Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Naona wengine hawataki tu kumuelewa Mag3. Ni hivi:
  1. Mwaka 1957, kulikuwa na watanganyika waafrika 8,665,336 nchi nzima.
  2. Wasukuma walikuwa asilimia 12.6 ya watanganyika waafrika, kwa hiyo walikuwana idadi ya 1,091,832.
  3. Mwaka huo huo, mji wa Dar es Salaam ulikuwa na watu 128,742; Tanga 38,053; Mwanza 19,877;Tabora 15,361; Moshi 13,726; Arusha 10,038 na Bukoba 5,276.
  4. Mwaka huo ni asilimia 4.4 ya wakazi wa Tanganyika ndio waliokuwa wanaishi mijini.
  5. Kutokana na ukweli huu, hao watu ambao Mohamed Said anawapigia debe waliokuwa wakiishi kwenye kitongoji kimoja tu cha mji wa Dar es Salaam wasingeweza kufanya lolote hata kama waswahili wote wa Dar es Salaam, Tanga na Tabora wangewaunga mkono.
  6. Miaka ile huku walikokuwa wakiishi watanganyika wengi, mswahili alikuwa anachukuliwa kama mtu asiyeweza kuaminika ndiyo maana wakina Sykes wasingeweza kuwashawishi watu wa huko kuungana nao. Mtu ambaye wangemwamini ni mshamba mwenzao na hasa kama atatambulishwa na watu wa kwao wanaowaamini. Mtu mwenye sifa hii alikuwa Julius Kambarage Nyerere na pengine Oscar Kambona. Sehemu za pwani, Bibi Titi Muhamed alichangia mno kuvuta wanawake na wame zao kuingia TANU.
Ndi maana, tunawashangaa watu wanaotaka kutuambia kuwa bila hao jamaa wa gerezani na misheni kota, mpambano usingefanikiwa. Ni matusi makubwa.

Amandla.....
Asante Fundi Mchundo na sasa umefika wakati wa kutoa somo kwa watu kama Mohamed Said ambao porojo za mitaani za wazee wao wa Gerezani wanaamini zingeweza kuwaletea uhuru Watanganyika.
Fact No 1: TAA ilikuwa ni chama cha Wafanya kazi serikalini kama zilivyokuwa vyama vingine tu vya wafanya kazi kama wa reli, madereva, makuli, wafanyakazi viwandani n.k.
Fact No 2: TAA haikujisgughulisha katu na mambo ya kisiasa kabla ya 1952 na hiyo ilibainishwa fika katika katiba yake.
Fact No 3: Wafanyakazi wote kwa ujumla wao kwa wakati huo walikuwa ni asilimia ndogo sana ya Watanganyika.
Fact No 4: Wanachama wa TAA kwa ujumla wao walikuwa asilimia ndogo sana ya wafanyakazi nchi nzima ya Tanganyika.
Fact No 5: Ni Mwalimu Nyerere aliyeleta changamoto ndani ya TAA na hasa wazo la kupigania uhuru.
Fact No 6: Changamoto alizoleta Mwalimu ndani ya TAA ndio chanzo cha kukubalika kwake na kuchaguliwa kuwa Raisi wa kwanza wa TAA iliyokuwa na mwelekeo wa kisiasa.
Fact No 7: Mwalimu hakusita kuionya TAA kwamba kama haikuwa tayari kuwashirikisha Watanzania walio wengi basi haitafika popote. Hawa Watanganyika aliokuwa akiwasema Mwalimu ni wakulima kwa ujumla wao kupitia vyama vyao vya Ushirika.
Fact No 8: Baada ya hiyo Changamoto, Mwalimu ndiye alikabidhiwa jukumu la kuandaa katiba mpya iliyokuja kuzaa chama cha siasa kilichoshirikisha wakulima na wafanyakazi, TANU.
Fact No 9: Majimbo yaliyoongoza kwa idadi ya watu na vyama vya ushirika vya wakulima yalikuwa majimbo matatu tu - Jimbo la Ziwa, Jimbo la Kaskazini na Jimbo la Nyanda za juu Kusini.
Fact No 10: Hivyo vyama vya Ushirika vya Wakulima vilijiunga na TAA/TANU kwa ushawishi wa mtu moja tu waliyemwamini, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mwaka 1955 vyama vingine vyote vya Wafanyakazi navyo vikajiunga na kukazaliwa a united front - Tanganyika Federation of Labour.

Mpaka hapo yatosha kwa leo nitaendelea...............
 
mwingine huyu! Kwanini wasimfunze kuvaa kanzu na sio suruali ya Mwingereza (ambapo JKN aliijua alipokuwa huko kwa Mwingereza akisoma) maana mnachopigania hapa ni udini! Mawazo mafupi yanadhani Nyerere alikuwa hajui suruali na sio mtindo wa wakati huo kuvaa kaptula na stockings! Ikumbukwe Nyerere alikuwa ametoka kusoma Scotland! na kuna uwezekano yeye ndiye alifundisha hao wazee kuvaa vitu kama suruali na chupi maana kanzu zilikuwa zikivaliwa utupu...!

Unanchekesha, huko Scotland hujui wanachovaa?
nyerere_1954.jpg

 
Shukran sana Mzee Mwanakijiji.

Hayo ndiyo hasa ninayosema wakti wote. kama unaona kuwa kuna mushkeri wowote katika makala yake basi mtu makini anachukua jukumu la kwenda kuwahoji hao uliowataja na kuja na majibu muafaka wa makala ake na kuleta weledi mkubwa wa kuonyesha kuwa umeifanyika kazi waraka wake katika kuweka historia iliyo sahihi na kusiwe na kuchakachuwa kwa aina yoyote.

sasa suala hilo linabaki kwetu hadhira kuwauliza hao ili kujua ukweli au uchakachuaji wa makala yake ili tuweze kumpongeza au hata kumlaani kwa kupotosha historia.

ndio maana kila wakti nasimama kusema kuwa kazi ya mwandishi ni kuandika pasi na kuegemea upande wowote ila kazi ya uamuzi ni a wasomaji.

Sasa tusimame na kuamua kwa hoja zenye mashiko.

Ahsante kwa ufafanuzi wako.

Mwalimu, wajua vyema kabisa jukumu la kwanza ni kuwa huru kwa pande zote. Jukumu la M. Said ni kuhakikisha kuwa anafanya kazi hiyo kwa huo uhuru na siyo kutegea kuwa mtu mwingine atafanya kile ambacho yeye anataka kufanya. Huwezi kwenda kutafuta ushahidi wa tukio halafu unapofika pale unaanza kuchagua:

a. Kisu chenye damu nitachukua lakini panga lenye damu sitachukua
b. Nitamhoji aliyekuwa amesimama kushoto halafu yule aliyesimama kulia sitomhoji
c. Nitauliza jirani wa upande wa kushoto lakini yule wa nyumba ya mbele au wa upande wa kulia sitomhoji.

Ukakusanya huo ushahidi ukaupeleka watu wauone na ukatengeneza kesi vizuri kweli. Ukasema "huu ndio ushahidi nilionao". Sasa watu wa upande wa utetezi - tena kwenye preliminaries za disclosures - wakakuhoji - kwanini "hukumhoji aliyesimama upande wa kulia au wa kushoto au kwanini hukuuchukua upanga? halafu wewe - ukiwa msomi na mwelewa - unasema "ushahidi nilioupata huo ninatosheleza wale wa utetezi wakitaka waende na wenyewe wakaulize.

Well hili si la kufikirika. Juzi Italia wamemuachia binti wa Kimarekani kwenye tuhuma za uuaji. Na walimuachia kwa sababu moja tu Polisi walikuwa sloppy and unprofessional; waliacha crime scene ikata contaminated kiasi kwamba walijenga "reasonable doubt" kwa jaji. Ushahidi wao japo ulikuwa mzuri sana haukuwa mzuri wa kutosha kumfunga mtoto wa watu maisha!

Sasa Bw. Said anafanya vyema kutuletea ushahidi lakini ushahidi anaoleta ni ule unaosema "Uislamu..." au "Waislamu..." na ushahidi mwingine wowote anaukataa au anatuambia "si mkaende kuuleta nyie". Sasa ndugu yangu wewe ni mwanasheria unajua vyema kuwa huo si ushahidi tena bali ni ushahidi wenye ajenda siyo ya kutenda haki tena bali ya kupindisha haki. Kwamba, tunataka Nyerere afungwe na kutupwa maisha kwa sababu ya ushahidi dhaifu.

Ninachosema ni kuwa kabla hujasema sisi wengine twende tukatafute huo ushahidi mwingine tukubaliane kumkata M. Said atupe ushahidi wote; akisema Mwinyi alisema - tunataka aende kumhoji Mwinyi; akisema Mama Maria alisema atuambie alimhoji lini; haitoshi kusema ut "Mzee x,y alimuambia babangu na babangu alinisimulia" halafu sisi na akili timamu tukubali tu! Ni sawasawa na kutuchezea akili. Kwa mfano, mojawapo ya vitabu vinavyoangaliwa kuwa vinaonesha jinsi kanisa lilivyotenda na kujiweka juu ni kile cha John Sivalon. Kitabu hiki kimekuwa kama msahafu wa aina yake kwa wale wenye kuamini juu ya Mfumo Kristu na baadhi yao ni watu wenye elimu ya akhera na ya dunia. Lakini je, ni yote yanayosemwa kwenye kitabu hicho ni ya kweli pasi na shaka? Au yanachukuliwa kuwa ni ya kweli na sahihi kwa sababu aliyeandika ni Padre?

Sivalon ameishi Tanzania kwa muda mrefu, amepata Masters yake ya Sociology UDSM na kufundisha hapo vile vile kwa muda mrefu tu je M. Said amewahi kuchukua muda kwenda kumhoji kuhusu yaliyomo kwenye kitabu cha Kanisa Katolikia na Siasa za Tanzania Bara? Of course, waweza kuniambia - Kwanini wewe usimtafute - which will bring me back to the question of selective process ya kuchagua ushahidi gani unafaa.

Tumhumize ndugu yetu ili historia yake ionekane kweli ni historia na siyo histohisia aweze kuzungumza na wale ambao bado wako hai na wanajatwa kwenye kitabu chake bila kumpa undani wa yale anayodai watu hao aidha wamesema au kufanya. Unaonaje hili?
 
Fundi Mchundo,

Nakuunga mkono katika juhudi hizi za kuandika historia ya nchi yetu
na kumpa kila mtu haki yake. Nimegundua kosa kuhusu katiba.
Nyerere hakutayarisha katiba mpya soma hapa chini:

"Uongoziwa TAA haukurasimu katiba mpya. Katiba ya TANU ilinukuliwa neno
kwa neno kutokaConvention Peopleís Party (CPP) ya Kwame Nkrumah, kwa
kutia TANU mahali paCPP."

Kuhusu TFL hii ilikuja baadae. Mwaka 1955 chama kilichoanzishwa kilikuwa

Tanganyika Railway African Union (TRAU) babu yangu Salum Abdallah
akiwa Mwenyekiti muasisi na katibu wake Kassanga Tumbo.


Mohamed

 
Tumeona Mohamed Said akitubwagia kinaga ubaga vitabu alivyoandika na "papers" alizoandika, mihadhara aliyoitowa / hudhuria vyuo mbali mbali duniani, Jee, na wewe upo tayari kutuwekea hapa ili tujuwe "credibility" yako katika historia? au ndio wakudonyoa donyoa mtandaoni? na ya kuhadithiwa na wazee wako ambao hata dalili hautupi walikuwa na harakati zipi katika siasa au jamii wakati huo? Tuwekee wazi ili tusikuone kama ni mpiga porojo tu.
Yaani wazee wa Mohammed peke yake ndio credible. Mwingine akielezea aliyosimuliwa na wazee wake unauliza credibility yake? Talk about double standards.
 
Yaani wazee wa Mohammed peke yake ndio credible. Mwingine akielezea aliyosimuliwa na wazee wake unauliza credibility yake? Talk about double standards.

Mohamed Said kaelezea vitabu alivyokwishaandika, papers zake, vyuo na makongamano tofauti duniani alivyohudhuria.

Kawataja wazee wake ni kina nani na walikuwa wanafanya nini.

Huyo Mag3 hakuna kimoja katika haya aliyotuwekea wazi hata jina lake na nasaba yake hajaiweka wazi.

Hatuna reference yake hata moja ya amma kwa kitabu au paper ya history. Isitoshe, ameanza kwa kejeli na matusi, jee hapo kuna "credibility" yoyote ambayo kwa ujasusi wako unaweza kuitetea?
 
Fundi Mchundo,

Nakuunga mkono katika juhudi hizi za kuandika historia ya nchi yetu
na kumpa kila mtu haki yake. Nimegundua kosa kuhusu katiba.
Nyerere hakutayarisha katiba mpya soma hapa chini:

"Uongoziwa TAA haukurasimu katiba mpya. Katiba ya TANU ilinukuliwa neno
kwa neno kutokaConvention Peopleís Party (CPP) ya Kwame Nkrumah, kwa
kutia TANU mahali paCPP.
"

Kuhusu TFL hii ilikuja baadae. Mwaka 1955 chama kilichoanzishwa kilikuwa

Tanganyika Railway African Union (TRAU) babu yangu Salum Abdallah
akiwa Mwenyekiti muasisi na katibu wake Kassanga Tumbo.


Mohamed


Iliamuliwa na kina nani kuwa katiba ya TANU inukuu toka kwa ile ya Ghana?
 
Wanaukumbi,

Nimeona mahala pawili katajwa Oscar Kambona kama Katibu Mwenezi
wa kwanza wa TANU. Hili ni kosa. Nafasi hiyo ilishikwa na kwa mara ya
kwanza na Zuberi Mtemvu. Mtemvu aliingia TANU hata kabla chama
chenyewe akijaanzishwa. Halikdhalika safari ya kwanza kuitangaza TANU
ilifanywa na Mtemvu na Nyerere Morogoro. Mengine soma hapa chini:

"Mtemvu ni mmoja wa wanachama wa mwanzo shupavu na msomi kabisa kujiunga na TANU.Katika nyaraka za Sykes kuna “note” ya mwaka 1954 aliyoandika Zuberi Mtemvu kwapenseli kumpelekea Ally Sykes akimtaarifu kuwa kakutana na Ally Mwinyi Tambwena amemweleza kuhusu chama kipya cha siasa kinachotaka kuanzishwa. Katika“note” ile Mtemvu anamfahamisha Ally Sykes kuwa Ally Mwinyi Tambwe kakubalikukiunga mkono chama hicho kipya. Mtemvu alimjulisha Ally Sykes kuwa Tambwekukubali kujiunga na TANU lilikuwa jambo zuri sana. Tambwe, Mngazija wakati huo alikuwa katibu waAl Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika. Tambwe alimwahidi Mtemvu kuwaingiza TANUwanachama wengine wanaounga mkono harakati zile. Katikasiku za mwanzo nafasi ya katibu mwenezi ilikuwa ikishikwa na viongozi mbalimbali baina ya Mtemvu Denis Phombeah, Oscar Kambona,
Iddi Faizi Mafongo naStephen Mhando."

Mohamed


 
Iliamuliwa na kina nani kuwa katiba ya TANU inukuu toka kwa ile ya Ghana?

Mwanakijiji,

Nimeliona kosa na nimeeleza kile ninachokijua ili kusahihisha.
Haikuwa nia yangu kuwa tuingie katika mabishano kwa hilo.

Hiyo katiba ilianza kushughulikiwa siku nyingi sana hata kabla
Nyerere hajakutana na Abdulwahid Sykes.

Najua nani aliyekuwa akiifanyia kazi ile katiba lakini sitokwambia
kwa kuchelea kukuweka katika dhiki.

Naomba uridhike na ukweli kuwa Nyerere hakuandika katiba.

Mohamed
 
Mohamed Said na wapenzi wake wanataka kupaka rangi upepo siyo? Ni kupoteza muda kutaka kuandika historia mara mbili. Kimsingi anachotetea Mohamed si kingine bali udini uchwara ambao hauwezi kutusogeza mbele. Kwanini haelekezi mawazo yake kwenye kupinga ufisadi unaofanywa na watatwala wetu waislamu na wakristo? Hizi siasa za ki-al-Shabaab haziwezi kufua dafu kwa Tanzania ya sasa. Na isitoshe kwa wanaofuatilia maandiko ya Mohamad Said, mara zote amekuwa na obssessed na kumchukia Mwalimu Nyerere ambaye historia yake inajulikana. Ingawa kila mtu ana haki ya kuwa na msimamo, mawazo na hisia zake,hivi vitu vinapo kuwa mgando kiasi fulani maana ya kuwa navyo inapotea. Huwezi ukamfundisha samaki kuogelea hata ungekuwa mvuvi au baharia. Watanzania wanajua historia yao na cha mno si kwamba uhuru wetu ulidaiwa na waislam tena wa Dar Es Salaam. Mohamad Said aende mikoani aone wakereketwa waanzilishi wa Tanu na michango mikubwa waliyotoa. Ingawa anaowataja siku zote kama vile Sykes na wengine walitoa michango, hawakuwa peke yao. Kuna hadi wahindi waliotoa michango ukiachia mbali wazungu waliopigania uhuru kama akina Breyson, Manning na Bablo Johannse aliyekuwa katibu wa Nyerere kutaja kwa uchache. Mohamad Said aachane na mawazo kufu na mfu kama ya akina Ditopile waliokuwa wakijivunia kuwaambia watu kuwa wamekuja na tongotongo wakasahau kuwa nao walitimuliwa toka jijini na kuishia huko Kazimzumbwi kutokana na kutokuwa na mipango madhubuti ya kupata riziki. Tusiandike makala bali kumshauri Mohamad Said kama anatafuta kuzeeka basi atafute jambo jingine kama ni kugombea ushehe Bakwata au kwenda kujilimia magimbi huko kwao. Huu ni ushauri wa bure lakini wa bei mbaya.
 
Wanaukumbi,

Nimeona mahala pawili katajwa Oscar Kambona kama Katibu Mwenezi
wa kwanza wa TANU. Hili ni kosa. Nafasi hiyo ilishikwa na kwa mara ya
kwanza na Zuberi Mtemvu. Mtemvu aliingia TANU hata kabla chama
chenyewe akijaanzishwa. Halikdhalika safari ya kwanza kuitangaza TANU
ilifanywa na Mtemvu na Nyerere Morogoro. Mengine soma hapa chini:

"Mtemvu ni mmoja wa wanachama wa mwanzo shupavu na msomi kabisa kujiunga na TANU.Katika nyaraka za Sykes kuna "note" ya mwaka 1954 aliyoandika Zuberi Mtemvu kwapenseli kumpelekea Ally Sykes akimtaarifu kuwa kakutana na Ally Mwinyi Tambwena amemweleza kuhusu chama kipya cha siasa kinachotaka kuanzishwa. Katika"note" ile Mtemvu anamfahamisha Ally Sykes kuwa Ally Mwinyi Tambwe kakubalikukiunga mkono chama hicho kipya. Mtemvu alimjulisha Ally Sykes kuwa Tambwekukubali kujiunga na TANU lilikuwa jambo zuri sana. Tambwe, Mngazija wakati huo alikuwa katibu waAl Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika. Tambwe alimwahidi Mtemvu kuwaingiza TANUwanachama wengine wanaounga mkono harakati zile. Katikasiku za mwanzo nafasi ya katibu mwenezi ilikuwa ikishikwa na viongozi mbalimbali baina ya Mtemvu Denis Phombeah, Oscar Kambona,
Iddi Faizi Mafongo naStephen Mhando."

Mohamed



Mtemvu alikuwa Katibu Mwenezi wa TANU kwa mara ya kwanza mwaka gani na Oscar alishika nafasi hiyo kwa mara ya kwanza mwaka gani?
 
Mohamed Said kaelezea vitabu alivyokwiandika, papers zake, vyuo na makongamano tofauti duniani alivyohudhuria.

Kawataja wazee wake ni kina nani na walikuwa wanafanya nini.

Huyo Mag3 hakuna kimpja katika haya aliyotuwekea wazi hata jina lake na nasaba yake hajaiweka wazi.

Hatuna reference yake hata moja ya amma kwa kitabu au paper ya history. Isitoshe, ameanza kwa kejeli na matusi, jee hapo kuna "credibility" yoyote ambayo kwa ujasusi wako unaweza kuitetea?

Acha uvivu. Angalia:


[URL]http://www.paulbomani.com/quotes.htm


[/URL]
 
Mwanakijiji,

Nimeliona kosa na nimeeleza kile ninachokijua ili kusahihisha.
Haikuwa nia yangu kuwa tuingie katika mabishano kwa hilo.

Hiyo katiba ilianza kushughulikiwa siku nyingi sana hata kabla
Nyerere hajakutana na Abdulwahid Sykes.

Najua nani aliyekuwa akiifanyia kazi ile katiba lakini sitokwambia
kwa kuchelea kukuweka katika dhiki.


Naomba uridhike na ukweli kuwa Nyerere hakuandika katiba.

Mohamed

sasa hapo ndugu yangu ndio wengine tunapata tatizo kwa sababu si kwamba unataka kutusaidia kujua bali kutuchagulia unachotaka tujue. Miye swali langu kwa kweli ni genuine ili kuelewa lakini kuniambia hutaki kuniambia ili usije nitie dhiki ni kama unaona unataka kunikomoa na hivyo kuendeleza kitu cha "selective history" ambayo unatupatia. Nyerere hakuandika yaweza kabisa kuwa kweli lakini alikuwa na mchango gani katika uandishi wa hiyo katiba? Je huyo aliyeandika (ambaye humtaji) alimshirikisha Nyerere au kiongozi mwingine yeyote au alijifanyia mwenyewe hiyo kazi chumbani na kuwaletea wakaipitisha tu?
 
Naona ROHO zenu zishaanza KUKUUMENI. Bado tutakuja na vitabu maalum ambayo vitafundishwa ktk shule zote za Kiislamu na hizo zenu za Kanisa ili mpate kujua ukweli. WTZ washaanza kujua ukweli kwamba Nyerere ni MYTH ya Wakatoliki.

MYTH za UHURU wa TZ

Historia feki ya Nyerere kwamba ndiye aliyekuwa muasisi wa Taifa so called "Baba wa Taifa?"

Nyerere katoka ktk ELITE family, baba yake alikuwa CHIFU; lakini ktk historia tunaambiwa alikuwa "mlalahoi"

Nyerere alitumiwa na Wakatoliki Wazungu lakini tunaambiwa alikuwa hapendi "Wazungu?" kwa sababu alikuwa na msimamo mkali kuhusu Ubepari.

Lakini wamesahau Nyerere alipelekwa kusoma ktk shule ELITE huko ULAYA lakini tunaambiwa alikuwa hataki kitu chochote kutoka kwa Wazungu.

Najua wadau mnazo MYTH nyingi sana za Nyerere na UHURU.
 
Duh nafyonza elmu taratibu.
Naufuatilia huu mjadala kwa karibu sana. Ila mkuu unaweza kudondosha "Mzozo wa ardhi ya wameru?" Nadhani litakuwa jambo la thawabu tukimkumbuka Kirilo Japhet kwenye harakati zetu za uhuru.
 

1. Wakuu hivi hii historia inayodaiwa kupotoshwa imeandikwa katika vitabu gani? Orodha tafadhali.

2. Kilichopotoshwa ndani ya vitabu hivyo ni nini?

3. Waandishi wa vitabu hivyo ni akina nani? Na waliandika kwa maelekezo ya nani?

4. Ni vitabu vipi tunaruhusiwa kuviamini kuwa vimeandika historia ya kweli kuhusu uhuru wa Tanganyika? Au havipo?

5. Nini maoni kuhusu kupindishwa kwa historia hii ya uhuru wa Tanganyika kutoka kwa wanaharakati walio hai mpaka sasa?

6. Nini mchango wa wanachi wa kawaida "accross" Tanganyika katika harakati hizi za uhuru?????

7. Kuna kumbukumbu yeyote ya mikutano baina ya serikali ya kikoloni na viongozi wa kitanganyika kabla ya TANU kuhusu uhuru?

8. Ili tuwe "specific" zaidi uhuru wa Tanganyika uliodaiwa kabla ya kuundwa kwa TANU katika historia "stahili" ulidaiwaje? Kwa maandamano?, kwa sabotage? Kwa bunduki? Kwa mikutano?

9. Je ni akina nani walioshiriki katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika wakatoswa kwenye serikali ya Tanganyika huru? Na ni kwa sababu gani?

10. Nini kifanyike kuhakikisha historia ya uhuru wa Tanganyika inawekwa sawa na haipindishwi tena kama ilivyo katika madai ya baadhi yetu humu.

 
Naona ROHO zenu zishaanza KUKUUMENI. Bado tutakuja na vitabu maalum ambayo vitafundishwa ktk shule zote za Kiislamu na hizo zenu za Kanisa ili mpate kujua ukweli. WTZ washaanza kujua ukweli kwamba Nyerere ni MYTH ya Wakatoliki.

MYTH za UHURU wa TZ

Historia feki ya Nyerere kwamba ndiye aliyekuwa muasisi wa Taifa so called "Baba wa Taifa?"

Nyerere katoka ktk ELITE family, baba yake alikuwa CHIFU; lakini ktk historia tunaambiwa alikuwa "mlalahoi"

Nyerere alitumiwa na Wakatoliki Wazungu lakini tunaambiwa alikuwa hapendi "Wazungu?" kwa sababu alikuwa na msimamo mkali kuhusu Ubepari.

Lakini wamesahau Nyerere alipelekwa kusoma ktk shule ELITE huko ULAYA lakini tunaambiwa alikuwa hataki kitu chochote kutoka kwa Wazungu.

Najua wadau mnazo MYTH nyingi sana za Nyerere na UHURU.

Sijui alikuambia nani hayo madudu? Na itasikitisha kama uliamini hayo bila hata kujiuliza. Aliyechukia wazungu angawaweka kwenye nafasi za u waziri kwenye serikai yake? Hivi hujajiuliza kwanini Wazungu wengi hawakukimbia Tanzania baada ya uhuru kwa kuhofia kubaguliwa na watu weusi walio wengi? Sasa leo unaambiwa Nyerere alichukia Uislamu na Waislamu unakubali tu bila kujiuliza... ?
 
Back
Top Bottom