Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa


Inna Lillahi wainna ilaihi rajihunnah
 
Nauliza hv nyerere ndo aloteta huo mfumo kristu.?wakolön walitugawa ili watutawale na ikumbukwe kwamba wakolon walikuwa wazungu kwa hyo ni wakristu..nyerere kajitahid kuweka usawa kupitia azimio la arusha mkaleta la zanzibar afu mnasema nyerere kaleta mfumo kristu asa angewasaidiaje..au labda mtu aniambie kuwa nyerere ndo alovunja azimio la arusha?
 

Hhahahaaha...sasa MS you are a very strange person bro! kwani huyu Magotti anatofauti gani na wewe? It is the precise thing of what people have accused you in this thread. Kuandika bila kuhoji upande wa pili! Perhaps, na wewe ungetake trouble kufanya yale unayomtuhumu Magotti tungekuwa na narrative tofauti. Lakini majibu yako ni yale ya 'na wengine wakaandike historia yao...' Basi na Magotti atasema hivyo hivyo!!

Nafurahi kuona kwamba na wewe umeigundua hiyo double standard, tragically wewe hujioni kwamba you have done exactly the same thing! Na implication yake ingawa unai admitt kwenye kitabu cha Kawawa..kwako huioni! Duh...

Tatizo MS you 'know alot of things', lakini unasahau kwamba humu JF watu tunasoma kama wewe na kufanya 'analysis' so we dont simply swallow stuffs! Ndo maana watu hapa wanakujibu kwa hoja. Strange world? uhhh???
 
Hakuna kinachobadilishwa wala kubatilishwa bali inaongezwa yale yalio ondolewa kwa makusudi kabisa kwa nia maalu.

Kumbuka hata mbuyu ulianza kama mchicha. Miaka 50 kazi kwenu kila kitu kipo hadharani.
Yaliondolewa wapi na nani? Tunamshukuru Mungu asiye na DINI ambaye ameifikisha TANZANIA hapa ilipo. Hatuna DINI ya TAIFA, hatuchagui wala kuteua viongozi wetu kwa kushauriana na Maaskofu wala Masheikh. Tunachanganyika vilivyo kuanzia ndoa, familia, makazi, shule, ajira, misiba, starehe, humu JF, michezo, miziki,....
 

Soma vizuri posts utajuwa tatizo liko wapi. Kwa ufupi azimio la arusha lilikuwa ni kuuleta mfumokristo "mkitaka msitake" na si kuliondoa.
 

Soma kitabu cha Sivalon.
 

Mkandara,

ndugu yangu elewa utafiti siku zote unapingwa kwa utafiti na sio hisia kutoka kichwani mwako. Kama unavyomuona Mohamed Said anaweka mpaka data na source zake kwetu sote na wewe jitahidi sana kama una data au source zozote tuwekee.

Kwani wengi tunamjua Nyerere akitaka lake liwe halitumia kila hila na linafanikiwa. Enzi za Nyerere saa hizi Mohamed Said tusingekuwa nae kabisa au sote hapa tungekuwa tunamkimbia. Kwani Nyerere angetukama wote pamoja na jamii na maswahiba zake wote kisha kutupoteza. Ni nani asiyejua hayo.

Ni nani asiyejua kuwa Nyerere hakupenda kufanya kazi na watu wasomi wanaojiamini alipenda wasomi wasiojiamini na waoga ili aweze kuwaendesha atakavyo yeye. Na hicho ndio mbegu mbaya aliyoipandikiza kwenye uchumi wa Tanganyika mpaka sasa mnakuwa masikini asiyat.

Kumbuka sasa tupo dunia ya uwazi na ukweli. Mohamed said anafanya kazi ambayo wengi waislam walishindwa kuifanya. Kwani waislam wameamrishwa wanapoona maovu basi wayakemee ima kwa mikono yao, au mdomo wao au kwa imani dhaifu kuyachukia moyoni mwao.

Mohamed amekemea kwa mkono wake kwa kupoteza muda na mali zake (fedha) kufanya utafiti na kisha kuuweka hadharani na hata JK Nyerere ameupata na kuusoma kwa kina sana lakini hakuwa na la kukosoa. Kwani kila kitu kina karne yake.

nakupongeza sana Mohamed Said. Allah akubariki sana.
 

Katika hili ahali yangu hakuna siasa hapa.
Kinachotakiwa ni kuhakikisha keki ya taifa inaliwa na wote kwa usawa pasi na dhulma wala ubaguzi wa aina yoyote. Kwani siku zote kwenye dhulma hakuna haki. Na pasipo na haki basi hakuna amani.

Sasa sote tuombe amani ya kweli sio ya kinafiki.
 

Barubaru,

Amin, Amin, Amin ndugu yangu Amin.
Allah aturidhie na atupe ushindi na aiweke nchi yetu kwenye salama na amani kila mtu aishi kwa haki na usawa na dhulma zote zitokomee.

Amin.

Mohamed
 
Barubaru,
Ukiweka kando chuki zako mbili dhidi ya Mwalimu. Ukaufungua ubongo wako utagundua kuwa UNAONGOPA na KUMSINGIZIA mambo mengi sana Mwalimu. Mwalimu aliwaweka ndani wahalifu tu. Mwalimu wala hakuwachukia wasomi. Alijenga vyuo vikuu vya nini sasa! Mohamed huyu unayemsema hapa amekuwepo tangu enzi za Mwalimu na UDINI wake huuhuu. Na sio yeye tu.
Najua unamchukia Mwalimu kwa Ukristo wake na pia kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao ninyi wa-Oman na Waarabu wengine mnadhani hata mapinduzi ya Zanzibar yana mkono wa Mwalimu. Hamtamsamehe. Mkipata mijadala na hoja kama hii mnakomaa kwelikweli.
 

Siku zote anayesema fulani mchawi basi mchawi ni yeye. Kwani alijuaje kuwa ni mchawi?.

Tatizo ni wavivu wa kusoma vitabu bali wamezoea kubebwa na mfumo wa kupenda kurahisishiwa kila kitu. Msomeni kitabu cha Padre Silvalon ameweka bayana kila kitu.
 

Masanja,

Mei sisomwi JF tu.
Hapa naja kwa msimu.

Mimi kila wakiingia wanafunzi wapya vyuoni Marekani na Ulaya na ikiwa somo watakalochukua ni African History, Islam and Politics basi jua nasomwa na kitabu changu mwalimu anafundishia.

Hilo la kwanza mimi nina "paper" katika somo hili hesabu yake sizijui.

Jambo la pili.

Hushangai kila akitajwa mtu nakuwekea bandiko lake tena ni "paragraph" moja tu.
Huu ni utafiti wa "lifetime."

Fananisha utapata jibu.

Mohamed
 

WC,

Alokwambia historia haijabadilika nani?
Toka huko uliko fungua macho, sikiliza, soma utatambua nyakati zimepita.

Kuna shule za Waislam zinatoa zawadi ya Sheikh Hassan bin Amir kwa mwanafunzi bora.
Kuna zawiyya zinaitwa Sheikh Suleiman Takadir nk. nk.

Kabla ya sasa ulisikia neno "mfumokristo" likirushwa hewani na radio mubashar "live?"

Ndugu yangu uko dunia gani?

Mohamed
 

MM,

Shida kubwa itakukuta kusimama na mimi katika mnakasha.
Nimekusoma.

Huwezi kuivunja historia niloandika kwa bandiko katika JF.
NARUDIA...andika kitabu au angalau "paper."



Mohamed
 

WC,

Huko ni kuishiwa na Sera.

Lakini nitakudondolea kidogo tu. Mimi nimefanya kazi enzi za Nyerere mara tu baada ya kumaliza UDSM shahada ya uchumi na nimefanya nae kwa ukaribu sana nikiwa kitengo cha Bajeti wizara ya fedha (muungano). Namjua vilivyo.

Lakin tuache hayo. Mimi nakwambia mtu yeyote makini na aliyekuwa anajiamini na kuthamini taratibu na kaanun za taaluma yake Nyerere hakumpenda .

Mfano ni waziri wetu wa fedha Edwin Mtei, Abdurahman Babu,Idi Simba (enzi za azimio la Arusha) na wengine wengi sana ambao Mohamed said amewabainisha na kuwataja.

Na ninaposema Nyerere nu muasisi wa Ulanguzi wa bidhaa hapo Tanganyika nafikiri sitakuwa nimesema uongo. Kwani haijawahi tokea ulanguzi wa kitu chochote iwe sabuni, kiberiti au hata chakula kabla ya uhuru 1961.Watu wakti wa ukoloni waliishi maisha bora sana na kila kitu kilikuwa kinapatikana madukani. Na ulanguzi huo ndio sasa umekuwa na kupevuka na kuwa ufisadi.

sasa nibainishie ni kipi nitachomtuhumu Nyerere ambacho si cha kweli?

Suala la muungano nafikiri nimeliweka bayana kwenye barza za faida za muungano kwa Znz?

Lakini likuuliza tokea huko awali na hujanipa jibu. Je unajuwa TZ kwanini ni masikini wakati ndio ilikuwa nchi tajiri kabla uhuru kuliko nchi zote za afrika mashariki na kati?
 
Huyo ndiyo Mkandara .'ashomile'..! Inasikitisha sana kuona jinsi taasisi nyingi za waislam zilivyokosa watu wa calibre ya Mkandara...!

Sweke34,

Ni kwa kuwa hujui.

Ingekuwa hapa ni uwanja wangu ningekupa kisa cha Ubay bin Kaab.
Kwako wewe kumsifia Mkandara kuwa Muislam "hodari" umemmaliza.

Na ukisikia siku mimi nimesifiwa na watu kama nyinyi basi jua hamna kitu nishawageuka Waislam.
Hii ndiyo historia ya Uislam na ndiyo Qur'an yenyewe na ndiyo kauli yake Allah SW.

Kama Mkandara ni Muislam khasa jua kwake leo ni siku ya msiba mkubwa.
Mtafute Muislam yeyote akupe kisa cha Mtume SAW na Ubayy bin Kaab utaelewa haya nilokueleza.

Kutokujua nako hakika kuna raha yake.
"Ignorance is bliss."

Mohamed
 

Mwanakijiji,

narejea tena kusema unakuwa uwatendei haki wanajamii hususan wale wenye kiu kubwa sana ya kuona na kuyasoma yale yaliyosahaulika katika historia ya uhuru wa Tanganyika. Na kumbuka kwa msomi huwa siku zote hakosoi kitu pasi na kuonyesha njia sahihi ni ipi. Kwani tunaamini uongo ukikaa muda mrefu basi unageuka kuwa kweli.

Naungana na Mohamed Said hapa anaposema.
MM,

Shida kubwa itakukuta kusimama na mimi katika mnakasha.
Nimekusoma.

Huwezi kuivunja historia niloandika kwa bandiko katika JF.
NARUDIA...andika kitabu au angalau "paper."



 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…