Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Sasa kama unajua kuwa mtafiti hawezi kufanya utafiti wa kila kitu kwenye jambo analolitafiti, sasa kwa nini mnapiga kelele kwa wazee wa Gerezani kusahauliwa, wakati na nyie watoto wa Gerezani mmewasahau wazee wa Nyamagana waliopigania Uhuru ambao nao Historia "Rasmi' iliwasahau?

Kuna mtafiti akajua kila kitu. Hebu nitajieni utafiti uliofanyika ukataja kila kitu. Mie ningelikuwa supervisor wako katika utafiti ukiniletea research ukasema umegusa kila mahali nakupa 0 kwasababu ni uongo na hujafanya kazi. Professor Albert Einstein mwenyewe ambaye wazungu wanasema ndio mtu mwenyewe akili nyingi duniani alipofanya utafiti wake wa theory of relativity alishindwa kuelezea uhusiano wa sub atomic particles and speed of light. Mwezi uliopita wanasayansi kama 10 kutoka ujerumani, us, uk na norway wameweza kugundua kuwa sub atomic particles travell faster than the speed of light. Hivyo kuleta challenge kwa theories za Einstein na mfumo mzima wa maisha yetu.

Hakuna ukamilifu katika binaadamu mkamilifu mmungu peke yake. Ila kuna kujitahidi na Mohamed Said amejitahidi kuleta aliyogundua na kuweka evidence zake na nyie andikeni ya kwenu na wazee wenu tuyasome.
 
Sasa kama unajua kuwa mtafiti hawezi kufanya utafiti wa kila kitu kwenye jambo analolitafiti, sasa kwa nini mnapiga kelele kwa wazee wa Gerezani kusahauliwa, wakati na nyie watoto wa Gerezani mmewasahau wazee wa Nyamagana waliopigania Uhuru ambao nao Historia "Rasmi' iliwasahau?

Kuandika historia ya wazee wa Nyamagana ni kazi yako wewe mtoto wa Nyamagana kuwaandika mchango wao katika uhuru wa Tz. Usitegemee mtu kutoka sehemu nyingine akufanyie hilo.

Sasa kazi kwako kuwatendea haki wazee hao kuandika historia zao na kuziweka katika kitabu ili vizazi na vizazi wajue hilo na kuwapa hishma yao.

kazi kwako. sio kulalama
 
Hongereni sana mzee Mohamed Said kwa mafanikio hayo. Lakini je mafanikio hayo yana tija gani kwangu mimi na watanzania wengine wasio waislam?Mafanikio hayo yamejenga shule ngapi, hospitali ngapi, yamesomesha watoto wangapi?Yamepunguza umaskini kiasi gani kwa watanzania? yamepambana kiasi gani na ufisadi unaotishia kuangamiza taifa letu?yameleta umoja na upendo kiasi gani miongoni mwa watanzania? yamejenga fursa za ajira kiasi gani kwa vijana wetu wa Tanzania?

Gwalihenzi,

Wewe uanzungumzia umoja na upendo.
Isome historia ya kudai uhuru wa Tanganyika uuone upendo wa Waislam na uone wamelipwa nini baada ya kufanikisha uhuru.

Mambo ya ufisadi sisi yanatuhusu kitu gani wakati hayo maadaraka yote ni himaya ya mfumokristo?
Mfumokristo umewanyima Waislam kazi na elimu halafu unatuuliza mbegu ambayo sisi hatukuipanda?

Mohamed
 
Kuna mtafiti akajua kila kitu...

Hii hoja ndugu yangu si yangu bali ni ya kundi lenu mkiongozwa na Mohamed Said. M ohamed Said alisema mgawanyo wa madaraka Tanzania ni kwa wakristo ni 83% na Waislamu ni 17% sisi tukauliza kama ni hivyo hao wengine wasio waislam na wakristo wanawekwa wapi kwenye hizo takwimu?
 
Kuandika historia ya wazee wa Nyamagana ni kazi yako wewe mtoto wa Nyamagana kuwaandika mchango wao katika uhuru wa Tz. Usitegemee mtu kutoka sehemu nyingine akufanyie hilo.

Kwa hiyo waliowasahau wazee wa Gerezani hawana Kosa??
 
NARUDIA KUBANDIKA TENA HILI BANDIKO KWANI SIELEWI NI KWANINI FAIZAFOXY NA MOHAMED SAID HAWATAKI KUNIJIBU SWALI LANGU HILI.

Waislamu wana Nguzo zao tano wanazoziamini kama ndiyo msingi wa dini yao. Kama kweli waislamu wa Tanzania tangu Tanganyika walikuwa wanakandamizwa, ni nguzo ipi kati ya hizi tano ambayo waislam wa Tanzania wanakatazwa kuitimiza na Serikali kwa sababu serikali inadhibitiwa na MfumoKristu?

1. Kushahadia

2. Kuswali swala tano

3. Kufunga

4. Kutoa zaka

5. Kuhiji kwa mwenye uwezo

Kama waislamu wangekuwa wanakandamizwa katika hizo nguzo tano za uislamu ningeelewa hoja za MS. MS na wenzake watuambie ni wapi na ni lini waslamu walikatazwa kwenda kuhiji, kuswali. kufunga kwa Sunnah na Kufunga Ramadhani, kutoa zaka au kushahadia. Sijawahi kuona mfumo wa serikali ukikataza wakristo kusilimu au waislamu kujenga misikiti au kuadhini. Naijua misikiti ambayo iko katikati ya makazi ya watu kwenye mchanganyiko wa wakristo na waislamu na sijawahi kusikia serikali ikikataza waislamu kuadhini kwa sababu 'wanawasumbua" wasio waislamu kwa adhana zao.

Waislamu wanapotaka kwenda Mecca kuhiji hakuna siku walikatazwa kwenda badala yake serikali mara kadhaa imewahi kutoa fedha kusaidia waislamu kwenda kuhiji, sasa hapo waislamu wanakandamizwaje na huo mfumokristu na inakuwaje mfumokristu unashindwa kuzuia waislamu kuhiji, kusilimisha wakristo au kuadhini?

Hivi karibuni serikali si ilishawahi kutoa zaidi ya Shilingi Bilioni 2 kusafirisha mahujaji kwenda Mecca kuhiji? Kanisa lilikuwa wapi kuizuia serikali kutoa fedha hizo??
 
Hii hoja ndugu yangu si yangu bali ni ya kundi lenu mkiongozwa na Mohamed Said. M ohamed Said alisema mgawanyo wa madaraka Tanzania ni kwa wakristo ni 83% na Waislamu ni 17% sisi tukauliza kama ni hivyo hao wengine wasio waislam na wakristo wanawekwa wapi kwenye hizo takwimu?

Kigarama,

Wengine?
Propaganda hizo zimepitwa na wakati humu tuko sisi na nyinyi basi.

Hii kufunika kichwa mwili wote uko nje haisaidii chochote.

Nchi imeachiwa tatizo kubwa sana la udini ulowanyanyasa Waislam kwa miaka tulikabili tatizo hili na tuliondoe.
Wahindu sijui Wapagani sijui nani hawahusiki kabisa na haya.

Unadhani Geofrey Sawaya na mifuko yakeya fedha alitumwa na Wapgani?

Mohamed
 
Hii hoja ndugu yangu si yangu bali ni ya kundi lenu mkiongozwa na Mohamed Said. M ohamed Said alisema mgawanyo wa madaraka Tanzania ni kwa wakristo ni 83% na Waislamu ni 17% sisi tukauliza kama ni hivyo hao wengine wasio waislam na wakristo wanawekwa wapi kwenye hizo takwimu?

Kweli hizo ratio ya 83% to 17% ina shortfall but halibadilishi hali halisi ya ofisi za serikalini ambapo majority ya wafanyakazi ni wakristo na waislamu wakiwa wa kutafuta. Hembu fanya survey serikalini utapatwa na mshangao. Kuna taasisi moja ya serikali kwanza sikukuta hata mwislamu nilipoenda kikazi. Kuiingia siku ya kwanza wakanikaribisha na miziki ya kanisani na inapigwa siku nzima ofisini (ni ofisi ya serikali hiyo), na nafahamu fika vijana wa kiislamu wana graduate katika fani hiyo wengi wapo mtaani hawana kazi. Nikajiuliza au pengine hawaombi kazi lakini kuna watu nawafahamu nikawauliza mliomba kazi pale wakanijibu ndio lakini hawakufanikiwa mara 4 wengineo.

Vile vile vyeo humo kazini ni vya kikanisa kwani kuna baba mchungaji, msaidizi wa mchungaji . Nikawa katika mshangao na butwaa bosi anaitwa baba mchungaji, msaidizi wake msaidizi wa baba mchungaji. Wakianza mikutano bwana yesu asifiwe. Hizi taasisi zetu zina mambo ingia uyaone tuna safari ndefu sana mmungu atusaidie. Nikamaliza kazi iliyonipeleka na kuondoka. Hivyo anachokizungumza Mohamed ni kweli na kipo fanya survey utakiona.
 
Kigarama,

Wengine?
Propaganda hizo zimepitwa na wakati humu tuko sisi na nyinyi basi.

Hii kufunika kichwa mwili wote uko nje haisaidii chochote.

Nchi imeachiwa tatizo kubwa sana la udini ulowanyanyasa Waislam kwa miaka tulikabili tatizo hili na tuliondoe.
Wahindu sijui Wapagani sijui nani hawahusiki kabisa na haya.

Unadhani Geofrey Sawaya na mifuko yakeya fedha alitumwa na Wapgani?

Mohamed

Mbona swali ni rahisi tu Mohamed kwa nini unazunguka. Umesema mgawanyo wa madaraka Tanzania kwenye mkutadha wa kidini ni Wakristo 83% na Waislam 17% sisi swali letu ni dogo tu. Tanzania hakuna wenye dini nyingine. Na wao kwenye huo mgawanyo wako wamechukua asilimia ngapi?
Sasa kati yangu mimi na wewe nani anapiga propaganda??
 
Vile vile vyeo humo kazini ni vya kikanisa kwani kuna baba mchungaji, msaidizi wa mchungaji . Nikawa katika mshangao na butwaa bosi anaitwa baba mchungaji, msaidizi wake msaidizi wa baba mchungaji. Wakianza mikutano bwana yesu asifiwe. Hizi taasisi zetu zina mambo ingia uyaone tuna safari ndefu sana mmungu atusaidie. Nikamaliza kazi iliyonipeleka na kuondoka. Hivyo anachokizungumza Mohamed ni kweli na kipo fanya survey utakiona.
kuna mambo mengi ya kujiuliza, hao uliowakuta ofisini walikuhudumia, ulijuaje kama wanaitana "baba mchungaji. Lakini kama ungechunguza sana unaweza kuona labda na kabila lao pia ni moja!!
 
kuna mambo mengi ya kujiuliza, hao uliowakuta ofisini walikuhudumia, ulijuaje kama wanaitana "baba mchungaji. Lakini kama ungechunguza sana unaweza kuona labda na kabila lao pia ni moja!!

Wewe jiulize mengi ila mie ndio niliyaona hivyo na nikawa na mshangao sana. Hata kama wametoka kabila moja what can you explain about kuweka nyimbo za ubeti 12, nyimbo za mapambio na sala ya bikira maria, neno la mungu ofisini . Vile vile kukosekana kwa mwislamu hata mmoja hapo ofisini unaweza kulibainishaje coincidence, lack of skills, favoritism, nepotism or what??? Mwislamu akiweka quran na qassida si mngelipiga makelele mpaka magazetini? NSSF tu mkiona watu wanaenda msikitini kufanya ibada yao ya wajibu mnalalama humu jamvini kila siku. Hizo ndio ofisi za serikali fanya utafiti uyaone.

Sikuwa na haja ya kuyachunguza zaidi kwani sicho kilichonipeleka huko nilienda kwa kazi maalum nikaondoka ya ngoswe nikamuachia ngoswe.
 
Mwambie basi Mohamed yeye mwenyewe aseme kwamba takwimu zake zina "Shortfall" ili wafuasi wake wasizipe "uzito" wowote.

Yes figure ya 83% na 17% ina walakini kwanini basi wewe usianzie hapo katika utafiti wako kuja kumkosoa Mohamed Said. Pengine taarifa alizonazo Mohamed ndio zinasema hivyo sasa fanya utafiti kuzikosoa na vile vile kukosoa anachokisema Mohamed. Kwani kuna tatizo gani? Vile vile hatujamilazana kuhusu Mkwawa nilipotea kidogo nitasoma post zako kuona kama ulijibu maswali yangu au ndio kama wengineo mna beat around the bush.
 
Mbona swali ni rahisi tu Mohamed kwa nini unazunguka. Umesema mgawanyo wa madaraka Tanzania kwenye mkutadha wa kidini ni Wakristo 83% na Waislam 17% sisi swali letu ni dogo tu. Tanzania hakuna wenye dini nyingine. Na wao kwenye huo mgawanyo wako wamechukua asilimia ngapi?
Sasa kati yangu mimi na wewe nani anapiga propaganda??

Kigarama,

Dini zinazoweza kusababisha matatizo ni mbili tu.
Tushughulishwe na haya.

Mohamed
 
Yes figure ya 83% na 17% ina walakini.

Huu "walakini" ndiyo tunataka yeye mwenyewe Mohamed asema kwamba takwimu zake hizi ambazo amekuwa akizunguka ulimwenguni pote akizielezea ni "batili" na kama ni batili basi na hoja yenyewe ni batili pia!! Kama unasema umeshindwa kubeba kitu kwa sababu una mkono mmoja, basi ikija kugundulika kwamba una mikono yote miwili basi hoja yenyewe ya kwa nini umeshindwa kubeba hicho kitu, inakufa kifo cha kawaida (natural death).
 
Kweli hizo ratio ya 83% to 17% ina shortfall but halibadilishi hali halisi ya ofisi za serikalini ambapo majority ya wafanyakazi ni wakristo na waislamu wakiwa wa kutafuta. Hembu fanya survey serikalini utapatwa na mshangao. Kuna taasisi moja ya serikali kwanza sikukuta hata mwislamu nilipoenda kikazi. Kuiingia siku ya kwanza wakanikaribisha na miziki ya kanisani na inapigwa siku nzima ofisini (ni ofisi ya serikali hiyo), na nafahamu fika vijana wa kiislamu wana graduate katika fani hiyo wengi wapo mtaani hawana kazi. Nikajiuliza au pengine hawaombi kazi lakini kuna watu nawafahamu nikawauliza mliomba kazi pale wakanijibu ndio lakini hawakufanikiwa mara 4 wengineo.

Vile vile vyeo humo kazini ni vya kikanisa kwani kuna baba mchungaji, msaidizi wa mchungaji . Nikawa katika mshangao na butwaa bosi anaitwa baba mchungaji, msaidizi wake msaidizi wa baba mchungaji. Wakianza mikutano bwana yesu asifiwe. Hizi taasisi zetu zina mambo ingia uyaone tuna safari ndefu sana mmungu atusaidie. Nikamaliza kazi iliyonipeleka na kuondoka. Hivyo anachokizungumza Mohamed ni kweli na kipo fanya survey utakiona.

Mdondoaji,

Zipo taarifa za uhakika kabisa kuwa kuna nchi rafiki na Tanzania imeasa serikali yetu kuiambia inacheza na moto.

Mohamed
 
Huu "walakini" ndiyo tunataka yeye mwenyewe Mohamed asema kwamba takwimu zake hizi ambazo amekuwa akizunguka ulimwenguni pote akizielezea ni "batili" na kama ni batili basi na hoja yenyewe ni batili pia!! Kama unasema umeshindwa kubeba kitu kwa sababu una mkono mmoja, basi ikija kugundulika kwamba una mikono yote miwili basi hoja yenyewe ya kwa nini umeshindwa kubeba hicho kitu, inakufa kifo cha kawaida (natural death).

Santuri imekwema katika kijishimo.

Mohamed
 
Vile vile hatujamilazana kuhusu Mkwawa nilipotea kidogo nitasoma post zako kuona kama ulijibu maswali yangu au ndio kama wengineo mna beat around the bush.

Hata mimi sijamalizana na Mkwawa, kwani sasa hivi nataka kujua kama Mkwawa alikuwa ni shujaa kweli au alikuwa ni Dikteta wa zama zake. Mkwawa aliua watu wengi sana bila ya sababu. Lakini kuhusu dini yake wenzio walishafunga mjadala wake, na tangu jumatano ile nimepata "ushahidi" mwingi zaidi kuthibitisha kwamba Mkwawa hakuwa na dini. Jamaa alikufa akiwa na miaka 40 tu lakini kwenye utawala wake wa miaka 18 alishaua ndugu zake kwa dazeni!!
 
Back
Top Bottom