Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Ile kwamba Hanga alilawitiwa gerezani kabla ya kifo chake, lawama yote ni kwa JKN yote sababu ya "Muungano" ambao ulikuwa ni "hirizi tosha ya kumkinga Karume?" Swali ni jee, "hirizi" in what sense? Hapa ni wazi Mwandishi anachukulia kwamba presumed super-natural effects za "hirizi" are real and effective, and could be taken in a literal sense.
 
Duh mkuu wangu bado unaliendeleza barza.... Heee ama kweli wajua kuuza kitabu... Kwa hili la Hanga nakuomba sana tena sana funga safari nenda Zanzibar mtafute Nassoro Moyo atakueleza kwa ufasaha kilichotokea (kama atapenda) maana yeye na marehemu H. Hanga walikuwa kundi moja..

Mkandara,

Labda nikuambie wewe ndiye ufunge safari uende Zanzibar ukamuulize Mzee Moyo unamjuaje Mohamed Said?

Huenda labda vilevile hujui mimi nilikuwa msaidizi wa Dr Harith Ghassany mwandishi wa "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru."

Nadhani unakifahamu kitabu hiki.

Mohamed
 
Duh mkuu wangu bado unaliendeleza barza.... Heee ama kweli wajua kuuza kitabu... Kwa hili la Hanga nakuomba sana tena sana funga safari nenda Zanzibar mtafute Nassoro Moyo atakueleza kwa ufasaha kilichotokea (kama atapenda) maana yeye na marehemu H. Hanga walikuwa kundi moja..

Mkandara,

Labda wewe ndiye wa kufunga safari uende Unguja kumuuliza Mzee Moyo ananifahamuje?

Mohamed
 
Ile kwamba Hanga alilawitiwa gerezani kabla ya kifo chake, lawama yote ni kwa JKN yote sababu ya "Muungano" ambao ulikuwa ni "hirizi tosha ya kumkinga Karume?" Swali ni jee, "hirizi" in what sense? Hapa ni wazi Mwandishi anachukulia kwamba presumed super-natural effects za "hirizi" are real and effective, and could be taken in a literal sense.

Ndjabu,

Sijui unataka kufanikiwa katika nini kwa hiyo post.

Lakini ili unielewe mimi na umuelewe Kassim Hanga tuingie katika darsa:

Mama yangu mdogo Bi Mtoro bint Mohamed alikuwa akiishi Mtaa wa Gogo. Huu nikatika mitaa midogo sana ya Dar es Salaam hazikuzidi nyumba ishirini hivi.Bendi maarufu ya Kilwa Jazz ilikuwa kwenye kona ya Mtaa wa Gogo na Mchikichi kwenyenyumba ya mama yake rafiki yangu Abdu Kigunya. Mbele ya nyumba yaoikifika kama saa tisa, kumi, laasiri, wazeewalikuwa wanaweka jamvi pale, wanacheza bao. Sasa hivi ukenda pamejengwamajumba ya maghorofa nyumba ya mama yake Abdul Kigunya imetoweka. Abdallah Kassim Hanga akija pale mtaa wa Gogo,kona na Mtaa wa Mchikichi kucheza bao na watu wa kawaida sana wazee wa palemtaani. Hapa ndipo kwa mara ya kwanza nilipomuona Abdallah Kassim Hanga kwamara ya kwanza. Hata hivyo katika kusoma magazeti yale ya zamani "Ngurumo" na"Mwafrika" wakati ule wa mapinduzi ya Zanzibar picha ya Kassim Hanga nawanamapinduzi wengine kama Abdulrahman Babu, Abeid Amani Karume picha zaozilikuwa maarufu katika magazeti hayo. Siku zote nikipita pale nilikuwa nikimuona Hanga kaliinamia bao "anasafiri,""anatakata" kama wacheza bao wanavyopenda kusema. Kwa ajili hii Hanga akawa mtuambae popote nitakapomuona nitamtambua. Wakati ule Hanga alikuwa waziri katikaserikali ya muungano na mawaziri wakitembeya na magari meusi ya Kiingereza yakiitwa"Humber." Sikumbuki kumuona Hanga hata siku kuja pale kwenye baraza yake nagari. Siku zikapita mapinduzi yanaendelea lakini mara moja moja mimi nikisikiababa yangu akizungumza na rafiki zake kutoka Unguja kwa sauti ya chini kunong'onakuhusu baadhi ya rafiki zake kuwa wametiwa gerezani Unguja na wengine wameuawa.Mimi mdogo wala sijui hayo mapinduzi kitu gani. Ila nakumbuka mimi na rafikizangu tulijipanga Barabara ya Uhuru siku ile Karume na Nyerere walipokuwakatika gari moja wamesimama wanawapungia mkono wananchi.Nyerere alikuwa ametokaUwanja wa Ndege kumpokea Karume. Hii ni ile siku Karume alikuja Dar es Salaam kuunganishaTanganyika na Zanzibar kuwa nchi moja iliyokuja kujulikana kama Tanzania. Sasa siku moja pale Mnazi Mmoja ndipo ulipokuwa uwanja wetu wa kuchezampira siku hiyo tumeona toka asubuhi pilikapilika panafungwa vipaza sauti nawatu wanashughulika kuweka maturubai. Kumbe siku hiyo palikuwa na mkutano wahadhara. Mkutano huu ulikuwa nyuma ya Ukumbi wa Arnautoglo ambako kulikuwa na barya NUTA ikijulikana kama "Kibarua Bar." Nilikuwa sijamuona Hanga kwa muda mrefuna kisa chake ni kuwa tayari nilikuwa nimeshaanza sekondari na sasa kuhanjakwenda kwa mama yangu mdogo kila siku kukawa kumepungua kiasi. Lakini bado nikijana mdogo. Nyimbo za TANU Youth League za Makongoro na Mwinamila na ngoma yaKinyamwezi "Hiyari ya Moyo" zimeshaanza kabla ya mkutano kuvutia watu na kamakawaida ya watoto ikawa lazima nasi tujumuike kwenda kusikiliza. Mwinamila nikama baba yetu maana mwanae mmoja akiitwa Miraji ni golikipa wa timu yetu yampira, kisha katika wale akina mama wachezaji kulikuwa na bibi mmoja akija sananyumbani kwetu. Nafika pale kwenye mkutano namuona Hanga kakalishwa kwenye kitilakini kadhoofu, si yule Hanga niliyemzoea kumuona takriban miaka mitatuiliyopita akicheza bao pale Mtaa wa Gogo. Kumbe alikuwa jela. Sasa kumbe sikuile Hanga katolewa jela Ukonga kaletwa pale mkutanoni kuja kuadhiriwa naNyerere. Namuona Hanga mimi kwa macho yangu ya kitoto na miwaniyake ile. Hanga alikuwa mwembamba na mrefu na alikuwa na thick hair. Alikuwa mtu mwenye kupendeza. Kaja pale na usoulionyong'onyeya. Lakini sisi watoto hatujui kinachotendeka. Watoto waKiswahili miaka 14, 15, 16, ni wadogo. Hatujui kinatendeka nini. Lakini miminajua kuwa yule pale Hanga namuona kuwa ni mfungwa maana sasa pale uwanjaniwatu weshaanza kumzungumza. Hanga miwani iko puani uso umemparama kama jiwe la kiama, madevu yamemjaa. Anaadhiriwa! Juakali linampiga vizuri. Kwa pale kukaa na kajiinamia nilijuwa kuwa mambo simazuri upande wake. Huruma ikawa inanijia katika moyo wangu lau kama simjui kwakaribu lakini Hanga akija kwetu kucheza bao na wazee wangu. Nyerere yuko juuya kilinge anazungumza kwa madaha nakujiamini na wote wanasikiliza. Katika watu waliomzunguka Hanga namuona HamzaAziz na Mzee Omari Londo. Hawa wote ni watu maarufu mimi nanyanyukia Gerezani,Dar es Salaam nawaona. Nyerere alikuwa ni muongeaji ana kipaji hicho. Nilipokujakuwa mtu mzima na kuelewa mambo nikajajua kuwa kuna kumuuwa mtu kiungwana. Sikuile pale Mnazi Mmoja Nyerere alikuwa keshammaliza Hanga. Siku ile Nyererealikuwa ansoma khitma ya Hanga. Nakumbuka tokeo moja wakati Nyerere anahutubiaanamuonyesha kidole Hanga anamtuniza anasema "Hili, hili, hili. Hana lolote.Hakuna lolote anaweza kufanya huyu. Afadhali huyu mwanzake (Nyerere ananyooshakidole kwa Babu)." Dunia nin ndogo sana. Miaka mingi baadae nimekutana naBabu, London nikashindanae siku nzima pamoja na Ahmed Rajab tulikuwa na safariya kwenda Brixton. Babu alikuwa kachoka na mguu mmoja anavuta. Afya yake kwakweli haikuwa nzuri. Nikakumbuka ule mkutano wa Mnazi Mmoja miaka mingi yanyuma. Turudi kwa Hanga. Ukitizama kwenye "Tanganyika Standard," wakati ulebado halijakuchukuliwa na serikali, wakati ule mhariri alikuwa Muingereza,Brandon Grimshaw picha ya Hanga imetolewa katika gazeti. Mimi kwa jicho langu nimeona picha ile yaHanga alipokuwa pale mkutanoni kwa sababu baba yangu mimi akinunua TanganyikaStandard kila siku. Picha ya Hanga iko mbele na madevu na miwani yake. Si mimitu, watu wengi wanakumbuka hiki kisa. Baba yangu hakuwa mwanasiasa hata wakugusia jambo lakini alikuwa na marafiki wengi Unguja. Kati ya marafiki zakezake walikuwa Jaha Ubwa na Abdulaziz Twala.. Wakitembeleana zamani wakati wa Pasakakwenye siku za "sports." Baba yangu alikuwa mpenzi wa "Black Birds" bendi yawatoto wa mjini katika miaka ya 1950. Black Birds ikienda Unguja nadhani kulendo walikofanya urafiki na hawa jamaa wa Zanzibar. Picha yangu mimi yaMzanzibari, wakija nyumbani kwetu, unamuamkia na suala la kwanza lilikuwa "Weweumeshahitimu?." (Maana yake ushamaliza mashaf). Nakumbuka ule ulimbwende wa wakezao wakijanao nyumbani kwetu, yalemavazi, mabuibui, uturi ule, vile vyakula wakiandaa nyumbani pale. Hii ndopicha yangu ya Mzanzibari wakati mimi nakua . Palikuwa na picha ukutani ya marahemu baba yangu na kinaJaha Ubwa. Ile picha ghafla ikatoweka pale ukutani. Ikawa haionekani tena. Baadaenikajafahamu kuwa baba aliiondoa pale alipopata taarifa ya vifo vya rafiki zakewameuliwa na serikali ya mapinduzi. Nakumbuka baba alikuwa akizungumza habariza akina Twala alikuwa akinong'ona. Nahisi mzee alikuwa ana hofu. Kunong'ona nidalili ya hofu, wasiwasi, na woga. Mimi juu ya udogo wangu nilihisi kuna kitukibaya kimetendeka. Lakini baba lazima aulize hatima ya familia ya rafiki zake .Vipi wake zao, watoto vipi? Hata hivyo hawezi kusema kwa sauti. Miaka ikapitana mimi nikawa mtu mzima na ninauelewa wa dunia kwa kiasi changu. Nikajakufahamiana na Ali Nabwa na tukawa marafiki wakubwa. Hapo ndipo nilipopatahistoria ya Zanzibar na mapinduzi kwa undani wake. Alinieleza mauajiyaliyotokea Zanzibar. Nikamwambia mimi baba yangu alikuwa ana akifahamiana naakina Twala na Jaha Ubwa. Alishangaa lakini taarifa zile zikamfanya awe karibuna mimi na yeye akaanza kunifungulia kifua chake kunieleza aliyoyashuhudiaZanzibar baada ya kuuliwa Karume mwaka 1972. Hapo ndipo aliponifunulia mengikuhusu mauaji yaliyotokea Zanzibar baada ya mapinduzi. Nilijuabaadaye sana kuwa kumbe na yeye Nabwa alikuwa ametoka jela alikufungwa baada yakifo cha Karume. Lakini kubwa katika historia ya Hanga ni kuwa yeye ndiye alikuwa kinara wa mapinduziya Zanzibar. Kuwa Hanga ndiye aliyekuwa kinara wa mapinduzi hili sasa baada yakutoka kitabu cha Dr. Harith Ghassany "Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru"Aliyodhihirisha Dr Ghassany katika kitabu kile sasa si shida kuambua kuwakinara wa mapinduzi alikuwa Hanga lau kama hatajwi kwa sifa hiyo katikahistoria ya Zanzibar. kahili si jambolenye shaka tena. Dunia hakika ni ndogo sana na binadamu hawezi kujua kadar.Nilijikuta ghafla bila kutegemea mimi ni mtafiti msaidizi wa Dr Harith Ghassanywakati anakuja Tanga kutoka Oman kutafiti kambi za Wamakonde wakata mkongewalikoshiriki katika mapinduzi ya Zanzibar. Kitabu hiki kimeweka wazi mengi ambayo hayakuwa yakifahamika kuhusumapinduzi ya Zanzibar. Hapa ndipo sasa nilipoanza kurudisha fikra zangu nakumbukumbu za Hanga upya kama nilivyokuwa namuona nilipokuwa kijana mdogo. KilaDr Ghassany alipokuwa akinifunulia aliyokuwa anayajua kuhusu mapinduzi ndivyonilivyozidi kupigwa na butwaa na mshangao mkubwa. Kumbe ni Hanga wala si Karumeau Umma Party ndiyo aliyepanga mapinduzi akiasidiwa na Oscar Kambona, VictorMkello na serikali ya Tanganyika. Kumbe Wamakonde walivushwa kwenda kupinduaserikali ya Mohamed Shamte, Kumbe si Hamada aliyemuua Karume… Ikiwa mipango yote ya mapinduzi kaifanya Hanganasjisemea moyoni, Hanga hatoweza kuutua mzigo wa roho zilizopotea katikamapinduzi hayo. Ikawa sasa najisemea mwenyewe kimoyomoyo ikiwa Hanga atalaumiwakwa vifo vya maelfu ya Wazanzibari waliouliwa wakati wa mapinduzi, nanialaumiwe kwa mauti yaliomfika yeye Hanga tena kwa kuuliwa kishenzi kwani hapananeno zaidi ya hilo linaloweza kutosheleza kuelezea jinsi Hanga alivyouliwa. Nilipofikahapa nikawa sasa nayatazama mauaji ya Hanga kwa sura nyingine kabisa ilikuwakama kichekesho, maajabu au kioja cha aina yake. Kwa wale waliouliwa katikamapinduzi waliopoteza roho na kutangulia mbele ya haki yao yalikuwa yamekwisha.Lakini kwa wale wajane na mayatima waliobakia nyuma na kuhangaika, kifo chaHanga na wenzake katika wale waliofanikisha mapinduzi, kuuliwa kwao kulikuwamiujiza ya aina yake, uchawi usioelezeka nani fundi wake. Ilikuwa sasa vigumukueleza. Ingeeleweka vyema endapo kisasi cha kuitoa roho ya Hanga kingetimizwakwa mikono ya maadui zake waliopinduliwa. Umauti haukumfika Hanga namna hiyo. Wale wajanena mayatima walililipiziwa kisasi na watu waliokuwa maadui wakubwa wa haowaliopinduliwa. Vipi Hanga kiongozi mkuu wa mapinduzi aje kuwa adui wamapinduzi yenyewe kiasi cha kuwa hukumu ya kumtosheleza haikuwa kifo tu balikifo cha kishenzi? Nilikaa chini na kuwaza fikra za Hanga zilikuwaje palealipokuwa peke yake ndani ya selo Ukonga Prison…usiku ukimpita bila ya hatalepe la usingizi akiwaza yanayomkabili. Nini kilikuwa kikimpitikia katikaubongo wake wakati wauaji wake walipomtoa katika selo yake na yeye akawakabiliilhali akijua kuwa walikuwa wamekuja kuitoa roho yake. Fikra yake ilikwendawapi? Ilikwenda kwa Sultan Jamshid bin Abdullah na Masultani wengine waliopitaambao wameiaga dunia mikono yaoikiwa haina damu, au kwa Abeid Amani Karume aliyeingia madarakani kwa mapangaya Wamakonde wakata mkonge kutoka kambi ya Sakura na kijiji cha Kipumbwi -Tanga? Fikra ya Hanga ilielekea wapi? Kwa Nyerere aliyemsaliti?Hakika ni wazi Hanga hakutegemea mapinduzi aliyoyaasisiyangemgeukia na kuwa sababu ya yeye kutolewa roho kwa kuuliwa kishenzi. Jambola kusikitisha ni kuwa hadi pale alipokamatwa na kuwekwa jela Ukonga nakufikishwa mbele ya mkutano wa hadhara na kuadhiriwa na Nyerere tayari alikuwakeshapoteza kila kitu achilia mbali dira ya mapinduzi aliyokusudia ingeongozaZanzibar. Hanga hakuwa kamwe na uwezo wa kumfanya Karume lolote kwani Karumetayari alikuwa chini ya mbawa za Nyerere, ngome ambayo Hanga asingewezakuitikisa achalia mbali kuisogelea na kuibomoa. Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar ilikuwa hirizi tosha ya kumkingaKarume.Katika mkasa wa kuuliwa kwaHanga ndipo msemaji mmoja akasema, "Maiti toka makaburini mwao walionyeshaujuzi wa kufanya miujiza na uchawi wao kwani laiti kifo cha Hangakingesababishwa na wale waliyopinduliwa kisasi chake kingekuwa cha kutisha.Ilibidi Hanga kwa miujiza ya maiti zile auliwe na wale wale aliowawekamadarakani watu ambao hapakuwepo na sababu ya wao kumuona adui." Halikudondokachozi kwa kifo cha Hanga. Kila aliyepata mnong'ono wa kuuliwa kwake alikuwakimya kama vile ile taarifa ya kifo haimuhusu." Hakika dunia inazunguka.

Mohamed
 
Hivi huyu Mag3 alishaelezea ile Historia yake ya makabila 50 ya Mara kudai Uhuru?

FF,

Mag3 bado hajaeleza habari za Musoma.
Mie bado nazisubiri kwa hamu.

Imekuwa bora umemkumbusha.

Mohamed

PS: Bi Faiza ukumbi umepooza we miss you plenty. MS
 
FF,

Mag3 bado hajaeleza habari za Musoma.
Mie bado nazisubiri kwa hamu.

Imekuwa bora umemkumbusha.

Mohamed

PS: Bi Faiza ukumbi umepooza we miss you plenty. MS

Nipo ndugu yangu, nilipigwa ban nikawa sionekani lakini napita napita humu kupata darsa, tuko pamoja.
 
Mohamed Said,

..tuhuma dhidi ya Kassim Hanga zilikuwa ni nini?

..unakumbuka ni tuhuma gani Nyerere alizitoa dhidi ya Hanga kwenye mkutano wa hadhara?

..Kwanini Nyerere hakumuacha huku bara kama ilivyokuwa kwa Abdulrahman Babu?

..yuko Col.Mahfudhi naye alikuwa anatakiwa Zanzibar lakini akaishia huku Bara, na baadaye akawa assigned kijeshi Mozambique.

..nauliza haya maswali kwasababu style ya Nyerere ilikuwa siyo kuua. Yeye kama alikuwa hakutaki basi alikutupa kizuizini kama ilivyotokea kwa kina Christopher Kassanga Tumbo, na Joseph Kassela Bantu, ambao walikaa kizuizini kwa miaka 20+.
 
Mohamed Said,

..tuhuma dhidi ya Kassim Hanga zilikuwa ni nini?

..unakumbuka ni tuhuma gani Nyerere alizitoa dhidi ya Hanga kwenye mkutano wa hadhara?

..Kwanini Nyerere hakumuacha huku bara kama ilivyokuwa kwa Abdulrahman Babu?

..yuko Col.Mahfudhi naye alikuwa anatakiwa Zanzibar lakini akaishia huku Bara, na baadaye akawa assigned kijeshi Mozambique.

..nauliza haya maswali kwasababu style ya Nyerere ilikuwa siyo kuua. Yeye kama alikuwa hakutaki basi alikutupa kizuizini kama ilivyotokea kwa kina Christopher Kassanga Tumbo, na Joseph Kassela Bantu, ambao walikaa kizuizini kwa miaka 20+.

JK,
Nakushauri ukisome kitabu cha Dr Harith Ghassany "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru" utapata yote humo ndani.

Mohamed
 
Sheikh Mohamed Said,

..Thanx.

..nimesoma kile kingine "kuusuta uongo..."

..there r very sad things that have been reported in the book.

..tatizo ni kukosekana kwa ujasiri miongoni mwa wa-Zenj kukubali kwamba tatizo linaanza na wao wenyewe.

..in the end mwandishi anamtupia lawama zote Mwalimu Nyerere.

..the author is even claiming that there was no racism in Zanzibar!!!

..sasa hiki kitabu cha Ghassany kina lipi jipya ambalo halijaripotiwa kule kwenye "kuusuta uongo..."?
 
Sheikh Mohamed Said,

..Thanx.

..nimesoma kile kingine "kuusuta uongo..."

..there r very sad things that have been reported in the book.

..tatizo ni kukosekana kwa ujasiri miongoni mwa wa-Zenj kukubali kwamba tatizo linaanza na wao wenyewe.

..in the end mwandishi anamtupia lawama zote Mwalimu Nyerere.

..the author is even claiming that there was no racism in Zanzibar!!!

..sasa hiki kitabu cha Ghassany kina lipi jipya ambalo halijaripotiwa kule kwenye "kuusuta uongo..."?

JK,

Utajua Insha Allah ukikisoma kitabu.

Mohamed
 
Kitu kimoja nilicho na hakika nacho kwa asilimia 100% ni kwamba wale wote wenye mapenzi ya kweli kwa taifa letu la Tanzania wanasita sana kuchangia hii hoja inayofinyangwafinyangwa na huyu anayejiita Mohamed Said. Bila kumung'unya maneno nayaita madai ya Mohamed Said la kutoa elimu ya historia ya kweli ni porojo hatari iliyojaa uchochezi ambayo lengo lake hasa ni kuleta uhasama wa kidini miongoni mwa wananchi. Sijui anachotegemea kufaidika nacho kwa kupanda hii mbegu ya hatari ambayo nina hakika mtu kama Mohamed Said anajua fika madhara yake.

Mohamed Said ni kama kipofu ambaye baada ya kusimuliwa na wazee kwamba tembo ni mnyama mkubwa kuliko wanyama wengi anapata nafasi ya kumpapasa tembo. Kwa bahati mbaya anaupapasa mguu wa tembo na si mwili wote halafu katika imani yake anadai anao uwezo wa kutoa somo kuhusu umbo la mnyama tembo na ushuhuda wake, kuwa tembo ni kama gogo la mti mkubwa, ndio ukweli na anayesema tofauti hajui kitu. Watu wote wanaolalamikiwa na Mohamed Said kuwa walisahauliwa, wengi wao walikuwa wakazi wa Dar es Salaam eneo la Gerezani.

Kabla ya uhuru Tanganyika iligawanywa katika majimbo makuu manane na katika majimbo yote hayo, jimbo la pwani kwa ujumla lilikuwa moja ya majimbo yaliyokuwa nyuma kimaendeleo kiuchumi, kielimu na kisiasa na hiyo ni licha ya kuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni yalikuwa Dar es Salaam. TAA ilianzishwa na watumishi wa serikali (civil servants) na kwa wakati wote kazi kubwa ya TAA ilikuwa ni kulalamika ikidai haki ya wafanyakazi bila upendeleo na hasa ubaguzi wa rangi katila utumishi kubwa ukiwa uonevu dhidi ya wazawa, mtu mweusi.

Jimbo la Ziwa ni moja ya majimbo yaliyokuwa mbele kiuchumi, kielimu na kisiasa na kama kuna kitu kinaweza kudaiwa kuwa kilisahaulika katika harakati ya kupigania uhuru ni mchango wa Jimbo la Ziwa (Bukoba, Mwanza, Mara na Shinyanga) Jimbo la Ziwa ndilo lililoongoza kwa idadi ya watu, idadi ya makabila, idadi ya mali asili na idadi ya machifu ambao nafasi yao ilikuwa kubwa tu katika kuhamasisha watu. Moja wa watu ambao mchango wao nitautaja kidogo tu ingawa alifanya jitihada kubwa labda zaidi ya wazee wa Mohamed Said ni Paul "Kishamapanda" Bomani.



Historia ya harakati za uhuru ni zaidi ya porojo za Mohamed Said, watu walipigania uhuru kama Watanganyika na bila kubaguana kikabila, kidini wala kijinsia. Ndio maana mimi sitaki kabisa kuwa na majibizano na huyu Mohamed Said moja kwa moja ila kwa kuwa hoja ileletwa JF, akae tayari kupewa somo kuhusu umbile zima la mnyama tembo na sio mguu moja wa tembo alioupapasa. Hapa mimi nitaongea sana kuhusu mchango wa Jimbo la Ziwa na baadaye kuonyesha jinsi maadui wa nchi yetu wanavyowatumia kidini watu kama huyu Mohamed Said.



Baadaye nitaeleza jinsi Mkoa wa Mara yenye makabila karibu hamsini yalivyoweza kushirikiana bila mfarakano na kuitikia mwito wa Mwalimu Nyerere katika hizo harakati za kudai uhuru. Je mwamko wa wakazi wa jimbo la Ziwa ulikuwaje na mapokezi gani aliyapata kila wakati Mwalimu aliporudi kwenye hili jimbo ambalo idadi ya wakazi wake kwenye miaka ya 50s ilikuwa mara tatu ya majimbo mengi Tanganyika kama Pwani. Pia nitaonyesha ni wakati gani walianza kuyasikia hayo majina anayodai Mohamed Said ya wazee wa Gerezani Dar es Salaam !

Mag3,

Kabla ya kumjibu ndugu Mohamedi Said ingebidi ufanye utafiti. Si kweli jimbo la pwani lilikuwa nyuma kiuchumi, kisiasa na kielimu. Jimbo la pwani lilikuwa linajumlisha Morogoro, Pwani na Dar Es Salaam. Lilikuwa linazalisha sana mkonge na korosho. Hayo ndio yaliokuwa mazao makubwa ya biashara Tanganyika. Na katika maeneo yote yaliyokuwa na mashamba ya mkonge kulikuwa na shule. Mabaki ya mashamba hayo yapo na shule zipo.

Miongozini mwa shule za mwanzo kwa ajili ya waafrika zilijengwa DSM, Mchikichini na Mzimuni. Baba yangu alitokea mikoani kuja kupata elimu DSM.

Na katika mwishoni mwa miaka ya 50, wanafunzi wa DSM waliandamana kupinga sera za elimu zilizokataza wanafunzi mwenye umri mkubwa kwenda middle schools.

Vilevile DSM ilikuwa na vyama vya wafanyakazi. Chama chenye nguvu kubwa kilikuwa cha bandari. Na kwa kuwa mizigo mingi ilikuwa inapitia bandarini, migomo yao ilikuwa ina nguvu kubwa.

Vilevile tutakuwa hatusemi ukweli kama tutayaangalia majimbo ya mkoloni kama identity moja. Ingawaje wahaya, wasukuma, wakerewe, wakurya, wazanaki ... yako kwenye kanda ya ziwa, maendeleo ya kiuchumi na kielimu ni tofauti na hayahusiani. Hivyo utakuwa hutendi haki kumfanya Msukuma wa Shinyanga ajisifie maendeleo ya Mhaya wa Kanyigo.

Sipo hapa kumtetea Mohamedi Said. Lakini kuna ukweli historia imewasahau watu. Na si kweli waliosoma walikuwa na mwamko wa uhuru. Wasomi wengi tu waliogopa kujiunga na mapambano kwa kuogopa kupoteza kazi.
 
dah hadithi bado zinaendelea na kujirudia!!.....sasa naamini kuwa lile kabila ni wabishi......maswali hawajibu....."darsa" tu kwa kwenda mbele, iwe pumba iwe mchele.....ni kanyaga twende...duh
 
JK,
Nakushauri ukisome kitabu cha Dr Harith Ghassany "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru" utapata yote humo ndani.

Mohamed
jK,
Nakushauri utapoteza muda wako bure kusoma kitabu cha Dr Harith Ghassany. Ni upotoshaji mwingine wa historia. Kama title yake inavyosema, baada ya kuondolewa ukoloni Zanzibar uhuru wa kikweli haujapatikana. If you believe that, go ahead and read the book, but don't say I didn't warn you.
 
jK,
Nakushauri utapoteza muda wako bure kusoma kitabu cha Dr Harith Ghassany. Ni upotoshaji mwingine wa historia. Kama title yake inavyosema, baada ya kuondolewa ukoloni Zanzibar uhuru wa kikweli haujapatikana. If you believe that, go ahead and read the book, but don't say I didn't warn you.

Jasusi,

Sijui kwa nini unamkatisha tamaa JK kusoma kitabu cha Dr Ghassany.
Ataweza vipi kupambanua ukweli ikiwa hatosoma?

Hivi kweli ni haki wewe uwe ndiyo muamuzi wa mawazo yake?

Naweka hapa kwa faida ya JK na wanaukumbi kwa ujumla pitio la kitabu hicho "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru" niloandika kitabu kilipotoka:

Mohamed Omari Mkwawa
Mwaka1995 wakati wa uchaguzi wa kwanza wa vyama vyingi Tanzania nilibahatika kufuatana na mgombeaurais wa CUF Prof. Ibrahim Haruna Lipumba katika kampeni za uchaguzi katikamikoa ya Kilimanjaro na Tanga. Prof. Lipumba alifanya mkutano mkubwa sana Tangamano kiasi chakuishtua CCM. Baada ya mkutano ule Prof. Lipumba na ujumbe wake walialikwanyumbani kwa mama mmoja akijulikana kama MamaUmmie (sasa ni marehemu) ambako walifanyiwa dhifa kubwa. Kote tukipita mitaa yaTanga msafara wetu ulikuwa ukishangiliwa kwa nguvu sana. CUF ilikuwa imeingia Tanga kwa kishindokikubwa. Mimikazi yangu ilikuwa kuangalia niliyokuwanayaona na kupiga picha. Kwa hakikanilikuwa nikishuhudia historia ikijiandika. Historia ambayo ilikuwa imeshahibianasana na ile ya wakati wa kudai uhuru wa Tanganyikakatika miaka 1950. Lakini ninalotaka kusema si hili bali ni picha ambayoniliipiga ndani ya nyumba ya Mama Ummie. Picha hii ilikuwa inamuonyesha mzeemmoja wa makamo aliyevaa fulana ya CUF mbele ikiwa na picha ya Prof. Lipumba.Mzee huyu alikuwa amekaa nyuma ya Prof. Lipumba. Kwa wakati ule picha hiihaikuwa na maana yoyote kwangu na hata nilipokuwa naitazama mara kwa mara surayake si iliyokuwa inanivutia bali ile fulana ya CUF aliyovaa ambayo ilikuwa napicha ya rafiki yangu Prof. Lipumba.Munguana mipango yake. Mihangaiko ya kutafuta riziki yakanihamishia Tanga na nikawakaribu sana nabaadhi ya viongozi wa CUF na wanachama wake. Sasa hapa ndipo nilipokujakuonana usokwa uso na mzee yule kwenye picha yangu niliyoipiga hata kwa wakati ule ilikuwamiaka mingi iliyopita. Jina la huyu mzee wangu ni Mohamed Omar Mkwawa. Ilikuwa katika barza yetu ya kawaida yakunywa kahawa na kula pweza huku tukijadili historia ya Tanzania ambako siku moja Mzee Mkwawaalinambia, "Mohamed nataka nikuambie kitu. Unajua mimi nimehusika sana katika mapinduzi ya Zanzibar?" NilimuangaliaMzee Mkwawa kwa makini. Fikra yangu ya utafiti na uandishi ishashtuka haipo tenausingizini. Mzee Mkwawa aliendelea, "Mimi ndiye niliyekuwa nikiwavushaWamakonde kutoka Kipumbwi kwenda Zanzibarkuipigia kura ASP na wakati wa mapinduzi mie ndiye niliyewavusha Wamakondekwenda kuipindua serikali ya Jamshid." Sasa moyo wangu ukaanza kudunda kwanguvu. Naisemesha nafsi yangu, "Huyu mzee anajua uzito wa maneno haya?" Tuishiehapa. Kuanzia siku ile nikawa sasa namtazama Mzee Mkwawa kwa jicho jingine naheshima yangu kwake ikawa imepanda maradufu. Nilikuwa nimeshatambua kuwa MzeeMohamed Omari Mkwawa alikuwa mmoja wa wanahistoria waliosahaulika katikahistoria ya Tanganyika na Zanzibar. Juu ya hayonilishangazwa na kitu kimoja. Iweje leo huyu mwanamapinduzi wa ASP ambae AbeidAmani Karume alimpa jina la "Tindo" kwa ujasiri wake amekuwa mstari wa mbeleCUF chama ambacho kinanasibishwa na Hizbu hasimu mkubwa wa ASP?
Dr Harith Ghassany
Nilikutanana DrHarith Ghassany mwaka 1999 nyumbani kwake Maskati, Oman. Naikumbukasiku ile kama jana vile. Kanipeleka kwakemwenyeji wangu Farouk Abdulla lakini kabla ya kunipeleka nilikuwa nimeshalisikiajina lake mara nyingi sana pale Maskati kilanikikutana na jamaa wenye asili ya Tanzaniajina lake litaibuka. Katika fikra yangu ikanijiakuwa Dkt Ghassany atakuwa ni mtu mzima. Sielewe kwa nini nilipata picha hii.Tulipopiga hodi na akatokea Dkt Ghassany kuja kutufungulia mlango nikapata mshangaomkubwa. Aliyekuwambele yangu alikuwa ni kijana mdogo sanatofauti na nilivyodhani. Kwa njia ya utani hata kabla sijatoa salamu. NikamgeukiaFarouk nikasema,"Ah! Dkt Ghassany, Dkt Ghassany, Dkt mwenyewe ndiye huyu?" Milana tamaduni za watu wa pwani wakikutana hazipishani. Maskhara ni dalili yamapenzi. Dkt Ghassany pale pale alipokea yale maskhara na akajibu,"Bwana wanguwe wanakutisha bure kwani we ulidhani litakuwa jitu kubwa?" Urafiki na udugu wetuumedumu hadi leo na ndipo katika mazungumzo aliponifahamisha kuwa anatakakuandika historia ya kweli ya mapinduzi ya Zanzibar. Hapo ndipo nilipomjuvya kuhusu MzeeMkwawa na nikamuomba aje Tanga amuhoji.Kitukimoja mashuhuri kwa mashujaa wa harakati za siasa katika Tanzania ni kuwa takriban wote wana hali ngumu sana za maisha. Sikujuavyema hali ya Mzee Mkwawa hadi nilipofika nyumbani kwake na Dkt Ghassany. Utuuzima na udhaifu wa maisha ulikuwa umempiga barabara. Nilimjulisha Dkt Ghassanykwa Mzee Mkwawa na kuwaacha waendelee na maongezi yao. Niliporudi mchana kumchukua Dkt Ghassanyrafiki yangu alinambia nimuache nije jioni kumfuata. Niliporudi jioni nilimkutaDkt Ghassany amechoka na uso umesawijika. Tukiwa ndani ya gari yangu tunaondoka nikamuuliza kulikoni.Dkt Ghassany akanambia maneno ambayo hadi leo yamebaki kichwani mwangu,"Mohamedufunguo wa kitabu changu anao Mzee Mkwakwa na kama nisingeonana nae utafitiwangu wote wa kabla ungelikuwa hauna maana yoyote." DktGhassany alikuwa amechukuliwa na Mzee Mkwawa katika safari ya zaidi ya nusukarne. Mzee Mkwawa akimshika mkono kwanza kumpeleka Pembaambako akiwa kijana wa kiasi cha miaka 25 akifanya kazi ya uashi. Huo ndioulikuwa wakati wa siasa za ASP na Hizbu zimepamba moto. Mzee Mkwawa alikuwa mmojawa wachezaji wa ngoma ile hata kama alikuwa anatoka Tanganyika. Dkt Harith akavushwa nakuletwa pwani ya Kipumbwi na Sakura ambako Mzee Mkwawa alikuwa akisimamia kambiya mafunzo iliyokuwa msituni ya wakata mkonge wengi wao wakiwa Wamakonde, kambiambayo ilitoa askari waliotumika kuipindua serikali ya Mohamed Shamte 12 Aprili1964. DktGhassany hakuwa amejitayarisha kwa haya. Alishangwazwa na uwezo wa kumbukumbuwa Mzee Mkwawa, akitaja majina na mahali na akirudia mazungumzo neno kwa nenokati yake na maofisa wa serikali ya Tanganyikakutoka vyombo vya usalama waliomtia katika operesheni maalum ya kuipindua Zanzibar kutoka Tanganyika. Majina ya AbdullaKassim Hanga, Jumanne Abdallah, Ali Mwinyi Tambwe, Victor Mkello, Oscar Kambonana wengine yakawa yanadondoka moja baada ya lingine. Taarifa hizi ndizozilizommaliza Dkt Ghassany na kumsawajisha uso.Mimibinafsi nilipigwa na butwaa. Nilibaini kama alivyobaini Dkt Ghassany kuwa MzeeMkwawa alikuwa hazina na tulikuwa tumevumbua mgodi wa dhahabu. Kazi yetu sasailikuwa kuchimba tu. Kumekuwa na uvumi kwa miaka mingi katika duru za wanasiasawapya na wa zamani na katika wanafunzi wa historia ya Tanzania na Mapinduzi yaZanzibar kuwa Ali Mwinyi Tambwe alihusika sana katika kupinduliwa kwa serikaliya Zanzibar lakini hakuna aliyejuwa ni kwa kiwango gani na alihusika vipi.Lakini zito ni kuwa yeye mwenyewe akiudhika sana mtu akimuuliza habari zile. Kwa niniilikuwa hivyo? Kitabu cha KwaheriUkoloni, Kwaheri Uhuru cha Dkt Ghassany kilikuja kutoa majibu. Hakunabinadamu apendae historia yake ihusishwe na mauaji na dhulma na kufutwa kwanchi yake.Kwakipindi cha takriban miaka saba Dkt Ghassany alikuwa akija Tanga kwa mahojianona Mzee Mkwawa na katika kipindi hicho Mzee Mkwawa alitupeleka Kipumbwi naSakura na kutuonyesha sehemu zile ambazo walikuwa na kambi na wakifanya mazoeziya kivita na matumizi ya silaha. Mkahawa ambao wale wakata mkonge walikuwawakila chakula cha usiku kabla ya kuvushwa kwa vyombo vya bahari kwenda Unguja badoupo hadi leo ingawa kwa sasa kijumba kile hakitumiki tena kamamkawaha. Endapo itakuja siku serikali ya Zanzibaritataka kuhifadhi historia ya Mapinduzi ya Zanzibar bila shaka moja ya vituvitakavyokuwa katika makumbusho ni picha ya hicho kibanda.
Victor Mkello
Kipumbwihaijabadilika iko kama vilevile iliyokuwamiaka ya 1960. Kipumbwi imebaki vilevilekama kijiji cha uvuvi. Mzee Mkwawa alitupelekahadi sehemu ambapo bahari imeingia katika kijiji lakini sehemu hiyo imefunikwana mikoko mingi na vichaka. Tuliingia ndani na kuangalia mandhari ya palemahali. Hakika pale palikuwa sehemu nzuri ya kujificha. Leo imekuwa sehemu hiini maarufu kwa watu wa magendo. MzeeMkwawa alitueleza kuwa hapo ndipo walipojificha na ndipo walipopandia vyombovyao kwa usiri mkubwa wakati wote wakiwa wamevaa nguo matambara na kofia zamakuti kama wavuvi. Tanga ilikuwa kituo muhimucha kufanikisha mapinduzi ya Zanzibar.Haikuwa bure kuwa Ali Mwinyi Tambwe, Jumanne Abdallah na Victor Mkello walikuwahapo na wala haistaajabishi kwa Dkt Ghassany kutueleza kuwa vinara wa mapinduzikwa upande wa bara, Mkello na wenzake, walisubiri taarifa za mapinduzi katikamkesha ndani ya ofisi ya TANU Tanga.Napendakukiri kuwa sikupata kushiriki kamamsikilizaji wa mahojiano wakati wa utafiti wa Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.Kazi yangu kubwa sanailikuwa kufungua milango na kumwendesha daktari. Kwa ufupi kazi yangu ilikuwakumwekea mwandishi mazingira mazuri ili kazi yake iwe nyepesi. Kwa hakikailikuwa kazi ambayo na mimi vilevile nilisoma, kujifunza mengi na kupata faidakubwa. Katika haya nakumbuka sakata la kumtafuta Victor Mkello. Leo si wengiwanaomjua Victor Mkello au hata kupata kusikia jina lake likitajwa.Lakini kwa sisi tuliokuwa wadogo tukiwa shule katika miaka ya 1960 Mkelloalikuwa hapungia katika magazeti ya Ngurumona Mwafrika. Mzee Mkwawa ndiyealiyetusaidia kumtafuta alipo. Victor Mkello ndiyo aliyekuwa "Amiri Jeshi Mkuu"wa lile jeshi la Wamakonde lililokuwa na makao yake makuu katika mashamba yamkonge ya Sakura na Kipumbwi. Bila ya kupata kauli ya Mkello kitabu kisingewezakuandikika.Ilichukuamuda kuweza kumpata. Kwanza tulikwenda Muhezaambako ndiko kwao. Huko tukaambiwa kuwa hakuwapo hapo bali kwa muda mrefualikuwa Tanga. Mwishowe tulimkuta nyumbani kwake Nguvu Mali. Mkelloalikuwa katika kitanda cha mauti. Kisukari kilikuwa kikimla kiwiliwili chake.Hakuwa anaweza kunyanyuka kitandani wala kukaa. Kwa hakika alikuwaanasikitisha. Huyu hakuwa Victor Mkello niliyekuwa namsoma katika magazeti walayule ambae Mzee Mkwawa alikuwa akituelezea. Mtu mjanja aliepambana na Magirikiwamiliki wa mashamba ya mkonge akitetea haki za Waafrika katika miaka ya 1960.Huyu kwa kweli hakuwa yule Victor Mkello aliyekuwa akisaidiana na TANU naMwalimu Julius Nyerere kupigania uhuru wa Tanganyika. Hiki mbele yetukilikuwa kivuli chake. Hapakuwa na wasiwasi wowote Victor Mkello alikuwaakisubiri malaika wa mauti amtembelee na yeye hilo alikuwa akilijua fika.VictorMkello na Mzee Mkwawa wanamapinduzi waliofutwa katika historia walitazamana nawakasalimiana kama vile hakuwapata kujuana. Jichola Mkello lilikwenda kwa Dkt Ghassany kisha likaangukia kwangu kisha likarudikwa mwanamapinduzi mwenzake Mzee Mkwawa. Baada ya utambulisho uliofanywa naMzee Mkwawa nilihisi woga na wasiwasi kwenye sura ya Victor Mkello. Hakuwaanaamini kuwa Dkt Ghassany katoka Maskati kwa ajili ya utafiti wa historia nahili lilijidhihirisha alipofunua kinywa kuzungumza. Victor Mkello alikuwa nahisia kuwa alifuatwa kukamatwa kwa vifo vya Waarabu vilivyotokea Zanzibar wakati wamapinduzi ili apelekwe Mahakama ya Kimataifa. Baadae Dkt Ghassanyalinifahamisha kuwa jinsi Waingereza walivyomueleza katika taarifa zao za siriambazo yeye alizisoma Londonzimeafikiana kabisa na jinsi alivyomuona pale. Waingereza walimsifia Mkello kwakusema kuwa alikuwa bingwa wa kuteleza kamasamaki ndani ya maji. Kufupishamaelezo. Ilichukua karibu miaka mitatu kwa Victor Mkello kukubali kuzungumza kuhusumapinduzi ya Zanzibar.Dkt Ghassany akienda Maskati na kurudi Tanga na kila akienda kwa Victor Mkello,Mkello hakuwa tayari kueleza kile alichokijua kuhusu mapinduzi ya Zanzibar. Kilanilipokwenda na Dkt Ghassany kumuona Mkello hali yake ilikuwa inazidikudidimia. Sasa alikuwa kakatwa mguu mmoja kwa ajili ya kisukari. Ilikuwakatika hali ile katika siku zake za mwisho ndipo siku moja alipomwambia DktGhassany aje siku ya pili na yeye atazungumza na angependa azungumze mbele yamkewe ili amkumbushe pale atakapokuwa kasahau kitu. Hapandipo ilipo moja ya sehemu tamu kabisa ya kitabu hiki Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru. Victor Mkello Amiri Jeshi Mkuu waMamluki wa Kimakonde alizungumza. Mimi sikushiriki katika mazungumzo yalenilijiweka pembeni ili Mkello azungumze na Dkt Ghassany kwa utulivu. Nilikuwanimeegesha gari yangu karibu ya msikiti jirani ya nyumba ya Mkello nikimsubiridaktari akamilishe upasuaje mgonjwa apate nafuu. Mwendo wa Dkt Ghassany wakudunda alipokuwa ananijia pale nilipoegesha gari ulidhihirisha furaha yake.Haukupitamuda mrefu baada ya mazungumzo yale na Dkt Ghassany, Victor Mkello akaaga duniakimya kimya. Hakuna mtu aliyejua kifo chake kama ilivyokuwa vifo vingi vyamashujaa waliopigania uhuru wa Tanganyika.Hakuna hata gazeti moja lililotoa taazia yake wala hotuba hazikusomwa kaburinikwake. Mkello aliondoka katika historia ya Tanzaniakimya kama jinsi mamluki wake walivyokuwa wakiingia Zanzibarkimya kimya usiku mkuu na kwa siri, mapanga yaomakali ya kukata mkonge yakiwa chini ya nguo zao za ndani yakisubiri kuivamia Zanzibar na kuua watuwasio na hatia. Kazi hii kwao haikuhitaji mafunzo kwani mafunzo walikuwanayo muda mrefu katika kazi yao ya kukata mkongekatika mashamba ya mkonge ya Tanga. Pigo moja lilitosha kuangusha chini janizito la mkonge seuze kiungo cha binadamu. Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuruni kitabu kilichoandikwa kwa staili ya pekee wahusika wenyewe wa matokeo katikamapinduzi kujitolea kueleza kile kilichotokea katika mapinduzi, kabla na baadayake. Kuanzia mipango ya kuangusha serikali ya Zanzibar hadi katika kuwaua walewaliokujakushukiwa kuwa ni maadui wa mapinduzi hadi kufikia hata kuweka wazijinsi walivyoshiriki katika mengi ya kusikitisha kupelekea hata msomajikujiuliza kwa nini hawa watu baada ya miaka yote hiyo kupita wameamua kuelezayote hayo. Vipi Abdallah Kassim Hanga, Othman Shariff, Mdungi Ussi, Jaha Ubwa,Abdulaziz Twala na wengineo walivyouliwa, nani alitoa amri ya mauaji, nanialiwauwa na katika mazingira gani. Kifo cha Karume mwenyewe kwa mtutu wabunduki hakikuwekewa pazia na chanzo cha kuamuliwa kuwa auawe ni tofauti yakilichozoeleka kuelezwa. Karumehakuuawa na "wapinga mapinduzi" kama ilivyozoeleka kuelezwa katika historiarasmi.Kwa kumaliza tusubiri mapitio ya kitabu hiki na ni wazikuwa wasomaji watapata mengi ya kuelimisha na kuhuisha. Tunategemea wasomi wasomo la historia watakaopitia kitabu hiki watatufanyia hisani kubwa kwakuwaleta katika picha wahusika wakuu wa mapinduzi – Mwalimu Julius Nyerere –fundi mkuu mwenye kishindo kikubwa lakini hakisikiki, mkono wake wa chuma hauonekani,uso wake nyuma ya pazia, Abdallah Kassim Hanga – kiongozi hasa na mpangaji wamapinduzi, Victor Mkello – mtumishi wa Hanga na Nyerere bila ya yeye mwenyewe kujua kati ya haowawili nani aliyekuwa bingwa kumshinda mwenzake katika mchezo mchafu wa siasa yakuiuwa Zanzibar na Wazanzibari na wengineo. Lakini juu ya hayo yote mipango hii ilikuwa ni ya akinaNyerere, Hanga na Mkello pekee? Dkt Ghassany anaeleza nini kuhusu mkono wa Waingereza, Algeria,Misri, Wachina, Warusi, Marekani na Mayahudi? Nini kilichowasukuma hao wotekatika mapinduzi ya Zanzibar?Nini kilimsukuma Nyerere, kuwapindua Waislam walioupigania Uhuru wa Tanganyika na baadae kuwapinduwa Waislamwalioupigania Uhuru wa Zanzibar na kuendeleakuwadhibiti hata baada ya kuipindua Zanzibar?Nini kilichowasukuma Waingereza na Wamerekani kuachia mapinduzi yafanyike?Lakini kubwa zaidi kipi kilichowasukuma Wayahudi kuingia na kusaidia mapinduzi,ni ile chuki yaoya asili dhidi ya Waarabu au kulikuwa na jengine ambalo liliwatia khofu? Nakwanini kitabu kiitwe Kwaheri UkoloniKwaheri Uhuru: Zanzibarna Mapinduzi ya Afrabia? Kitabu kina majibu ya haya maswali mengine ambayobado hayajaulizwa na chemchemu mpya za utafiti.Dkt Ghassany anastahili pongezi kubwa sanakwa kuinusuru historia ya mapinduzi ya Zanzibarna kuwaamsha Wazanzibari na Watanganyika toka lepe zito la usingizi iliwajitambue na wamjue adui yao.Anastahiki pongezi kubwa zaidi si kwa kukiandika kitabu cha Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru bali kwakutumia mrengo usiokuwa na mrengo. Huna pa kumuweka Dkt Ghassany na baada yakumaliza kukisoma kitabu ukaridhika napo. Kamautafikiria kuwa kitabu ni cha CUF basi baada ya kusoma mpaka mwisho utavunjikamoyo. Kama utamtumbukiza ndani ya CCM basiataelea. La kama unataka upae nje ya masunduku na mapakacha basi utamuonakatulia ndani ya uhuisho wa Zanzibarna Tanganyika/Tanzania Mpya – ambayo itafuata mfumo wa Umoja wa Ulaya (EuropeanUnion) ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kwaheri Ukoloni,Kwaheri Uhuru ni ngoma nzito ambayowatu wameanza kuicheza hata mdundo haujaanza kupigwa! Tayari imeshaingia katikarikodi za Hansard za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tayari imeshasikikakatika Sauti ya Marekani. Tayari daktari anafuatilia kwa karibu ukweli waMaridhiano na kuwa kwa mara nyengine tena ukweli wake umeshaanza kupotoshwa nawaroho na tayari historia mpya na kubwa zaidi hata kuliko ile ya Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 imeshaanzakuvurugwa. Kwa hivi sasa muamko wa vijana juu ya Muungano nimkubwa na japokuwa wamekaa kimya kuhusu Mapinduzi, mie naamini kwamba'hawataki' kuyagusa Mapinduzi kwa sasa ili kutotibua hali ya maelewanoilokuwepo Zanzibarkwa sasa katika kipindi hichi. Hii ni kwasababu Mapinduzi ndo yanayo-define'utaifa' wa Zanzibar na kwa hiyo Mapinduzi nijambo nyeti linalogusa moja kwa moja uhalali wa Serikali ya Zanzibar iliopo. Kwa vile bado Serikali yaUmoja wa Kitafa bado ni changa, kuyapinga Mapinduzi kwa sasa sio jambo labusara, kwani kutaweza kurudisha machafuko na kutokuelewana miongoni mwaWazanzibari. Sababu ni kwamba bado kuna wananchi kadhaa hawajuikiini cha Mapinduzi na kwao Mapinduzi ndio uhuru kamaupotoshaji wa makusudi wa kiini cha Mapinduzi hayo unavyoelekeza. Pia kunabaadhi ya viongozi kwa utashi wao wa kisiasa na maslahi yao, kupitia ushawishi walionao kwa wafuasiwao, wataleta mtafaruku pindi watu watakapoyaponda Mapinduzi hadharani nahatimae ni machafuko baina ya Wazanzibari wenyewe kwa wenyewe. Mwanauchumi maarufu kutoka Ghana,George Ayittey, anatafautisha baina ya kizazi cha Chita na kizazi cha Kiboko. Kizazi cha zamanini kile cha "kiboko" ambacho ni kizazi kivivu na hakishi kulalamika juu yaukoloni. Kizazi kipya ni kile cha "Cheetah" (Duma) ambacho kimeamua kuzikamatahatamu za mustakbali wake ndani ya mikono yaowenyewe, badala ya kuwasubiri kuendeshwa na wanasiasa ambao kivitendo huyawekamaslahi yaobinafsi mbele zaidi kuliko maslahi ya nchi na ya wananchi. Kizazi kipya cha duma cha Kizanzibari chenye kukisomakitabu cha Kwaheri Ukoloni, KwaheriUhuru! hakitaki kuzisikia hadithi za paukwa pakawa za Katiba au kero zaMuungano. Wakitakacho ni nchi mbili, serikali mbili, na baada ya hapo ndipowataamua aina ya Muungano wautakao. KwaheriUkoloni, Kwaheri Uhuru! kimeliamsha Taifa lililolazwa na kwa hivi sasaWazanzibari wanadai Mapinduzi ya Muungano ambayo yalianza Zanzibar tarehe 5 Novemba, 2009. Suala, ni jee, duma wa Kitanganyika au wa KitanzaniaBara na yeye atadai Mapinduzi ya Muungano na kuanzisha mchakato mpya wamashirikiano baina nchi mbili huru ya Zanzibarna ya Tanganyika/Tanzania? Au kiboko cha Tanganyika/Tanzania Bara na wafuasi waowalioko Zanzibar wataendelea kuyalinda mapinduziyao ya Zanzibarili kuulinda muungano wenye kutawaliwa na Tanganyika/Tanzania Bara? Watengenezaji wa filamu Hollywoodwana mtindo wa kumaliza senema zao za matokeo ya kweli kwa kueleza katikamaandishi yale yaliyowafika wahusika wa kisa kilichotengenezwa hiyo senema.Huonyesha majina na mwisho wa hao wahusika, kama wahai, wako wapi, wamekufa na kama wamekufa ni kwa kuuliwa au kwa amri ya Mungu nk.Katika Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru majinaya wahusika machache ambayo yametajwa katika makala haya yako kamahivi:1. MohamedOmar Mkwawa: Yu hai naanaishi Makorola Tanga2. AbeidAmani Karume: Ameuawa19723. Abdallah Kassim Hanga: Ameuawa 1967/684. Mustafa Songambele Yuhaianaishi Songea.5. Victor Mkello Amekufakifo cha kawaida 6. Ali Mwinyi Tambwe Baadaya mapinduzi alikuja kuhusika katika mchakato wa kuunda muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Amekufa kifo cha kawaida.7. Jumanne Abdallah Alitumikiaserikali kwa muda mrefu hadi alipofariki kifo cha kawaida8. Oscar Kambona Aligombanana Nyerere na akakimbia nchi mwaka 1967 na kwenda kuishi uhamishoni Uingereza9. Kuna vigogo kadhaa ambavyo viko hai na kwa sasawameomba majina yaoyahifadhiwe.10. Kizazi kipya cha duma kitakachokuja kuliunganishaBara la Afrika kwa kuufuata mfumo wa Umoja wa Ulaya (EU) badala yakuwangangania mapacha wa Mapinduzi na Muungano ambao wameunganishwa na kutengwana kitabu cha Dkt. Ghassany, KwaheriUkoloni, Kwaheri Uhuru! Mohamed
 
jK,
Nakushauri utapoteza muda wako bure kusoma kitabu cha Dr Harith Ghassany. Ni upotoshaji mwingine wa historia. Kama title yake inavyosema, baada ya kuondolewa ukoloni Zanzibar uhuru wa kikweli haujapatikana. If you believe that, go ahead and read the book, but don't say I didn't warn you.

Jasusi,

Sijui kwa nini unamkatisha tamaa JK kusoma kitabu cha Dr Ghassany.
Ataweza vipi kupambanua ukweli ikiwa hatosoma?

Hivi kweli ni haki wewe uwe ndiyo muamuzi wa mawazo yake?

Naweka hapa kwa faida ya JK na wanaukumbi kwa ujumla pitio la kitabu hicho "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru" niloandika kitabu kilipotoka:

Mohamed Omari Mkwawa
Mwaka1995 wakati wa uchaguzi wa kwanza wa vyama vyingi Tanzania nilibahatika kufuatana na mgombeaurais wa CUF Prof. Ibrahim Haruna Lipumba katika kampeni za uchaguzi katikamikoa ya Kilimanjaro na Tanga. Prof. Lipumba alifanya mkutano mkubwa sana Tangamano kiasi chakuishtua CCM. Baada ya mkutano ule Prof. Lipumba na ujumbe wake walialikwanyumbani kwa mama mmoja akijulikana kama MamaUmmie (sasa ni marehemu) ambako walifanyiwa dhifa kubwa. Kote tukipita mitaa yaTanga msafara wetu ulikuwa ukishangiliwa kwa nguvu sana. CUF ilikuwa imeingia Tanga kwa kishindokikubwa. Mimikazi yangu ilikuwa kuangalia niliyokuwanayaona na kupiga picha. Kwa hakikanilikuwa nikishuhudia historia ikijiandika. Historia ambayo ilikuwa imeshahibianasana na ile ya wakati wa kudai uhuru wa Tanganyikakatika miaka 1950. Lakini ninalotaka kusema si hili bali ni picha ambayoniliipiga ndani ya nyumba ya Mama Ummie. Picha hii ilikuwa inamuonyesha mzeemmoja wa makamo aliyevaa fulana ya CUF mbele ikiwa na picha ya Prof. Lipumba.Mzee huyu alikuwa amekaa nyuma ya Prof. Lipumba. Kwa wakati ule picha hiihaikuwa na maana yoyote kwangu na hata nilipokuwa naitazama mara kwa mara surayake si iliyokuwa inanivutia bali ile fulana ya CUF aliyovaa ambayo ilikuwa napicha ya rafiki yangu Prof. Lipumba. Munguana mipango yake. Mihangaiko ya kutafuta riziki yakanihamishia Tanga na nikawakaribu sana nabaadhi ya viongozi wa CUF na wanachama wake. Sasa hapa ndipo nilipokujakuonana usokwa uso na mzee yule kwenye picha yangu niliyoipiga hata kwa wakati ule ilikuwamiaka mingi iliyopita. Jina la huyu mzee wangu ni Mohamed Omar Mkwawa. Ilikuwa katika barza yetu ya kawaida yakunywa kahawa na kula pweza huku tukijadili historia ya Tanzania ambako siku moja Mzee Mkwawaalinambia, “Mohamed nataka nikuambie kitu. Unajua mimi nimehusika sana katika mapinduzi ya Zanzibar?” NilimuangaliaMzee Mkwawa kwa makini. Fikra yangu ya utafiti na uandishi ishashtuka haipo tenausingizini. Mzee Mkwawa aliendelea, “Mimi ndiye niliyekuwa nikiwavushaWamakonde kutoka Kipumbwi kwenda Zanzibarkuipigia kura ASP na wakati wa mapinduzi mie ndiye niliyewavusha Wamakondekwenda kuipindua serikali ya Jamshid.” Sasa moyo wangu ukaanza kudunda kwanguvu. Naisemesha nafsi yangu, “Huyu mzee anajua uzito wa maneno haya?” Tuishiehapa. Kuanzia siku ile nikawa sasa namtazama Mzee Mkwawa kwa jicho jingine naheshima yangu kwake ikawa imepanda maradufu. Nilikuwa nimeshatambua kuwa MzeeMohamed Omari Mkwawa alikuwa mmoja wa wanahistoria waliosahaulika katikahistoria ya Tanganyika na Zanzibar. Juu ya hayonilishangazwa na kitu kimoja. Iweje leo huyu mwanamapinduzi wa ASP ambae AbeidAmani Karume alimpa jina la “Tindo” kwa ujasiri wake amekuwa mstari wa mbeleCUF chama ambacho kinanasibishwa na Hizbu hasimu mkubwa wa ASP?
Dr Harith Ghassany
Nilikutanana DrHarith Ghassany mwaka 1999 nyumbani kwake Maskati, Oman. Naikumbukasiku ile kama jana vile. Kanipeleka kwakemwenyeji wangu Farouk Abdulla lakini kabla ya kunipeleka nilikuwa nimeshalisikiajina lake mara nyingi sana pale Maskati kilanikikutana na jamaa wenye asili ya Tanzaniajina lake litaibuka. Katika fikra yangu ikanijiakuwa Dkt Ghassany atakuwa ni mtu mzima. Sielewe kwa nini nilipata picha hii.Tulipopiga hodi na akatokea Dkt Ghassany kuja kutufungulia mlango nikapata mshangaomkubwa. Aliyekuwambele yangu alikuwa ni kijana mdogo sanatofauti na nilivyodhani. Kwa njia ya utani hata kabla sijatoa salamu. NikamgeukiaFarouk nikasema,”Ah! Dkt Ghassany, Dkt Ghassany, Dkt mwenyewe ndiye huyu?” Milana tamaduni za watu wa pwani wakikutana hazipishani. Maskhara ni dalili yamapenzi. Dkt Ghassany pale pale alipokea yale maskhara na akajibu,”Bwana wanguwe wanakutisha bure kwani we ulidhani litakuwa jitu kubwa?” Urafiki na udugu wetuumedumu hadi leo na ndipo katika mazungumzo aliponifahamisha kuwa anatakakuandika historia ya kweli ya mapinduzi ya Zanzibar. Hapo ndipo nilipomjuvya kuhusu MzeeMkwawa na nikamuomba aje Tanga amuhoji. Kitukimoja mashuhuri kwa mashujaa wa harakati za siasa katika Tanzania ni kuwa takriban wote wana hali ngumu sana za maisha. Sikujuavyema hali ya Mzee Mkwawa hadi nilipofika nyumbani kwake na Dkt Ghassany. Utuuzima na udhaifu wa maisha ulikuwa umempiga barabara. Nilimjulisha Dkt Ghassanykwa Mzee Mkwawa na kuwaacha waendelee na maongezi yao. Niliporudi mchana kumchukua Dkt Ghassanyrafiki yangu alinambia nimuache nije jioni kumfuata. Niliporudi jioni nilimkutaDkt Ghassany amechoka na uso umesawijika. Tukiwa ndani ya gari yangu tunaondoka nikamuuliza kulikoni.Dkt Ghassany akanambia maneno ambayo hadi leo yamebaki kichwani mwangu,”Mohamedufunguo wa kitabu changu anao Mzee Mkwakwa na kama nisingeonana nae utafitiwangu wote wa kabla ungelikuwa hauna maana yoyote.” DktGhassany alikuwa amechukuliwa na Mzee Mkwawa katika safari ya zaidi ya nusukarne. Mzee Mkwawa akimshika mkono kwanza kumpeleka Pembaambako akiwa kijana wa kiasi cha miaka 25 akifanya kazi ya uashi. Huo ndioulikuwa wakati wa siasa za ASP na Hizbu zimepamba moto. Mzee Mkwawa alikuwa mmojawa wachezaji wa ngoma ile hata kama alikuwa anatoka Tanganyika. Dkt Harith akavushwa nakuletwa pwani ya Kipumbwi na Sakura ambako Mzee Mkwawa alikuwa akisimamia kambiya mafunzo iliyokuwa msituni ya wakata mkonge wengi wao wakiwa Wamakonde, kambiambayo ilitoa askari waliotumika kuipindua serikali ya Mohamed Shamte 12 Aprili1964. DktGhassany hakuwa amejitayarisha kwa haya. Alishangwazwa na uwezo wa kumbukumbuwa Mzee Mkwawa, akitaja majina na mahali na akirudia mazungumzo neno kwa nenokati yake na maofisa wa serikali ya Tanganyikakutoka vyombo vya usalama waliomtia katika operesheni maalum ya kuipindua Zanzibar kutoka Tanganyika. Majina ya AbdullaKassim Hanga, Jumanne Abdallah, Ali Mwinyi Tambwe, Victor Mkello, Oscar Kambonana wengine yakawa yanadondoka moja baada ya lingine. Taarifa hizi ndizozilizommaliza Dkt Ghassany na kumsawajisha uso. Mimibinafsi nilipigwa na butwaa. Nilibaini kama alivyobaini Dkt Ghassany kuwa MzeeMkwawa alikuwa hazina na tulikuwa tumevumbua mgodi wa dhahabu. Kazi yetu sasailikuwa kuchimba tu. Kumekuwa na uvumi kwa miaka mingi katika duru za wanasiasawapya na wa zamani na katika wanafunzi wa historia ya Tanzania na Mapinduzi yaZanzibar kuwa Ali Mwinyi Tambwe alihusika sana katika kupinduliwa kwa serikaliya Zanzibar lakini hakuna aliyejuwa ni kwa kiwango gani na alihusika vipi.Lakini zito ni kuwa yeye mwenyewe akiudhika sana mtu akimuuliza habari zile. Kwa niniilikuwa hivyo? Kitabu cha KwaheriUkoloni, Kwaheri Uhuru cha Dkt Ghassany kilikuja kutoa majibu. Hakunabinadamu apendae historia yake ihusishwe na mauaji na dhulma na kufutwa kwanchi yake. Kwakipindi cha takriban miaka saba Dkt Ghassany alikuwa akija Tanga kwa mahojianona Mzee Mkwawa na katika kipindi hicho Mzee Mkwawa alitupeleka Kipumbwi naSakura na kutuonyesha sehemu zile ambazo walikuwa na kambi na wakifanya mazoeziya kivita na matumizi ya silaha. Mkahawa ambao wale wakata mkonge walikuwawakila chakula cha usiku kabla ya kuvushwa kwa vyombo vya bahari kwenda Unguja badoupo hadi leo ingawa kwa sasa kijumba kile hakitumiki tena kamamkawaha. Endapo itakuja siku serikali ya Zanzibaritataka kuhifadhi historia ya Mapinduzi ya Zanzibar bila shaka moja ya vituvitakavyokuwa katika makumbusho ni picha ya hicho kibanda.
Victor Mkello
Kipumbwihaijabadilika iko kama vilevile iliyokuwamiaka ya 1960. Kipumbwi imebaki vilevilekama kijiji cha uvuvi. Mzee Mkwawa alitupelekahadi sehemu ambapo bahari imeingia katika kijiji lakini sehemu hiyo imefunikwana mikoko mingi na vichaka. Tuliingia ndani na kuangalia mandhari ya palemahali. Hakika pale palikuwa sehemu nzuri ya kujificha. Leo imekuwa sehemu hiini maarufu kwa watu wa magendo. MzeeMkwawa alitueleza kuwa hapo ndipo walipojificha na ndipo walipopandia vyombovyao kwa usiri mkubwa wakati wote wakiwa wamevaa nguo matambara na kofia zamakuti kama wavuvi. Tanga ilikuwa kituo muhimucha kufanikisha mapinduzi ya Zanzibar.Haikuwa bure kuwa Ali Mwinyi Tambwe, Jumanne Abdallah na Victor Mkello walikuwahapo na wala haistaajabishi kwa Dkt Ghassany kutueleza kuwa vinara wa mapinduzikwa upande wa bara, Mkello na wenzake, walisubiri taarifa za mapinduzi katikamkesha ndani ya ofisi ya TANU Tanga. Napendakukiri kuwa sikupata kushiriki kamamsikilizaji wa mahojiano wakati wa utafiti wa Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.Kazi yangu kubwa sanailikuwa kufungua milango na kumwendesha daktari. Kwa ufupi kazi yangu ilikuwakumwekea mwandishi mazingira mazuri ili kazi yake iwe nyepesi. Kwa hakikailikuwa kazi ambayo na mimi vilevile nilisoma, kujifunza mengi na kupata faidakubwa. Katika haya nakumbuka sakata la kumtafuta Victor Mkello. Leo si wengiwanaomjua Victor Mkello au hata kupata kusikia jina lake likitajwa.Lakini kwa sisi tuliokuwa wadogo tukiwa shule katika miaka ya 1960 Mkelloalikuwa hapungia katika magazeti ya Ngurumona Mwafrika. Mzee Mkwawa ndiyealiyetusaidia kumtafuta alipo. Victor Mkello ndiyo aliyekuwa ”Amiri Jeshi Mkuu”wa lile jeshi la Wamakonde lililokuwa na makao yake makuu katika mashamba yamkonge ya Sakura na Kipumbwi. Bila ya kupata kauli ya Mkello kitabu kisingewezakuandikika. Ilichukuamuda kuweza kumpata. Kwanza tulikwenda Muhezaambako ndiko kwao. Huko tukaambiwa kuwa hakuwapo hapo bali kwa muda mrefualikuwa Tanga. Mwishowe tulimkuta nyumbani kwake Nguvu Mali. Mkelloalikuwa katika kitanda cha mauti. Kisukari kilikuwa kikimla kiwiliwili chake.Hakuwa anaweza kunyanyuka kitandani wala kukaa. Kwa hakika alikuwaanasikitisha. Huyu hakuwa Victor Mkello niliyekuwa namsoma katika magazeti walayule ambae Mzee Mkwawa alikuwa akituelezea. Mtu mjanja aliepambana na Magirikiwamiliki wa mashamba ya mkonge akitetea haki za Waafrika katika miaka ya 1960.Huyu kwa kweli hakuwa yule Victor Mkello aliyekuwa akisaidiana na TANU naMwalimu Julius Nyerere kupigania uhuru wa Tanganyika. Hiki mbele yetukilikuwa kivuli chake. Hapakuwa na wasiwasi wowote Victor Mkello alikuwaakisubiri malaika wa mauti amtembelee na yeye hilo alikuwa akilijua fika. VictorMkello na Mzee Mkwawa wanamapinduzi waliofutwa katika historia walitazamana nawakasalimiana kama vile hakuwapata kujuana. Jichola Mkello lilikwenda kwa Dkt Ghassany kisha likaangukia kwangu kisha likarudikwa mwanamapinduzi mwenzake Mzee Mkwawa. Baada ya utambulisho uliofanywa naMzee Mkwawa nilihisi woga na wasiwasi kwenye sura ya Victor Mkello. Hakuwaanaamini kuwa Dkt Ghassany katoka Maskati kwa ajili ya utafiti wa historia nahili lilijidhihirisha alipofunua kinywa kuzungumza. Victor Mkello alikuwa nahisia kuwa alifuatwa kukamatwa kwa vifo vya Waarabu vilivyotokea Zanzibar wakati wamapinduzi ili apelekwe Mahakama ya Kimataifa. Baadae Dkt Ghassanyalinifahamisha kuwa jinsi Waingereza walivyomueleza katika taarifa zao za siriambazo yeye alizisoma Londonzimeafikiana kabisa na jinsi alivyomuona pale. Waingereza walimsifia Mkello kwakusema kuwa alikuwa bingwa wa kuteleza kamasamaki ndani ya maji. Kufupishamaelezo. Ilichukua karibu miaka mitatu kwa Victor Mkello kukubali kuzungumza kuhusumapinduzi ya Zanzibar.Dkt Ghassany akienda Maskati na kurudi Tanga na kila akienda kwa Victor Mkello,Mkello hakuwa tayari kueleza kile alichokijua kuhusu mapinduzi ya Zanzibar. Kilanilipokwenda na Dkt Ghassany kumuona Mkello hali yake ilikuwa inazidikudidimia. Sasa alikuwa kakatwa mguu mmoja kwa ajili ya kisukari. Ilikuwakatika hali ile katika siku zake za mwisho ndipo siku moja alipomwambia DktGhassany aje siku ya pili na yeye atazungumza na angependa azungumze mbele yamkewe ili amkumbushe pale atakapokuwa kasahau kitu. Hapandipo ilipo moja ya sehemu tamu kabisa ya kitabu hiki Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru. Victor Mkello Amiri Jeshi Mkuu waMamluki wa Kimakonde alizungumza. Mimi sikushiriki katika mazungumzo yalenilijiweka pembeni ili Mkello azungumze na Dkt Ghassany kwa utulivu. Nilikuwanimeegesha gari yangu karibu ya msikiti jirani ya nyumba ya Mkello nikimsubiridaktari akamilishe upasuaje mgonjwa apate nafuu. Mwendo wa Dkt Ghassany wakudunda alipokuwa ananijia pale nilipoegesha gari ulidhihirisha furaha yake. Haukupitamuda mrefu baada ya mazungumzo yale na Dkt Ghassany, Victor Mkello akaaga duniakimya kimya. Hakuna mtu aliyejua kifo chake kama ilivyokuwa vifo vingi vyamashujaa waliopigania uhuru wa Tanganyika.Hakuna hata gazeti moja lililotoa taazia yake wala hotuba hazikusomwa kaburinikwake. Mkello aliondoka katika historia ya Tanzaniakimya kama jinsi mamluki wake walivyokuwa wakiingia Zanzibarkimya kimya usiku mkuu na kwa siri, mapanga yaomakali ya kukata mkonge yakiwa chini ya nguo zao za ndani yakisubiri kuivamia Zanzibar na kuua watuwasio na hatia. Kazi hii kwao haikuhitaji mafunzo kwani mafunzo walikuwanayo muda mrefu katika kazi yao ya kukata mkongekatika mashamba ya mkonge ya Tanga. Pigo moja lilitosha kuangusha chini janizito la mkonge seuze kiungo cha binadamu. Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuruni kitabu kilichoandikwa kwa staili ya pekee wahusika wenyewe wa matokeo katikamapinduzi kujitolea kueleza kile kilichotokea katika mapinduzi, kabla na baadayake. Kuanzia mipango ya kuangusha serikali ya Zanzibar hadi katika kuwaua walewaliokujakushukiwa kuwa ni maadui wa mapinduzi hadi kufikia hata kuweka wazijinsi walivyoshiriki katika mengi ya kusikitisha kupelekea hata msomajikujiuliza kwa nini hawa watu baada ya miaka yote hiyo kupita wameamua kuelezayote hayo. Vipi Abdallah Kassim Hanga, Othman Shariff, Mdungi Ussi, Jaha Ubwa,Abdulaziz Twala na wengineo walivyouliwa, nani alitoa amri ya mauaji, nanialiwauwa na katika mazingira gani. Kifo cha Karume mwenyewe kwa mtutu wabunduki hakikuwekewa pazia na chanzo cha kuamuliwa kuwa auawe ni tofauti yakilichozoeleka kuelezwa. Karumehakuuawa na ”wapinga mapinduzi” kama ilivyozoeleka kuelezwa katika historiarasmi. Kwa kumaliza tusubiri mapitio ya kitabu hiki na ni wazikuwa wasomaji watapata mengi ya kuelimisha na kuhuisha. Tunategemea wasomi wasomo la historia watakaopitia kitabu hiki watatufanyia hisani kubwa kwakuwaleta katika picha wahusika wakuu wa mapinduzi – Mwalimu Julius Nyerere –fundi mkuu mwenye kishindo kikubwa lakini hakisikiki, mkono wake wa chuma hauonekani,uso wake nyuma ya pazia, Abdallah Kassim Hanga – kiongozi hasa na mpangaji wamapinduzi, Victor Mkello – mtumishi wa Hanga na Nyerere bila ya yeye mwenyewe kujua kati ya haowawili nani aliyekuwa bingwa kumshinda mwenzake katika mchezo mchafu wa siasa yakuiuwa Zanzibar na Wazanzibari na wengineo. Lakini juu ya hayo yote mipango hii ilikuwa ni ya akinaNyerere, Hanga na Mkello pekee? Dkt Ghassany anaeleza nini kuhusu mkono wa Waingereza, Algeria,Misri, Wachina, Warusi, Marekani na Mayahudi? Nini kilichowasukuma hao wotekatika mapinduzi ya Zanzibar?Nini kilimsukuma Nyerere, kuwapindua Waislam walioupigania Uhuru wa Tanganyika na baadae kuwapinduwa Waislamwalioupigania Uhuru wa Zanzibar na kuendeleakuwadhibiti hata baada ya kuipindua Zanzibar?Nini kilichowasukuma Waingereza na Wamerekani kuachia mapinduzi yafanyike?Lakini kubwa zaidi kipi kilichowasukuma Wayahudi kuingia na kusaidia mapinduzi,ni ile chuki yaoya asili dhidi ya Waarabu au kulikuwa na jengine ambalo liliwatia khofu? Nakwanini kitabu kiitwe Kwaheri UkoloniKwaheri Uhuru: Zanzibarna Mapinduzi ya Afrabia? Kitabu kina majibu ya haya maswali mengine ambayobado hayajaulizwa na chemchemu mpya za utafiti. Dkt Ghassany anastahili pongezi kubwa sanakwa kuinusuru historia ya mapinduzi ya Zanzibarna kuwaamsha Wazanzibari na Watanganyika toka lepe zito la usingizi iliwajitambue na wamjue adui yao.Anastahiki pongezi kubwa zaidi si kwa kukiandika kitabu cha Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru bali kwakutumia mrengo usiokuwa na mrengo. Huna pa kumuweka Dkt Ghassany na baada yakumaliza kukisoma kitabu ukaridhika napo. Kamautafikiria kuwa kitabu ni cha CUF basi baada ya kusoma mpaka mwisho utavunjikamoyo. Kama utamtumbukiza ndani ya CCM basiataelea. La kama unataka upae nje ya masunduku na mapakacha basi utamuonakatulia ndani ya uhuisho wa Zanzibarna Tanganyika/Tanzania Mpya – ambayo itafuata mfumo wa Umoja wa Ulaya (EuropeanUnion) ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kwaheri Ukoloni,Kwaheri Uhuru ni ngoma nzito ambayowatu wameanza kuicheza hata mdundo haujaanza kupigwa! Tayari imeshaingia katikarikodi za Hansard za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tayari imeshasikikakatika Sauti ya Marekani. Tayari daktari anafuatilia kwa karibu ukweli waMaridhiano na kuwa kwa mara nyengine tena ukweli wake umeshaanza kupotoshwa nawaroho na tayari historia mpya na kubwa zaidi hata kuliko ile ya Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 imeshaanzakuvurugwa. Kwa hivi sasa muamko wa vijana juu ya Muungano nimkubwa na japokuwa wamekaa kimya kuhusu Mapinduzi, mie naamini kwamba'hawataki' kuyagusa Mapinduzi kwa sasa ili kutotibua hali ya maelewanoilokuwepo Zanzibarkwa sasa katika kipindi hichi. Hii ni kwasababu Mapinduzi ndo yanayo-define'utaifa' wa Zanzibar na kwa hiyo Mapinduzi nijambo nyeti linalogusa moja kwa moja uhalali wa Serikali ya Zanzibar iliopo. Kwa vile bado Serikali yaUmoja wa Kitafa bado ni changa, kuyapinga Mapinduzi kwa sasa sio jambo labusara, kwani kutaweza kurudisha machafuko na kutokuelewana miongoni mwaWazanzibari. Sababu ni kwamba bado kuna wananchi kadhaa hawajuikiini cha Mapinduzi na kwao Mapinduzi ndio uhuru kamaupotoshaji wa makusudi wa kiini cha Mapinduzi hayo unavyoelekeza. Pia kunabaadhi ya viongozi kwa utashi wao wa kisiasa na maslahi yao, kupitia ushawishi walionao kwa wafuasiwao, wataleta mtafaruku pindi watu watakapoyaponda Mapinduzi hadharani nahatimae ni machafuko baina ya Wazanzibari wenyewe kwa wenyewe. Mwanauchumi maarufu kutoka Ghana,George Ayittey, anatafautisha baina ya kizazi cha Chita na kizazi cha Kiboko. Kizazi cha zamanini kile cha “kiboko” ambacho ni kizazi kivivu na hakishi kulalamika juu yaukoloni. Kizazi kipya ni kile cha “Cheetah” (Duma) ambacho kimeamua kuzikamatahatamu za mustakbali wake ndani ya mikono yaowenyewe, badala ya kuwasubiri kuendeshwa na wanasiasa ambao kivitendo huyawekamaslahi yaobinafsi mbele zaidi kuliko maslahi ya nchi na ya wananchi. Kizazi kipya cha duma cha Kizanzibari chenye kukisomakitabu cha Kwaheri Ukoloni, KwaheriUhuru! hakitaki kuzisikia hadithi za paukwa pakawa za Katiba au kero zaMuungano. Wakitakacho ni nchi mbili, serikali mbili, na baada ya hapo ndipowataamua aina ya Muungano wautakao. KwaheriUkoloni, Kwaheri Uhuru! kimeliamsha Taifa lililolazwa na kwa hivi sasaWazanzibari wanadai Mapinduzi ya Muungano ambayo yalianza Zanzibar tarehe 5 Novemba, 2009. Suala, ni jee, duma wa Kitanganyika au wa KitanzaniaBara na yeye atadai Mapinduzi ya Muungano na kuanzisha mchakato mpya wamashirikiano baina nchi mbili huru ya Zanzibarna ya Tanganyika/Tanzania? Au kiboko cha Tanganyika/Tanzania Bara na wafuasi waowalioko Zanzibar wataendelea kuyalinda mapinduziyao ya Zanzibarili kuulinda muungano wenye kutawaliwa na Tanganyika/Tanzania Bara? Watengenezaji wa filamu Hollywoodwana mtindo wa kumaliza senema zao za matokeo ya kweli kwa kueleza katikamaandishi yale yaliyowafika wahusika wa kisa kilichotengenezwa hiyo senema.Huonyesha majina na mwisho wa hao wahusika, kama wahai, wako wapi, wamekufa na kama wamekufa ni kwa kuuliwa au kwa amri ya Mungu nk.Katika Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru majinaya wahusika machache ambayo yametajwa katika makala haya yako kamahivi: 1. MohamedOmar Mkwawa: Yu hai naanaishi Makorola Tanga2. AbeidAmani Karume: Ameuawa19723. Abdallah Kassim Hanga: Ameuawa 1967/684. Mustafa Songambele Yuhaianaishi Songea.5. Victor Mkello Amekufakifo cha kawaida 6. Ali Mwinyi Tambwe Baadaya mapinduzi alikuja kuhusika katika mchakato wa kuunda muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Amekufa kifo cha kawaida.7. Jumanne Abdallah Alitumikiaserikali kwa muda mrefu hadi alipofariki kifo cha kawaida8. Oscar Kambona Aligombanana Nyerere na akakimbia nchi mwaka 1967 na kwenda kuishi uhamishoni Uingereza9. Kuna vigogo kadhaa ambavyo viko hai na kwa sasawameomba majina yaoyahifadhiwe.10. Kizazi kipya cha duma kitakachokuja kuliunganishaBara la Afrika kwa kuufuata mfumo wa Umoja wa Ulaya (EU) badala yakuwangangania mapacha wa Mapinduzi na Muungano ambao wameunganishwa na kutengwana kitabu cha Dkt. Ghassany, KwaheriUkoloni, Kwaheri Uhuru! Mohamed
 
dah hadithi bado zinaendelea na kujirudia!!.....sasa naamini kuwa lile kabila ni wabishi......maswali hawajibu....."darsa" tu kwa kwenda mbele, iwe pumba iwe mchele.....ni kanyaga twende...duh

Ogah,

Ikiwa moyo wako ni safi haujaathirika na hasad basi katika darsa langu utakuwa umejifunza mengi sana.

Ikiwa una hasad darsa halina maana yoyote kwako.

Na hasad nikatika maradhi mabaya kabisa.

Mohamed
 
Ustaadh Moh'd naona unamwaga nondo sio polepole. Haya endeleeni kutujuza hizi habari.
 
Muulizeni Kigarama mbona hajamtaja Muhenga wala Mwambambe kwani inasemekana Mwambambe alikuwa anaonekana ni nuksi na dosari katika historia ya wahehe. Tutaendelea kesho wacha niwaacheni leo nilikuwapo wakuu.
Hoja ilikuwa ni kama Mkwawa alikuwa ni Muislam au la, na wala hoja haikuwa mkwawa alipataje utawala wa Wahehe. Kuna wengi sikuwataja kama kina Mayagila, mdegela, Mdemu na wengineo. Inshaalah watakuwemo kwenye Historia fupi ya Mkwawa.
 
Back
Top Bottom