Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Oook

Nimekuelewa!! Ila Miaka hiyo ndugu yangu watu walikuwa Bado Wana kisirani!! Cha kutopendana hasa hasa north Provience Ndo maana wakamuweka muhutu mwenzao awaongoze!! Lakin Sasa hivi wameshakuwa wamoja!! Wanaoana Sema Bado katika 100 hawakosi 2 so msafara wa mamba na kenge wamo!!

Hata wahuko Uganda unaosema Ni wale ambao wazazi wao Bado wanaona ututsi na uhutu deal!! Wakiwa nchi za watu
Okay mkuu muhimu kuna amani basi na idumu milele.... Karibu sana Tanzania usafishe macho ujiji kwetu huku
 
A
Acha propaganda wazungu waliondoka sababu askari wao waliuawa na interehamwe so wakaona kwanini hasara ilihali vita haiwahusu!!! So irrespective kauawa nani au nani wao wangeondoka tu maana walipewa amri

Otherwise msimamo wangu bado ni ule ule kagame ni dikteta na ana siasa chafu.... Kma hapendi democracy aifute sio anasema kuna uchaguzi huku hataki competition niliona mdahalo wake na wagombea wenzake yaani wanamsifia badala ya kupambana naye nkajua mapandikizi tu

Aweke usawa..... Aombe msamaha wahutu... Ajisalimishe mahakamani..... Aachie wafungwa wa kisiasa.... Aeleze ukweli wa genocide.... Aeleze aliemuua rwigyema... Hapo ndio watu wata move on sio sasa ambapo wana maswali ma uchungu kibao
Ahhha hhha haha mkuu naweza kuipata wapi huo mdahalo?
 
A

Ahhha hhha haha mkuu naweza kuipata wapi huo mdahalo?
Mkuu niliuangalia Rwanda TV iko kwenye baadhi ya ving'amuzi hapa TZ nikaona wanavyosweat yaani wanamsifia nikajua macampaign manager wake nakuja kushangaa mdahalo unaisha eti wanatambulishwa kma wagombea urais!!!

Asee nilicheka sana
 
Rwanda....hivi kweli PK anapendwa na wanyarwanda hata kwa asilimia 50 kweli??
 
Mnasubiri nini wakuu?? Mbona alisema kuwa kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake ameamua aishie hapo!!! Keshasema vita imeisha,wahutu ni wauaji na kagame ndio steringi sasa mnataka nini Kingine??
Japo unachuki bnafsi na kagame ila Kartika jamii ya wanyarwanda wote ukiunganisha wahutu watusi na watwa hakuna genius kama kagame kwa karne hii na huyo Pk ni level ya akina Roosevelt ama George Washington, kubali kataa unamchukia kwa sababu ya akili zake the guy is very smart upstairs na akifa huenda asitokee myarwanda mwingine wakumfikia hata japo nusu ya uwezo wake, the man is very talented na watu wa Aina yake hawazaliwi kila siku, punguza kumtazama kwa jicho la chuki, jamaa ni moja Kati ya waafrika wachache waliopata fursa wakiwa na uwezo na uwezo wake utainufaisha Rwanda for 100yrs ahead trust my words
 
Japo unachuki bnafsi na kagame ila Kartika jamii ya wanyarwanda wote ukiunganisha wahutu watusi na watwa hakuna genius kama kagame kwa karne hii
Lini nimemchukia kagame?? Mbona thread kibao humu namsifia sana..... Nachopingana na kagame ni eneo la UDIKTETA na UKABILA basi hapo tu mengine yote namuunga mkono hasa mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa aliyoyaleta ntakuwa mwendawazimu kupinga hilo

, kubali kataa unamchukia kwa sababu ya akili zake
Kwanini nimchukie kwa akili zake kwani ninagombea naye urais 2024 ama mie ni kilaza hadi nimuonee wivu?? Na nani kasema kagame ndio brightest au kisa ni maarufu kuliko wanyarwanda wengine?? Kuna wenye akili wengi tu Rwanda hata nmesoma nao most tutsis are bright sana tu so kagame sio wa kwanza na sio wa mwisho

na akifa huenda asitokee myarwanda mwingine wakumfikia hata japo nusu ya uwezo wake, the man is very talented na watu wa Aina yake hawazaliwi kila siku,
Embu uache slave mentality ya kuamini wengine hawawezi ila kagame tu...... Na ndio hiki kinaua Afrika mtu mmoja kujiona ana akili kuliko wengine.... Sasa kwa mfano leo akifa ghafla si ina maana Rwanda itaporomoka?? Haijalishi una akili kiasi gani mbona Mahathir mohammed licha ya kwamba aliitoa singapore kwenye jalala na sasa ni top hapa duniani ila aliachia ngazi?? Kwanini unaamini hakuna wengine?? Umewajaribu?? Unajua baraza la mawaziri la kagame au kisa unamjua kagame tu basi ndio unamuona anafaa pekee..... Ni vizuri kufanya succession plan nzuri ili hata likitokea lolote nchi hainguki sio kuaminishana kwa kuwa ana akili sana basi atawale milele BIG NO.... Nchi haitostawi kwa akili za mtu mmoja bali MFUMO otherwise huyo mtu akifa nchi nayo inakufa kama PATRICE LUMUMBA NA ZAIRE

punguza kumtazama kwa jicho la chuki, jamaa ni moja Kati ya waafrika wachache waliopata fursa wakiwa na uwezo na uwezo wake utainufaisha Rwanda for 100yrs ahead trust my words
Sina chuki na kagame mkuu ila ukweli lazima usemwe kwenye issue ya UTAWALA amechemka sana.... Hivi kwa maendeleo yote yale alikuwa na haja ya kuogopa wapinzani?? Yule binti si bora angemuibia kura tu kuliko kumtesa vile then wwe huoni shida?? Yukwapi ingabire?? Yukwapi nyamwasa?? Kwanni hataki mawazo mbadala??

Kingine ni issue ya genocide kagame anaficha mengi sana na anapotosha dunia ndio maana kwa hili huwa nampinga wazi wazi bila kupepesa macho hata humu nlitoka mapovu sana maana ni propaganda tupu facts ni 20%....

Mfano Bold anasema eti kagame hakuua ruhengeri?? Ina maana risasi za RPF zililenga wanajeshi wa serikali pekee ila alishindwa kutwambia kivipi wahutu 40,000 walikutwa wamechinjwa na wengine kukimbia makazi!! Kulingana na ripoti za human rights watch!!

Kagame namkubali sana ila kwa hili la genocide hapana ntampinga kma alivyofanya Mch Mtikila hadi anaingia kaburini

Long live East Africa
Long live Rwanda
 
Back
Top Bottom