Tunashukuru kwa uchambuzi wa familia ya Mkwawa,
Ila mambo mawili matatu naomba ufafanuzi. Kwanza ilikuwaje hadi Rumaliza alifanikiwa kupenya katika ngome ya wahehe na kupata influence kubwa? Pia BG Martin (1969) (Article nilishaitaja nyuma sina umuhimu wa kuirudia) alisema haya naomba unijibu:-
Mkwawa and Rumaliza became blood-brothers, and Rumaliza doubtless gave his ally advice on rebuilding in stone his earth fortress at Kalenga, near Iringa, against the day of German attack. On 30th October 1894 Rumaliza was in the fort with Mkwawa when it was asaulted by the Germans. Mkwawa commited suicide four years later, while Rumaliza escaped to Zanzibar by fishing boat to evade the Germans.
Huu ukaribu wa Rumaliza na Mkwawa ulikuwa wa nini mnaweza kufafanua hadi wa kufa na kufaana?
Labda nikuongezee nondo nyengine Edward Simpson et.al. (2008) katika kitabu chake kinachoitwa Stuggling with History: Islam and Cosmopolitan in Western Indian Ocean anasema:-
The sultan with help of Qadiriyya movement helped islamisation of uhehe and unyamwezi region during the first decade of the twentieth region and after 1880. (1880-1910).
Hapa nauliza je Mkwawa alikufa mwaka gani?
Na pengine hao wazee watuambie after the Germans defeated Wahehe. Moja ya masharti waliyokubaliana baina ya wahehe na wajerumani ni kuwa Wajerumani watatawala wahehe ila wahehe watabakiwa na mambo yao binafsi (Kama anavyoreport Marcia Wright.). Moja ya masuala hayo ufundishwaji wa lugha ya Kiswahili na UISLAMU (references Marcia Wright, 1968, Local roots in German East Africa, Journal of African History, Cambridge University Press)
Jambo hili lilipingwa sana wamissionary wa kijerumani unaweza kutupatia maelezo ya kwanini walilipinga?