Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Ndio maana nashindwa kujibizana na watu wa aina yako na hii itakuwa mara yangu ya mwisho kurespond kwa hizi hoja za kipuuzi na kwangu anayezileta nina jina moja tu kwake, ni mpuuzi, period. Unajua wakazi wengi wa Dar es Salaam waliishi kwenye nyumba za aina gani wakati tunapata uhuru ? Unajua nyumba za mbavu za mbwa kama alivyoziita Al Haji Ali Hasan Mwinyi ? Hapo nyuma nimekuuliza kama unaijua "Operation Makuti" ilifanyika wakati gani na lengo lake lilikuwa nini. Je unajua sura ya Dares Salaam ilivyobadilika katika kipindi cha miaka mitano baada ya uhuru ? Tuchukue mfano mdogo tu wa Magomeni;

Unajua mitaa ya Uweje, Idrisa, Sikukuu n.k ilivyokuwa wakati wa uhuru na ilivyoweza kubadilika miaka mitano baadaye. Unajua mitaa karibu yote iliwekewa lami na hali hii iliwapa shida sana Waswahili waliozoea kuchimba mashimo ya taka barabarani na walivyolalamika kuhusu hizo barabara za lami ? Je unajua hadi public toilets mitaani ilijengwa lakini tabia za uswahilini zikazaa sokomoko nyingine katika utumiaji na utunzaji wake ? FaizaFoxy, usitake twende huko, maendeleo yaliyofanyika Magomeni, Ilala hadi Temeke yalikuwa makubwa lakini watu wake hawakuwa tayari kwa hayo maendeleo.

The bottomline ni kwamba watu wa Dar walikuwa wazito katika kuitikia mabadiliko hasa katika nyanja ya maendeleo. Utalia nikikusimulia jumba la kwanza la DDC lilipojengwa Kariakoo na kuwekewa vyoo vya kisasa. Matengenezo makubwa ilibidi yafanyike baada ya muda mfupi na ramani mpya zitayarishwe kwa sababu wakazi wengi wa Kariakoo walipata taabu ku "cope" na vifaa vingi vya kisasa vilivowekwa humo. Kama kuna kitu kimoja kilichoshusha hadhi ya taifa jipya la Tanganyika ni makao makuu ya taifa kuwa Dar es Salaam. Lakini tusiende huko !

Wewe unataka kunihadithia kwetu? labda mimi ndio nikupe somo, lakini naona Mohamed Said darsa lake umelipata na hukumtaja tena jina, Umegwaya kwani kisha sema ukimtaja jina tu, anashusha Nyundo.

Lingine lote povu. Sisi tumepewa darsa humu, hatutukani.

Dar Es Salaam, mpaka "carnival" tulikuwa nazo kabla ya Nyerere kuja (si kuwa Rais tu), utatueleza nini wakuja?

Carnival+(11).jpg







Hiyo DDC yenyewe unayoisema "Msimbazi" ndio wewe ulipoingia Dar ukakumbana nayo nini? ukaiona ya maana? Unanchekesha.

Maswali yangu kutokana na maneno yako mwenyewe, umeshindwa kuyajibu umekuja povu linakutoka, inaonesha ni vipi una maneno ya kubuni-buni tena yasiyokuwa na maana hata kidogo ndio maana ukiulizwa hayohayo wewe mwenyewe yanakutoa povu na unashindwa kujitetea. Pole sana.

Nachukulia hayo mawili ya mwanzo umeshindwa kuyajibu, nakuja na maswali mengine kutokana na mabandiko yako, natokea kulekule mwanzo, ya huku ntayakuta kama hujayaondoa.
 
Bila kumung'unya maneno nayaita madai ya Mohamed Said la kutoa elimu ya historia ya kweli ni porojo hatari iliyojaa uchochezi ambayo lengo lake hasa ni kuleta uhasama wa kidini miongoni mwa wananchi. Sijui anachotegemea kufaidika nacho kwa kupanda hii mbegu ya hatari ambayo nina hakika mtu kama Mohamed Said anajua fika madhara yake.

Kwa kuwa yale maswali yangu mawili ya mwanzo (nayaweka kiporo) umeshindwa kuyajibu na badala yake ukaja na povu la ajabu la kuwatukana wakazi wote wa Dar Es Salaam nikachukulia kuwa hizo ni chuki binafsi zako, ingawa hao hao wasiojuwa kutumia vyoo ndio waliompokea Nyerere mjini. Naendelea:

1) Kama unayosema ya Mohamed Said kuwa ni porojo, nakuomba tuthibitishie na tuoneshe hapa aliloandika Mohamed Said hili hapa (utuwekee) na utuoneshe uporojo wake nawe utupe lako lisilokuwa porojo kugaragaza "porojo" za Mohamed Said. Hili si swali tunataka ukweli kutoka kwako. Ukishindwa basi wewe ndio utakuwa mleta porojo.

2) Ukishindwa kuweka kama nilivyotaka namba 1, huoni kuwa wewe na wenzako mkiongozwa na Nyerere ndio mliopanda, kupalilia na kukaribia kuvuna hizo mbegu za hatari?

3) Huoni kuwa Mohamed Said anatanabahisha dunia kabla ya kuanza kuvuna mlichokipanda, kumbuka mavuno yake yatakuwa kwa sote na si kwenu tu, ili ikiwezekana kisivunike hicho kilichopandwa?

Fikiria kabla hujajibu, usije na mapovu kama kawaida yako. Kuwa muungwana japo kidogo, unajuwa sisi watu wa pwani hatujazoea purukushani hupenda mambo kwa raha. Tartiiibu.
 
Faizafoxy,
You are amazing. Umejiunga JF May 9, 2011 na leo una mabandiko 5055. Kuna wengine hapa wamejiunga 2006 na hata mabandika alfu hawajafikisha. Lady, you are amazingi!
 
Faizafoxy,
You are amazing. Umejiunga JF May 9, 2011 na leo una mabandiko 5055. Kuna wengine hapa wamejiunga 2006 na hata mabandika alfu hawajafikisha. Lady, you are amazingi!

Hii ngoma nzito.
 
Believe me.. unlike you.. naweza kumchallenge mtu yeyote ambaye ameumbwa na ana ubongo kama mimi. Believe me I can. If you can't.. I don't blame you.. si wote wenye uwezo huo. Pole kwa hiyo we kaa pembeni niache miye nizungumze na Shehe Said hapa maana najifunza mengi kweli kweli na si utani kuna mengi ambayo nayajua leo hii kuhusu historia yetu (siyo ya wazee wake) kuliko nilivyokuwa najua mwanzoni na maswali yangu si ubishi tu bali ni katika kujua bila kulazimishwa kukubali bila kuridhika kiakili.


Hakuna umuhimu wowote wa kuwa critics if your goals is to challenge the person and not gain any knowledge from that person. Is that you Mwkjj? Let's be honest...
 
Dar Es Salaam. Ndio hilo linawauma hakuna zaidi.

Nimechunguza maandiko mengi ya Mag3 na nimegundua ana Chuki yake binafsi na Mji wa Dar na wakazi wake ambao wengi wao ni Waislamu. Hii yote inaonesha ni jinsi gani hizi shule za Kanisa wanazoma hawa akina Mag3 zinavyowaandaa hawa Christians Fundamentalists.
 
Nimechunguza maandiko mengi ya Mag3 na nimegundua ana Chuki yake binafsi na Mji wa Dar na wakazi wake ambao wengi wao ni Waislamu. Hii yote inaonesha ni jinsi gani hizi shule za Kanisa wanazoma hawa akina Mag3 zinavyowaandaa hawa Christians
Fundamentalists.
Na ninyi je, hichi anachowapandikizia Mohammed Said ni nini? Mapenzi kwa Wakristo? Unapomnyooshea mtu kidole kumbuka vinne vinakunyooshea weye.
 
Hakuna umuhimu wowote wa kuwa critics if your goals is to challenge the person and not gain any knowledge from that person. Is that you Mwkjj? Let's be honest...

ooh noooo.. miye nauliza maswlai ili nijue zaidi; lakini sikubali majibu yasiyoweza kushawishi akili kwa sababu tu mtu anayeyota anadai ni ya kweli. Hatuzungumzi hesabu hapa wala hatubishanii kanuni fulani ya kupata jawabu la formula ya kikemia. Tunachozungumzia ni vitu ambavyo viko very subjective katika historia.

Sasa mtu akisema "Bw. X alisema b, c na z" tunaweza tukakubali lakini tukikubali bila kuuliza alisema wapi, lini na kwa nani na kuna ushahidi gani tutakuwa hatujitendei haki katika jitihada ya kutaka kujua zaidi. Binafsi ningependa sana Bw. Said atuambiea vile ambavyo ni factual au historical facts ambavyo mtu yeyote anaweza kuviona au kuvifuatilia na kuvithibitisha. Hapa ndipo penye kujifunza.

Bahati mbaya wengine hawataki kujifunza kutoka kwa Bw. Said wanataka tukubali kwa sababu "Bw. Said kasema".

Well, wewe ni mmoja wao?
 
Na ninyi je, hichi anachowapandikizia Mohammed Said ni nini? Mapenzi kwa Wakristo? Unapomnyooshea mtu kidole kumbuka vinne vinakunyooshea weye.

Kuzungumzia historia kwa upande wa pili hakuonyeshi kuwa na chuki na mtu fulani au dini fulani. MS anaelezea historia kwa upande wa pili ambayo haikuzungumziwa ktk vitabu vya pro-Nyerere. Hapo hamna kupandikiza chuki, bali ni kuelezea ukweli.

Chukulia mfano historia ya slavery. Je ni wazungu wote ndiyo walishiriki na utumwa USA? au ilikuwa ni biashara ya matajiri tu? Jibu- utagundua kwamba hii biashara ya utumwa ilifanywa na wazungu wengi ambao walikuwa wafanyabiashara na matajiri.

Je kuna Wazungu ambao walikuwa watumwa? Jibu- Yes, kulikuwa na wazungu ambao walikuwa wanauzwa kama vile watumwa lakini walikuwa na freedom tofauti na black.

Sasa ukija ktk historia ya TZ utagundua kwamba siyo Wakristo wote walifaidika na mfumo huu wa Kristo, lakini majority ya wale waliokuwa kama second citizens utagundua walikuwa ni Waislamu.

MS anajaribu kuelezea ukweli halisi ulivyo na siyo kupandikiza chuki kama unavyosema wewe.

Kumbuka Civil Rights movement in USA- Je ilikuwa ni ya kupandikiza Chuki between citizens? au ilikuwa ni kudai haki za msingi ambazo kila binadamu (raia) anahitaji?

Historia inavyoelezewa na MS, kwa mimi naiona ni sawa na Civil Rights movement.
 
ooh noooo.. miye nauliza maswlai ili nijue zaidi; lakini sikubali majibu yasiyoweza kushawishi akili kwa sababu tu mtu anayeyota anadai ni ya kweli. Hatuzungumzi hesabu hapa wala hatubishanii kanuni fulani ya kupata jawabu la formula ya kikemia. Tunachozungumzia ni vitu ambavyo viko very subjective katika historia.

Sasa mtu akisema "Bw. X alisema b, c na z" tunaweza tukakubali lakini tukikubali bila kuuliza alisema wapi, lini na kwa nani na kuna ushahidi gani tutakuwa hatujitendei haki katika jitihada ya kutaka kujua zaidi. Binafsi ningependa sana Bw. Said atuambiea vile ambavyo ni factual au historical facts ambavyo mtu yeyote anaweza kuviona au kuvifuatilia na kuvithibitisha. Hapa ndipo penye kujifunza.

Bahati mbaya wengine hawataki kujifunza kutoka kwa Bw. Said wanataka tukubali kwa sababu "Bw. Said kasema".

Well, wewe ni mmoja wao?

Historia haiandikwi kwa upande mmoja tu, bali ni pande zote mbili au tatu zaidi. Chukulia mfano-historia ya Civil War in USA- Je North walikwenda kupigana vila vita kwa sababu ya kuwaokoa African-Slaveries? Ukiisoma hii historia kwa upande wa North tu- utagundua kwamba vita vya Civil War- North walikwenda kuivamia South kwa ajili ya kuwaokoa African Slavery.

Je hoja ya inaingia akilini- Yes. Je ni kweli? Inabidi uangalie upande wa pili South.

Kwa mujibu wa South- Civil War ilikuwa zaidi ktk kiuchumi zaidi na siyo kama vile wanavyosema North. Je nani ni mkweli? Lincoln au Southern people?

Hapo inabidi uangalie factors ktk social lives, economic opportunity ktk North au South kwa Black ili ugundue nani ni mkweli au wote ni wa kweli.

Sasa ukija ktk issue ya TZ. Lazima tuangalie some factors ambazo zinagusia point ambazo MS anajaribu kuziweka. Ukiangalia point za MS, utagundua zina 100% true based on the reality.
 
Kuzungumzia historia kwa upande wa pili hakuonyeshi kuwa na chuki na mtu fulani au dini fulani. MS anaelezea historia kwa upande wa pili ambayo haikuzungumziwa ktk vitabu vya pro-Nyerere. Hapo hamna kupandikiza chuki, bali ni kuelezea ukweli.

Sasa ukija ktk historia ya TZ utagundua kwamba siyo Wakristo wote walifaidika na mfumo huu wa Kristo, lakini majority ya wale waliokuwa kama second citizens utagundua walikuwa ni Waislamu.

MS anajaribu kuelezea ukweli halisi ulivyo na siyo kupandikiza chuki kama unavyosema wewe.
Historia inavyoelezewa na MS, kwa mimi naiona ni sawa na Civil Rights movement.
Nadhani kuna kitu ima hujakielewa au umekielewa vibaya. Hakuna mtu anayepinga tu maandishi ya Mohamed, ila watu wanapinga upotoshaji wa makusudi wenye lengo la chuki.

Mohamed amesema ile ni historia ya wazee wake wa Gerezani, haki kabisa. Kabadilika na kusema ni ya Uislam, haki kabisa. Tusichokubali ni yeye kuficha ukweli wa historia anayorekebisha ili tukubaliane na yake . Amejitokeza wazi kuwa yeye ni kiongozi wa waislam wanaozunguka Tanzania kueleza dhulma kama alivyoianisha katika vitabu vyake. Na anazidi kumwaga 'data' za kutetea uislam(haki yake kabisa) na ameachana na Tanganyika. Uliyebaki unaamini ni upande wa pili wa historia ya Tanganyika pengine ni peke yako. Mohamed hayuko huko.

Unaposoma kitu lazima ufikiri hiyo ndio inaitwa critical thinking. Hivi Mohamed akiandika makala kuwa Nyerere alikuwa mwarabu wa Madinah utakubali tu kuwa ni historia ya ukweli na ya upande wa pili!!

Ni kwa kuhoji ndio tumeelewa kuwa Mohamed anamsingizia Nyerere kuua baraza la wazee wa TANU kwasababu hajui kamati kuu ya TANU anayodai ina asilimia 98 waislam. Alipataje asilimia kama hajui nani ni yupi. Hapo kuna ukweli na wewe bado unaamini kuna ukweli.

Ni kwa kuhoji ndio maana tumejua kuwa Mohamed anachuki na Nyerere na watu wengine. Ameelezea jinsi Nyerere alivyoishi hadi kupelekewa kitoweo, jinsi alivyovaa soksi hadi magotini, na jinsi alivyopewa chumba cha kulala achilia mbali sh kadhaa kwenda kununua mboga.
Tulitegemea mtu anayemjua Nyerere kiasi hiki angejua amefika lini Dar es Salaam, Mohamed hajui. kuna ukweli hapo.
 
Nadhani kuna kitu ima hujakielewa au umekielewa vibaya. Hakuna mtu anayepinga tu maandishi ya Mohamed, ila watu wanapinga upotoshaji wa makusudi wenye lengo la chuki.

Mohamed amesema ile ni historia ya wazee wake wa Gerezani, haki kabisa. Kabadilika na kusema ni ya Uislam, haki kabisa. Tusichokubali ni yeye kuficha ukweli wa historia anayorekebisha ili tukubaliane na yake . Amejitokeza wazi kuwa yeye ni kiongozi wa waislam wanaozunguka Tanzania kueleza dhulma kama alivyoianisha katika vitabu vyake. Na anazidi kumwaga 'data' za kutetea uislam(haki yake kabisa) na ameachana na Tanganyika. Uliyebaki unaamini ni upande wa pili wa historia ya Tanganyika pengine ni peke yako. Mohamed hayuko huko.

Unaposoma kitu lazima ufikiri hiyo ndio inaitwa critical thinking. Hivi Mohamed akiandika makala kuwa Nyerere alikuwa mwarabu wa Madinah utakubali tu kuwa ni historia ya ukweli na ya upande wa pili!!

Ni kwa kuhoji ndio tumeelewa kuwa Mohamed anamsingizia Nyerere kuua baraza la wazee wa TANU kwasababu hajui kamati kuu ya TANU anayodai ina asilimia 98 waislam. Alipataje asilimia kama hajui nani ni yupi. Hapo kuna ukweli na wewe bado unaamini kuna ukweli.

Ni kwa kuhoji ndio maana tumejua kuwa Mohamed anachuki na Nyerere na watu wengine. Ameelezea jinsi Nyerere alivyoishi hadi kupelekewa kitoweo, jinsi alivyovaa soksi hadi magotini, na jinsi alivyopewa chumba cha kulala achilia mbali sh kadhaa kwenda kununua mboga.
Tulitegemea mtu anayemjua Nyerere kiasi hiki angejua amefika lini Dar es Salaam, Mohamed hajui. kuna ukweli hapo.

He we'go again critical thinking!! C'mon man..

Kwani historia ikizungumzia Waislamu haipo ktk Tanganyika? MS anazungumzia mchango mzima wa Waislamu ktk Uhuru wa Tanganyika. Sasa huo si upande wa pili wa historia ktk Tanganyika?

Chukulia mfano, historia ya Marekani inapoandikwa kama vile mchango wa African American ktk mapinduzi ya Marekani. Je unajua maana yake nini? Je Unajua kwanini imeandikwa mchango wa African-American?

Jibu-
Nchi inapokuwa na raia ambao wanafanywa kama second citizens, unapozungumzia historia au jambo lolote ktk jamii lazima useparate (race, religion) in order to send the message to the audience.

MS kuzungumzia Waislamu ktk historia haina maana kwamba ni historia ya Waislamu pekee; bali ni ya nchi nzima. Kwa nini anafanya hivyo. ni same issue ya African-American. Waislamu TZ wanafanywa kama second citizens. Kwa hiyo, in order for Muslims to be respected and treated equally same like other citizen, inabidi Muslims waende extra miles. Hapo ndipo watu kama MS wanaamua kuchukua muda kufanya jambo hili muhimu ambalo litasaidia kuongeza Civil Rights ndani ya TZ ktk miaka ijayo.
 
Kumbuka Civil Rights movement in USA- Je ilikuwa ni ya kupandikiza Chuki between citizens? au ilikuwa ni kudai haki za msingi ambazo kila binadamu (raia) anahitaji?

Historia inavyoelezewa na MS, kwa mimi naiona ni sawa na Civil Rights movement.

Mfano wako huu ni mzuri sana; civil rights ilikuwa siyo kwa ajiliya kuonesha chuki dhidi ya weupe bali kuonesha ubovu wa mfumo wa ukandamizaji. Matokeo yake hata watu weupe wengi walishiriki kwa sababu walikubaliana na msingi (premise) ya hoja. Kina Martin Luther walikuwa hawahubiri chuki dhidi ya watu weupe hata chembe, walikuwa hata hawahubiri chuki dhidi ya vyama vya siasa; walikuwa wanahubiri chuki ya mfumo mbaya na waliutambua mfumo huo kuwa msingi wake na sera yake ni ubaguzi wa rangi.

Hoja zao zilikuwa universal na ukweli wake ulikuwa intrinsic in nature. Ndio maana kuna post moja jana niliandika kwa M. SAid sijui hata kama aliijibu kuwa anakemea mfumo ambao haupo; Mfumo Kristu unaodaiwa haupo upo mfumo ufisadi lakini yeye na wengine wenye kukubaliana naye hawataki kuungalia. Wanapozungumzia "mfumo Kristu" utafikiri wanasema kuwa hakuna Wakristu maskini, hakuna wakristu ambao maisha yao na ya watoto na familiia zao yanaathiriwa na mfumo wa ufisadi. Kw akujaribu kuangalia matatizo ya mfumo wetu kuwa ni ya kidini badala ya corruption - M. Said na wengine wanapoteza sana.

Na bahati mbaya badala ya kuwaleta pia Wakristu waone uzito wa hoja zao na uhalali wake wanatumia muda mrefu kuwashambulia hata Wakristu ambao kimsingi wanatambua dhulma inayoletwa na ufisadi. Tukubaliane kwanza kuwa tatizo letu kama taifa ni ufisadi ambao unaathiri Wakristu na Waislamu, Wenye imani na wasio na imani, Waswahili na Wachagga, Wazaramo na Wasukuma na kutoka hapo kwa pamoja tukitumia kanuni za haki, usawa, utu na upendo kuweza kuuvunja vunja mfumo huu ili tujenge mfumo ambao utaheshimu utu na haki ya kila Mtanzania bila kujali wazazi wake wanavaa nguo gani, wanasali wapi au majina yao yanaendana na dini gani.

Unasemaje?
 
Nadhani kuna kitu ima hujakielewa au umekielewa vibaya. Hakuna mtu anayepinga tu maandishi ya Mohamed, ila watu wanapinga upotoshaji wa makusudi wenye lengo la chuki.

Mohamed amesema ile ni historia ya wazee wake wa Gerezani, haki kabisa. Kabadilika na kusema ni ya Uislam, haki kabisa. Tusichokubali ni yeye kuficha ukweli wa historia anayorekebisha ili tukubaliane na yake . Amejitokeza wazi kuwa yeye ni kiongozi wa waislam wanaozunguka Tanzania kueleza dhulma kama alivyoianisha katika vitabu vyake. Na anazidi kumwaga 'data' za kutetea uislam(haki yake kabisa) na ameachana na Tanganyika. Uliyebaki unaamini ni upande wa pili wa historia ya Tanganyika pengine ni peke yako. Mohamed hayuko huko.

Unaposoma kitu lazima ufikiri hiyo ndio inaitwa critical thinking. Hivi Mohamed akiandika makala kuwa Nyerere alikuwa mwarabu wa Madinah utakubali tu kuwa ni historia ya ukweli na ya upande wa pili!!

Ni kwa kuhoji ndio tumeelewa kuwa Mohamed anamsingizia Nyerere kuua baraza la wazee wa TANU kwasababu hajui kamati kuu ya TANU anayodai ina asilimia 98 waislam. Alipataje asilimia kama hajui nani ni yupi. Hapo kuna ukweli na wewe bado unaamini kuna ukweli.

Ni kwa kuhoji ndio maana tumejua kuwa Mohamed anachuki na Nyerere na watu wengine. Ameelezea jinsi Nyerere alivyoishi hadi kupelekewa kitoweo, jinsi alivyovaa soksi hadi magotini, na jinsi alivyopewa chumba cha kulala achilia mbali sh kadhaa kwenda kununua mboga.
Tulitegemea mtu anayemjua Nyerere kiasi hiki angejua amefika lini Dar es Salaam, Mohamed hajui. kuna ukweli hapo.

Nguruvi3,

Nimekusoma lakini sitikujibu kwa yote uliyosema kwa kuwa naamini
kwa kiasi hiki tulichofikia ukumbi unanifahamu na wanaijua kalamu
yangu.

Ila nitakueleza kitu kimoja.

Nisingefika hapa ingekuwa kalamu yangu inakashifu watu kwa hiyo
nakusihi usitake kuwaongopea watu kuwa naandika kumsimanga
na kumtukana Nyerere.

Sijafanya na sitofanya Insha Allah.

Mimi nimefunzwa adab na wazee wangu. Angakia lugha yangu na
fananisha na wengine humu ukumbini.

Hakuna mtu anaeweza kutia maneno mdomoni kwangu.

Mimi hata kama sikuweka jina wasomaji wangu huwa wanaweza
kunitambua na kusema hii ni kalamu ya Mohamed Said.

Mimi ni "scholar" na "scholar" haandiki kashfa na matusi. Nina mada
wala sijui hesabu yake katafute tusi mle ndani kama utalikuta.

Kwa hiyo Nguruvi3 tujadiliane kiiungwana na tusisingiziane.

Mwisho.

Nani kakuambia mimi sijui Nyerere kafika lini Dar es Salaam wakati nimeeleza
hapa ukumbini kuwa baba yangu alijulishwa kwa Nyerere nyumbani kwa
Abdulwahid Sykes...

Isitoshe nimeeleza Nyerere aliingizwa vipi TAA Makao Makuu New Street basi
inishinde mwaka alofika Dar es Salaam?

Soma nyuzi zangu jibu limo humo.

Mohamed


PS: Kitoweo...kisa cha Mshume Kiyate na Nyerere kimechapwa na Mwananchi gazeti lenye
heshima ingelikuwa ni kisa cha kumkashifu Nyerere wasingekubali kukichapa. Mzee Mshume
na Nyerere walikuwa mtu na mwanae katika uhusiano wao na pamoja walipigania uhuru wa
Tanganyika.
 
Mzee Said kati ya wazee wote ambao umezungumza nao kuna yeyote ambaye amewahi kukuambiwa Nyerere alitumia neno lolote dhidi ya Uislamu au Mwislamu kwao kuonesha chuki, kisirani au kutokuwa tayari kufanya kazi na Waislamu katika muda wote waliomfahamu Nyerere?
 
ooh noooo.. miye nauliza maswlai ili nijue zaidi; lakini sikubali majibu yasiyoweza kushawishi akili kwa sababu tu mtu anayeyota anadai ni ya kweli. Hatuzungumzi hesabu hapa wala hatubishanii kanuni fulani ya kupata jawabu la formula ya kikemia. Tunachozungumzia ni vitu ambavyo viko very subjective katika historia.

Sasa mtu akisema "Bw. X alisema b, c na z" tunaweza tukakubali lakini tukikubali bila kuuliza alisema wapi, lini na kwa nani na kuna ushahidi gani tutakuwa hatujitendei haki katika jitihada ya kutaka kujua zaidi. Binafsi ningependa sana Bw. Said atuambiea vile ambavyo ni factual au historical facts ambavyo mtu yeyote anaweza kuviona au kuvifuatilia na kuvithibitisha. Hapa ndipo penye kujifunza.

Bahati mbaya wengine hawataki kujifunza kutoka kwa Bw. Said wanataka tukubali kwa sababu "Bw. Said kasema".

Well, wewe ni mmoja wao?

Mwanakijiji,

Soma kozi ya Research Methodology kuna mahali utafundishwa kuwa huwezi kutoa "source" zako khasa inapokuwa umeelezwa jambo "in confidence."

Mohamed
 
Mwanakijiji,

Soma kozi ya Research Methodology kuna mahali utafundishwa kuwa huwezi kutoa "source" zako khasa inapokuwa umeelezwa jambo "in confidence."

Mohamed


Hii ni mara ya kwanza unadai kutumia privilege hii ya kuwa umeambiwa vitu in confidence. Na nina uhakika inaweza kukupa kinga kwa mengi kweli. Maana sasa hata waliohai unaweza ukatumia tu kuwa uliambiwa kuwa "in confidence". Je katika huko "in confidence" kuna mtu aliwahi kukuambia alimsikia Nyerere akisema jambo dhidi ya Waislamu au Uislamu?

Usitaje majina unaweza kusema "ndio" au "Hapana" au "sitaki kujibu"
 
Mzee Said kati ya wazee wote ambao umezungumza nao kuna yeyote ambaye amewahi kukuambiwa Nyerere alitumia neno lolote dhidi ya Uislamu au Mwislamu kwao kuonesha chuki, kisirani au kutokuwa tayari kufanya kazi na Waislamu katika muda wote waliomfahamu Nyerere?

Mwanakijiji,

Tutakwenda awamu baada ya awamu tuanze na hii:
"Ili tume ya uchunguzi ya Waislam iwezekufanya kazi yake vyema na bila upendeleo, ilikuwa lazima ile tume ya Waislamiiombe serikali izuie propaganda iliyokuwa ikiendeshwa na wale waliokuwawamejitenga na EAMWS, wakitumia jukwa la radio ya serikali na magazeti ya TANU.Tume ya Waislam ilikutana na Waziri wa Habari na Utangazaji, Hasnu Makame,ofisini kwake tarehe 20 Novemba, 1968, kujadili tatizo lile. [1]Hii haukusaidia kitu. Propaganda dhidi ya uongozi wa EAMWS iliendelea kwa nguvuzote. Mashambulizi kutoka pande tatu yaliyopangwa vyema yalikuwa kazini. BenjaminiMkapa akitumia gazeti la Nationalist ataandika habari yoyote ya Adam Nasibu,Martin Kiama akitumia Radio Tanzania atatumia habari ile kama habari muhimukatika radio na habari hiyo itatangazwa kutwa nzima huku ofisi ya rais ikiwakimya kwa fitna ile. Lile kundi la waliojitenga na umma wa Waislam Adam Nasibuakiwa kama msemaji wao mkuu wakawa wakati mwingine kwa mastaajabu makubwawakawa wanakiuka hata misingi ya akida ya Tanzania, wakitoa madai ya ubaguzi arangi, wakikazania lazima EAMWS ivunjwe. Adam Nasibu alinukuliwa na TheNationalist akisema kuwa: "Waislam lazima wafahamishwe kwa nini EastAfrican Muslim Welfare Society iwe na katiba ambayo inaendana na mwelekeo wanchi. Hatujui nafasi ya Aga Khan katika nchi yetu na ndiyo maana tunamkataa." [1]
Lakini cha kushangaza zaidi ilikuwa uleukimya wa serikali kuhusu matakwa ya kundi la Adam Nasibu lililokuwa likidaikuwa Waislam wachanganye dini na siasa katika suala hili, wakati ilikuwaikijulikana wazi kuwa kufanya hivyo ni mwiko mkubwa katika siasa za Tanzania. Haya yote mbali, lile la kushangaza hasa nakitu ambacho kilikuwa kigeni katika Tanzania ilikuwa yale madai ya kuingizaubaguzi wa rangi katika siasa za Tanzania. Ilikuwa inastaajabisha kuonamagazeti ya TANU yaliyokuwa na sifa ya kuheshima haki za binadamu yakichapishana kuzipa uzito wa hali ya juu habari za kundi dogo la Waislam waliokuwawanawalaumu Waislam wenzao wa Kiismailia kwa kutozaliwa weusi. Miaka kumiiliyopita watu wa Tanganyika, Waislam wenyewe waliokuwa ndiyo walioanzisha nakuijenga TANU, walipambana vikali dhidi ya siasa za kibaguzi za Zuberi Mtemvuna chama chake cha African National Congress. Mtemvu alishindwa na matokeo yakeikawa Tanganyika kuwa na serikali ya watu wote isiyobagua rangi na ikitawalaraia wa rangi zote kwa misingi ya haki. Kwa ajili hii nchi ikawa haina msuguanokwa ajili ya ubaguzi wa rangi. Haya matokeo mapya yalikuwa hayaendani namisingi ya TANU.
Ilipofikia hali hii, rais wa EAMWS, TewaSaid Tewa na makamo wake Bibi Titi Mohamed, waliamua kulipeleka suala hili kwaJuluis Nyerere, Rais wa Tanzania na mwenyekiti wa TANU, chama tawala. chanzocha uadui huu inatulazimu turudi nyuma hadi mwaka wa 1963, katika siku zamwanzo za uhuru, katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya TANU [1]uliofanyika Ukumbi wa Karimjee.
Kama ilivyokwishaelezwa hapo mwanzonikuwa mwaka 1963 ulikuwa mwaka wa mambo mazito. Ilikuwa ndiyo mwaka ambao KanisaKatoliki liliteua wagombea wake wapambane na wagombea wa TANU waliokuwa Waislamkatika uchaguzi wa serikali za mitaa kule Kigoma na Bukoba. Ulikuwa ndiyo mwakaambao Rais wa TANU, Nyerere alipombana na EAMWS kupitia Bilali Rehani Waikela.Mwaka Watu hawa walikuwa wakichekeana jino pembe. Lakini ili tuelewa mwaka wa 1963 ndiyo ulikuwa mwaka ambaoHalmashauri Kuu ya TANU ilivunja Baraza la Wazee wa TANU lililokuwalimetawaliwa na Waislam kwa madai kuwa baraza hilo lilikuwa ëlikichanganya dinina siasaí. Mwaka 1963 ulikuwa mwaka muhimu kwa Halmashauri Kuu ya TANU kwasababu ilikuwa mwaka ambao ilifanya maamuzi nyeti ya kidini. Mwaka ule BibiTiti na Nyerere walishambuliana kwa maneno ndani ya Halmashauri Kuu yA TANUkuhusu jambo jingine tena la dini lililokuwa likihusu EAMWS.
Wanakamati wawili wa Halmashauri Kuu yaTANU, Selemani Kitundu na Rajab Diwani, waliiomba Halmashauri Kuu ya TANUimjadili Aga Khan na nafasi yake kama patroni wa EAMWS. Kitundu na Diwaniwalidai kuwa wana habari Aga Khan anataka kuitawala Tanganyika kupitia Waislamna EAMWS. Kwa ajili hii basi wakapendekeza EAMWS ifungiwe. Nyerere aliwaungamkono Selemani Kitundu na Rajab Diwani. Bibi Titi akasimama kishujaa dhidi yaDiwani, Kitundu na Nyerere, akasema hakuna kati yao aliyekuwa na haki yakuifungia jumiaya yoyote ya Waislam. Kama walikuwepo watu ndani ya EAMWS ambaowalikuwa wanakwenda kinyume na sheria basi watu hao wapelekwe mahakamani nasheria ichukue mkondo wake. Bibi Titi akaendelea na kusema kuwa EAMWS imekuwepokabla ya TANU na siku zote imekuwa ikitoa huduma kwa Uislam. Inasemekana hasirazilipanda na kukawa na kutoleana maneno kati ya Bibi Titi na Nyerere. Bibi Titiakamwambia Nyerere yeye hamuogopi yeyote ila Allah.
Tuhuma zile dhidi ya Aga Khan na EAMWShazikuweza kuthibitishwa na Halmashauri Kuu ya TANU ikaliacha jambo lile kwawakati ule. Lakini Nyerere alikuwa amefedheheka. Kuanzia hapo akajenga chukidhidi ya Bibi Titi na kumweka Rajab Diwani na Selemani Kitundu karibu yake.Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1965 Bibi Titi na Tewa wakapoteza viti vyao kwawatu ambao walikuwa hata hawafahamiki ñ A.M. Mtanga na Ramadhani Dollah.Iliaminika kuwa Nyerere alikuwa anahusika na kuanguka kwa Bibi Titi na Tewa.Kuanzia hapo mambo yakawa dhahiri. Nyerere alikuwa amewatangazia vita wotewawili, Bibi Titi na Tewa. Nyerere alikuwa sasa ana imani kuwa wale maadui zakewawili walikuwa wamekwisha kisiasa. Lakini kilichokuwa kkimuudhi Nyerere zaidiilikuwa taarifa ambazo alikuwa akizipata kuwa Tewa alikuwa akipewa mapokezimakubwa sana na Waislam katika ziara zake huko mikoani kama rais wa EAMWS. [1]
Sasa mwaka wa 1968, Bibi Titi na Tewawalipokwenda kumuona Nyerere kuhusu jambo lililokuwa linawahusu Waislam,Nyerere alikuwa amejitayarisha vyema. Kiwanuka ameueleza mkutano huu vizurisana: "Viongozi hawa wawili wa Waislamwalimueleza Mwalimu masikitiko yao jinsi radio ya serikali na magazeti ya TANUyalivyokuwa yakiandika habari kuhusu matatizo yale ya Waislam. Walidai kuwaTANU ilikuwa ikichanganya dini na siasa. Waliokuwa wakimtahadharisha kuhusujambo hilo hawakuwa wengine ila marafiki zake wa zamani na wa kutumainiwa, Tewana Bibi Titi. Marafiki wa kutumainiwa kwa sababu ilikuwa Titi aliyemuunga mkonoNyerere katika siku za mwanzo za TANU, pale Suleiman Takadir ñ mmoja wa wazeewa TANU ñ aliposema kuwa TANU ilikuwa na Ukristo kama Mwalimu na Rupia, rais namakamo wake walivyokuwa Wakristo. Yeyemwenyewe akiwa Muislam hasa, aliipatia TANU ushindi kwa kuthibitisha kuwaTanzania, Tanganyika kama ilivyokuwa ikijulikana wakati ule, ilikuwa mbele, naUislam unafuata nyuma. Leo, alikuwa anazungumzia jambo ambalo yeye mwenyewealilishinda katika miaka ya 1950. Jibu walilopata kutoka kwa Mwalimu lilikuwa lakusisimua. Mpashaji wangu habari anasema lilikuwa jibu la mkato. ëMmeamuakunipiga vita, jiandaeni." [1]
Mwalimu Nyerere alikuwa anawaambia TewaSaid Tewa na Bibi Titi Mohamed uso kwa macho wajiandae kwa kile kilichokuwadhahiri: vita ya msalaba dhidi ya umoja wa Waislam. Sheikh Suleiman Takadiraliyaona haya na aliiomba TANU toka mwaka wa 1958 pawepo na uhakika kuwaWakristo ambao walikuwa wanapanda migongo ya Waislam na kuchukua uongozihawatakuja kuwafanyia uadui Waislam pale Waislam watakapokuwa sasa wanatakakugawana madaraka ya kuongoza nchi sawa na Wakristo baada ya uhuru. Tewa SaidTewa, muasisi wa TANU, waziri katika serikali ya kwanza ya uhuru, balozi katikaJamuhuri ya watu wa China na Rais wa baraza la Tanzania la EAMWS, pamoja naBibi Titi, mwanamke aliowakusanya wanawake wote nyuma ya Mwalimu Nyerere naTANU, walikuwa wakisemwa na Nyerere kama vile watoto wadogo wa shule waliokuwawatukutu kwa sababu tu, walikuja kumfahamisha Rais kuhusu kukiukwa kwa maadiliambayo ilihitaji yeye ashughulikie mara moja na kutoa uamuzi."
 
Hii ni mara ya kwanza unadai kutumia privilege hii ya kuwa umeambiwa vitu in confidence. Na nina uhakika inaweza kukupa kinga kwa mengi kweli. Maana sasa hata waliohai unaweza ukatumia tu kuwa uliambiwa kuwa "in confidence". Je katika huko "in confidence" kuna mtu aliwahi kukuambia alimsikia Nyerere akisema jambo dhidi ya Waislamu au Uislamu?

Usitaje majina unaweza kusema "ndio" au "Hapana" au "sitaki kujibu"

Mwanakijiji,

Usinitie huko mimi si mtu wa nipe nikupe mimi mtu mwingine kabisa na kwa lugha nyepesi nakuambia hivi: Huna lazima ya kuamini nisemayo. Mie najua haiwezekani kwa watu wote kuniamini.

Mengi sana nimeelezwa na watu "in confidence" mengi sana na wengine waliogopa kuzungumza na mimi. Soma hii tabaruku yangu:

"Ninapenda kuwashukuru wale wote waliokubali kuwahojiwa nami lakini wameomba nistiri majina yao. Na kwa wale waliokataa kuzungumza nami kuhusu somo hili si kwa ubaya bali kwa hofu, na kwa wachapaji walioogopa kuchapisha kitabu hiki na vilevilevi kwa wale walioona bora kukaa kimya, lazima nikubali, kwamba hao wote kwa ujumla wao na kwa namna yao ya ajabu wamechangia katika kufanikisha kitabu hiki."

Mohamed
 
Back
Top Bottom