Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Alafu ona jamani tupo tunalumbana humu jamaa ndo hivo tena kaacha kushusha uzi kimya
 
Damnnn!!!I hope kagame anaijua histotia yake vizur,thus kuwamaliza wapinzani Kwake its not a BIG ISSUE,hii mbegu bado ipo ktk Ardhi yenye rutuba.,Ina mwagiwa maji ya kutosha,na still Inakua,SHIIIIT
 
KILIO CHA MIFEREJI YA DAMU IENDAYO ETHIOPIA



SEHMU YA NNE




Kabla ya mvua ni mawingu.! Je, kabla ya mawingu ni nini?

JUA KALI…

Katika mapambano yoyote yale mara nyingi ili kufikia lengo unapaswa kufanya mambo ya mzunguko mno kana kwamba unatoka nje ya lengo hilo lakini hatimaye uje kutimiza lengo hilo hilo.

Nitaomba kunena kwa mifano ya uhalisia…

Nimekuwa nikieleza mara kadhaa kwamba nimesoma masomo ya bibilia darasani kwa muda wa miaka sita. Nakumbuka nikiwa kijana wa sekondari mwalimu wangu wa somo la ‘Divinity’ tuliwahi kujadili nae sana kuhusu kisa cha wana wa Israel kutoka Misri kwenda Kanani. Mimi na wanafunzi wenzangu kwenye mjadala huo tulikuwa tunauliza ni kwa nini wana wa Israel watumie miaka arobaini kusafiri kutoka Misri kwenda Kanani wakati kiuhalisia kwa mwendo wa kutembea kwa miguu hata sasa kama utatembea utatumia kama siku tatu tu hivi kama utapita njia sahihi ambayo imekuwa inatumiwa na watu tangu mwanzoni mwa kizazi agano jipya (miaka ya 300 B.C na kuendelea mpaka sasa).

Tulilikoleza swali letu zaidi kwa kuongeza hoja ya kwamba wana wa Israel kama ambavyo tunasoma kwenye vitabu vitakatifu ni kwamba, katika safari yao hii mbele yao, juu angani kulikuwa na kama wingu au muda mwingine nguzo ya moto ambayo iliwa inawaongoza njia ya kupita. Tulijenga hoja kwamba nguzo hii ya moto na hilo wingu wingu lilikuwa lina wamiss lead kufuata muelekeo na njia ambayo siyo sahihi n hiki ndicho kiliwafanya wazunguke jangwani kwa miaka takribani arobaini ambapo kiuhalisia walipaswa kutumia siku tatu tu.

Tulijenga hoja kwamba, kama ambavyo tunasioma kwenye bibilia, yafaa kusema kwamba nguzo hiyo ya moto na wingu hilo vilikuwa ni vitu vya kimiujiza kutoka kwa Mwenyezi Mungu mwenyewe, sasa kwa nini Mwenyezi Mungu awaongoze watu wake kwenye njia ambayo si sahihi? Kutokana na ukaribui wa Misri na Israel hii ina maana kwamba kwa muda wa miaka arobaini ambayo wana wa Israel walikuwa wanarandaranda jangwani, ‘they were moving in circles’… walikuwa wanazunguruka milima tu kufuata wingu na nguzo ya moto. Yaani wanaweza wakapiata sehemu ‘A’ alafu mwakani wakapita tena pale pale bila kujua. Walikuwa hawaendi mbele, walikuwa wanazunguruka tu milima na majangwa. Tukauliza, kwa nini Mwenyezi Mungu awafanye namna hii ‘wateule’ hawa?

Mwalimu wetu huyu, nguli wa theolojia na masula ya ‘Uungu’ alitupatia majawabu kadhaa ambayo mengine yalikuwa yanatokana na tafasiri za kimantiki na mengine kutokana na tafasiri za kitheolojia. Mfano, alitueleza kwamba Mwenyezi Mungu hakutaka kizazi kilichotoka Misri kiingie kanani na badala yake alitaka watoto wao tu ndio waingie kanani. Kwa hiyo kwa miaka arobaini ile kizazi kile kilichotoka kanani chote kilipotea na kuibuka kizazi kipya cha watoto ambao walilzaliwa ndani ya miaka hiyo arobaini. Lakini pia alitueleza kwamba Mwenyezi Mungu alikuwa anataka kuwaonyesha wana wa Israel ukuu wake na miujiza yake… ndipo hapa alitupa mifano ya Mana kudondoka kutoka mbinguni, makundi ya ndege aina ya kware kudondoka ili Waisrael wachinje na kula baada ya kulalama kuwa wameikosa sana nyama… na mifano mingine mingi.

Mfalme Mutara III ambaye ana undugu wa kihistoria na baba yake Kagame, Mr. Geogratias

Lakini binafsi yangui jawabu ambalo lilinikosha zaidi lilikuwa ni nadharia aliyotupa mwanatheolojia huyu pamoja na mstari kwen ye biblia uliosema kuwa “..,nataka kuifundisha mikono yako kupigana vita..”

Kwamba Mwenyezi Mungu alikuwa anataka kuwafundisha Waisrael namna ya kupambana vita kabla hawajaingia kanani. Kwa hiyo kwa miaka hiyo arobaini waliyokuwa wanarandaranda jangwani walikutana na misuko suko mingi ya mapambano ya kivita ambayo iliwafanya wawe bora katika medani hizo za kivita. Hii ilikuja kuwasaidia pia pindi walipoingia Kanani ambako walikuta kuna taifa la watu ambao wanaishi hapo na walikuwa hodari kweli kweli katika vita. Mojawapo ya wapelelezi waliotumwa na Musa kwenda kuipeleleza kanani na wakazi wake, alieleza kuwa watu hao ni wenye miraba minne na hodari kweli kweli mpaka alifikia hatua ya kusema “…sisi ni kama panzi tu mbele yao..”

Lakini uzoefu wa miaka arobaini ya mapambano ya vita uliwawezesga Israel kuivamia kanani na kuua wakazi wake wote na kuifanya nchi yao, nchi yao ya ahadi, nchi yao ya maziwa na asali. Jawabu hili la mwanatheolojia yule ndilo ambalo lilinikosha zaidi.

Kwa nini nimeeleza haya yote…

Katika sehemu iliyopita nilieleza kuhusu vikundi vidogo vidogo vya wapiganaji wa kitusi waliopo kwenye kambi za wakimbizi ambavyo viliitwa ‘Inyezi’. Vikundi hivi mara kwa mara vilikuwa vinavamia Rwanda kwa majaribio ya kuipindua serikali lakini bila mafanikio yoyote kwa muda wa zaidi ya miaka thelathini.

Licha ya nia ‘njema’ ya vikundi hivi kutaka kuipindua serikali lakini katika picha kubwa zaidi vilikuwa vinaongeza tu mateso kwa Watusi wenzao ambao bado walikuwa wamebakia nchini Rwanda. Kwa sababu kila jaribio la mapinduzi lilipokuwa likifanywa na vikundi hivi vya Inyezi, serikali ya Rwanda yenye mlengo wa Kihutu iliwatia jela watusi waliopmo ndani ya nchi na kuua mamia wengine kwa lengo la kutuma ujumbe kwa Watusi wengine kwamba wanatakiwa ‘kuwa wapole’. Wasilete fyokofyoko zozote.

Lakini mateso ya Watusi yalipoongezeka chini ya Rais Juvenal Habyarimana, kulikuwa na ulazima wa jambo fulani kufanyika. Lakini wapo Watusi wenye kuona kwa jicho la tatu ambao walijua kabisa kwaba jambo hilo haliwezi kufanikishwa na vikundi vya Inyezi kutoka kwenye kambi za ukimbizi. Walifahamu fika kwamba jambo hilo linapaswa kuwa la kimkakati na utekelezaji wa weledi wa hali ya juu kabisa. Wanahitaji ‘kutoka nje ya lengo ili kutimiza lengo’. Wanahitaji ‘kurandaranda jangwani kwa miaka arobaini kabla ya kuingia kanani’. Wanahitaji kupotea jangwani ili wafike nyumbani.

Watusi hawa ambao walipata ‘maono’ haya niliwaeleza katika sehemu iliyopita, walikuwa ni Fred Rwigyema na Paul Kagame.

Nitaeleza nadharia hii ya krandaranda jangwani kwa miaka arobaini inashabihiana vipi na kilichofanywa na Kagame na mwenzake Rwigyema… lakini kabla hatujaenda huko nhebu tuwafahamu japo kwa uchache… paul Kgame na Fred Rwigyema ni akina nani?



Fred Gisa Rwigyema

Alipozaliwa jina ambalo alipewa na wazazi wake aliitwa Emmanuel Gisa, alizaliwa tarahe 10 April mwaka 1957 kijijini Mukiranza katika eneo maarufu la Gitamara kusini mwa Rwanda. Katika machafuko ya mwaka 1959 na 1960 ambayo pia yalimuondoa Mflame Kigeri na kukomesha utwala wa Kifalme wa Watusi, visa ambavyo nilivieleza katika sehemu iliyopita, Fred pamoja na familia yake walikimbia nchi ya Rwanda na kwenda Uganda kwenye kambi za wakimbizi.


Akiwa nchini Uganda na hasa alipokuwa sekondari alikutana na kuwa marafiki na Salim Saleh (jina halisia alipozaliwa aliitwa Caleb Akandwanaho) mdogo wake Rais Yoweri Museni. Wote wawili mwaka 1976 walipomaliza shule ya upili walisafiri mpaka hapa Tanzabnia kuungana na kaka yake Salim Saleh, yaani Bw. Yoweri Museveni ambaye alikuwa ameanzisha vugi vugu la FRONASA (Front For National Salvation). Vuguvugu hili ambalo mwanzoni lilianza kama kikundi tu cha wanaharakati ambao walikuwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam ambako Museveni alikuwa anasomea shahada yake ya uchumi na sayansi ya siasa. Lakini baadae harakati hizi zilipamba moto na kuzaliwa kikundi cha waasi wa FRONASA chini ya uongozi wa Yoweri Museveni ambacho mwanzoni kilikuwa na lengo kuu moja la kumuondoa madarakani Rais Dikteta wa Uganda kipindi hicho, Nduli Idd Amin Dadaa. Ndicho kikundi hiki ambacho Fred Rwigyema na Salim Saleh walikuja kujiunga nacho walipoingia Tanzania.

Baadae Fred na wenzake welipelekwa na Museveni nchini msumbiji katika harakati za wenzao wa FRELIMO, hii nitaeleza zaidi hapo baadae.



Paul Kagame

Paul Kagame amezaliwa kwenye kijiji kinachoitwa Tambwe pia maeneo ya kusini mwa Rwanda mwaka 1957, tarehe 23 October. Baba yake anayeitwa Deogratias familia yao ilikuwa na ukaribu sana na familia ya kifalme kipindi hicho Rwanda bado ikitambulika kama ‘Kingdom of Rwanda’. Pia Mr. Deogratia familia yao pia ilikuwa na undugu wa karibu na Mfalme Mutara III lakini baba yake Paul Kagame hakupendelea kutumikia mfumo wa kiserikali mfano labda kuwa afisa fulani wa serikali au mpambe wa mfalme, badala yake aligeukia masuala ya biashara ambayo alifanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Pia mama yake Paul Kagame, Asteria Rutagambwa, anatokea kwenye familia ya Malkia wa mwisho wa Rwanda, Rosalia Gicanda.

Baada ya machafuko ya mwaka 1959 na mwaka 1960 ambayo niliyaeleza kwenye sehemu zilizopita, ambayo yalisababisha maelfu ya Watusi kukimbia Rwanda, familia ya akina Paul Kagame nayo ilikuwa ni moja ya familia ambazo zilikimbilia kwenye kambi ya wakimbizi nchini Uganda. Ikumbukwe kwamba kipindi ambacho familia yao inakimblia Rwanda, Paul Kagame alikuwa ni mtoto wa miaka miwili tu. Kwa hiyo ni vizuri kukumbuka huko mbele tunavyoendelea na makala hii kwamba Paul Kagame amekulia nje ya Rwanda. Kwamba alirejea Rwanda walau kwenda kuugusa mchanga wa ardhi ya nchi yake tayari akiwa ni mtu mzima kabisa.

Walipofika Uganda yeye na familia yake waliishi katika kambi ya wakimbizi ya Nshungerezi iliyopo kaskazini mwa Uganda mkoa mdogo wa Toro. Ni mahala hapa kwenye kambi ya wakimbizi na kwenye hali hii ya utoto ndipo ambapo Paul Kagame na Fred Rwigyema walikutana na kuwa marafiki wa ‘kufa na kuzikana’.

Kagame alianza shule ya msingi kwenye shule maalumu ambayo ilijengwa karibia na kambi, maalumu kwa ajili ya watoto wa wakimbizi ‘kutoa tongotongo’ walau. Mwenyewe Paul Kgame anasema kwamba kitu kikubwa ambacho alijifunza kwenye shule hii ya wakimbizi ambacho anakithamini zaidi mpaka leo hii ilikuwa nikijua lugha ya Kingereza na pia kuweza kuelewa na kujichanganya (integrate) na tamaduni za Uganda.

Kutokana na kufanya vizuri sana darasani kushinda watoto wenzake wengine wa kikimbizi alipofikisha umri wa miaka tisa alihamishiwa kwenye mojawapo ya shule zenye heshima kubwa sana kipindi hicho ambayo ilikuwa inaitwa Rwengoro Primary School ambayo ilikuwa umbali wa kilomita zipatazo 16 kutoka kwenye kambi ya wakimbizi ambayo alikuwa anaishi na familia yake. lakini Licha ya umbali huu mkubwa kutoka kati ya shule anayosoma na kwenye kambi ya wakimbizi ambayo walikuwa wanaishi na familia yake, Paul Kagame alimaliza shule hii ya msingi kwa kupata alama za juu zaidi kuliko mwanafunzi yeyote yule kwenye Wilaya nzima.

Kutokana na kupata alama za juu kiasi hicho, Paul Kagame alipelekwa kwenye shule ya upili ambayo tunaweza kusema ndiyo ilikuwa bora zaidi nchini Uganda kwa kipindi hicho ambayo inaitwa Ntare School. Hii ndiyo shule ambayo pia hata Yoweri Museveni alisoma.

Mwanzoni masomo yake hapa shule ya Ntare yalienda vizuri sana, lakini muda si muda mambo yakaanza kubadilika.

Mwaka 1975 baba yake mzazi Kagame, Mr. Deogratias alifariki dunia tukio ambalo lilimuumiza moyo sana Kagame na kumpa msongo mkubwa wa mawazo. Lakini pia kabla ya kidonda cha kuondokewa na baba yake hakijapoana mwaka uliofuata rafiki yake kipenzi Fred Rwigyema aliondoka kwenda mahala kusikojulikana bila kumuaga yeyote yule. (nilieleza hapo juu kuwa mwaka huu ndio ambao Fred alijiunga na vuguvugu la FRONASA chini ya Yoweri Museveni… lakini hakuna ambaye alikuwa analijua hili kwa kipindi hicho).

Matukio haya makubwa mawili, baba yake kufariki na baadae rafiki yake kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha, kulimfanya Kagame awe kama vile ‘nusu amechanganyikiwa’. Ilikuwa karibia kila siku walimu shuleni kwake Ntare wanaletewa kesi ya Paul Kagame kupigana na wanafunzi wenzake. Alikuwa akimsikia mtu anatamka neno hata liwe dogo kiaisi gani lakini kama lina uelekeo la kuikosoa au kukashifu Rwanda basi atakuvaa na kuanza kurusha ngumi.

Mabadiliko yake haya hasi ya kitabia yalifanya maendeleo yake kitaalumu kushuka na pia walimu kuchoka utovu wake wa nidhamu na hatimaye kutimuliwa hapa Ntare School. Wazazi wake walipambana na akapata nafasi shule ya Old Kampala Secondary ambako alimalizia huko shule yake ya upili lakini akiwa na alama za chini kabisa kuliko ilivyo kawaida yake.

Baada ya kumaliza shule ya upili Paul Kagame alikuwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo. Alikuwa anajihisi kama vile amepotea na kupoteza dira ya maisha. He needed to find himself. Alikuwa anahitaji sababu ya kuendelea kuishi. Na si kuishi tu bali pia kuishi kwa kutimiza kusudi la yeye kuwepo duniani.

Paul Kagame alihitaji kuamsha tena hari na morari ndani yake. Na ndipo hapa ambapo alikata shauri ya kuitembelea nchi yake ya Rwanda kwa mara ya kwanza kabisa tangu alipoondoka akiwa na miaka miwili tu.

Hii ilikuwa ni mwaka 1977 ambapo Kagame alikata shauri ya kwenda Rwanda kwa mara ya kwanza maishani mwake. Safari yake hii ya Rwanda ndiyo ambayo iliamsha hari na morali ya kumjenga Kgame huyu ambaye tunaye siku hii ya leo. Nitarudi kueleza.


e5be1373cf0138788c2f508cfd6b60c0.jpg

Mfalme Mutara III ambaye ana undugu na baba yake Kagame

3466a0d5de421e0f254c9499623096f8.jpg

Best Friends Paula Kagame na Fred Rwigyema enzi za ujana wao



Itaendelea...

The Bold
To Infinity and Beyond

0718 096 811 - Whatsapp only
Pia follow and subscribe kwa ajili ya kupata notification kwa urahisi zaidi pindi nikipost kitu kipya.
 
Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij adden



bwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush[/USER
 
Ahsante kwa muendelezo. Ila usichelewe sana kurudi.
 
Very interesting story ...the bold kazi nzuri usichelewe kurudi mkuu
 
This is too short...kama orgasm ya jogoo,but you are f**cng genious
 
Kamanda umerudi, maana Muda sana naona hata Nifah last seen July, sijui amepatwa na nini ahsante kwa maarifa
 
OK something to ask,,rafiki take Paul bwana Fred alibadilisha jina,mdogo wa Museveni ni Salim na hata mtoto wa mseveni wanamajina ya kiislam,,swali he jima la yoweri museveni ni jina lake kweli au akibadili na kwa lengo gani make majina ya nduguzr ni tofauti na lake au ndo Yale Yale ya Walwa kuitwa Pombe?
 
Watutsi ndio hawa akina Jestikilla,akina Gentamycine,etc?

Kupitia hawa wawili tu nimeelewa kwanini hawakuelewana na wenzao Wahutu..I can see why.

Jestikilla na Gentamycine kwanza wana matusi mpaka basi...Wanatukana for the sake of it...Kujisifu halafu na dharau...Cha ajabu ukiangalia thread zao zinaonesha wana akili ndogo sana...Hilo ndio ajabu...

Ila sio wote,kuna Watutsi smart kama Munyambo P,etc...These guys are smart,class act dudes!!

Kulikua na tatizo kubwa...sishabikii genocide ila hawa Watutsi wana mapungufu yao makubwa kama wanadamu,they should check themselves.

RIP wote waliouawa kinyama...Mungu wao atawatolea haki.
 
Back
Top Bottom