Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Usipotoshe Mambo Mohamed, mimi sihoji hizo sajara na nyaraka za wazee wako. Nasema kuhusu"Tanganyika Intelligence Report" ambazo zimetolewa na wale unaowashutumu kuusimika "mfumo kristu" Tanganyika. Jee nyaraka zao unaziamini kwa kuwa zimemtaja Abdluwahid sykes?

Tuoneshe ushahidi wa hilo, mimi nnavyojuwa mfumokristo umeletwa na Nyerere na ndio maana anapigiwa debe kupewa "utakatifu", Utakatifu na wewe Rais uliyeiacha nchi hohehahe "failed economy" utoke wapi?
 
Siku moja nilimuuliza Mohamed kwamba mbona kwenye masimulizi yake sioni jina la MARTIN KAYAMBA? Mpaka leo Kimyaaa!!
 
Siku moja nilimuuliza Mohamed kwamba mbona kwenye masimulizi yake sioni jina la MARTIN KAYAMBA? Mpaka leo Kimyaaa!!

Ndio hulioni. Sasa wewe kama unayajuwa ya huyo unaemtaja si utuletee hapa tufaidike, kwanini umngoje Mohamed Said?
 
Nguruvi3, Kigarama, Mag3, Mzee Mwanakijiji..

Ebu na nyie jipangeni kama itawezekana muungane kwa pamoja muandike histori ya Uhuru wa Tanganyika..

Tena itakuwa vizuri mpinge yote yale ambayo sio ya kweli kwenye kitabu cha Mohamed Said..

Inawezekana kuna mashujaa wengine nyie mnawajua waliopigania uhuru wetu Mohamed Said, hawakuandika kutokana na udini wake dhidi ya ukirstu..

Na hicho kitabu ndio kitakuwa historia kamili ya uhuru wa Tanganyika sababu kitaandikwa kwa pamoja na magwiji niliowataja..

Tunakisubili kwa hamu...
 
Nnayasoma sana tena.

Ungeandika "Nnayasoma tena sana" lakini kwa kuandika "Nnayasoma sana tena" sentensi yako yako inakuwa "tasa" kwani inashindwa kuzaa lengo lililokusudiwa.

Ngoja nikwambie kitu, hata sisi ni watu wa pwani kama nyie tofauti yetu ni vizazi. Wenzetu inawezekana mmezaliwa zama za kuzaliana nyumbani, wenzenu tumezaliwa Ocean Road Hospital mita chache kutoka pale kwenye lile jumba jeupe la Magogoni. Na kama anavyosema Khadija Kopa, basi huo nao kwa zama hizi umjini. Usidhani kila mwana JF ambaye yumo humu anayepingana na Mohamed si mtu wa pwani!!
 
Nguruvi3, Kigarama, Mag3, Mzee Mwanakijiji..

Ebu na nyie jipangeni kama itawezekana muungane kwa pamoja muandike histori ya Uhuru wa Tanganyika..

Tena itakuwa vizuri mpinge yote yale ambayo sio ya kweli kwenye kitabu cha Mohamed Said..

Inawezekana kuna mashujaa wengine nyie mnawajua waliopigania uhuru wetu Mohamed Said, hawakuandika kutokana na udini wake dhidi ya ukirstu..

Na hicho kitabu ndio kitakuwa historia kamili ya uhuru wa Tanganyika sababu kitaandikwa kwa pamoja na magwiji niliowataja..

Tunakisubili kwa hamu...

Hawawezi, hao ni wapiga porojo wa JF. Wataanzia wapi? wao wangoje kulalamika tu humu. Ritz, kazi ya Mohamed Said imeshaota mizizi na hakuna wakuing'oa, ukweli haufutiki.

"naatamanaaani na kujaribu siweeezi".
 
Nguruvi3, Kigarama, Mag3, Mzee Mwanakijiji..

Ebu na nyie jipangeni kama itawezekana muungane kwa pamoja muandike histori ya Uhuru wa Tanganyika..

Tena itakuwa vizuri mpinge yote yale ambayo sio ya kweli kwenye kitabu cha Mohamed Said..

Inawezekana kuna mashujaa wengine nyie mnawajua waliopigania uhuru wetu Mohamed Said, hawakuandika kutokana na udini wake dhidi ya ukirstu..

Na hicho kitabu ndio kitakuwa historia kamili ya uhuru wa Tanganyika sababu kitaandikwa kwa pamoja na magwiji niliowataja..

Tunakisubili kwa hamu...

Ushauri wako ni wa maana sana ingawa natofautiana na wewe kwenye hoja ya "Historia kamili". duniani hakuna Historia Kamili. Kwa mfano mpaka sasa Rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad anaamini kwamba mauaji ya Wayahudi ni hadithi za kutunga tu kwani isingewezekana kwa wayahudi zaidi ya milioni 6 kuuawa kirahisi na Manazi wa Ujerumani.

Lakini hata Rwanda watu wanasema Wahutu wenye msimamo mkali waliwaua Watutsi na wahutu wenye msimamo wa wastani (Moderate) lakini hivi hakuna watutsi waliowaua wahutu au watutsi wenzao wenye msimamo wa wastani? Hiyo ndiyo Historia, hakuna iliyo kamili.
 
Hawawezi, hao ni wapiga porojo wa JF. Wataanzia wapi? wao wangoje kulalamika tu humu. Ritz, kazi ya Mohamed Said imeshaota mizizi na hakuna wakuing'oa, ukweli haufutiki.

"naatamanaaani na kujaribu siweeezi".
Kazi ya mzee Mohamed Said imeota mizizi kwenye kikundi kidogo cha 'Wachochezi wa kidini ' kama wewe.
 
Siku moja nilimuuliza Mohamed kwamba mbona kwenye masimulizi yake sioni jina la MARTIN KAYAMBA? Mpaka leo Kimyaaa!!

Kigarama,

Nimepata humu ndani kujibu kuhusu Martin Kayamba lakini simkumbuki aloniuliza.
Kayamba alikuwa kibaraka wa Waingereza na akijikomba sana kwao.

Yeye ni "contemporary" wa Kleist Sykes na maisha yao wote yamo katika "Modern Tanzanians" cha John Iliffe.

Chungulia hapo chini Erika Fiah kasema nini kuhusu Kayamba:

"Kalamu ya Fiahilikuwa haina muhali. Katika rambirambi alizotoa za kijeuri na za dharau juu yakifo cha Martin Kayamba,[1]Fiah aliomboleza kwa kusema kwamba Waafrika hawakunufaika kwa elimu ya Kayambawala kwa wadhifa wake kama karani wa kaimu Katibu Mkuu."[1]
Ukipenda unaweza kumsoma Kayamba katika kitabu hiki:
Kayamba, Martin,The Autobiography ofMartin Kayamba, "The Story of Martin Kayamba Mdumi, MBE, of the Bondei Tribe" MargeryPerham, (ed) Ten Africans, 5-272.
Mwenyewe umeona umeuliza swali gumu sana na shingo unatoa.
Ndiyo maana dada yangu FF husema "usinchekeshe."

Mie mabuku yote hayo nishayanywa miaka mingi ilopita.

Mohamed


 
Usipotoshe Mambo Mohamed, mimi sihoji hizo sajara na nyaraka za wazee wako. Nasema kuhusu"Tanganyika Intelligence Report" ambazo zimetolewa na wale unaowashutumu kuusimika "mfumo kristu" Tanganyika. Jee nyaraka zao unaziamini kwa kuwa zimemtaja Abdluwahid sykes?

Kigarama,

Hebu nionyeshe hicho kipande.

Mohamed
 
Ni 'dikteta' Nyerere anayevaa soksi ndeefu! ndiye aliyejenga shule ya Kibaha ambayo rais wa nchi hii amesomea. Sijui Nyerere alisahauje kuwa ni mwislam maana angeondoa jina lake ASAP.

Wapo waliopeleka watoto wao kupata elimu ilikopatikana, Mohamed anawashauri wazee na kusifia kuwa bora hawakupeleka watoto wao kwenye shule za makanisa( jambo jema kama ana mbadala), kinachoshangaza yeye asubuhi na mapema anapanda ndege kwenda Marekani na Ulaya kutoa mihadhara kwenye vyuo vya kanisa na sio Saudia, Bharain, Syria au Yemen.

Wakati Mohamed, anasema lugha ya kiingireza inapanda kwake hadi kumuumbua afisa mhusika, akirudi nyumbani anashauri wenzake wafundishe watoto wao Irab za kiarabu!

Wakati Mohamed anakwenda shule kufuatilia maendeleo ya mwanae na kuona kadhulumiwa na mwalimu asiye na dini(hakusema ana dini gani) mwalimu mkuu akabadili maksi(mwl mkuu hakumtaja dini). Mohamed hajaenda Kilwa kufanya utafiti kwanini sekondari ifungwe kwa kukosa wanafunzi!

Nguruvi3,

Tunaridi alif kwa kijiti!

Mohamed
 
Ushauri wako ni wa maana sana ingawa natofautiana na wewe kwenye hoja ya "Historia kamili". duniani hakuna Historia Kamili. Kwa mfano mpaka sasa Rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad anaamini kwamba mauaji ya Wayahudi ni hadithi za kutunga tu kwani isingewezekana kwa wayahudi zaidi ya milioni 6 kuuawa kirahisi na Manazi wa Ujerumani.

Lakini hata Rwanda watu wanasema Wahutu wenye msimamo mkali waliwaua Watutsi na wahutu wenye msimamo wa wastani (Moderate) lakini hivi hakuna watutsi waliowaua wahutu au watutsi wenzao wenye msimamo wa wastani? Hiyo ndiyo Historia, hakuna iliyo kamili.

Historia huandikwa na Mohamed Said kaandika na nyinyi hamuipendi, kwanini? kila tukiwauliza ni nani aliyetajwa humo hakuwepo au hakufanya kilichoandikwa hakuna, mnakuja ma ra nani kakuambia, mara sijui fulani na fulani kwanini hukuwaandika.

Kwanini hao mnaosema hawajaandikwa msiandike nyinyi. Mohamed Said kawaandika aliowaandika na wa kabla ya Mohamed Said wa Magogoni kule mlishawahi kuwauliza kwanini hawa aliowaandika Mohamed Said nyinyi hamkuwaandika?

Mohamed Said kaona hawakuandikwa, akaanza kuwaandika na sasa MashaAllah, ni miaka inakwenda hakuna kati yenu aliyethubutu kusema huyo hakuwepo au huyo hakuenda na baiskeli rufiji katika harakati za kutafuta madaraka ya Tanganyika au Nyerere hakukaa kwa Sykes alipokuja Dar au Dossa hakumpakia kwenye gari lake au Msume hakumpa chakula au Nyerere hakusahau wadhifa wa Abdul Wahida TAA.

Naona hakuna anaeyapinga yote hayo. Au kuna aneyapinga hayo? Mzee Mwanakijiji alikuja na hoja yake humu, ikasambaratishwa kwa post moja tu, hajairudia tena, tena ikafifirishwa hoja na majibu, haimo tena humu, kama imo nionesheni. Kwanini?
 
Kitu kimoja nilicho na hakika nacho kwa asilimia 100% ni kwamba wale wote wenye mapenzi ya kweli kwa taifa letu la Tanzania wanasita sana kuchangia hii hoja inayofinyangwafinyangwa na huyu anayejiita Mohamed Said. Bila kumung'unya maneno nayaita madai ya Mohamed Said la kutoa elimu ya historia ya kweli ni porojo hatari iliyojaa uchochezi ambayo lengo lake hasa ni kuleta uhasama wa kidini miongoni mwa wananchi. Sijui anachotegemea kufaidika nacho kwa kupanda hii mbegu ya hatari ambayo nina hakika mtu kama Mohamed Said anajua fika madhara yake.


Mohamed Said ni kama kipofu ambaye baada ya kusimuliwa na wazee kwamba tembo ni mnyama mkubwa kuliko wanyama wengi anapata nafasi ya kumpapasa tembo. Kwa bahati mbaya anaupapasa mguu wa tembo na si mwili wote halafu katika imani yake anadai anao uwezo wa kutoa somo kuhusu umbo la mnyama tembo na ushuhuda wake, kuwa tembo ni kama gogo la mti mkubwa, ndio ukweli na anayesema tofauti hajui kitu. Watu wote wanaolalamikiwa na Mohamed Said kuwa walisahauliwa, wengi wao walikuwa wakazi wa Dar es Salaam eneo la Gerezani.

Kabla ya uhuru Tanganyika iligawanywa katika majimbo makuu manane na katika majimbo yote hayo, jimbo la pwani kwa ujumla lilikuwa moja ya majimbo yaliyokuwa nyuma kimaendeleo kiuchumi, kielimu na kisiasa na hiyo ni licha ya kuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni yalikuwa Dar es Salaam. TAA ilianzishwa na watumishi wa serikali (civil servants) na kwa wakati wote kazi kubwa ya TAA ilikuwa ni kulalamika ikidai haki ya wafanyakazi bila upendeleo na hasa ubaguzi wa rangi katila utumishi kubwa ukiwa uonevu dhidi ya wazawa, mtu mweusi.

Jimbo la Ziwa ni moja ya majimbo yaliyokuwa mbele kiuchumi, kielimu na kisiasa na kama kuna kitu kinaweza kudaiwa kuwa kilisahaulika katika harakati ya kupigania uhuru ni mchango wa Jimbo la Ziwa (Bukoba, Mwanza, Mara na Shinyanga) Jimbo la Ziwa ndilo lililoongoza kwa idadi ya watu, idadi ya makabila, idadi ya mali asili na idadi ya machifu ambao nafasi yao ilikuwa kubwa tu katika kuhamasisha watu. Moja wa watu ambao mchango wao nitautaja kidogo tu ingawa alifanya jitihada kubwa labda zaidi ya wazee wa Mohamed Said ni Paul "Kishamapanda" Bomani.



Historia ya harakati za uhuru ni zaidi ya porojo za Mohamed Said, watu walipigania uhuru kama Watanganyika na bila kubaguana kikabila, kidini wala kijinsia. Ndio maana mimi sitaki kabisa kuwa na majibizano na huyu Mohamed Said moja kwa moja ila kwa kuwa hoja ileletwa JF, akae tayari kupewa somo kuhusu umbile zima la mnyama tembo na sio mguu moja wa tembo alioupapasa. Hapa mimi nitaongea sana kuhusu mchango wa Jimbo la Ziwa na baadaye kuonyesha jinsi maadui wa nchi yetu wanavyowatumia kidini watu kama huyu Mohamed Said.



Baadaye nitaeleza jinsi Mkoa wa Mara yenye makabila karibu hamsini yalivyoweza kushirikiana bila mfarakano na kuitikia mwito wa Mwalimu Nyerere katika hizo harakati za kudai uhuru. Je mwamko wa wakazi wa jimbo la Ziwa ulikuwaje na mapokezi gani aliyapata kila wakati Mwalimu aliporudi kwenye hili jimbo ambalo idadi ya wakazi wake kwenye miaka ya 50s ilikuwa mara tatu ya majimbo mengi Tanganyika kama Pwani. Pia nitaonyesha ni wakati gani walianza kuyasikia hayo majina anayodai Mohamed Said ya wazee wa Gerezani Dar es Salaam !

Bado nasubiri habari za Musoma...

Mohamed
 
Kigarama,

Nimepata humu ndani kujibu kuhusu Martin Kayamba lakini simkumbuki aloniuliza.
Kayamba alikuwa kibaraka wa Waingereza na akijikomba sana kwao.

Yeye ni "contemporary" wa Kleist Sykes na maisha yao wote yamo katika "Modern Tanzanians" cha John Iliffe.

Chungulia hapo chini Erika Fiah kasema nini kuhusu Kayamba:

"Kalamu ya Fiahilikuwa haina muhali. Katika rambirambi alizotoa za kijeuri na za dharau juu yakifo cha Martin Kayamba,[1]Fiah aliomboleza kwa kusema kwamba Waafrika hawakunufaika kwa elimu ya Kayambawala kwa wadhifa wake kama karani wa kaimu Katibu Mkuu."[1]
Ukipenda unaweza kumsoma Kayamba katika kitabu hiki:
Kayamba, Martin,The Autobiography ofMartin Kayamba, “The Story of Martin Kayamba Mdumi, MBE, of the Bondei Tribe” MargeryPerham, (ed) Ten Africans, 5-272.
Mwenyewe umeona umeuliza swali gumu sana na shingo unatoa.
Ndiyo maana dada yangu FF husema "usinchekeshe."

Mie mabuku yote hayo nishayanywa miaka mingi ilopita.

Mohamed


Katika maswali mugumu niyajuayo mimi hilo halimo. Hujajibu swali langu.Pamoja na kwamba kweli Kayamba alilewa "uzungu" na kuwadharau waafrika wenzake. Lakini hana mchango wowote kwenye ukombozi wa nchi hii??
 
Historia huandikwa na Mohamed Said kaandika na nyinyi hamuipendi, kwanini? kila tukiwauliza ni nani aliyetajwa humo hakuwepo au hakufanya kilichoandikwa hakuna. mnakuja ma ra nani kakuambia, mara sijui fulani na fulani kwanini hukuwaandika.

Unafikiri hata Salman Rushdie nukuu alizozitumia kuandikia kitabu chake cha "Satanic Verses" hazikutoka kwenye Quran? Kwa nini waislam walimpinga hadi kumtangazia "Fatwa". Wewe unamuunga mkono Rushdie kwa sababu nukuu zake zilitoka kwenye Quran??
 
Back
Top Bottom