Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Kuna mtu kanitukana na kwa kuwa mimi si mtu wa matusi bali hoja
nimeamua kujiweka pembeni.

Sheikh wangu Maalim Haruna (Mungu amrehemu)akitueleza katika madras
wakati anatufunza adab za mnakasha (majadiliano) kuwa dalili ya kwanza
ya mtu kushindwa ni ukali na lugha zisizokuwa kiungwana.

Dalili ya pili ni kukutukana kabisa.

Sheikh akaendelea kusema kuwa akitoka hapo katika matusi atakutoa ngeu.

Akashauri kuwa unaejadiliananae akifika daraja ya kukutukana basi jiondoe.

Hii ni salama kwake yeye na kwako mtu kuepusha shari ndiyo ustaarabu.

Waungwana wasomi hawakejeliani katika mnakasha wala hawatukanani.


Mohamed

Sheikh Mohammed.. nikupe pole kwa mitusi uliyoporomoshewa na Mag3. Licha ya kukiri kama umri wake ni mkubwa zaidi ya wa kwako lakini majibu yake yaliyoambatana na kejeli ni kiashiria kama kuna walakini kwa mchangiaji huyu. Woga anaozidi kuoonyesha kwa kuficha jina lake na kujiita mag3 ni kielelezo kingine cha kumtambua aina ya mtu unayejadiliana nae.

Ikiwa anashindwa hata kuthubutu kutaja jina lake na kuishia kuporomosha matusi ni dalili ya mtu muoga anaethubutu kutoa matusi nyuma ya pazia.

Ila nukta ya kukumbuka.... kitendo chake cha kukiri kama yeye licha ya umri huooo mkubwa alioutaja ya kuwa hajawahipo kusikia majina ya bwana wakubwa hawa uliowataja ni kielelezo kingine cha kujua kiwango cha uweledi wa historia ya nchi hii. Ila napata faraja kama .. mtu huyu na wengine wenye muelekeo wake watafaidika sana kwenye munakasha huu.

Mods
Nimestushwa kuona thread hii ilihali kuna thread mama inaendelea.... falsafa ya kuanzisha thread hii sijaijua. Maana huku ni madongo tu baina ya pande mbili..ilihali kwenye ile thread mama kuna mtiririko wa majadiliano ya madda husika. Ushauri wangu..hii thread iunganishwe na ile ya awali

Shkh Yahya.
 
Mkuu Jasusi achana na huyu mpuuzi, tatizo ni kwamba watu wengi makini wamekuwa wakiyapuuzia haya makala yake ya kichochezi na hatari yake ni kuwa uwongo ukiachiwa nafasi ya kujirudia rudia mwisho wapo watakaoamini kuwa ni kweli vile. Mimi wakati naanza shule 1953, huyo Mohamed Said alikuwa hata hajazaliwa kama alivyokiri kwenye majibu yake hapo nyuma.

Mimi ni mzaliwa wa kanda ya Ziwa na wakati tunapata uhuru mwaka nilikuwa Sekondari lakini pamoja na kuwa tulikuwa tunafuatilia sana matukio ya kisiasa, sikuwahi kuwaona au hata kuwasikia hao anaodai Mohamed kuwa walikuwa vinara wa harakati za kudai uhuru Tanganyika. Je hii ni kwa sababu nilizaliwa nje ya Dar es Salaam au kwa ni sababu hao wazee wa Mohamed hawakujulikana nje ya Dar es Salaam.

Pamoja na kwamba mwaka 1965 tayari nilikwishahamia Dar es Salaam kuendelea na masomo yangu, sikuyasikia haya majina hadi miaka ya 1970 ! Baada ya hapo nilijaribu sana kuwadadisi wazee mbali mbali, Musoma, Mwanza hadi Bukoba lakini sikuweza kumpata mzee ambaye kwa hakika angeweza kunisimulia mchango wa hawa wazee wa Gerezani alikozaliwa Mohamed Said katika kudai uhuru wa Tanganyika.

TAA kwa upande mwingine ilianzishwa na watumishi wa serikali chini ya utawala wa kikoloni na haihitaji akili yoyote ya ziada kukisia kuwa wengi wa hawa watumishi walikuwa wa aina gani. Ni vigumu sana kusema kwa uhakika ni lini TAA iliyoanzishwa mwaka 1929 ilianza kuwa na msimamo wa kisiasa lakini upepo wa uhuru kwa nchi nyingi za Kiafrika ulianza kuvuma kwa kasi miaka ishirini baadaye.

Harakati za TAA zilipoonyesha dalili ya kudai mambo nje ya haki za wafanya kazi ilibidi kuchagua moja ama ujiuzulu uunge mkono TAA bila kificho au uendelee na ajira lakini usionyeshe wazi msimamo wako. TAA ikawa imefikia kikomo chake na ikawa sasa ni lazima kizaliwe chombo cha kisiasa ambacho malengo yake na dhumuni lake ni kuiondoa serikali ya kikoloni kwa kudai uhuru kamili.

Madai ya Mohamed Said ni kama leo kudai kuwa wote walioko serikalini hawaungi mkono madai ya Chadema dhidi ya serikali, la hasha, wapo lakini wakijionyesha wazi wazi wakati huu nafikiri sote tunajua serikali ya CCM itakavyowashughulikia. Kulikuwa na faida kubwa kwa wanaharakati wengine kubaki ndani ya serikali ya mkoloni kama ilivyo sasa hivi kwa Chadema kuwa na watu wake ndani ya serikali ya CCM.

TAA ya Mwanza mpaka mwaka 1948 ilikuwa na wanachama kama 3,000 lakini mwaka 1952 kwa jitihada za Bomani wanachama wa TAA waliweza kuongezeka hadi kufikia 30,000 na ni mwaka moja baadaye ndiyo Katibu Mkuu wa TAA kama anavyodai Mohamed Said alipotembelea Mwanza. Lakini wakati huo tayari Mwalimu Nyerere anaiongoza TAA baada ya kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Raisi wake.

Walikuwapo watu kama Masanja Shija Raisi wa kwanza wa Victoria Federation Cooperative Union (VFCU) na Makamu wake akiwa Daudi Kabeya Murangira wa Majita aliyeuza boti zake za uvuvi. Jamani wana JF, Tanganyika ilikuwa zaidi ya Wazee wa Mohamed Said wa Gerezani na Kariakoo na ukweli ni kwamba Watanganyika walihitaji kuhamasishwa kutoka Mtwara hadi Sirari, Dar es Salaam hadi Kasulu !

Mwalimu Nyerere hakuwa mtoto yatima, alizaliwa katika ukoo wa kichifu na familia kubwa iliyojaa wazee wa busara wa Kizanaki ambao walimpa baraka zao zote awakabili wakoloni bila woga. Mwalimu Nyere kila aliporudi Musoma hakusahau kufika kuvuka mto Mara kwenda kumsalimia Chifu Odemba Kagose wa Buturi Ujaluoni kupata ushauri wake kwa mambo mbali mbali.

Wana JF, ni wakati sasa wa kuwakataa hawa wachochezi, ni wakati wa kumwambia Mohamed Said kuwa hata uvumilivu una mwisho. Wamekuwa wakipata free ride wakipanda hizi mbegu za chuki miongoni mwa wananchi huku sisi great thinkers tukikaa kando, no enough is enough, ukweli lazima waambiwe hata kama unauma kiasi gani.

Majuzi hapa tumeshuhudia Marekani, watu wa kilichoitwa tea party wakiibua mambo yasiyo na ukweli na kuyarudia rudia hadi wakawateka wale wenye uwezo mdogo wa kufikiri ! Mohamed Said ni wa kuogopwa kama ukimwi ! Mohamed Said sasa aanze kuorodhesha majina ya wazee wake waliojiuzulu kwenye utumishi serikalini ili kupigania uhuru wa Tanganyika ili wajadiliwe hapa JF kwa sababu TAA ilikuwa ya Watumishi wa serikali.

nafurahi kuwa zile hoja zinazostahili kujadiliwa na watu wenye hadhi ya forum hii zimeanza kujitokeza tena na kwa kweli zinachokonoa bongo na fikra za watu hadi inatia msisimko.

kuna ushahidi wa wazi kuwa kuna vipande vya historia vimezuiwa ama kupotoshwa kwa makusudi(sielewi ni kwa maslahi ya nani) na tumekuwa miaka yote tukiaminishwa kwamba harakati za kupigania uhuru ziliasisiwa,kuratibiwa na hata kufanikishwa na MWALIMU!! siku zote tumeshindwa kujiuliza maswali madogo tu kuwa kwa nchi kubwa kama TZ ambayo ilikuwa haina miundombinu kama ilivyo sasa, mwalimu aliwezaje kupata fedha,wenyeji n.k mpaka TANUikaweza kukubalika nchi nzima.
nisingepedna kuingia ndani zaidi lakini naamini kitu kimoja ambacho hata mwalimu nyerere alikuwa anakiamini nacho ni wakati makabila madogomadogo, masikini na yasiyo na elimu ya tanzania yakiunganisha nguvu na fedha zao kwa ajili ya mapambano dhidi ya ukoloni,, na wakati mwalimu nyerere akiwa sambamba na wananchi wenzke toka katika jamii hizi masikini,, yale makabila yanayojiona leo hii kuwa ni makabila ya wasomi,wenye fedha na madaraka ndio yaliyokuwa hayataki kujishughulisha na harakati za kupigania uhuru na hawakuwa tayari hata kutoa michango ya fedha kusaidia harakati hizo,kwa vile wengi wao walikuwa wanafanya kazi katika serikali ya kikoloni, hawakuona ubaya wa ukoloni na hivyo hawakuona maana ya uhuru,
wale wachache wenye upeo na uelewa wa hali ya juu( nyerere,paul bomani,rashid kawawa,abbas mtemvu, abdul sykes.oscar kambona n.k) walikuwa wanapata support kubwa toka makabila madogodogo na yasiyo maarufu hivi sasa.

ushahidi uko wazi kwani hata mikutano muhimu kabisa ya TANU ilikuwa ikifanyika maeneo hayo,ofisi za kwanza kabisa za TANU zilifunguliwa maeneo hayo na hata wanaharakati wa mwanzo kabisa wa sisa za kudai uhuru walitoka maeneo hayo.

Hata mwalimu angekuwa hai leo na umuulize kama ni busara sisi wa TZ tumchague raisi kutoka makabila fulanifulani(siyataji) mwalimu angesema HAPANA tena kwa herufi kubwa kabisa kwani makabila haya yana sifa kubwa tatu nazo ni 1.usaliti-haswa kama usaliti wake utampa faida ya kifedha 2.uoga- haswa kama uoga wake utamfaya asipoteze kile anachokipata kwa muda huo. 3. ubinafsi- kwa kuamini kwa sababu wao wengi wamesoma na wanafedha basi wao ndio bora na haki kuliko wengine na kudhani kwamba wao ndio mabwana nasisi wengine tubaki kuwa watwana
 
nafurahi kuwa zile hoja zinazostahili kujadiliwa na watu wenye hadhi ya forum hii zimeanza kujitokeza tena na kwa kweli zinachokonoa bongo na fikra za watu hadi inatia msisimko.
kuna ushahidi wa wazi kuwa kuna vipande vya historia vimezuiwa ama kupotoshwa kwa makusudi(sielewi ni kwa maslahi ya nani) na tumekuwa miaka yote tukiaminishwa kwamba harakati za kupigania uhuru ziliasisiwa,kuratibiwa na hata kufanikishwa na MWALIMU!! siku zote tumeshindwa kujiuliza maswali madogo tu kuwa kwa nchi kubwa kama TZ ambayo ilikuwa haina miundombinu kama ilivyo sasa, mwalimu aliwezaje kupata fedha,wenyeji n.k mpaka TANUikaweza kukubalika nchi nzima.
nisingepedna kuingia ndani zaidi lakini naamini kitu kimoja ambacho hata mwalimu nyerere alikuwa anakiamini nacho ni ..
wakati makabila madogomadogo, masikini na yasiyo na elimu ya tanzania yakiunganisha nguvu na fedha zao kwa ajili ya mapambano dhidi ya ukoloni,, na wakati mwalimu nyerere akiwa sambamba na wananchi wenzke toka katika jamii hizi masikini,, yale makabila yanayojiona leo hii kuwa ni makabila ya wasomi,wenye fedha na madaraka ndio yaliyokuwa hayataki kujishughulisha na harakati za kupigania uhuru na hawakuwa tayari hata kutoa michango ya fedha kusaidia harakati hizo,kwa vile wengi wao walikuwa wanafanya kazi katika serikali ya kikoloni, hawakuona ubaya wa ukoloni na hivyo hawakuona maana ya uhuru,
wale wachache wenye upeo na uelewa wa hali ya juu( nyerere,paul bomani,rashid kawawa,abbas mtemvu, abdul sykes.oscar kambona n.k) walikuwa wanapata support kubwa toka makabila madogodogo na yasiyo maarufu hivi sasa. ushahidi uko wazi kwani hata mikutano muhimu kabisa ya TANU ilikuwa ikifanyika maeneo hayo,ofisi za kwanza kabisa za TANU zilifunguliwa maeneo hayo na hata wanaharakati wa mwanzo kabisa wa sisa za kudai uhuru walitoka maeneo hayo.
Hata mwalimu angekuwa hai leo na umuulize kama ni busara sisi wa TZ tumchague raisi kutoka makabila fulanifulani(siyataji) mwalimu angesema HAPANA tena kwa herufi kubwa kabisa kwani makabila haya yana sifa kubwa tatu nazo ni 1.usaliti-haswa kama usaliti wake utampa faida ya kifedha 2.uoga- haswa kama uoga wake utamfaya asipoteze kile anachokipata kwa muda huo. 3. ubinafsi- kwa kuamini kwa sababu wao wengi wamesoma na wanafedha basi wao ndio bora na haki kuliko wengine na kudhani kwamba wao ndio mabwana nasisi wengine tubaki kuwa watwana
Banned 4 ever,
Mbona na wewe umekuja na theories zako ambazo hazina mashiko? Wasukuma ni kabila dogo? Unajua wewe mchango wao katika harakati za uhuru? Wahaya ni kabila dogo, na hawa mchango wao je? Na Wachagga, na Wanyakyusa?

Ni kweli wafanyikazi katika serikali ya wakoloni hawakuruhusiwa kushiriki katika harakati za kupigania uhuru, lakini kuna waliothubutu kwa kutoa michango yao kwa siri.
 
Kitu kimoja nilicho na hakika nacho kwa asilimia 100% ni kwamba wale wote wenye mapenzi ya kweli kwa taifa letu la Tanzania wanasita sana kuchangia hii hoja inayofinyangwafinyangwa na huyu anayejiita Mohamed Said. Bila kumung'unya maneno nayaita madai ya Mohamed Said la kutoa elimu ya historia ya kweli ni porojo hatari iliyojaa uchochezi ambayo lengo lake hasa ni kuleta uhasama wa kidini miongoni mwa wananchi. Sijui anachotegemea kufaidika nacho kwa kupanda hii mbegu ya hatari ambayo nina hakika mtu kama Mohamed Said anajua fika madhara yake.

Mohamed Said ni kama kipofu ambaye baada ya kusimuliwa na wazee kwamba tembo ni mnyama mkubwa kuliko wanyama wengi anapata nafasi ya kumpapasa tembo. Kwa bahati mbaya anaupapasa mguu wa tembo na si mwili wote halafu katika imani yake anadai anao uwezo wa kutoa somo kuhusu umbo la mnyama tembo na ushuhuda wake, kuwa tembo ni kama gogo la mti mkubwa, ndio ukweli na anayesema tofauti hajui kitu. Watu wote wanaolalamikiwa na Mohamed Said kuwa walisahauliwa, wengi wao walikuwa wakazi wa Dar es Salaam eneo la Gerezani.

Kabla ya uhuru Tanganyika iligawanywa katika majimbo makuu manane na katika majimbo yote hayo, jimbo la pwani kwa ujumla lilikuwa moja ya majimbo yaliyokuwa nyuma kimaendeleo kiuchumi, kielimu na kisiasa na hiyo ni licha ya kuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni yalikuwa Dar es Salaam. TAA ilianzishwa na watumishi wa serikali (civil servants) na kwa wakati wote kazi kubwa ya TAA ilikuwa ni kulalamika ikidai haki ya wafanyakazi bila upendeleo na hasa ubaguzi wa rangi katila utumishi kubwa ukiwa uonevu dhidi ya wazawa, mtu mweusi.

Jimbo la Ziwa ni moja ya majimbo yaliyokuwa mbele kiuchumi, kielimu na kisiasa na kama kuna kitu kinaweza kudaiwa kuwa kilisahaulika katika harakati ya kupigania uhuru ni mchango wa Jimbo la Ziwa (Bukoba, Mwanza, Mara na Shinyanga) Jimbo la Ziwa ndilo lililoongoza kwa idadi ya watu, idadi ya makabila, idadi ya mali asili na idadi ya machifu ambao nafasi yao ilikuwa kubwa tu katika kuhamasisha watu. Moja wa watu ambao mchango wao nitautaja kidogo tu ingawa alifanya jitihada kubwa labda zaidi ya wazee wa Mohamed Said ni Paul "Kishamapanda" Bomani.



Historia ya harakati za uhuru ni zaidi ya porojo za Mohamed Said, watu walipigania uhuru kama Watanganyika na bila kubaguana kikabila, kidini wala kijinsia. Ndio maana mimi sitaki kabisa kuwa na majibizano na huyu Mohamed Said moja kwa moja ila kwa kuwa hoja ileletwa JF, akae tayari kupewa somo kuhusu umbile zima la mnyama tembo na sio mguu moja wa tembo alioupapasa. Hapa mimi nitaongea sana kuhusu mchango wa Jimbo la Ziwa na baadaye kuonyesha jinsi maadui wa nchi yetu wanavyowatumia kidini watu kama huyu Mohamed Said.



Baadaye nitaeleza jinsi Mkoa wa Mara yenye makabila karibu hamsini yalivyoweza kushirikiana bila mfarakano na kuitikia mwito wa Mwalimu Nyerere katika hizo harakati za kudai uhuru. Je mwamko wa wakazi wa jimbo la Ziwa ulikuwaje na mapokezi gani aliyapata kila wakati Mwalimu aliporudi kwenye hili jimbo ambalo idadi ya wakazi wake kwenye miaka ya 50s ilikuwa mara tatu ya majimbo mengi Tanganyika kama Pwani. Pia nitaonyesha ni wakati gani walianza kuyasikia hayo majina anayodai Mohamed Said ya wazee wa Gerezani Dar es Salaam !
Nimefika hapo kwenye red highlight nikapoteza mvuto wa thread yako. Nenda kaongopee wajinga wenzako huko. Na acha kupotosha uhalisia wa historia yetu. I am sure historia ya ukweli itakuwa wazi si muda mrefu. mmejitahidi sana kufanya historia ya kweli lakini time to ome out is on.
 
Nguruvi3 said:
Laah la la! Mkuu Mag3, ahsante sana umenikumbusha kisa kimoja. Unajua hilo la wanawake wa Kipare lilitokana na mambo kadhaa. Mwingereza aliweka kodi ya kichwa na wakati huo ilikuwa ni kubwa sana.
Wanaume wa Kipare wakalazimika kulala maporini ili wasikamatwe. Wake zao wakaungana na kuwatia ushujaa wa kupambana.

Wanaume woote( aliyebaki alikuwa mahututi) na wale vijana waliotoka jando wakaungana bila kujali dini zao au koo zao. Wakabeba mishale na mikuki na kuandamana kwa miguu kutoka upare milimani, zaidi ya KM 180 kwenda Boma la iliyokuwa makao makuu ya Pare, Same.

Maandamano yalikuwa ya amani lakini tayari kwa lolote lile. Mwingereza DC alipoona Boma limevamiwa akapiga simu kwa Gavana na kutoa amri ya kufuta kodi hio hapo hapo.

Wazee wakarudi mshaujaa. Hiyo inaitwa KODI YA MBIRU. Muulize mzee yoyote wa kipare mwenye 70+ atakueleza. Hili nimeelezwa na wazee wangu na wapo hai baadhi, kama kuna anayetaka ushaidi ahlan wahsalan, nitatoa nauli, malazi na chakula Tukawahoji wazee wangu.

Ndiyo maana wakati wa kupigania uhuru Nyerere alikubalika sana huko. Je hawa hawakuwa wapigania uhuru!
Na hao akina mama aliotaja Mag3 na kwingine huko, je si wapigania uhuru wa Tanganyika!



Nguruvi3,

..umenikumbusha vipindi vya michezo ya redio enzi zile za RTD[radio tanzania dar-es-salaam]

..hawa walikuwa na vipindi vya maigizo redioni ambapo waliigiza mapambano ya Mtwa Mkwawa,Mtemi Isike, Mangi Meli, etc etc.

..mgomo wa kodi ya MBIRU ulikuwa ni moja ya matukio yaliyoigizwa ktk vipindi hivyo vya redio.

..kitu cha kufurahisha ni kwamba mgomo wa MBIRU ulitumia dhana ya NON VIOLENCE. wananchi walikusanyika bomani kwa DC bila kufanya vurugu yoyote ile.

..kiongozi wa mgomo wa Mbiru alikuwa ni Paulo Mashambo ambaye alikuwa mwalimu na Mchungaji wa Kanisa la Wasabato. Pamoja na hayo mgomo huo ulijumuisha watu wa imani mbalimbali. Kumbuka, kati ya makabila yenye mchanganyiko wa imani za Kiislamu na Kikristo kwa kiwango kikubwa ni hili la Wapare.

..mgomo wa MBIRU ulidumu kwa zaidi ya MIEZI MIWILI!!!

..kumbukumbu haziwekwi tu, lakini hivi mgomo wa Mbiru una tofauti kubwa na yale yaliyofanyika mwaka huu Tahrir square?

..hawa wazee waliweza vipi ku-organize wanaume wa wilaya nzima ya Pare kwa muda mfupi, mfano wa Tahrir square, bila facebook wala Twitter??!!

Mag3 said:
The Pare Union formed in 1946 was one of Tanzania's first ethnic-based nationalist movements to begin activism against the colonial system. Among many grievances, was the exploitation through the production of export crops particularly Sisal and Coffee. One important historical event is that ofMbiru, a protest during the colonial period by the Pare people which involved refusal to pay tax. It was led by Paulo Kajiru of Mamba.

Like many other ethnic-based political groups in Tanganyika, The Pare Union then became part of the TAA which later became the TANU in 1954. This avoided groups like the Pare Union forming into full political parties that were ethnic in orientation.

Mag3,

..Katibu Mkuu wa Pare Union, akiitwa Elias Kissenge, alikuja kuwa Katibu Mkuu wa Tanu, kipindi fulani.

..mikoani Tanu ilirithi mitandao iliyokuwa imeshaanzishwa na hivi vyama vidogo vidogo vya kikabila.

..pia kuna migogoro ilikuwa inafukuta baina ya Muingereza na wazalendo ambayo nayo ilirahisisha mapokezi ya Tanu huko mikoani. Particularly hapo nikumbushe mgogoro wa ardhi ktk eneo la Wasukuma.


 
Naona kila wanapojaribu huwa wanashindwa hata pa kuanzia na wanaamuwa kuanza na matusi. Pole Sheikh Mohamed kwa kutusiwa bila sababu.

Halafu wamejaribu kufika mpaka Upare wakakumbana na TAA sasa waeleze hao wapare kwanini waliungana na TAA na waasisi wa TAA ni kina nani.

Naona wanakuja na hadithi zisizo na mpango wala kichwa wala miguu. Wasomi hao. Wanashangaza!
 
Kuna mtu kanitukana na kwa kuwa mimi si mtu wa matusi bali hoja
nimeamua kujiweka pembeni.

Sheikh wangu Maalim Haruna (Mungu amrehemu)akitueleza katika madras
wakati anatufunza adab za mnakasha (majadiliano) kuwa dalili ya kwanza
ya mtu kushindwa ni ukali na lugha zisizokuwa kiungwana.

Dalili ya pili ni kukutukana kabisa.

Sheikh akaendelea kusema kuwa akitoka hapo katika matusi atakutoa ngeu.

Akashauri kuwa unaejadiliananae akifika daraja ya kukutukana basi jiondoe.

Hii ni salama kwake yeye na kwako mtu kuepusha shari ndiyo ustaarabu.

Waungwana wasomi hawakejeliani katika mnakasha wala hawatukanani.


Mohamed

Huyo shehe wako kakudanganya, mimi ninavyo wajua waisilamu hawana mchezo wakidai hoja yao hatakama haina msingi, wako tayari hatakufa kusimamia anochokiamini hata kama ni ushenzi, yuko teyari kukuua ili usimsumbue, kama huyo shehe wako angekuwa hai nadhani kwa sasa angeshakuwa chriatian tena born again.
 
Kitu kimoja nilicho na hakika nacho kwa asilimia 100% ni kwamba wale wote wenye mapenzi ya kweli kwa taifa letu la Tanzania wanasita sana kuchangia hii hoja inayofinyangwafinyangwa na huyu anayejiita Mohamed Said.

Bila kumung'unya maneno nayaita madai ya Mohamed Said la kutoa elimu ya historia ya kweli ni porojo hatari iliyojaa uchochezi ambayo lengo lake hasa ni kuleta uhasama wa kidini miongoni mwa wananchi. Sijui anachotegemea kufaidika nacho kwa kupanda hii mbegu ya hatari ambayo nina hakika mtu kama Mohamed Said anajua fika madhara yake.

Mohamed Said ni kama kipofu ambaye baada ya kusimuliwa na wazee kwamba tembo ni mnyama mkubwa kuliko wanyama wengi anapata nafasi ya kumpapasa tembo. Kwa bahati mbaya anaupapasa mguu wa tembo na si mwili wote halafu katika imani yake anadai anao uwezo wa kutoa somo kuhusu umbo la mnyama tembo na ushuhuda wake, kuwa tembo ni kama gogo la mti mkubwa, ndio ukweli na anayesema tofauti hajui kitu. Watu wote wanaolalamikiwa na Mohamed Said kuwa walisahauliwa, wengi wao walikuwa wakazi wa Dar es Salaam eneo la Gerezani.

Kabla ya uhuru Tanganyika iligawanywa katika majimbo makuu manane na katika majimbo yote hayo, jimbo la pwani kwa ujumla lilikuwa moja ya majimbo yaliyokuwa nyuma kimaendeleo kiuchumi, kielimu na kisiasa na hiyo ni licha ya kuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni yalikuwa Dar es Salaam. TAA ilianzishwa na watumishi wa serikali (civil servants) na kwa wakati wote kazi kubwa ya TAA ilikuwa ni kulalamika ikidai haki ya wafanyakazi bila upendeleo na hasa ubaguzi wa rangi katila utumishi kubwa ukiwa uonevu dhidi ya wazawa, mtu mweusi.

Jimbo la Ziwa ni moja ya majimbo yaliyokuwa mbele kiuchumi, kielimu na kisiasa na kama kuna kitu kinaweza kudaiwa kuwa kilisahaulika katika harakati ya kupigania uhuru ni mchango wa Jimbo la Ziwa (Bukoba, Mwanza, Mara na Shinyanga) Jimbo la Ziwa ndilo lililoongoza kwa idadi ya watu, idadi ya makabila, idadi ya mali asili na idadi ya machifu ambao nafasi yao ilikuwa kubwa tu katika kuhamasisha watu. Moja wa watu ambao mchango wao nitautaja kidogo tu ingawa alifanya jitihada kubwa labda zaidi ya wazee wa Mohamed Said ni Paul "Kishamapanda" Bomani.



Historia ya harakati za uhuru ni zaidi ya porojo za Mohamed Said, watu walipigania uhuru kama Watanganyika na bila kubaguana kikabila, kidini wala kijinsia. Ndio maana mimi sitaki kabisa kuwa na majibizano na huyu Mohamed Said moja kwa moja ila kwa kuwa hoja ileletwa JF, akae tayari kupewa somo kuhusu umbile zima la mnyama tembo na sio mguu moja wa tembo alioupapasa. Hapa mimi nitaongea sana kuhusu mchango wa Jimbo la Ziwa na baadaye kuonyesha jinsi maadui wa nchi yetu wanavyowatumia kidini watu kama huyu Mohamed Said.



Baadaye nitaeleza jinsi Mkoa wa Mara yenye makabila karibu hamsini yalivyoweza kushirikiana bila mfarakano na kuitikia mwito wa Mwalimu Nyerere katika hizo harakati za kudai uhuru. Je mwamko wa wakazi wa jimbo la Ziwa ulikuwaje na mapokezi gani aliyapata kila wakati Mwalimu aliporudi kwenye hili jimbo ambalo idadi ya wakazi wake kwenye miaka ya 50s ilikuwa mara tatu ya majimbo mengi Tanganyika kama Pwani. Pia nitaonyesha ni wakati gani walianza kuyasikia hayo majina anayodai Mohamed Said ya wazee wa Gerezani Dar es Salaam !


Tatizo lako linaloonekana hapa ni uelewa wako mdogo. Ni kweli kabisa watanganyika walipigania ardhi yao bila kujali dini zao na ndo maana watu wa Dar ambao wengi wao walikuwa wenye maamuzi ya juu walikuwa wa dini fulani lakini walimfuata julius nyerere akiwa wa dini tofauti pale pugu kuja kushirikiana nao. na kumbuka kwanza alikataa kwa sababu yeye alikuwa ameajiriwa na huku akihoji kuhusu kipato lakini wazee wa Dar walijitolea na kuingiza mifukoni kwao na kumlipa nyerere mshahara.

Kumbuka hao watu walifikia hata kufunga saumu kumuombea nyerere mema. Ila sasa baada tu ya kupata uhuru, wewe mwenyewe unajionea hali halisi ya hizo jamii.

Na ndo maana hata unathubutu bila HATA AIBU kusema eti walikuwa nyuma kisiasa na porojo zingine. unakera kwa kweli.
 
Nguruvi kasema reference yake ni "wazee wake" kitu ambacho M. Said nacho anatumia je inatosha mtu kusema "wazee wangu waliniambia" kuwa ni ushahidi tosha usiohitaji kuhojiwa? Reference ya vyanzo visivyoaminika yaweza kunukuliwa kila mahali lakini je ni kweli? Kwa mfano, mtu anaweza kusema "Mwinyi alimuambia Malima x,y" lakini Malima ni marehemu na Mwinyi yupo lakini Mwinyi hajahojiwa bado unaweza kusema huko ni kuonesha weledi wa kufanya utafiti? Fikiria kwamba, karibu wengi wanaoshtumiwa au kuwekewa maneno na Bw. Said wamekufa lakini wale wengine wanaotajwa wakiwa bado hai hajawahoji yeye mwenyewe angalau kupata mawazo yake. Kwa mfano, mtu anaweza vipi kusema Nyerere alikuwa na chuki na Uislamu au Waislamu bila kwenda kujaribu kukaa na mke wa Nyerere ambaye bado yuko hai, ana akili timamu na nina uhakika angeweza kabisa kueleezea na kutoa msaada wa taarifa mbalimbali? Kweli unaweza kuita huo ni uchunguzi wa kisomi? KUrusha references tu si usomi au weledi kwani kama hujibu maswali yanayotokana na references hizo na kutuambia tu kuwa "kama hamuamini basi, kama mnaamini safi".

nadhani anachofanya Bw. Said ni chema sana lakini hakifanyi chote au kwa nia safi ambayo ni kuongezea ujuzi. Yeye anachotaka ni a. Ikubalike Nyerere hakuwa na mchango wa kipekee katika harakati za Uhuru kulinganisha na wapigania uhuru wengine. b. Waislamu ndio pekee waliokuwa wanataka Uhuru na Wakristu walikuwa hawataki kwa sababu walikuwa wananufaika na ukoloni (rejea kitabu chake hicho cha Sykes) na c. Waislamu wameonewa na Kanisa na kanisa bado linawaoena Waislamu and by extension Wakrisu wanawakandamiza Waislamu.

Yote haya anayejenga kwenye hoja ya "wazee wangu". Really? Hana ushahidi ambao anaweza akautoa mahakamani ukasimama siyo dhidi ya Nyerere wala siyo dhidi ya Kanisa. Ana tuhuma nyingi nzito ambazo zintolewa vidhibiti vingi lakini kila akihojiwa kuhusu hivyo vidhibiti anasepa.

Mohamed Said anapotaja wazee wake anaonesha na nini walikifanya na dalili anaziweka wazi, sasa huyo aliyeambiwa na wazee wake bila kutupa dalili za hao wazee walikuwa kina nani walikuwa na harakati zipi, tumuamini vipi?
 
Huyo shehe wako kakudanganya, mimi ninavyo wajua waisilamu hawana mchezo wakidai hoja yao hatakama haina msingi, wako tayari hatakufa kusimamia anochokiamini hata kama ni ushenzi, yuko teyari kukuua ili usimsumbue, kama huyo shehe wako angekuwa hai nadhani kwa sasa angeshakuwa chriatian tena born again.

Wacha kupoteza mtiririko thread... huna la kuchangia baki msimaji ..
 
Huyo shehe wako kakudanganya, mimi ninavyo wajua waisilamu hawana mchezo wakidai hoja yao hatakama haina msingi, wako tayari hatakufa kusimamia anochokiamini hata kama ni ushenzi, yuko teyari kukuua ili usimsumbue, kama huyo shehe wako angekuwa hai nadhani kwa sasa angeshakuwa chriatian tena born again.
Changia hoja acha kuleta porojo za kipuuzi.
 
Mkuu Jasusi achana na huyu mpuuzi, tatizo ni kwamba watu wengi makini wamekuwa wakiyapuuzia haya makala yake ya kichochezi na hatari yake ni kuwa uwongo ukiachiwa nafasi ya kujirudia rudia mwisho wapo watakaoamini kuwa ni kweli vile. Mimi wakati naanza shule 1953, huyo Mohamed Said alikuwa hata hajazaliwa kama alivyokiri kwenye majibu yake hapo nyuma.

Mimi ni mzaliwa wa kanda ya Ziwa na wakati tunapata uhuru mwaka nilikuwa Sekondari lakini pamoja na kuwa tulikuwa tunafuatilia sana matukio ya kisiasa, sikuwahi kuwaona au hata kuwasikia hao anaodai Mohamed kuwa walikuwa vinara wa harakati za kudai uhuru Tanganyika. Je hii ni kwa sababu nilizaliwa nje ya Dar es Salaam au kwa ni sababu hao wazee wa Mohamed hawakujulikana nje ya Dar es Salaam.

Pamoja na kwamba mwaka 1965 tayari nilikwishahamia Dar es Salaam kuendelea na masomo yangu, sikuyasikia haya majina hadi miaka ya 1970 ! Baada ya hapo nilijaribu sana kuwadadisi wazee mbali mbali, Musoma, Mwanza hadi Bukoba lakini sikuweza kumpata mzee ambaye kwa hakika angeweza kunisimulia mchango wa hawa wazee wa Gerezani alikozaliwa Mohamed Said katika kudai uhuru wa Tanganyika.

TAA kwa upande mwingine ilianzishwa na watumishi wa serikali chini ya utawala wa kikoloni na haihitaji akili yoyote ya ziada kukisia kuwa wengi wa hawa watumishi walikuwa wa aina gani. Ni vigumu sana kusema kwa uhakika ni lini TAA iliyoanzishwa mwaka 1929 ilianza kuwa na msimamo wa kisiasa lakini upepo wa uhuru kwa nchi nyingi za Kiafrika ulianza kuvuma kwa kasi miaka ishirini baadaye.

Harakati za TAA zilipoonyesha dalili ya kudai mambo nje ya haki za wafanya kazi ilibidi kuchagua moja ama ujiuzulu uunge mkono TAA bila kificho au uendelee na ajira lakini usionyeshe wazi msimamo wako. TAA ikawa imefikia kikomo chake na ikawa sasa ni lazima kizaliwe chombo cha kisiasa ambacho malengo yake na dhumuni lake ni kuiondoa serikali ya kikoloni kwa kudai uhuru kamili.

Madai ya Mohamed Said ni kama leo kudai kuwa wote walioko serikalini hawaungi mkono madai ya Chadema dhidi ya serikali, la hasha, wapo lakini wakijionyesha wazi wazi wakati huu nafikiri sote tunajua serikali ya CCM itakavyowashughulikia. Kulikuwa na faida kubwa kwa wanaharakati wengine kubaki ndani ya serikali ya mkoloni kama ilivyo sasa hivi kwa Chadema kuwa na watu wake ndani ya serikali ya CCM.

TAA ya Mwanza mpaka mwaka 1948 ilikuwa na wanachama kama 3,000 lakini mwaka 1952 kwa jitihada za Bomani wanachama wa TAA waliweza kuongezeka hadi kufikia 30,000 na ni mwaka moja baadaye ndiyo Katibu Mkuu wa TAA kama anavyodai Mohamed Said alipotembelea Mwanza. Lakini wakati huo tayari Mwalimu Nyerere anaiongoza TAA baada ya kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Raisi wake.

Walikuwapo watu kama Masanja Shija Raisi wa kwanza wa Victoria Federation Cooperative Union (VFCU) na Makamu wake akiwa Daudi Kabeya Murangira wa Majita aliyeuza boti zake za uvuvi. Jamani wana JF, Tanganyika ilikuwa zaidi ya Wazee wa Mohamed Said wa Gerezani na Kariakoo na ukweli ni kwamba Watanganyika walihitaji kuhamasishwa kutoka Mtwara hadi Sirari, Dar es Salaam hadi Kasulu !

Mwalimu Nyerere hakuwa mtoto yatima, alizaliwa katika ukoo wa kichifu na familia kubwa iliyojaa wazee wa busara wa Kizanaki ambao walimpa baraka zao zote awakabili wakoloni bila woga. Mwalimu Nyere kila aliporudi Musoma hakusahau kufika kuvuka mto Mara kwenda kumsalimia Chifu Odemba Kagose wa Buturi Ujaluoni kupata ushauri wake kwa mambo mbali mbali.

Wana JF, ni wakati sasa wa kuwakataa hawa wachochezi, ni wakati wa kumwambia Mohamed Said kuwa hata uvumilivu una mwisho. Wamekuwa wakipata free ride wakipanda hizi mbegu za chuki miongoni mwa wananchi huku sisi great thinkers tukikaa kando, no enough is enough, ukweli lazima waambiwe hata kama unauma kiasi gani.

Majuzi hapa tumeshuhudia Marekani, watu wa kilichoitwa tea party wakiibua mambo yasiyo na ukweli na kuyarudia rudia hadi wakawateka wale wenye uwezo mdogo wa kufikiri ! Mohamed Said ni wa kuogopwa kama ukimwi ! Mohamed Said sasa aanze kuorodhesha majina ya wazee wake waliojiuzulu kwenye utumishi serikalini ili kupigania uhuru wa Tanganyika ili wajadiliwe hapa JF kwa sababu TAA ilikuwa ya Watumishi wa serikali.

Tumeona Mohamed Said akitubwagia kinaga ubaga vitabu alivyoandika na "papers" alizoandika, mihadhara aliyoitowa / hudhuria vyuo mbali mbali duniani, Jee, na wewe upo tayari kutuwekea hapa ili tujuwe "credibility" yako katika historia? au ndio wakudonyoa donyoa mtandaoni? na ya kuhadithiwa na wazee wako ambao hata dalili hautupi walikuwa na harakati zipi katika siasa au jamii wakati huo? Tuwekee wazi ili tusikuone kama ni mpiga porojo tu.
 
Tatizo lako linaloonekana hapa ni uelewa wako mdogo. Ni kweli kabisa watanganyika walipigania ardhi yao bila kujali dini zao na ndo maana watu wa Dar ambao wengi wao walikuwa wenye maamuzi ya juu walikuwa wa dini fulani lakini walimfuata julius nyerere akiwa wa dini tofauti pale pugu kuja kushirikiana nao. na kumbuka kwanza alikataa kwa sababu yeye alikuwa ameajiriwa na huku akihoji kuhusu kipato lakini wazee wa Dar walijitolea na kuingiza mifukoni kwao na kumlipa nyerere mshahara. Kumbuka hao watu walifikia hata kufunga saumu kumuombea nyerere mema. Ila sasa baada tu ya kupata uhuru, wewe mwenyewe unajionea hali halisi ya hizo jamii. Na ndo maana hata unathubutu bila HATA AIBU kusema eti walikuwa nyuma kisiasa na porojo zingine. unakera kwa kweli.

Mchangiaji mkubwa wa harakati za kugombea uhuru alikuwa akiitwa John, muumini wa kanisa Anglikana (sio mkatoliki au muislamu).

Katibu Mkuu wa kwanza ambae alizunguka nchi nzima kuhamasisha watu alikuwa anaitwa Oscar, muumini wa kanisa Anglikana... lakini hawa uwaoni wewe unamuona yule mzee tunayeambia alikuwa akikusanya nyanya na kabechi kupeleka nyumbani kwa Mwalimu!

Unayekera ni wewe.

Amandla.
 
Naona wengine hawataki tu kumuelewa Mag3. Ni hivi:
  1. Mwaka 1957, kulikuwa na watanganyika waafrika 8,665,336 nchi nzima.
  2. Wasukuma walikuwa asilimia 12.6 ya watanganyika waafrika, kwa hiyo walikuwana idadi ya 1,091,832.
  3. Mwaka huo huo, mji wa Dar es Salaam ulikuwa na watu 128,742; Tanga 38,053; Mwanza 19,877;Tabora 15,361; Moshi 13,726; Arusha 10,038 na Bukoba 5,276.
  4. Mwaka huo ni asilimia 4.4 ya wakazi wa Tanganyika ndio waliokuwa wanaishi mijini.
  5. Kutokana na ukweli huu, hao watu ambao Mohamed Said anawapigia debe waliokuwa wakiishi kwenye kitongoji kimoja tu cha mji wa Dar es Salaam wasingeweza kufanya lolote hata kama waswahili wote wa Dar es Salaam, Tanga na Tabora wangewaunga mkono.
  6. Miaka ile huku walikokuwa wakiishi watanganyika wengi, mswahili alikuwa anachukuliwa kama mtu asiyeweza kuaminika ndiyo maana wakina Sykes wasingeweza kuwashawishi watu wa huko kuungana nao. Mtu ambaye wangemwamini ni mshamba mwenzao na hasa kama atatambulishwa na watu wa kwao wanaowaamini. Mtu mwenye sifa hii alikuwa Julius Kambarage Nyerere na pengine Oscar Kambona. Sehemu za pwani, Bibi Titi Muhamed alichangia mno kuvuta wanawake na wame zao kuingia TANU.
Ndi maana, tunawashangaa watu wanaotaka kutuambia kuwa bila hao jamaa wa gerezani na misheni kota, mpambano usingefanikiwa. Ni matusi makubwa.

Amandla.....
 
Naona wengine hawataki tu kumuelewa Mag3. Ni hivi:
  1. Mwaka 1957, kulikuwa na watanganyika waafrika 8,665,336 nchi nzima.
  2. Wasukuma walikuwa asilimia 12.6 ya watanganyika waafrika, kwa hiyo walikuwana idadi ya 1,091,832.
  3. Mwaka huo huo, mji wa Dar es Salaam ulikuwa na watu 128,742; Tanga 38,053; Mwanza 19,877;Tabora 15,361; Moshi 13,726; Arusha 10,038 na Bukoba 5,276.
  4. Mwaka huo ni asilimia 4.4 ya wakazi wa Tanganyika ndio waliokuwa wanaishi mijini.
  5. Kutokana na ukweli huu, hao watu ambao Mohamed Said anawapigia debe waliokuwa wakiishi kwenye kitongoji kimoja tu cha mji wa Dar es Salaam wasingeweza kufanya lolote hata kama waswahili wote wa Dar es Salaam, Tanga na Tabora wangewaunga mkono.
  6. Miaka ile huku walikokuwa wakiishi watanganyika wengi, mswahili alikuwa anachukuliwa kama mtu asiyeweza kuaminika ndiyo maana wakina Sykes wasingeweza kuwashawishi watu wa huko kuungana nao. Mtu ambaye wangemwamini ni mshamba mwenzao na hasa kama atatambulishwa na watu wa kwao wanaowaamini. Mtu mwenye sifa hii alikuwa Julius Kambarage Nyerere na pengine Oscar Kambona. Sehemu za pwani, Bibi Titi Muhamed alichangia mno kuvuta wanawake na wame zao kuingia TANU.
Ndi maana, tunawashangaa watu wanaotaka kutuambia kuwa bila hao jamaa wa gerezani na misheni kota, mpambano usingefanikiwa. Ni matusi makubwa.

Amandla.....

Naona umekuja na hadithi ndeefu na takwimu nyingi lakini hoja dhaifu sana. Mohamed Said anasema hao wazee wa hicho "kitongoji" ndio waliosahauliwa katika historia na ndio yeye ameamuwa kushika kalamu na kuandika historia yao na vipi walishiriki kikamilifu katika harakati za kujitwalia madaraka na hizo harakati walizianza kabla ya Nyerere kukaribishwa kuungana nao.

Kumbuka kuwa hicho "kitongoji" ndio kilikuwa mstari wa mbele katika harakati, hicho "kitongoji" ndio kilikuwa mwanzo wa vyama kama TAA kilicho zaa TANU, hicho "kitongoji" (Ashaakum si matusi) ndicho kilichomvalisha suruali Nyerere, nasikia alikuja na kaptura, na picha zake za zamani kweli zinaonesha akivaa kaptura ya Khaki na soksi ndefu mpaka karibu ya magoti na viatu vyeusi (kama wale wanaocheza ngoma za Kinyasa kama umebahatika kuwaona).

Kinachowekwa sawa ni kuwa siasa za harakati za kudai madaraka hazikuanzia kwa Nyerere na wala Nyerere sio muasisi wa hizo harakati, hao wazee wa hicho kitongoji ndio waasisi wa harakati zote zilizotufikisha kupewa madaraka na Umoja wa Mataifa. Ni matusi makubwa zaidi kuwaacha hao wazee katika historia hususan kwa mtoto wao Mohamed Said, msomi na mtunzi wa historia anaetambulika vyuo vingi vikuu duniani na ambae ameshaandika vitabu na "papers" nyingi zinazotumika katika vyuo vikuu. Ma sha Allah.
 
nafurahi kuwa zile hoja zinazostahili kujadiliwa na watu wenye hadhi ya forum hii zimeanza kujitokeza tena na kwa kweli zinachokonoa bongo na fikra za watu hadi inatia msisimko.
kuna ushahidi wa wazi kuwa kuna vipande vya historia vimezuiwa ama kupotoshwa kwa makusudi(sielewi ni kwa maslahi ya nani) na tumekuwa miaka yote tukiaminishwa kwamba harakati za kupigania uhuru ziliasisiwa,kuratibiwa na hata kufanikishwa na MWALIMU!! siku zote tumeshindwa kujiuliza maswali madogo tu kuwa kwa nchi kubwa kama TZ ambayo ilikuwa haina miundombinu kama ilivyo sasa, mwalimu aliwezaje kupata fedha,wenyeji n.k mpaka TANUikaweza kukubalika nchi nzima.
nisingepedna kuingia ndani zaidi lakini naamini kitu kimoja ambacho hata mwalimu nyerere alikuwa anakiamini nacho ni ..
wakati makabila madogomadogo, masikini na yasiyo na elimu ya tanzania yakiunganisha nguvu na fedha zao kwa ajili ya mapambano dhidi ya ukoloni,, na wakati mwalimu nyerere akiwa sambamba na wananchi wenzke toka katika jamii hizi masikini,, yale makabila yanayojiona leo hii kuwa ni makabila ya wasomi,wenye fedha na madaraka ndio yaliyokuwa hayataki kujishughulisha na harakati za kupigania uhuru na hawakuwa tayari hata kutoa michango ya fedha kusaidia harakati hizo,kwa vile wengi wao walikuwa wanafanya kazi katika serikali ya kikoloni, hawakuona ubaya wa ukoloni na hivyo hawakuona maana ya uhuru,
wale wachache wenye upeo na uelewa wa hali ya juu( nyerere,paul bomani,rashid kawawa,abbas mtemvu, abdul sykes.oscar kambona n.k) walikuwa wanapata support kubwa toka makabila madogodogo na yasiyo maarufu hivi sasa. ushahidi uko wazi kwani hata mikutano muhimu kabisa ya TANU ilikuwa ikifanyika maeneo hayo,ofisi za kwanza kabisa za TANU zilifunguliwa maeneo hayo na hata wanaharakati wa mwanzo kabisa wa sisa za kudai uhuru walitoka maeneo hayo.
Hata mwalimu angekuwa hai leo na umuulize kama ni busara sisi wa TZ tumchague raisi kutoka makabila fulanifulani(siyataji) mwalimu angesema HAPANA tena kwa herufi kubwa kabisa kwani makabila haya yana sifa kubwa tatu nazo ni 1.usaliti-haswa kama usaliti wake utampa faida ya kifedha 2.uoga- haswa kama uoga wake utamfaya asipoteze kile anachokipata kwa muda huo. 3. ubinafsi- kwa kuamini kwa sababu wao wengi wamesoma na wanafedha basi wao ndio bora na haki kuliko wengine na kudhani kwamba wao ndio mabwana nasisi wengine tubaki kuwa watwana
Wewe nawe una lako utakuwa masalia ya RIZ1 mie naanza hata kuwa na wasiwasi wa hizi harakati za kujivua gamba maana ikumbukwe 2005 tuliskia mengi sana kuhusu Sumaye na Salim lakini baada ya uchaguzi kashfa zile zikaja kujulikana ulikuwa uzandiki na chuki ya kundi fulani dhini ya watu fulani ili Kikwete apite kiurahisi! Sasa tunaanza kuambiwa ati Nyerere hakupewa usaidizi na makabila makubwa wakati ndiyo hayo yaliyompa idadi ya kuimiza wakoloni saa ya uhuru imewadia! Sisi si watoto wadogo humu ndani zile siasa zenu za Bagamoyo za maji taka zitashindwa maana tunawaangalia vizuri na kuwasoma itakapowadia muda mtajua msimamo wetu ni upi! Ila kwa kuwahakikishia tu hoja zenu nyie watu wa Azimio la Bagamoyo hazina mshiko na ni za kitoto sana...
 
Naona umekuja na hadithi ndeefu na takwimu nyingi lakini hoja dhaifu sana. Mohamed Said anasema hao wazee wa hicho "kitongoji" ndio waliosahauliwa katika historia na ndio yeye ameamuwa kushika kalamu na kuandika historia yao na vipi walishiriki kikamilifu katika harakati za kujitwalia madaraka na hizo harakati walizianza kabla ya Nyerere kukaribishwa kuungana nao.

Kumbuka kuwa hicho "kitongoji" ndio kilikuwa mstari wa mbele katika harakati, hicho "kitongoji" ndio kilikuwa mwanzo wa vyama kama TAA kilicho zaa TANU, hicho "kitongoji" (Ashaakum si matusi) ndicho kilichomvalisha suruali Nyerere, nasikia alikuja na kaptura, na picha zake za zamani kweli zinaonesha akivaa kaptura ya Khaki na soksi ndefu mpaka karibu ya magoti na viatu vyeusi (kama wale wanaocheza ngoma za Kinyasa kama umebahatika kuwaona).

Kinachowekwa sawa ni kuwa siasa za harakati za kudai madaraka hazikuanzia kwa Nyerere na wala Nyerere sio muasisi wa hizo harakati, hao wazee wa hicho kitongoji ndio waasisi wa harakati zote zilizotufikisha kupewa madaraka na Umoja wa Mataifa. Ni matusi makubwa zaidi kuwaacha hao wazee katika historia hususan kwa mtoto wao Mohamed Said, msomi na mtunzi wa historia anaetambulika vyuo vingi vikuu duniani na ambae ameshaandika vitabu na "papers" nyingi zinazotumika katika vyuo vikuu. MashAllah.
Mwingine huyu! Kwanini wasimfunze kuvaa kanzu na sio suruali ya Mwingereza (ambapo JKN aliijua alipokuwa huko kwa Mwingereza akisoma) maana mnachopigania hapa ni udini! Mawazo mafupi yanadhani Nyerere alikuwa hajui suruali na sio mtindo wa wakati huo kuvaa kaptula na stockings! Ikumbukwe Nyerere alikuwa ametoka kusoma Scotland! Na kuna uwezekano yeye ndiye alifundisha hao wazee kuvaa vitu kama suruali na chupi maana kanzu zilikuwa zikivaliwa utupu...!
 
Nakubaliana na Bwana Said na wachangiaji wengine kwamba kuna namna mbalimbali za uandishi wa historia. Hata hivyo, historia yoyote lazima ilenge kuunganisha jamii, na siyo kuisambaratisha. Hapo ndipo ninapotofautiana na Said. Nina hakika kwamba hata hicho anachotaka kutuaminisha kwamba ni mchango wa waislamu katika kuleta uhuru, siyo historia kamilifu ya waislamu. Ninachomaanisha hapa ni kwamba yeye anadhani "waislamu" ni wale waishio mikoa ya pwani tu, huku akisahau kwamba kuna waislamu wengine huko Tabora, Ujiji, Singida, Upareni, Karagwe, n.k.

Mimi binafsi sina tatizo na Bwana Said kuandika historia mbadala. Tatizo ninaliliona ni kutumia udini as a point of departure. Hili ni jambo hatari sana, na nashindwa kufahamu kwa nini Bwana Said haoni hatari anayoitengeneza. Said namfahamu binafsi. Ni mtu mzima mwenye akili zake, tena nzuri tu. Kwahiyo napata shida kidogo anapojivunia kwa aina ya uandishi anaofanya. Bwana Said, utambue kwamba duniani kote hakuna historia iliyokamilika. Historia ni mtazamo, na ni hali ya kawaida kabisa wanajamii kutofautiana mitazamo. Hata hivyo, wanajamii hao hao hufikia sehemu ya kukubaliana kutumia aina fulani ya historia, si kwa sababu ni sahihi sana, bali tu kwa sababu inawahakikishia mshikamano, usalama, na mahusiano mema. Historia yoyote yenye dalili za uchochezi haiwezi kukubalika kwa mtu yeyote mwenye akili timamu, hata kama ingekuwa ndiyo tafsiri halisi ya mambo yalivyotokea.

Hebu futailia hata kwenye familia na ukoo wako. Utakuta mambo mengi makubwa yaliyotendeka huko nyuma, lakini, kwa busara za wazee, walidhani wayaache kama yalivyo ili kudumisha mshikamano wa jamii zao. Sote tunajua kilichotokea Rwanda. Tunajua pia gharama kubwa wanayoitumia sasa hivi kujaribu kuirejesha nchi yao kwenye mshikamano. Gharama hizo ni pamoja na kuchambua kitu gani wakiandike na kipi wakiache kwa manufaa ya vizazi vyao vijavyo. Kwa hiyo, akitokea mnyarwanda mmoja mkereketwa, akataka kuandika hali halisi ilivyotokea (mfano, fulani ndiye alimchinja fulani, n.k.), hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kukubaliana kwamba "historia" ya aina hiyo iwe sehemu ya historia rasmi ya nchi. Itatusaidia nini kujua hali halisi, kama hiyo hali halisi mwisho wake ni vurugu, uvunjifu wa amani, na kuvunja utaifa?

Mimi ninawafahamu wazee kadhaa wa kwetu walioshiriki kuleta uhuru wetu, lakini wako nje ya historia rasmi. Pamoja na hayo, sioni busara ya kuchokonoa sana mambo ya aina hiyo kwa sababu mwisho wake ni kuleta vurugu na uvunjifu wa amani. Tanzania ina makabila zaidi ya 120, na naamini kwamba kila kabila lilikuwa na mtu aliyeshiriki kupigania uhuru. Lakini, kama kawaida ya historia zote, huwezi kumuingiza kila mtu. All histories are selective by nature. History is not just the study of the past, but the study of "significant" past. Simaanishi kwamba mchango wa waislamu haukuwa "significant." Naheshimu sana mchango wa waislamu. Hata hivyo, nadhani historia yetu imebeba majina kama Kawawa, Adam Sapi Mkwawa, n.k. Je, hao si waislamu? Waislamu lazima watoke mtaa wa Gerezani?

Bado nisingepata shida kama Bwana Said angejenga hoja kwamba baadhi ya waislamu "muhimu" wamesahauliwa na historia rasmi iliyopo. Hilo linawezekana, kwani history is constantly made and remade. Uandishi wa historia ni kazi ya mwanadamu, na hakuna mwanadamu aliyekamilika. Pamoja na hayo, nisingependa kujiaminisha kwamba wote waliosahauliwa kwenye hitsoria rasmi ya nchi wamesahauliwa kwa sababu ya dini zao, makabila yao, au kanda wanazotoka. Kama Bwana Said anadhani ana ushahidi wa kutosha juu ya hao waliosahaulika, angetusaidia sana endapo angetuhamasisha (na hasa wale wanaohusika na mitaala mashuleni/vyuoni) ili hayo majina anayodhani yamesaulika yaingizwe kwenye mchakato wa mitaala mipya ijayo. Hili linaweza kufanyika bila uchochezi wala kupandikiza mbegu za udini wala mfarakano. Nchi yetu tayari iko ICU kutokana na ufisadi na "siasa uchwara." Tukiongeza na haya ya udini sijui tutafika wapi.


Nawasilisha.
 
mwingine huyu! Kwanini wasimfunze kuvaa kanzu na sio suruali ya Mwingereza (ambapo JKN aliijua alipokuwa huko kwa Mwingereza akisoma) maana mnachopigania hapa ni udini! Mawazo mafupi yanadhani Nyerere alikuwa hajui suruali na sio mtindo wa wakati huo kuvaa kaptula na stockings! Ikumbukwe Nyerere alikuwa ametoka kusoma Scotland! na kuna uwezekano yeye ndiye alifundisha hao wazee kuvaa vitu kama suruali na chupi maana kanzu zilikuwa zikivaliwa utupu...!
GU
Bora umemjibu huyo bibi .... Nilishangaa sana huyu mama alivyokurupuka Udini ni kitu kibaya sana .... Yaani Nyerere katoka scotland na alikuwa ni mwalimu halafu unasema alikuwa hajui kuvaa suruali. Sasa hao wanafunzi aliokuwa anawafundisha si walikuwa hawavai nguo kabisa.. FF mama usikurupuke kumbuka kuwa hapa wapo watu makini
 
Back
Top Bottom