Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Usijisifie matusi unagain nini hasa kumtukana mtu usiyemjua ??? Anyway yaishe sitaki tuanzishe tena hapa mada za kikabila

Long live East africa community
Nyie ndo mlianzisha mnapopewa majibu yanayo wafaa mnaita mnaona ni matusi
 
Yale yalishapita sina haja ya kuelezea hapa nilikua mdogo enzi yanatokea lakini Rwanda yasonga mbele africa yasonga mbele tulishayasahau na hayawezi kujirudia pia Naomba africa iwe na Amani siombei yatokee Tanzania ingawa naona kuna dalili za Kutokea kuhusisha uvyama vyama huu ambao utawagawanya watanzania.Godbless Africa.

Haya bwana. Lakini umejibu kijujuu, ndugu. Haya ni mambo magumu kuliko ulivyojibu kirahisi. Asante kwa kujibu lakini
 
Haya bwana. Lakini umejibu kijujuu, ndugu. Haya ni mambo magumu kuliko ulivyojibu kirahisi. Asante kwa kujibu lakini
The bold keshasema chanzo ni watutsi kutesa wahutu ndio wahutu wakaamua kulipa kisasi na kuwaua watutsi mwaka 1994!

Ila yameshapita na wamesameheana hivyo tuwaombee yasijirudie tena

Ahsante
 
Hawa watu walituonyesha kuwa binadamu ni Kama mnyama tu, Yule wa mwituni,

Kufikia kuchukiana kiasi kile ni jambo la ajabu mno, la aibu mno. Jirani kwenda kumuua jirani., sio mmoja, ni makumi na mamia ya majirani kwenda kuwaua majirani zao - au kusaidia kwa namna moja ama ingine kufanya ubaya huo. Aibuu , aisee. Tusiwaombee warudi kule

Tangia miaka ile mpaka sasa binafsi nime jaribu kuangalia nini hasa kilisababisha Haya?

Ni story ndefu, acha nikomee hapa. Nisubirie gwiji the bold atiririke,

Tuiombee mema afrika
Wakitaka wasirudie mwambieni Pk aendeshe serikali kwa uwiano sio kujaza wale na kuwawinda kuwaua au kuwafunga hawa
 
Haya bwana. Lakini umejibu kijujuu, ndugu. Haya ni mambo magumu kuliko ulivyojibu kirahisi. Asante kwa kujibu lakini

Proudly Rwandese nikijibu deep inaingiza ela kwako we Mtz ebu zile ela za makinikia mshalipwa Bombadia imekuja pambanen na hali zenu waswahili
 
Proudly Rwandese nikijibu deep inaingiza ela kwako we Mtz ebu zile ela za makinikia mshalipwa Bombadia imekuja pambanen na hali zenu waswahili

Please extend your thinking. Hivi kuna sifa kuwa mkimbizi? Wakimbizi wanaleta disasters huko waendako, kwa namna moja au ingine
Jipangeni ili kusiwe na wakimbizi siku zijazo

Tz ina matatizo ya makinikia na mengine. Lakini matatizo yenu yanayopelekea au yaliyopelekea Yale mauaji yenu ya kimbari kwa kweli ni special, yalikuwa kipimo namna gani binadamu anaweza kushuka chini kabisa au uwezo wake unaweza kuwa wa chini kabisa, tena over a long time. Pray for Rwanda. Pray for Africa. Pray for a human kind
 
Please extend your thinking. Hivi kuna sifa kuwa mkimbizi? Wakimbizi wanaleta disasters huko waendako, kwa namna moja au ingine
Jipangeni ili kusiwe na wakimbizi siku zijazo

Tz ina matatizo ya makinikia na mengine. Lakini matatizo yenu yanayopelekea au yaliyopelekea Yale mauaji yenu ya kimbari kwa kweli ni special, yalikuwa kipimo namna gani binadamu anaweza kushuka chini kabisa au uwezo wake unaweza kuwa wa chini kabisa, tena over a long time. Pray for Rwanda. Pray for Africa. Pray for a human kind

Wap kuna wakimbizi we kambale kwi kwi kwi kwi [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Proudly Rwandese.
 
KILIO CHA MIFEREJI YA DAMU IENDAYO ETHIOPIA


SEHEMU YA TANO


Ni jambo la kusikitisha sana kwamba Historia yetu ambayo watoto wetu wanafundishwa mashuleni na kuandikwa kwenye vitabu imechujwa mno kiasi kwamba inakuwa kama ni hadithi tu za kusadikika.
Kwa mfano kama umebahatika kuijui historia ya ukweli kuhusu Vita ya Kagera kisha ukasoma 'version' ambazo zimeandikwa kwenye vitabu na kuaminishwa kwa umma, machozi yanaweza kukutoka.

Ubaya ni kwamba hata wale ambao wamebahatika kujua ukweli halisi wa matukio na vilivyo nyuma ya pazia hawawezi kuthubutu kutia mkono na kuandika kile ambacho wanakijua.

Ndio maana naamini ni busara hata kwangu pia niandike kwa sehemu kile ambacho historia zetu hakivisemi lakini pia ni muhimu kuandika kwa "ustaarabu" kwa faida ya pande zote.



Kutengenezwa kwa Jasusi Paul Kagame

Katika sehemu iliyopita nilieleza kwamba, Paul Kagame mwaka 1977 alitembelea nchi ya Rwanda ambapo hakuwahi kuikanyaga tangu alipokuwa mtoto wa miaka miwili tu. Paul Kagame alifanya safari hii kutokana na kukosa amani ndani ya moyo wake. Alikuwa anatafuta 'kusudi' lake la maisha. Katika kipindi hiki alikuwa amempoteza baba yake mzazi na pia rafiki yake kipenzi Fred Rwigyema alikuwa amepotelea kusikojulikana.

Kwa hiyo Paul Kagame alienda Rwanda kwa ajili ya 'soul searching'. Alikuwa anataka kupata hamasa kwenye roho yake ili aweze kujua kusudi la maisha yake.

Kutokana na historia ya familia yake kuwa na ushawishi kwa kiasi fulani (nilieleza kwamba baba yake ana undugu wa kiukoo na Mfalme Kigeli na mama yake ana undugu wa damu na Malkia wa mwisho wa Rwanda) kwa hiyo hizi safari zake za Rwanda alizifanya kwa siri kubwa pia ukizingatia kwamba serikali ilikuwa makini sana na watusi ambao wako nje ya Rwanda kama wakimbizi kutokana na harakati zao na kiu yao ya kutaka kuipindua serikali mara kwa mara.
Safari hii ilikuwa ya maana sana kwa Kagame na alijenga 'connection' ambazo zilikuja kumsaidia sana miaka ya baadae kwenye harakati zake.

Mwaka 1978 alifanya safari nyingine kwenda Rwanda na safari hii hakupitia mpaka wa Uganda bali aliingia kupitia Zaire (Congo). Kwa wiki kadhaa ambazo alikaa Kigali kwa siri kubwa, alitumia muda huo kuimarisha 'connection' ambazo alikuwa nazo na pia kusoma hali ya kisiasa na uimara wa serikali.

Safari hizi mbili ziliamsha hari kubwa mno katika nafsi ya Paul Kagame. Aliona kwa uhalisia kabisa mateso na manyanyaso ambayo watusi walikuwa wanapitia nchini Rwanda. Akajihisi kabisa kwamba alikuwa ana jukumu la kufanya kitu kuyamaliza mateso hayo.

Aliporejea nchini Uganda Kagame akageuka kama mwanaharakati hivi katika kambi za wakimbizi akihamasisha vijana wenzake kujizatiti na kuweka mipango ya kuikombia Rwanda.

Wakati huo huo, rafiki yake Fred Rwigyema ambaye alipotea bila yeyote kujua ni wapi alikuwa ameelekea… alikuwa nchini Tanzania katika kambi ya FRONASA chini ya uongozi wa Yoweri Musseveni ambao walikuwa wanaweka mikakati ya kumuondoka madarakani Dikteta Idd Amin.

Habari kuhusu kijana mahiri, mwanaharakati Paul Kagame zilimfikia Yoweri Musseveni na alitamani awe sehemu ya 'timu' yake.
Ndipo hapa ambapo Fred Rwigyema ambapo ndio kwanza alikuwa amerejea Tanzania kutoka msumbuji ambako alipelekwa na Musseveni kwenye mafunzo ya pamoja na wapiganaji FRELIMO juu ya vita za msituni…alitumwa kwenda nchini Uganda kwa ajili ya masuala kadhaa lakini mojawapo ilikuwa kumshawishi Paul Kagame kujiunga na wapiganaji wa Yoweri Musseveni walioko nchini Tanzania.


Sasa basi…

Kuna mahala mkoani Morogoro, sitapaja kwa jina au exactly sehemu gani… lakini ni nje ya mji kidogo kuna 'Espionage Farm' ya siri ambayo mwaka 1978 Paul Kagame na maafisa kadhaa wa kikundi cha FRONASA walikuwa recruited na kupata mafunzo ya Ujasusi na masuala ya Intelijensia.

Niseme kwamba Paul Kagame ni moja ya maafisa bora na hodari kabisa kuwahi kuzalishwa na Idara yetu Usalama wa Taifa.


Kagame amewahi kutumia kwenye 'high profile missions' kadhaa lakini kubwa zaidi ni ile ambayo aliongoza kikosi cha Intelijensia ya wapiganaji wa UNLA (Ugandan National Liberation Front) katika vita ya Kagera.

Tofauti na historia ilivyoandikwa kuhusu vita ya Kagera, lakini ukweli na uhalisia ni kwamba wapiganaji wa UNLA ambao walikuwa ni zaidi ya 20,000 walikuwa ni kiungo muhimu sana katika ushindi wa vita ya Kagera. Suala hili tutalizungumzia siku moja kama tukipata wasaa wa kuichambua vita ya Kagera.

Kuna kikao cha siri sana kilifanyika pale Moshi ambacho kinajulikana kana "Moshi Conference" ambacho kiliudhuliwa na watu adhimu kabisa wapatao 28 na mmoja wao alikiwa Paul Kagame.
Katika kipindi hiki, Rais ambaye alikuwa amepinduliwa na Amin na kukimbilia Tanzania, Bw. Milton Obote alikuwa na kikundi chake cha wapiganajia ambacho alikiita kwa jina la Kiswahili "KIKOSI MAALUM" ambacho makamanda wake walikuwa ni Tito Okello na David Oyite Ojok. Hawa nao pamoja na Obote mwenyewe walikuwepo kwenye kikao cha mjini Moshi.
Pia Yoweri Musseveni alikuwepo kuiwakilisha FRONASA. Pia walikuwepi wanaharakati wengine mashuhuri kama vile Akena p'Ojok, William Omaria, Ateka Ejalu, Godfrey Binaisa, Andrew Kayiira, Olara Otunnu pamoja na baadhi ya 'wakubwa' kutoka kwenye vyombo vya ulinzi vya nchi yetu ambao kwa sababu ya 'staha' sitaandika majina. Jumla walikuwa watu ishirini na wanane.

Kikao hiki kilizaa mpango mkakati wa kijeshi ambao ndio ulitumika kwenye vita ya Kagera na kumshinda Amin. Paul Kagame ndiye ambaye alibebeshwa mzigo wa mikakati ya Intelijensia ya kijeshi.

Octoba 1978 tukaingia vitani dhidi ya majeshi ya Amin. Licha ya swahiba wake Kanali Muammar Gaddafi kutuma wapiganaji 2,500 pamoja na silaha nzito za mivita na za kisasa kwa kipindi hichi kama vifaru aina ya T-54, T-55, magari ya kivita ya kisovieti aina ya BTR APC na Grad MRL pamoja na ndege za kivita aina ya MiG 21 na ndege hatari za kivita (supersonic bombers) aina ya Tu-22 kumsaidia Amin… ajabu ni kwamba licha ya majeshi ya amini kuwa imara kiasi hiki kwa maana ya vifaa vya kivita lakini mwanzoni mwa mwezi April 1979 tulimpiga Amin mpaka "Ikulu" na kumlazimu kukimbilia Libya kwa swahiba wake Gaddafi na baadae kukimbilia Saudi Arabia.

Siku moja kabla ya kutangaza kuisha kwa vita ya Kagera, yaani April 10 Tanzania tukamsimika Yusufu Lule kuwa Rais mpya wa Uganda. Yusufu Lule ameishi sana hapa Tanzania hasa baada ya Idd Amin kuingia madarakani.
Pamoja na hilo lakini akina Musseveni nao waliunda chombo chao cha kijeshi ambacho kiliitwa National Consultative Commission (NCC). Hiki kwa kiasi fulani ndio walikifanya kama chombo chenye maamuzi ya mwisho kuhusu nchi.

SILAHA NZITO ZA KIJESHI AMBAZO UGANDA ILIPOKEA KUTOKA KWA KANALI GADDAFI

c602b90a718adb6d70906ae3d79c1bbf.jpg

Vifaru aina ya T-54 na T-55

2743bb95c3a98150af0cb66d13f9067a.jpg

Supersonic Bomber Tu-22


c8c265894db490554db478de4e2fa40f.jpg

Ndege za kivita aina ya MiG-21

68fe96eca1cfee365ee5361c87c3b2f6.jpg

Gari za kivita aina ya Grad MRL



1fa390e0b95ce0e569636ce5414c5cb0.jpg

Gari za kivita aina ya BTR APC


Miezi miwili tu baada ya majeshi ya Tanzania kumsimika Yusufu Lule kuwa Rais, kukaanza kutokea mvutano mkali kati ya NCC ya kina Musseveni na Rais Yusuf Lule. Mvutano huu ulikuwa ni juu ya mamlaka ya Rais ambayo NCC walimuona Lule kama anavuka mipaka yake. Lule naye kwa upande wake alikuwa anaonekana hataki nchi kuingozwa na jeshi (NCC).
Hatimaye tarehe 10 June mwaka huo 1979 NCC kwa ushawishi mkubwa wa Musseveni wakamuondoa madarakani Godfrey Binaisa kuwa Rais mpya wa Uganda.

Kimsingi Binaisa alikuwa kama 'kikaragosi' tu lakini kiuhalisia NCC ndio walikuwa wanaongoza nchi.

Lakini taratibu naye utamu wa madaraka ukaanza kumkolea.

Ikumbukwe kwamba katika kipindi hiki chote Milton Obote bado alikuwa nchini Tanzania hajarejea Uganda.
Kulianza kuzuka taarifa kwamba mnadhimu mkuu wa jeshi Brigedia Jenerali David Oyite Ojok ambaye kipindi cha vita ya Kagera alikuwa kamanda wa jeshhi ka pamoja la Tanzania na UNLA, alikuwa anafanya maandalizi ya kuhakikisha Obote anarejea Uganda.


Jeneralari Ojok anatokea eneo la kaskazini mwa Uganda kama ilivyo kwa Obote. Licha ya Ojok kuanza mikakati ya kumrudisha Uganda Obote lakini pia kwenye jeshi nyadhifa za juu zote alikuwa anahakikisha zinashikiliwa na watu wanaotoka ukanda wa kaskazini mwa nchi.

Harakati zote hizi Binaisi aliziona kama juhudi za kumuondoa madarakani ili kusafisha njia kwa Obote kurejea madarakani.

Mwezi May 1980 Rais Godfrey Binaisa alimuondoa Ojok kwenye cheo cha Mnadhimu mkuu wa jeshi.
Suala hili lilipingwa vikali na NCC na wakafikia hatua ya kumuondoa madarakani Rais Binaisa na kuunda tume maalumu ambayo waliita Presidential Commision ambayo ndiyo ilifanya kazi ya kuongoza nchi badala ya Rais.
Tume hii wanakamati wake walikuwa ni Museveni, Oyite Ojok, Okello na Muwanga.
Muwanga alipewa cheo cha uenyekiti wa tume japokuwa kiuhalisia wenye nguvu za ushawishi kwenye tume walikuwa ni Museveni na Ojok.

Baada ya hapa ndipo ambapo hasa umahiri wa Paul Kagame unaonekana. Ikumbukwe kwamba wakati yote haya yaliendelea Paul Kagame alikuwa na ushawishi mkubwa sana kwenye jeshi la Uganda kutokana na umahiri wake wa masuala ya Intelijensia. Kwa hiyo yeye ndiye ambaye alikuwa anawashauri ni nani anafaa kuwa Rais na nani hafai.

Baada tu ya nchi kuanza kuongozwa na Tume maalumu niliyoitaja hapo juu, Ojok akaanza tena mipango ya kumrejesha Milton Obote ndani ya Uganda. Ilikuwa wazi kwamba Ojok alikuwa anataka Obote ashike madaraka. Lakini watu wengi wa kabila la Baganda/Waganda walikuwa wanampinga Obete kwa kuwa yeye ndiye ambaye alimpindua Mfalme wao wa Baganda miaka kadhaa nyuma na kushika Urais kabla ya yeye pia kupinduliwa na Ids Amin. Kwa hiyo kulikiwa na mvutano kati ya watu wa maeneo ya kaskazini na kusini mwa Uganda.

Ndipo hapa ambapo Paul Kagame akaona fursa. Kwamba 'vita ya panzi, furaha ya kunguru'.
Yoweri Museveni yeye hatokei Kusini wala Kaskazini mwa Uganda… yeye amezaliwa na kukulia eneo la magharibi mwa nchi linalopakana na Rwanda sehemu inaitwa Ntungamo. (Hii ni moja ya sababu ya baadhi ya watu kuamini ana asili ya Kitusi).
Kwa hiyo huu ugomvi wa watu wa kaskazini na wa kusini haukuwa na mslahi nao kabisa. Ndipo hapa kwa kushauriana na Paul Kagame wakaanza michakato ya siri pembeni ya kujitenga na NCC na UNLA japokuwa Museveni alikuwa na ushawishi kwenye vyombo vyote hivyo.

Hatimaye mwaka 1980 Milton Obote alirejea Uganda na kushiriki kwenye uchaguzi mkuu mwaka huo na "kushinda". Matokeo ya uchaguzi yalipingwa vikali na watu wengi akiwemo Yoweri Museveni.

Ndipo hapa ambapo Yoweri Museveni, Pual Kagame na Fred Rwigyema pamoja na Waganda wengine thelathini na saba tu walianzisha kikundi chao cha kijeshi walichokiita National Resistance Army (NRA) lengo kuu likiwa ni kumuondoa madarakani Rais mpya Milton Obote.

Kikundi hiki kiliendesha mapigano ya msituni dhidi ya majesho ya serikali kwa karibia miaka sita.
Licha ya udogo wake kwa idadi ya watu (japo baadae waliongezeka kuzidi watu arobaini wa awali) lakini ufanisi wao kwenye kushambulia kwa uhodar na kulichosha jeshi la serikali ulikuwa wa hali ya juu. Miaka hii sita ya kupambana na majeshi ya serikali yalidhihirisha namna ambavyo Paul Kagame alikuwa ni nguli wa 'psychological warfare' ambayo pia ilikuja kudhihirika kipindi cha mauaji ya kimbari (tutaongelea zaidi tukifika hapo).

Katika kipindi hiki cha vita kwa masuala ya kijeshi Paul Kagame alikuwa mtu muhimu na mwenye kuheshimika zaidi na wapiganaji wa NRA kuzidi hata Museveni mwenyewe. Nyadhifa zao ndani ya NRA zilikuwa karibia kwenye usawa mmoja.

Kwa upande wa jeshi la serikali hali ilianza kuwa tete. Kukaanza kutokea mifarakano ya kikabila kati ya wenyewe kwa wenyewe. Kaskazini mwa Uganda kuna makabila makuu mawili, Walangi (kabila wanalotokea Obote na Ojok) na Waacholi (kabila la Tito Okello ambaye kwa kipindi hicho alikuwa kamanda wa jeshi).
Askari wengi wa miguu walikuwa ni Waacholi na ndio ambao walikuwa wanakufa zaidi kwenye vita hiyo dhidi ya NRA. Walangi wengi walikuwa ni maafisa wa jeshi na 'Special Forces'. Kwa hiyo askari wa miguu wakaanza kushinikiza serikali ifanye mazungumzo na NRA na kumaliza vita.

2a65bde2afc19b9058e6f539fd24beae.jpg

Jeneralu David Oyite Ojok


9039b58848dcd66f718ce6d1efb4aab5.jpg

Yoweri Museveni na wapiganaji wa NRA msituni


Serikali ikafanya shingo ngumu na kukataa.

Wanasema lakuvunda halina ubani, mwezi Desemba 1983 Oyite Ojok alifariki kwa ajali ya ndege ambayo kuna kila dalili ya mkono wa Kagame. Kwa kipindi hicho Ojok ndiye alikiwa mkuu wa jeshi la Uganda. Ilikuwa inategemewa Obote amteue Tito Okello au mwenzake mwingine aliyeitwa Bazilio Olara-Okello (hakuna undugu wa damu kati yao licha ya kufanana ubini japo wanatokea kabila moja la Waacholi) ambaye naye alishiriki vita ya kumuondoa Idd Amin. Lakini ajabu Obote alimteua afisa wa chini kabisa wa jeshi aliyeitwa Smith Apon-Achak ambaye anatoka kabila lake la Walangi kuchukua nafasi ya Oyite Ojok.
Hii iliwafanya wanajeshi wenye asili ya kabila la Waacholi kumchukia Obote na serikali yake na hatimaye miaka miwili baadae kumpindua kutoka madarakani.

Baada ya Miltob Obote kupinduliwa na jeshi kutoka madarakani kukaanza mapigano baina ya vikundi vya msituni kila kimoja kikitaka kushika usukani wa kuongoza nchi. Ndipo hapa yalifanyika maongezi ya pamoja baina ya vikundi vyote vya msituni nchini Kenya chini ya Rais Daniel Arap Moi ili kuleta suluhu na kuweka muelekeo mpya wa nchi ya Uganda.


Tarehe 29 January mwaka 1986 Yoweri Kaguta Museveni akaapishwa kuwa Rais mpya wa Uganda.

Paul Kagame akateuliwa na Rais kuwa Chief of Millitary Intelligence.

Swahiba wake Fred Rwigyema akateuliwa kwenye wadhifa wa Waziri wa Ulinzi.

Pia baraza la mawaziri lilikuwa limejaa watusi kibao.

Kwa maneno mengine tunaweza kusema kuwa Paul Kagame alikuwa ameiweka Uganda kwenye kiganja chake cha mkono japo hakuwa Rais. Lakini mtandao wa ushawishi ambao alikuwa ameujenga ndani ya serikali ya Uganda, baraza la mawaziri na kwenye jeshi ulikuwa ni mkubwa na una nguvu zaidi hata ya Yoweri Museveni ambaye aliapishwa kuwa Rais. Uzuri ni kwamba Museveni anafahamu umahiri wa Paul Kagame na hakutaka kutengeneza mvutano wowote naye kwa kuwa alikiwa anajua lengo kuu la Kagame lilikuwa ni lipi. Kagame hakuwa na nia yoyote ile ya kuwa Rais wa Uganda au kuendelea kuliendesha jeshi la Uganda. Ndoto yake ilikuwa ni moja tu, ndoto ambayo aliipata mwaka 1978 alipotembelea kwa siri nchi yake ya Rwanda, kwamba siku moja anataka kuwaokoa ndugu zake watusi kutoka kwenye unyanyasaji, kuuwawa, kudhalilishwa na mateso ambayo walikuwa wanapitia katika nchi yao.

Na sasa alikuwa amekamilika kwa kila kitu. Alikuwa na uzoefu wa kutosha. Alikuwa na weledi wa kutosha, tunaweza kuthubutu kusema kwamba katika kipindi hiki hakuna ambaye alikuwa anaweza kufikia daraja la umahiri wa Kagame katika masuala ya Ujasusi Afika Mashariki yote.
Lakini pia alikiwa na ushawishi katika nchi za kimakakati ambazo zinapakana na Rwanda, kwa maana ya Congo (huku aliwapeleka wapiganaji wa NRA kupata mafunzo ya siri ya Special Forces kipindi cha mapigano ya miaka 6 msituni dhidi ya majeshi ya serikali ya Milton Obote). Lakini pia alikuwa na ushawishi nchini Tanzania (mtoto wetu tuliyemfunza wenyewe ujasusi na alitusaidia sana kwenye vita ya Kagera). Na hakuna haja hata ya kusema kiwango cha ushawishi ambacho alikuwa nacho nchini Uganda.

Mbele yake kulikuwa na jambo moja tu la mwisho ambalo alikuwa anatamani litimie kabla hajaondoka juu ya uso wa dunia. Kuiweka nchi ya Rwanda mkononi mwake.




ad22e730eeb86328bc2ed0aa239bf97a.jpg

Siku ya kuapishwa Yoweri Kaguta Museveni kuwa Raia mpya wa Uganda Tarehe 29, January 1986

662a61cf50f7de1317c68daab41c3343.jpg

Fred Rwigyema


2457551d22b55a695da47c8373a5bf59.jpg

Paul Kagame



Itaendelea....

The Bold - 0718 096 811 (Whatsapp only)
To Infinity and Beyond

Pls: follow, subscribe and nifuate WhatsApp
 
SEHEMU YA TANO

Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij adden


bwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush[/USER
 
Back
Top Bottom