Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

..........utafiti siku zote unapingwa kwa utafiti ............

Hivi msingi huo hapo juu mnautoa wapi?........

Kwanza Brother MS si mtafiti kwenye hizi simulizi...

Watafiti wengi tu waki-present paper zao iwe kwenye warsha, kongamano, semina etc...wanaosikiliza au kusoma...mwisho wa siku hutwanga maswali au hutoa hoja tofauti kama ipo...wakti mwingine humlazimu anayewakilisha paper kui-refine kazi yake kutokana na mchango wa waliosikiliza au kumsoma....

sasa kama wasikilizaji au wasomaji ni WAMEZAJI tu....basi tafiti nyingi zingekuwa ni waste of time
 

Ogah,

Tumefunzwa na wazee wetu kutojinasibu.
Lakini nakutambulisha tu kwa tahadhari.

Mimi ni "authority" katika "Islam and Politics in Tanzania."
Kilichonifikisha hapo ni kuwa nime "publish."

"Publishers" huniomba hata kufanya "review" ya vitabu vyao katika somo hili.
"Thesis" nyingi Marekani na Ulaya zina jina langu katika shukurani zao.
Hii ni zaidi ya miaka 20 sasa na hawa vijana (sasa ni watu wazima) leo ndiyo Wakuu wa Idara huko waliko.

Hawa hadi leo huniletea vijana wao kuja kunihoji.

Mohamed
 
Eeeh mkuu wangu subiri usifiwe mara unavaa joho mwenyewe!
 


"Thesis" nyingi Marekani na Ulaya zina jina langu katika shukurani zao.
Hii ni zaidi ya miaka 20 sasa na hawa vijana (sasa ni watu wazima) leo ndiyo Wakuu wa Idara huko waliko.



MS ebu waelze wanaokubishia japo thesis tatu kuu zinazoheshimika kwenye colllege au hata high school za huko zenye jina lako
 
MS ebu waelze wanaokubishia japo thesis tatu kuu zinazoheshimika kwenye colllege au hata high school za huko zenye jina lako

Imtiazi Yusuf "Islam and Politics in Tanzania" (sina hakika na hili jina sehemu ya mwisho)

Felicitas Becker "Becoming a Muslim in Mainland Tanzania..." (Hii ilikuwa thesis sasa ni kitabu)

James Brennan "Political history of Tanzania in 20th century"

Mohamed
 
MM,

Shida kubwa itakukuta kusimama na mimi katika mnakasha.
Nimekusoma.

Huwezi kuivunja historia niloandika kwa bandiko katika JF.
NARUDIA...andika kitabu au angalau "paper."



Mohamed
Sina shida ya kusimama na mtu yeyote kwenye mnakasha kama wewe unavyopenda kuuita, mimi siku zote husimama na UKWELI. Ukweli wa jambo hili kwangu ni kwamba kwa kuwa mimi nimechanganya dini zote mbili kwenye Familia yangu na Ukoo wangu, najua kwa hakika hakuna mahali hawa ndugu zangu wa Kiislamu walikwamishwa kujiendeleza kielimu wala kisiasa.

Ndugu yangu wa kwanza muislamu kupata shahada aliipata mwaka 1980 pale Milimani, na amekuwa akipanda ngazi mpaka sasa ni Mkurugenzi mwandamizi kwenye shirika kubwa la Umma. Ninao wadogo zangu watatu wana shahada (Mimi sina ingawa ni Mkristo) mpaka za uzamili na wote tunaheshimiana na kushirikiana bila ya kubaguana kwa misingi ya kidini. Mbona ukristo wangu haukunisaidia kupata shahada na wao mbona "mfumo Kristo" haukuwazuia wao kupata shahada??

Sihitaji mnakasha kutetea UKWELI kwamba mtu akinywa sumu ni LAZIMA atakufa. Hakuna mahali mimi nimeona watu wakibaguana kwa sababu ya dini zao. Mimi mwenyewe nimekula sana Futari na Daku kwa marafiki na ndugu zangu waislamu ingawa wao wanajua kwamba mimi ni Mkristo. Ni siku hizi tunaona mawazo chakavu kama yale ya kuamini ndugu wa Muislamu ni muislamu mwenzake.

Kama mtu kazaliwa na wazazi wakristo halafu akasilimu basi wale wazazi wake wanakoma kuwa ndugu zake na waislamu ndiyo wanakuwa ndugu zake?? Mungu gani nyie ambaye mnamzungumzia, ni mungu huyu ambaye anayejua nani anazini sasa hivi lakini bado kwenye nyumba hiyo hiyo ambayo watu wanazini mungu anainyeshea mvua!! Mugu wa upendo, mungu wa baraka??

Kama kweli waislamu wamedhulumiwa ni wepi. Ni wale waliokuwepo 1954 - 1961 au mpaka wanaozaliwa na kusilimu leo? Mwalimu kama binadamu alifanya makosa yakiwamo ya kuvunja vyama vya ushirika, kuvunja tawala za kikabila, kuvunja serikali za mitaa,kutaifisha mashule na Hospitali za mashirika ya umma, kutaifisha majumba ya watu waliyojenga kwa fedha zao tena nyingine za mikopo na mambo kadha wa kadha, lakini alifanya hivyo kwa nia njema na ndiyo maana hakuna mtu anayemtetea mwalimu bali wote wengine tunasema makosa ya Mwalimu yanasameheka kwani hakuyafanya kwa mtimanyongo.

Na mimi sioni sababu ya wewe kujisifia kwa kuandika vitabu au kuwa na machapisho lukuki kuhusu Historia ya nchi yetu, kwani kwa mfano hao unaosema siku hizi wanatoa tuzo kwa majina ya waislamu maarufu wa zamani kama ni jambo jipya, inabadili nini? Mimi nawajua baadhi ya waislam ambao ukiwaambia wawapeleke watoto wao kwenye seminary za waislamu badala ya zile za Wakristo wanazowapeleka, watakuangalia na kukuacha na ubozi wako. Nenda Kifungilo kaangalie kuna waislamu wangapi wanasoma pale na waulize mabinti hao wa kiislamu kama wanabaguliwa au kufelishwa kwa sababu ya Uislamu wao.
 

Kigarama,

Ni bahati mbaya sana huamini kama Waislam wanadhulumiwa lakini kwa jinsi unavyojieleza inaelekea Insha Allah endapo ukweli utakudhihirikia kuwa zimekuwepo njama dhidi ya Waislam bila shaka utawahurumia Waislam na utawaunga mkono.

Mohamed
 
Mtu ambaye ameonyesha ni sensitive maandishi kidogo tu anazira kujibu kwa madai kuwa 'ametukanwa'.
Hapa umemuitaje huyo unayemjibu?! Au na wewe 'umekuja kwa ghadhabu?
Si ajabu tukaambiwa ni type error!!! Hata wafuasi wake wote hawakuiona wamrekebishe na tunaambiwa wanafuatilia darsa kwa umakini mkubwa...!!
 


Hizi ndio tunaita porojo ambazo watu wamepigiana hadi wakaziamini. Nitajie watu watano tu waliopotezwa na Nyerere.



Ni hoja nyingine za hisia. Je ni kweli wale Waislamu waliokuwa wanafany akazi naye walikuwa ni "wasomi wasiojiamini"? Labda utoe mifano ni wasomi gani ambao walikuwa hawajiamini na wakafanya kazi na Nyerere? Je leo ni wasomi wanaojiamini wanafanya kazi na Kikwete?


Kumbuka sasa tupo dunia ya uwazi na ukweli. Mohamed said anafanya kazi ambayo wengi waislam walishindwa kuifanya. Kwani waislam wameamrishwa wanapoona maovu basi wayakemee ima kwa mikono yao, au mdomo wao au kwa imani dhaifu kuyachukia moyoni mwao.

Well, bahati mbaya ni kazi ambayo msingi wake ni ulaghai wa hisia siyo ukweli wa historia. Na ni wale ambao wanapenda masimulizi ya hisia - kama ya Alfu Leila Uleila - ndio wenye kuyashadadia na kuyaamini bila kuyahoji. Bahati mbaya sana kundi hili amelikosa hapa kwenye JF kwani wasomi wenye kujiamini wamemuuliza maswali ambayo kashindwa kujibu na sasa kakubali kuwa unahitajika utafiti mpana zaidi wa historia yetu siyo "utafiti" unaotokana na masimulizi ya wazee walioumizwa hisia zao ambao tunajua wazi kabisa jinsi walivyo mahiri katika kutia manjonjo, utamu na kukolezesha hoja zao kwa masimulizi ambayo hayana ushahidi katika historia.

Mohamed amekemea kwa mkono wake kwa kupoteza muda na mali zake (fedha) kufanya utafiti na kisha kuuweka hadharani na hata JK Nyerere ameupata na kuusoma kwa kina sana lakini hakuwa na la kukosoa. Kwani kila kitu kina karne yake.

Hakukuwa na cha kukosoa kwa sababu hakukuwa na utafiti. Ni sawasawa na kumuambia mtu akosoe simulizi la Alfu Leila Uleila kuhusu ukweli wa matukio yaliyomo ndani. Mtu yeyote atakuambia tu - well "its not history". Hata wewe huwezi kukosoa hilo simulizi kwa sababu hakuna cha kukosoa. Nyerere was way above hili la kuangalia hilo simulizi. Hakuna ushahidi wowote kuwa amewahi hata kukiona hicho kitabu.
 

Kigarama,

Ni bahati mbaya sana huamini kama Waislam wanadhulumiwa lakini kwa jinsi unavyojieleza inaelekea Insha Allah endapo ukweli utakudhihirikia kuwa zimekuwepo njama dhidi ya Waislam bila shaka utawahurumia Waislam na utawaunga mkono.

Mohamed

Waislamu wa Tanzania they have to be offended by this forced victim mentality ambayo unawalazimisha. Mnataka tukae na kuwaonea "huruma" Waislamu? Kweli kuna WAislamu humu ambao wanaweza kussimama na kusema wao ni "victims" wenye kuhitaji kuonewa huruma. Mnawaonea na hamuwatendei haki for perpetuating this constant sense of perpetual victimization! Mnataka Waislamu wa Tanzania watembee kichwa chini kuwa wanaonewa na kudhulumiwa; wasomi wa Kiislamu wajione duni mbele ya wenzao, mnataka Waislamu ambao wamefanikiwa kielimu na kimaisha wajisikie kuwa wako duni kwa sababu ni WAislamu. I hope and I really do that Tanzanian Muslims will ignore this forced sense of a victimhood.

Kweli kabisa, mafanikio ya hoja yako yanawashika wale tu ambao hawawezi kujihoji ambao wanaamini kabisa kuwa wao ni maskini kwa sababu ya Uislamu wao! Matokeo yake ni kuwa Waislamu wengi tu wanasonga mbele, wanasoma, wanapata ajira mbalimbali, wanaendelea hadi kikomo cha uwezo wao kujisomea mambo mbalimbali na sehemu mbalimbali, wakijihusisha na biashara, utafiti, elimu, siasa n.k na wakifurahia matunda ya uhuru ambayo wazee wetu waliyapigania. Waislamu hawa wamekataa kufanywa duni au hata kudhaniwa duni.

Na hawa siku moja wataanza kukupinga japo kwa kufanya hivyo imani yao itahojiwa. Maana Muislamu yeyote ambaye hakubaliana na hii dhana ya kuwa victim atahojiwa Uislamu wake au ataonekana anajikomba kwa Wakristu! I pray there are courageous Muslims out there who could challenge this forced sense of a victim ambayo inalazimishwa kwao. Mtoto wa Kiislamu mnamtaka akienda shule ajihisi yuko nyuma, akifeli ashuku kwa sababu ya dini yake na akishindwa alaumu Kanisa. Hamtaki kuona tatizo kwenye mfumo wetu wa kisiasa au hata katika mfumo wetu wakiuchumi.
 

Mohammed Said hawezi kusalimika kujibu hoja ambazo naweza kuziweka kwake. Hadi hivi sasa ameonesha hana uwezo huo zaidi ya kukimbilia kudai watu wengine waandike. Hawezi kutetea alichoandika yeye mwenyewe. Its as simple as that.
 
Mohammed Said hawezi kusalimika kujibu hoja ambazo naweza kuziweka kwake. Hadi hivi sasa ameonesha hana uwezo huo zaidi ya kukimbilia kudai watu wengine waandike. Hawezi kutetea alichoandika yeye mwenyewe. Its as simple as that.

Mwanakijiji,

Huko kote tushapita.
Siwezi kukuzuia kufikiri upendavyo.

Muhimu kwangu ni watu wajue ipo historia nyingine na hili ni maarufu ndani na nje ya nchi kupitia "papers" zangu na kitabu nilichoandika.

Historia rasmi leo ina mwenza.
Nami Insha Allah naendelea na darsa.


Mohamed
 

Mwanakijiji,

How I wish life was this simple.

Mohamed
 

Mwanakijiji,

Hili litakushtua sana.

Nyerere akinifahamu "by reputation."

Unakumbuka makala katika Africa Events (London) gazeti zima likakusanywa na kutia moto?
Unakumbuka mjadala ndani ya Kamati Kuu kuhusu "waandishi walokuwa wanajaribu kubadili historia?"

Unadhani hao "waandishi" alikuwa nani? Zingatia "alikuwa" na si "walikuwa."

Kitabu kipo katika maktaba yake Butiama.
Fanya uchunguzi.

Nyerere asingeweza kuacha kusoma kitabu cha Abdulwahid Sykes.
Ni kwa kuwa wewe hujui ule urafiki na udugu ulokuwa kati yao hadi mama zao hadi wake zao.

Mwanakijiji mimi nazungumza habari za nyumbani kwetu.
Asubuhi zikitolewa nguo za Abdu kufuliwa tena kwenye ndoo pale Kirk Street nyumbani kwa mamam yake Bi Mluguru ndani ya ndoo ile zipo pia nguo za Nyerere.

Hii ni ile TANU ya kutafuta uhuru ni ile Dar es Salaam ya 1950s.
Ndiyo nikasema zungumzeni mengine si haya ya wazee wangu na historia hii ya TANU.

Mwanakijiji utataabika sana na mimi hutowezi kunishinda asilani hata ukisaidiwa na dunia nzima katika historia hii.
Unajua mkabala na nyumba hii akiishi shangazi yangu wakati ule msichana ndiyo kaolewa akikaa na mumewe nyumba ya baba yake mume wake.

Mohamed
 


Punainen,

Ikiwa lipo kosa nakutaka radhi ndiyo ubinadamu.

Mimi sisusi kujibu lakini tambua sie tumelelewa katika misingi ya nidhamu ya hali ya juu kuhusu adabu.
Tumefunzwa kutotukana.

Sasa mimi mtu akinitusi sirejeshi tusi.
Namuepuka kuepusha shari.

Mohamed
 

Nikusahihishe kwanza. Historia haina mwenza. Kuna historia kamili au isiyokamilika. Historia 'rasmi' siyo lazima isiwe historia sahihi kwani rasmi yaweza kuwa ni historia sahihi lakini haijakamilika. Mtu akisema kuwa alipotoka Ubungo kwenda Kariakoo alipata maeneo ya Urafiki, Manzese na Magomeni halafu akaenda zake hadi Kariakoo anaweza kuwa ameelezea kitu sahihi kabisa na mtu wa kumwelewa atakuwa amemwelewa. Lakini akisema kuwa ndio ametaja sehemu zote alizopitia kwa hakiki siyo kamili kwani kuna maeneo mengine ambayo ameyaruka na hajatuelezea kama wakati anafanya hivyo alichepukia pembeni. Lakini kwamba ametuambia njia aliyoipitia kutoka Ubungo basi kwa kiasi kikubwa tutamwelewa.

Historia ambayo wengi wetu tumejifunza imetaja watu wengi sana na kinyume na unavyodai hakuna kitabu chochota kinachotumika katika shule za Tanzania (iwe msingi, sekondari au vyuo vikuu) ambayo inatumia kitabu 'rasmi' ambacho kinaelezea historia kuwa ya kupigania uhuru ilianzia na Nyerere mwaka 1954. HAKUNA KITABU HICHO.

Sasa uzuri wa historia ni kuwa ni somo ambalo linaweza kuongezewa taarifa zaidi ili kulifanya kuwa kamili zaidi na kuwasaidia watu kujua zaidi na zaidi. Nilipoagiza kitabu chako nilitaarajia kusoma historia yetu ya wazee wetu na mchango wa wale ambao walikuwa wamesahauliwa. Nilipokisoma taratibu nilianza kuona pattern ya ajabu ukitokea.

a. Kila mwenye jina la Kiislamu ulimuita Muislamu bila ya kujali kama alikuwa anaamini yale yale au hata kama alikuwa anashika dini. Wengine ambao unawataja kuwa ni "waislamu" kwa kweli kabisa walikuwa ni wenye imani za jadi zilichanganywa na Uislamu ndani yake na hata wengine wanaweza kabisa kuwa walikuwa ni washirikina! Lakini hili kwako si hoja kwani hoja kwako ilikuwa ni 'majina ya kiislamu".

b. Baada ya muda 'Waislamu' wakawa ni wale tu waliokuwa kwenye jumuiya fulani fulani watu wenye majina ya Kiislamu lakini hawakuwa kwenye jumuiya hiyo hawa ukaanza kuwapa makundi mengine lakini ukaanza kuwatofautisha kwa kuwataja kwa mahali wanakotoka.

c. Unapofika mwaka 1963 unaanza kuwagawa "Waislamu" siyo kwa imani zao au la bali kwa kuangalia waliokuwa ndani ya TANU na wale waliokuwa nje ya TANU. Waliokuwa ndani ya TANU wakaanza kuangaliwa kwa shuku na ilipofika wakati wa kuvunjwa EAMWS Waislamu wakawa ni wale tu waliohusiana na EAMWS lakini wale waliobakia ndani ya TANU na wakaunda BAKWATA hawakuwa WAislamu japo HAKUNA USHAHIDI hata mmoja kuwa waliopiga kura kule Iringa kulikuwepo na Wakristu, Maaskofu au Wachungaji. Kama kigezo chako cha kwanza cha "majina" kuwa ndio Uislamu ingetosha kabisa kufanya BAKWATA ni halali kwani wote walioanzisha walikuwa ni wenye majina ya Kiislamu!

d. Lakini kwa vile lengo lako lilikuwa kuandika habari za "Waislamu" ambao walikuwa wanakubaliana na wazee wako au ambao waliamini wameonewa basi ikabidi uhakikishe kabisa kuwa huandiki habari za Watu wengine ambao hawakuwa Waislamu japo michango yao labda ililinga na wengine hata ilizidi ya wale uliowaita 'wazee wako'. Lakini hukufanya hivi tu. Ukaamua pia kuwafuta Waislamu wengine wote ambao walikuwa hawakubaliana na wazee wako na kuwaweka kwenye footnotes za Kitabu au mwisho wa kitabu.

Sasa kumbe wakati unawatuhumu wengine kuwa wanafundisha historia "rasmi" ambayo imepotosha watu walitarajia kuwa na wewe ungeendika a more comprehensive history of Tanzania's early days. La hasha. Na wewe ukaenda kuandika historia yako 'rasmi' ambayo haikuwa na lengo jingine lolote bali kuonesha ukuu wa Waislamu katika harakati za kupigania uhuru na kuonesha kuwa wao ndio walitaka kuwa huru zaidi kuliko jamii nyingine. Kumbuka ukajikuta unatukuza watu fulani fulani tu na siyo ukweli wa historia. Wakati unamtuhumu Nyerere kupindisha historia kuwa alijipendelea na wewe mwenyewe ukafanya kile kile cha kupindisha historia na kuwapendelea Wazee wako. Wakati unamlaumu Nyerere kuandika historia ambayo imewaweka watu wengine pembeni - japo hakuna ushahidi wa Nyerere kuhusika kuandika historia - wewe mwenyewe ukaandika historia ukiwaacha watu wengine pembeni.

Kama vile wale wengine unadai walidai kuwa historia yao ilikuwa rasmi lakini haijakamilika wewe mwenyewe unadai sasa historia hii ya kwako ni 'kweli tupu' wakati nayo haijakamilika. Kubali yafuatayo kwanza:

a. HIstoria yako si kamili na haiwezi kuwa historia rasmi
b. Historia yako imeandikwa kwa ajili ya kuenzi wazee wako lakini siyo kwa ajili ya kuonesha ukweli wa historia
c. Historia yako imetokana zaidi na hisia kuliko historia.
d. Historia yako imelengwa katika kupotosha mchango wa Wazee wetu ili kuonesha upande mmoja wa wazee wetu (Waislamu wa Gerezani) walikuwa ndio magwiji wa uhuru wa Tanganyika na watu wengine wote wakiwa ni watu walionufaika na hao wazee wa Gerezani.
e. Historia yako ina lengo la kukana nafasi ya pekee (unique role) ya Nyerere kama Baba wa Taifa (hili jina hakuanza kuitwa baada ya kustaafu, upo ushahidi wa Kambona kumuita Nyerere "baba wa Taifa" katikati ya 1960s). Wazee wa Dar-es-Salaam walitambua nafasi hiyo ya Nyerere, waliiheshimu na waliishi naye katika uhusiano wa kuamianiana (patnership of trust).
f. HIstoria yako haitaki kukubali ukweli kwamba Nyerere kama Rais alikuwa na wajibu kwa Watanganyika wote na asingeweza katika dhamira safi kutoa upendeleo wa pekee kwa wazee fulani kana kwamba wazee wengine hawakushiriki. Kikundi cha wazee wanaomlalamikia Nyerere leo hii ni wale ambao walitarajia kuwa wangepata nafasi fulani au upendeleo fulani (Nyerere aliligusia hili katika hotuba yake ile ya 1962).

Kubali haya kwanza ili tuweze kusonga mbele.
 
Mwanakijiji,

Hili litakushtua sana.

Nyerere akinifahamu "by reputation."


Hakuna ushahidi wa hili mahali popote zaidi ya masimulizi ya watu ambao walikuwa wanakuambia ili ujisikie vizuri.


Unakumbuka makala katika Africa Events (London) gazeti zima likakusanywa na kutia moto?
Unakumbuka mjadala ndani ya Kamati Kuu kuhusu "waandishi walokuwa wanajaribu kubadili historia?"

Hakukuwa na mjadala huo wala ushahidi kuwa gazeti lilikusanywa na kutiwa moto kwa agizo la Nyerere. Bahati nzuri Nyerere alikuwa yuko madarakani, aliyekuwa madarakni yupo hai na hujawahi kumuuliza kujua nani alitoa agizo hilo. Akikuambia kuwa lilikuwa ni agizo lake yeye mwenyewe bila kuingiliwa na Nyerere huwezi kuomba radi utafikiri kakudanganya.

 
 
[
MM,

Mie sina tatizo unafikiriaje.

Nina "papers."
Nina kitabu kinasomwa kote kunakosomeshwa historia ya Afrika na Uislam.

Hapa JF hata ukisema kitu gani haiwezi kubadilisha ukweli huu.
Dawa ni wewe na wenzio kuandika kitabu.

Mohamed

Haijalishi kweli kama una papers kwani papers zinahitaji tafsiri tu na wao umechagua tafrisi ya kidini. Yawezekana kabisa kitabu chako kinasomwa sehemu mbalimbali lakini haimaanishi kuwa kinaaminiwa na pale ambapo kinaaminiwa yawezekana ni kwa sababu hao watu wanaokiamini na wenyewe ni wavivu wa kuhoji maswali sahihi kwa sababu wanaamini kimeandikwa with intellectual and academic honesty.

Dawa si kwa sisi kuandika vitabu - hilo labda litafanywa - dawa ni wewe uliyejenga hoja mbalimbali uzitetea hoja hizo kwa kutoa majibu yenye kushawishi akili na siyo yenye kushawishi hisia. Hata useme mara ngapi kuwa wazee wako walikuwa wanaishi mtaa gani na walikuwa karibu kiasi gani na kina Sykes au yeyote ule haifanyi historia unayosimulia kuwa kweli hasa kama iko contradictory, inconsistent and simply fabricated.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…