwa hiyo askari wa miguu wakaanza kushinikiza serikali ifanye mazungumzo na NRA na kumaliza vita.

Yoweri Museveni na wapiganaji wa NRA msituni

Serikali ikafanya shingo ngumu na kukataa.

Wanasema lakuvunda halina ubani, mwezi Desemba 1983 Oyite Ojok alifariki kwa ajali ya ndege ambayo kuna kila dalili ya mkono wa Kagame. Kwa kipindi hicho Ojok ndiye alikiwa mkuu wa jeshi la Uganda. Ilikuwa inategemewa Obote amteue Tito Okello au mwenzake mwingine aliyeitwa Bazilio Olara-Okello (hakuna undugu wa damu kati yao licha ya kufanana ubini japo wanatokea kabila moja la Waacholi) ambaye naye alishiriki vita ya kumuondoa Idd Amin. Lakini ajabu Obote alimteua afisa wa chini kabisa wa jeshi aliyeitwa Smith Apon-Achak ambaye anatoka kabila lake la Walangi kuchukua nafasi ya Oyite Ojok. Hii iliwafanya wanajeshi wenye asili ya kabila la Waacholi kumchukia Obote na serikali yake na hatimaye miaka miwili baadae kumpindua kutoka madarakani.

Baada ya Miltob Obote kupinduliwa na jeshi kutoka madarakani kukaanza mapigano baina ya vikundi vya msituni kila kimoja kikitaka kushika usukani wa kuongoza nchi. Ndipo hapa yalifanyika maongezi ya pamoja baina ya vikundi vyote vya msituni nchini Kenya chini ya Rais Daniel Arap Moi ili kuleta suluhu na kuweka muelekeo mpya wa nchi ya Uganda.

Tarehe 29 January mwaka 1986 Yoweri Kaguta Museveni akaapishwa kuwa Rais mpya wa Uganda.

Paul Kagame akateuliwa na Rais kuwa Chief of Millitary Intelligence.

Swahiba wake Fred Rwigyema akateuliwa kwenye wadhifa wa Waziri wa Ulinzi.

Pia baraza la mawaziri lilikuwa limejaa watusi kibao.

Kwa maneno mengine tunaweza kusema kuwa Paul Kagame alikuwa ameiweka Uganda kwenye kiganja chake cha mkono japo hakuwa Rais. Lakini mtandao wa ushawishi ambao alikuwa ameujenga ndani ya serikali ya Uganda, baraza la mawaziri na kwenye jeshi ulikuwa ni mkubwa na una nguvu zaidi hata ya Yoweri Museveni ambaye aliapishwa kuwa Rais. Uzuri ni kwamba Museveni anafahamu umahiri wa Paul Kagame na hakutaka kutengeneza mvutano wowote naye kwa kuwa alikiwa anajua lengo kuu la Kagame lilikuwa ni lipi. Kagame hakuwa na nia yoyote ile ya kuwa Rais wa Uganda au kuendelea kuliendesha jeshi la Uganda. Ndoto yake ilikuwa ni moja tu, ndoto ambayo aliipata mwaka 1978 alipotembelea kwa siri nchi yake ya Rwanda, kwamba siku moja anataka kuwaokoa ndugu zake watusi kutoka kwenye unyanyasaji, kuuwawa, kudhalilishwa na mateso ambayo walikuwa wanapitia katika nchi yao.

Na sasa alikuwa amekamilika kwa kila kitu. Alikuwa na uzoefu wa kutosha. Alikuwa na weledi wa kutosha, tunaweza kuthubutu kusema kwamba katika kipindi hiki hakuna ambaye alikuwa anaweza kufikia daraja la umahiri wa Kagame katika masuala ya Ujasusi Afika Mashariki yote.

Lakini pia alikiwa na ushawishi katika nchi za kimakakati ambazo zinapakana na Rwanda, kwa maana ya Congo (huku aliwapeleka wapiganaji wa NRA kupata mafunzo ya siri ya Special Forces kipindi cha mapigano ya miaka 6 msituni dhidi ya majeshi ya serikali ya Milton Obote). Lakini pia alikuwa na ushawishi nchini Tanzania (mtoto wetu tuliyemfunza wenyewe ujasusi na alitusaidia sana kwenye vita ya Kagera). Na hakuna haja hata ya kusema kiwango cha ushawishi ambacho alikuwa nacho nchini Uganda.

Mbele yake kulikuwa na jambo moja tu la mwisho ambalo alikuwa anatamani litimie kabla hajaondoka juu ya uso wa dunia. Kuiweka nchi ya Rwanda mkononi mwake.

Itaendelea...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera sana kaka kwa elimu hii adhimu, Ila pia nlipenda sana nijue duru za hivi sasa zinasema kua uhusiano wa kagame na mseveni ni kama unadorora labda hoja ni nini? Twaweza pata majibu kupitia hii simulizi au waweza nisaidia jibu binafsi kwa weledi wako juu ya hili, tafadhari nlipenda kiu tangu ikatwe.
 
Back
Top Bottom