Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa


hahaha unakosea walakini haimaanishi ni batili soma vizuri kiswahili. Walakini inaweza kuwa data alizonazo ziko biased, sample ndogo au pengine ni kweli hali iko hivyo serikalini. Sasa wewe unasema hizo taarifa ni batili tupe vigezo vyako na evidence zako!!!!!
 

Santuri imekwema katika kijishimo.

Mohamed

Sheikh maneno yako makali kweli kweli hili limenifanya nicheke sana,

Ni neno alikuwa akilitumia mzee wangu mtu akiwa hana cha kusema.

You made me laugh hahaha!!! Hi ni kali ya siku kwa leo.
 

Santuri imekwema katika kijishimo.

Mohamed
Kijishimo kilichochimbwa na Mohamed Said. Kwani hujasikia Sheikh wangu kwamba "mchimba mashimo huingia mwenyewe?" Hapa (83% Vs17%) ulitega swala lakini umeteguka mguu!!
 

walakini* nm [u-] defect; blemish, fault.(Kar) Kwa mujibu wa Kamausi ya TUKI. Walakini ni hitilafu na kama ni hitilafu basi si kitu sahihi na kama si kitu sahihi hakitegemewi kutoa majibu kamilifu na kwenye hoja majibu yasiyo kamilifu ni BATILI!!
 

Santuri imekwema katika kijishimo.

Mohamed
Siyo kwenye hizo takwimu zako zenye walakini hata katika hili "Santuri imekwama kwenye kijishimo"

NARUDIA KUBANDIKA TENA HILI BANDIKO KWANI SIELEWI NI KWANINI FAIZAFOXY NA MOHAMED SAID HAWATAKI KUNIJIBU SWALI LANGU HILI.

Waislamu wana Nguzo zao tano wanazoziamini kama ndiyo msingi wa dini yao. Kama kweli waislamu wa Tanzania tangu Tanganyika walikuwa wanakandamizwa, ni nguzo ipi kati ya hizi tano ambayo waislam wa Tanzania wanakatazwa kuitimiza na Serikali kwa sababu serikali inadhibitiwa na MfumoKristu?

1. Kushahadia

2. Kuswali swala tano

3. Kufunga

4. Kutoa zaka

5. Kuhiji kwa mwenye uwezo

Kama waislamu wangekuwa wanakandamizwa katika hizo nguzo tano za uislamu ningeelewa hoja za MS. MS na wenzake watuambie ni wapi na ni lini waslamu walikatazwa kwenda kuhiji, kuswali. kufunga kwa Sunnah na Kufunga Ramadhani, kutoa zaka au kushahadia. Sijawahi kuona mfumo wa serikali ukikataza wakristo kusilimu au waislamu kujenga misikiti au kuadhini. Naijua misikiti ambayo iko katikati ya makazi ya watu kwenye mchanganyiko wa wakristo na waislamu na sijawahi kusikia serikali ikikataza waislamu kuadhini kwa sababu 'wanawasumbua" wasio waislamu kwa adhana zao.

Waislamu wanapotaka kwenda Mecca kuhiji hakuna siku walikatazwa kwenda badala yake serikali mara kadhaa imewahi kutoa fedha kusaidia waislamu kwenda kuhiji, sasa hapo waislamu wanakandamizwaje na huo mfumokristu na inakuwaje mfumokristu unashindwa kuzuia waislamu kuhiji, kusilimisha wakristo au kuadhini?

Hivi karibuni serikali si ilishawahi kutoa zaidi ya Shilingi Bilioni 2 kusafirisha mahujaji kwenda Mecca kuhiji? Kanisa lilikuwa wapi kuizuia serikali kutoa fedha hizo??
 
walakini* nm [u-] defect; blemish, fault.(Kar) Kwa mujibu wa Kamausi ya TUKI. Walakini ni hitilafu na kama ni hitilafu basi sisi kitu sahihi na kama si kitu sahihi hakitegemewi kutoa majibu kamilifu na kwenye hoja majibu yasiyo kamilifu ni BATILI!!

Kutokuwa kikamilifu sio batili ndugu ni kwamba kiko limited in information usilazimishe ubatili bure lete evidence kuwa hicho kitu batili . Soma zaidi hapa kutoka Wikitionary inasema walakini ni dosari (limitations). Sasa kama tafiti yake ina dosari katika hizo figures lete zako zilizokamilika tuzisome usilazimishe ubatili kusupport unachokitaka hatuendi hivyo ndugu.

Ufafanuzi kutoka Wiktionary, kamusi iliyo huru
 
Kijishimo kilichochimbwa na Mohamed Said. Kwani hujasikia Sheikh wangu kwamba "mchimba mashimo huingia mwenyewe?" Hapa (83% Vs17%) ulitega swala lakini umeteguka mguu!!

Kigarama,

Wako waloteguka mguu lakini Alhamdulilah si mimi.
Ukitaka kupambana na mie katika haya ule ushibe na uage kwenu.

Wanohusika wako kimya mnajitahidi nyie wachezea pembeni.

Mohamed

 
Sheikh maneno yako makali kweli kweli hili limenifanya nicheke sana,

Ni neno alikuwa akilitumia mzee wangu mtu akiwa hana cha kusema.

You made me laugh hahaha!!! Hi ni kali ya siku kwa leo.

M,

Hiyo mie nimeidondoa kutoka "Conflict and Harmony in Zanzibar" kitabu cha Ali Muhsin Barwani.

Mohamed
 
Sheikh maneno yako makali kweli kweli hili limenifanya nicheke sana,

Ni neno alikuwa akilitumia mzee wangu mtu akiwa hana cha kusema.

You made me laugh hahaha!!! Hi ni kali ya siku kwa leo.
Huku ni kujifariji...na ndugu zangu kwa kweli mnaweza.
Nyerere alishawahi kusema kuna wajinga na wapumbavu...! Ujinga una nafuu kwa sababu ni mtu kutojua kitu ila ukieleweshwa utajua na ujinga utatoka. Wapumbavu ndiyo kama nyinyi....na hakika mtabaki wapumbavu siku zote.
Majitu yameshindwa hata kuunda chombo/taasisi inayowawakilisha waislam wote hata baada ya miaka 50 ya uhuru....kisa ? ..utasikia Kanisa lina mkono wake. Nyinyi ni watu wa aina gani kila kitu ni Kanisa tu?
Kuna shule moja iko maeneo yenye waislam wengi imefungwa...kisa?hakuna mwamko wa elimu ...hakuna wanafunzi...! ila utasikia kuna mpumbavu mmoja atakuambia Kanisa lina mkono wake. Mmejipandikiza wenyewe Inferiority Complex mbaya sana...!
 

Kigarama,

Wako waloteguka mguu lakini Alhamdulilah si mimi.
Ukitaka kupambana na mie katika haya ule ushibe na uage kwenu.

Wanohusika wako kimya mnajitahidi nyie wachezea pembeni.

Mohamed

Huu ndiyo upumbavu tunaousema. Mzee unazeeka vibaya sana!
 

Asante sana kwa kututukana kwani upumbavu ni tusi ila ujinga sio tusi. Very well tukirudi katika mada kwani yanayosemwa hapa ni uongo? Nani amewasambaratisha waislamu? In whose interest waislamu wamesambaratika kwa mujibu wa namna unavyofahamu wewe? Maandiko yako yamejaa dharau kebehi na udini na ndio tunakuja pale pale kati yetu sie na nyie nani wadini? Waislamu wengi wanasoma na wamesoma dude check your facts right ila wengi waliosoma hawana kazi ila wamejiajiri wenyewe au wameajiriwa katika private sector. Serikali ni mahsusi kwa wakristo na facts zipo ukitoka msome vizuri Mohamed Said.

Wakati wewe ukiwaaccuse waislamu being inferior perhaps you should asked yourself why? Are they second class citizen in their own country? Jibu unalo mwenyewe.
 
Tatizo lenu ndiyo hilo...mimi binafsi nimesoma na waislam wengi na wengi wao leo hii wamefanikiwa ile mbaya...iwe serikalini au kwenye private sectors..! kama kukosa ajira siyo vijana wa kiislam tu ..ni vijana wengi wa tanzania wamekosa ajira...!
Kwenye issue ya kusoma ni kwamba waislam wengi wamesoma lakini ukweli ni kwamba maeneo mengi yenye idadi kubwa ya waislam hawana mwamko na elimu..e.g watu wa kusini , pwani n.k ....huo ndiyo ukweli wenyewe na wala Kanisa halina mkono wake!

MDONDOAJI, TAASISI GANI INAWAKILISHA SAUTI YA WAISLAM WOTE?? ...BAKWATA???
 

this is what we call gogovivu material
 

Sweke34,

Ushahamaki unatokwa na matusi.
Sisi tushakuwa "majitu."

Sisi tuna "inferiority complex."ma?
Nani kasema?

Hivi wewe unavyosoma nyuzi zetu sie tumeelekea kuwa na "complex?"
Hebu pitia nyuzi zangu na niambie wapi na kitu gani kimekupa hisia hiyo.

Huwezi kutupa sisi maneno ya Nyerere.

Nyerere kasema hiki Nyerere kasema kile.
Mie?

Wewe ushafanya uchunguzi kwa Waislam ujue hivi sasa ana hadhi gani?
Uliza.

Sisi tumeshindwa kuunda chombo?
Kwani wewe huudhurii darsa zangu?

Unadhani sisi wajinga turudi kwenye enzi ya chombo kimoja kihujumiwe kirahisi.
Wewe ulipata kunijua mimi kama kiongozi wa Waislam kwa takriban miaka 20?

Basi tuko wengi na huwezi kuwajua utaona mambo yanakwenda tu.

East African Muslim Welfare Society (EAMWS) aliunda nani?
Al Jamiatul Islamiyya aliunda nani?

Au hujui kuwa ilihujumiwa na Nyerere akiwatuma akina Geofrey Sawaya mikoani kutoa milungura ili BAKWATA ipate viongozi?
Au hujui Rashid Kayugwa wa Usalama wa Taifa ndiyo alikuwa kiongozi wa fitna ile?
Au hujui Benjamin Mkapa na Martin Kiama ndiyo walikuwa wakitumia vyombo vya habari vya taifa kuipiga vita EAMWS?

Mie hapa nazungumza na watu wenye akili na tafakuri.
Wanatambua kwa dhati ya nafsi yao kuwa nisemayo yote ni kweli.
Haya yote ni katika historia ya Waislam wa Tanganyika.

Waambie wajitokeze wahusika wafanye mnakasha na mimi.
Jina langu si unaliona hapo chini?
Kitabu changu si hicho leo ndicho kinachotamba katika histroria ya uhuru wa Tanganyika.

Unatusimanga kwa shule mnazoziendesha kwa hela ya serikali (MoU)?
Huna hata soni kidogo ndugu yangu.

Unamsimanga yatima asiye na baba wala mama kwa nini siku ya Eid hana nguo za kuvaa akenda Mnazi Mmoja kucheza kama wenzake?
Hivyo si ndiyo unamkumbusha wazazi wake waliotangulia mbele ya haki?

Unategemea huyu mtoto atakujibu kuwa mie yatima sina wa kuninunulia nguo?
Sana sana atajiinamia alie kwa huzuni.

Wajerumani Manazi waliwaweka Wayahudi katika "ghetto" Poland Vita Kuu ya Pili.
Ghetto hakuna maji, choo wala umeme.

Kisha Wajerumani haohao wakawa wanawasema Wayahudi kuwa wachafu.

Nimetoa ushahidi wote jinsi Nyerere alivyotumia nafasi yake kama rais kutuhujumu Waislam tusiwe na maendeleo, tusijenge shule wala Chuo Kikuu halafu nawe unakuja na hoja hiyo hiyo mbona Waislam hamna hiki hamna kile...

Mohamed
 
WC,

ndio maana yya utafiti huwezi tafiti kila kitu. ...........
Watendee Haki hao wazee na kutoa taarifa na historia iliyofichika ya hao wazee kwa faida ya waTz wote.

Kila la kheir


Maneno safi kabisa.....with an open mind Brother MS inabidi aelewe hili bila kubagua......kwani yeye ni gwiji.........


absolutely right......hakuna anyepinga Brother MS kuandika yaliyoachwa katika historia.......na tunapenda kuona wengine wafanye hivyo........... kinachogomba......ni baadhi ya maelezo ya MS kuwa historia yake ndio kamili......na kwamba isingekamilika bila ya wazee wake wa gerezani.........

na wengine wanaosema kitabu chake lazima kijibiwe kwa kitabu......hii naiita NONSENSE

mtu anayesema JKN hakuwa na fadhila kwa Waislamu ni MPUUZI

Kila mtu anataka/wish historia iandikwe kwa ukamilifu wake, mamluki/wasaliti/wazalendo/mabaradhuli nk nk wote watajwe
 

Sweke,

Ndugu yangu punguza udini na ujinga ulionao kichwani. Kwanza umewasifu waislamu wamefanikiwa ile mbaya tena serikali na private (kuonyesha ulivyo mpuuzi). Hapo ukaja kusema maeneo mengi waliyo waislamu hawana mwamko wa elimu sasa nikuulize walifanikiwa vp hadi wakaweza na na mafanikio ile mbaya kwa mujibu unavyoona wewe?

Hapo hapo ukaconclude kuwa kukosekana kwa mwako wa elimu kwa waislamu kanisa halina mkono wake hata kidogo . Swali una evidence to justify your conclusion? Bakwata mie nishasema tangu zamani is defunct body iliyowekwa na kutetewa na serikali. Nimekupatieni papers za Dr Issa Ziddy na wengineo. Vile vile Mohamed Said ameyazungumzia hayo. jiulizeni nyie chombo gani ambacho hakikubaliwi na waislamu kiwe kinawakilisha waislamu?

Hujioni kama wewe ni mjinga aisee!
 

Unafikiria academic literature inaandikwaje? Lazima kazi unayoifanya kuna watu watatokea kuja kukukosoa ijapokuwa na wewe unakuwa umeongezea jambo katika historia. Sheikh Mohamed kaandika kuwakosoa wazee wa kigamboni kuwa Tanu haikuanzishwa na Nyerere bali Sykes. Vile kawakosoa kuwa waislamu hawako hivi leo kuna force behind it inayofanya iwe hivyo na kanisa katoliki linajulikana duniani nzima kwa uchochezi na rafu mbaya (mnajua aliyeanzisha American Civil War and Spanish civil war???? Rwanda genocide na vita vingi? someni historia mtajua vizuri). Sasa kama nyie hamuikubali hilo fanyeni utafiti tutawasoma na kuwajibu kwa utafiti mwengine. Ndio historia inaandikwa hivyo mkuu.

Kwenye historia hakuna zidumu fikra za mwenyekiti mtazamo wako makes no sense to me at all nenda nao katika siasa ila katika historia hatuangalii hivyo hata siku moja.
 
Mkuu Kikwebo, ashakumu si matusi, amakweli nyani haoni kundule - unawezaje kumtuhumu mwanamijiji kwamba anatumia ID mbalimbali kama vile Nguruvi3,Wild Card,Mag3 et.al na ukashindwa kumutuhumu mzee Mohamed Said kuwa naye anatumia ID ya ritz, Faiza,Barubaru na Mdondoaji kujenga na kueneza hisia zake za chuki kwa kutumia imani ya dini ya kiislam? Lakini sikushangai hata kidogo kwa sababu sumu ya ubaguzi ya mzee Mohamed Said imekutafuna kiasi kwamba husikii wala huambiwi jingine. Ubaya nikwamba ubaguzi wa kidini umemtafuna hata yeye mwenyewe mzee Mohamed kiasi kwamba ameanza kuwabagua hata waislam wenzake, kwake yeye waislam ni wale tu wanao shabikia mihadhara yake na wale wanao hudhuria sherehe za idd chini ya BAKWATA hao kwake sio wenyewe, kwani hao wapo kula wali na chai ya ikulu. Hii ndio taabu ya ubaguzi.
 
Mkuu Barubaru, shukurani kwa darsa ulilo nipa nakuomba usinichoke, nini kinakwamisha masheikh wapande hizo mbili wasikae pamoja na kulitatua tatizo?Huoni chuki na ubaguzi unaopandikizwa na mzee Mohamed unazidi kuwagawa waislam?Kama masheikh wa BAKWATA wanadharauliwa hivyo kwamba wao sio masheikh wa wawaislam sasa kumbe ni wawakristo au wasisi "atheists"? Unasababu ipi kunishutumu kwamba nachagua maneno mawili kukukosoa, wakati wewe ndie unae wabagua waislam wenzako?
 

Santuri imekwema katika kijishimo.

Mohamed

MS,

"Kijishimo" kinachokwamisha santuri umechimba wewe, fukia twendelee. Angalia mzunguko huu,
Hapa unachimba "kijishimo"

Mohamed Said said:
Sweke34,

Mgao wa madaraka baina ya Waislam na Wakrsto ni 83% kwa 17%.
Huu ndiyo mfumokristo tunaohoji.

Mohamed
Wanaomeza bila kutafuna wanaitikia "chorus"

FaizaFoxy said:
Hilo kundi inafaa lienziwe na liheshimiwe kwani lilikuwa na muono. Leo wangesikilizwa tusingekuwa hapa tulipo. 83% vs 17%
FaizaFoxy said:
Taifa linaloongozwa kwa kutumia "gospel of jesus christ" kama alivyosema Nyerere?
Taifa la 83% vs 17%?
FaizaFoxy said:
Kwa kuhakikisha 83% vs 17% inadumu

Unaulizwa swali juu ya "hisabati" hii ya "asilimia"


Jibu lake..

Mohamed Said said:
Sweke34,

Hiyo "religious distribution" isikutaabishe.

Mohamed

Hapa mtaalamu mmoja anakiri…

Mdondoaji said:
Kweli hizo ratio ya 83% to 17% ina shortfall but halibadilishi hali halisi ya ofisi za serikalini ambapo majority ya wafanyakazi ni wakristo na waislamu wakiwa wa kutafuta.

Anasisitiza tena…

Mdondoaji said:
Yes figure ya 83% na 17% ina walakini…

Ungeweza kusahihisha hii argument ambayo imeonesha wazi upungufu lakini wewe unachimba "kijishimo" kingine kwa kuwanyima "Utanzania" wenzetu wasiokuwa Waislamu au Wakristo…


Niliuliza mzee wetu Kingunge N. Mwiru dini yake ni ipi? Ukafunika. Ubaguzi unaendelea…

Mohamed Said said:
Kigarama,

Dini zinazoweza kusababisha matatizo ni mbili tu.
Tushughulishwe na haya.

Mohamed

Sisi na ninyi? Kwani tunapochangia mada hapa tunajitambulisha dini zetu? Unachimba "vijishimo" alafu unailalamikia santuri!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…