Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Currently...



Previously on this thread...





Need I say more?

Hahahahahah, ustake ncheke! hujui nilikuwa nasema nini? nilikuwa nawakumbusha kwanza ni Qur'an na kaja mgaltia mmoja humu kaiandika isivyo, wakajuwa kuwa atarudi na kuomba msamaha hajaja, nikawakumbusha tena, walipotowa kauli kwa hilo, mgalatia akarudi kuomba msamaha, au hujaona? Mohamed Said kaandika Historia na hilo halipingiki iwe ni mimi awe ni mwingine na Qur'an ikichezewa ndivyo sivyo ataacha yote kwanza amsulubu aliyeichezea Qur'an, matokeo unayajuwa, haina haja ya kuyarudia. Darsa Linaendelea na bado mpaka sasa hamjaja na kimoja cha kupinga yaliyandikwa, hapo sasa. Nyie mrukieni Faiza, mrukieni sijui kasema nini, kwanini, lakini hoja ipo pale pale.
 
Hapo Mgalanjuka mwenzio alitaka ku- twist mjadala kuhalalisha kwamba Mohamed lengo lake ni kuwa enzi wazee wake kama wapigania Uhuru wa Tanganyika na wala si kwa sababu ya udini wakati makala nzima imejaa maneno yenye kuonyesha utengano wa kidini.

Huwezi kabisa kutenganisha Waislaam na harakati za kutafuta madaraka. Hilo ukipenda usipende. Wale waliompokea Nyerere Dar. walikuwa dini ipi?
 
Kwa sababu sio ukweli imeshajifuta yenyewe, nakushangaa sana kwa kutumia nguvu kubwa kuielaza na kuwajengea hofu vijana wa kiislam kuwa wanaonewa wakati wenyewe ukweli wanauona. Nimekusikia kwenye clip zako YouTube ukitumia majina ya marehemu akiwemo marehemu Profesa Haroub Othman kuhalalisha chuki yako! Haroub hakuwa mwalimu wako peke yako, wengi tulifundishwa naye, kwa tulie mfahamu msomi yule hakuwa na fikra unazompandikizia wewe, unafanya hivyo kwakuwa unajua kwamba hataweza kuja kujitetea hapa.Waache vijana wa Tanzania wafurahie umoja wao, waache vijana wapambane na umaskini na ufisadi ktk nchi yao kwani matatizo hayo hayawatenganishi kwa imani zao, wote kwa pamoja wanajeruhiwa nayo. Kama kweli Mungu wako anasifa tatu yaani "Omnipotence, Omniscience na Omnipresence" basi nakusihi mwachie yeye atoe hukumu ya haki kwa chuki unayo mpakazi/mzuria mwalimu Nyerere dhidi ya uislam.La sihivyo njoo uuangane na mimi(Atheist) na wala usiusingizie usilamu kujenga sifa na chuki zako binafsi.


Si ukweli kuwa Nyerere alipokelewa na Abdul Wahid? si ukweli kuwa Nyerere hakuwa muasisi wa TAA? si ukweli kuwa Abdul Wahid ndio alitoa jina la TANU? ni kipi ambacho si ukweli? tuoneshe nukuu ya Mohamed Said ambayo si ukweli halafu wewe tupe iliyokweli, si kuandikia mate na wino upo. "si ukweli" huoneshi hilo "si ukweli" liko wapi, "si ukweli" huoneshi ukweli uko wapi.
 
Huyo aliniuliza kama najua maana ya "contradictions" hivyo nashangaa mara kawaita watu "wanafik wakubwa" then anawaambia "kazi yao imeota mizizi"

Sasa hiyo ni "contradiction"? wewe ya Faiza Foxy huyawzi, mambo yako wazi hapa ukumbini tupe nukuu za kusema hii si sawa, sawa hii hapa. Achana na Faiza Foxy kasema nini, mimi nimeandika historia? unanchekesha!
 
We acha tu! Natamani ningeweza kupata mkalimani awatafsirie wadau wote wa nje ya nchi alikopita MS vilivyomo kwenye hii thread!

"naatamaaaani na kujariiiibu siwezi".

Hapo sasa, nimesema Hamuwezi kuandika japo "credible paper" tu wacha historia. Mtabaki "natamani", "natamani", "kwanini", "kwanini", "Faiza Foxy kasema hivi", "Ritz kasema vile". Lakini kuja na kuonesha nukuu ya Mohamed Said ya vitabu na "paper" zake kuwa hii hapa haikuwa kama ulivyoandika, mpaka sasa hata mmoja wenu hajaweza. Vipiiiiii?
 
Ritz,

Unamchapa farasi aliyekufa.
Ukisoma jibu lake ndiyo utajua mengi zaidi...

Umetoa mifano ya kisomi kabisa anakupa habari za "Cock and Bull."
Hawa hawawezi kuja na historia nyingine.

Waandike nini?
Ndiyo maana waliipiga vita historia ya wazee wetu.

Kuna mradi wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere kuandika maisha yake.
Tuisubiri hiyo Insha Allah.

Mohamed

Mimi hoja yangu ni kwamba hakuna "Historia kamili" kama kungekuwa na hilo basi dunia nzima labda vitabu vya historia visingezidi mia!!

Hayo aliyoyaandika ndiyo "usomi" wenyewe eeenh!!?? Kweli mfumoKristu ulifanya kazi!!
 
Mimi hoja yangu ni kwamba hakuna "Historia kamili" kama kungekuwa na hilo basi dunia nzima labda vitabu vya historia visingezidi mia!!

Hayo aliyoyaandika ndiyo "usomi" wenyewe eeenh!!?? Kweli mfumoKristu ulifanya kazi!!

Tuletee nukuu za Mohamed Said kutoka kwenye kazi zake ulizosoma uje hapa utuambie hii siyo sawa na badala yake ni hii hapa. This is a challenge to you. Nakupa mwezi mzima, uje na mambo matatu tu ambayo yapo kwenye kazi za Mohamed Said ambayo siyo kweli na wewe utuoneshe mbadala ambayo ni ukweli. Ukiweza hilo ntajuwa kweli Kigarama ni mkweli, Tena jumuika na wenzako, Nguruvi, Mwana Kijiji, Mag3, Jasusi, Sweke34 na wengineo uwajuwao wewe wote kwa pamoja. Nakuambia "in advance" hamuwezi.
 
Sasa hiyo ni "contradiction"? wewe ya Faiza Foxy huyawzi, mambo yako wazi hapa ukumbini tupe nukuu za kusema hii si sawa, sawa hii hapa. Achana na Faiza Foxy kasema nini, mimi nimeandika historia? unanchekesha!

Achana na Faiza kasema nini?? Oh! ilikuwa sio part ya hii thread? Hiki ndo kichekesho haswaa... By the way nani ni mwongo/mnafiki kati ya cousin wako Zomba aliye ku-PM au MS uliyedai anacheza shere? ulisha-apologize kwa mmoja wao?

Sasa inanifanya niamini maneno ya Zomba (my cousin) ameni PM na kuniambia hakuna cha Mohamed Said wala Mwanakijiji wote hao ni system na wanawacheza shere
 
Achana na Faiza kasema nini?? Oh! ilikuwa sio part ya hii thread? Hiki ndo kichekesho haswaa... By the way nani ni mwongo/mnafiki kati ya cousin wako Zomba aliye ku-PM au MS uliyedai anacheza shere? ulisha-apologize kwa mmoja wao?
Mkuu, umemshika pabaya FaizaFoxy. Hatoki.....lol.
 
MM,

......Unadhani haya maswali katika JF itasaidia kitu?

Mohamed

Mtafiti halisi au Wanataaluma hawawezi kuwa na mtizamo kama huo hapo juu.......naendelea kukusanya UDHAIFU wa misingi ya mitizamo yako na kudhihirisha wepesi wa maandishi/simulizi zako
 
Mr Right,

Usibishane na Jasusi,

Kwa hakika mimi namuelewa sana Jasusi kwa nini fikra zake zinampeleka kutilia shaka kila jambo ambalo kwake analiona hili singeweza kufanya yeyote ila Nyerere.

Bahati mbaya sana na Nyerere akipenda sana watu waamini hivyo.

Akitaka sana kuwa harakati za uhuru zianze na yeye.

Kuna kisa cha kusisimua sana siku Abdulwahid anamfahamisha Nyerere kuhusu baba yake Kleist, kuwa alikuwa anazungumza Kijerumani na Kiingereza, akijua shorthand (hati mkato), akijua kupiga typewriter na akijua kuweka vitabu vya hesabu na ndiye alijenga ile ofisi ya TAA ambayo TANU ilizaliwa.

Abdu akamweleza pia yeye alitokea mwanafunzi wa kwanza Territorial Examination na alikuwa anasubiri kwenda Makerere ndipo alipotiwa jeshini KAR kwenda kupigana Burma.

Hapo wapo katika kuandika historia ya harakati ya kudai uhuru pamoja na Dr Kleruu.

Nyerere alitatazika sana.
Kwa fikra yake alidhani mambo yangeanza na yeye 1954 anakuta historia inarudi nyuma miaka ya 1920.

Bila shaka ilimjia fikra yake mwenyewe. Je yeye ana historia kama ile? Vipi baba yake? Jibu ni kuwa hapana hawana historia kama ile?
Ikabidi historia ile ihujumiwe na ule mswada hadi leo haujulikani ulipo.

Sasa mimi wala simlaumu Jasusi.
Hiki ni kitu kipya sana kwa wengi kwa hiyo kila lile ambalo waliona ni saizi ya Nyerere wakiambiwa hakufanya watalitia kasoro.

Nasema na siishi kusisitiza kuwa ikiwa mie nasema uongo waandike kitabu ukweli ujulikane.
Prof. Haroub alimuonya Nyerere kuwa akiwa kimya katika histroria niloandika itamuharibia sifa yake pakubwa.

Ndiyo sasa tunabishana Nyerere kasoma kitabu cha Mohamed Said au hakusoma...na hiki kitabu changu ndicho kilichosimama tunaingia mwaka wa 14 kuwa ndiyo historia ya kuaminika kuhusu uhuru wa Tanganyika na kinasomeshwa kote duniani.

Toleo la Kiswahili tunaingia chapa ya tatu na kwa kweli kitabu ni maarufu sana watu wakenda dukani wanasema "Nipe kitabu cha Abdu Sykes" na muuzaji anajua ni kitabu kipi.

Sahib wangu mmoja prof wa African History nimemueleza jinsi baadhi ya watu walivyokasirishwa kuona historia rasmi imetolewa manani kanishauri kufuatilia hilo kwa karibu na niandike "paper" Insha Allah watakuwa na kongamano mwaka kesho na angependa nihudhurie na niwasilishe mada hii.

Mohamed

Hapana. Mimi ninachotaka ni ushahidi kwa kila allegation unayoitoa. Ukishajipachika "urasmi" wa kila unachokisema unabeba mzigo mzito wa kutoa ushahidi wa allegations zako. Bila ushahidi nitaendelea kuamini kuwa hizi ni simulizi za kijiweni.
allegation kama hii:

Kwa fikra yake alidhani mambo yangeanza na yeye 1954 anakuta historia inarudi nyuma miaka ya 1920.

kwanza a/ ulikuwepo katika kikao hicho au uliwahi kuzungumza na Dr Klerru? na b/ Uliwahi kuzungumza na Abdulwahid na hii unanukuu kutoka kinywani mwake? Na hii ndiyo unayoita historia rasmi? na c/ uliwezaje kuingia kwenye fikra za Nyerere na kujua alichokuwa anakifikiria? Nenda Butiama ukatupigie picha kile kitabu ambacho umedai hapa kimo miongoni mwa collections za Nyerere.
 
Ndio hulioni. Sasa wewe kama unayajuwa ya huyo unaemtaja si utuletee hapa tufaidike, kwanini umngoje Mohamed Said?

kwa hiyo unakubali kuwa Brother MS anafanya kosa lile lile analodai wengine kulifanya?.......kuandika historia upya na kuacha kutaja washiriki wengine wa harakati za uhuru....
 
Nguruvi3, Kigarama, Mag3, Mzee Mwanakijiji..

Ebu na nyie jipangeni kama itawezekana muungane kwa pamoja muandike histori ya Uhuru wa Tanganyika..

Tena itakuwa vizuri mpinge yote yale ambayo sio ya kweli kwenye kitabu cha Mohamed Said..

Inawezekana kuna mashujaa wengine nyie mnawajua waliopigania uhuru wetu Mohamed Said, hawakuandika kutokana na udini wake dhidi ya ukirstu..

Na hicho kitabu ndio kitakuwa historia kamili ya uhuru wa Tanganyika sababu kitaandikwa kwa pamoja na magwiji niliowataja..

Tunakisubili kwa hamu...

Ungeelewa kinachokosolewa hapa...wala usingeandika hayo hapo juu....hebu jaribu kumuambia ajibu hoja/maswali anayoulizwa.......usiwe kama wajumbe wa gogovivu
 
Siku moja nilimuuliza Mohamed kwamba mbona kwenye masimulizi yake sioni jina la MARTIN KAYAMBA? Mpaka leo Kimyaaa!!

Kigarama,

Nimepata humu ndani kujibu kuhusu Martin Kayamba lakini simkumbuki aloniuliza.
Kayamba alikuwa kibaraka wa Waingereza na akijikomba sana kwao.

Yeye ni "contemporary" wa Kleist Sykes na maisha yao wote yamo katika "Modern Tanzanians" cha John Iliffe.

Chungulia hapo chini Erika Fiah kasema nini kuhusu Kayamba:

"Kalamu ya Fiahilikuwa haina muhali. Katika rambirambi alizotoa za kijeuri na za dharau juu yakifo cha Martin Kayamba,[1]Fiah aliomboleza kwa kusema kwamba Waafrika hawakunufaika kwa elimu ya Kayambawala kwa wadhifa wake kama karani wa kaimu Katibu Mkuu."[1]
Ukipenda unaweza kumsoma Kayamba katika kitabu hiki:
Kayamba, Martin,The Autobiography ofMartin Kayamba, “The Story of Martin Kayamba Mdumi, MBE, of the Bondei Tribe” MargeryPerham, (ed) Ten Africans, 5-272.
Mwenyewe umeona umeuliza swali gumu sana na shingo unatoa.
Ndiyo maana dada yangu FF husema "usinchekeshe."

Mie mabuku yote hayo nishayanywa miaka mingi ilopita.

Mohamed



Huu ndio ukwepaji wa kujibu maswali......Brother MS jibu swali!
 
quote_icon.png
By FaizaFoxy

Sasa inanifanya niamini maneno ya Zomba (my cousin) ameni PM na kuniambia hakuna cha Mohamed Said wala Mwanakijiji wote hao ni system na wanawacheza shere
Labda ....Zomba(her cousin) alim PM tena FF na kumuambia MS hayupo kwenye system.....ilikuwa ni false alarm tu..!
UNAFIKI huu ni kielelezo cha kwanini baada ya miaka 50 ya uhuru bado kuna watu wanasema kuna mfumo Kristo.
 
Huu ndio ukwepaji wa kujibu maswali......Brother MS jibu swali!
Yeye atakuambia andika 'paper ' na wewe......ila wale wa mihadhara ya nje ya nchi huwa anawajibu eti kwa sababu hawaulizi maswali kama ya humu ndani! sijawahi kuona 'scholar' aliye bogus kama Mohamed Said. Utaandikaje makala halafu ukashindwa kui defend kwa hoja?
 
Si ukweli kuwa Nyerere alipokelewa na Abdul Wahid? si ukweli kuwa Nyerere hakuwa muasisi wa TAA? si ukweli kuwa Abdul Wahid ndio alitoa jina la TANU? ni kipi ambacho si ukweli? tuoneshe nukuu ya Mohamed Said ambayo si ukweli halafu wewe tupe iliyokweli, si kuandikia mate na wino upo. "si ukweli" huoneshi hilo "si ukweli" liko wapi, "si ukweli" huoneshi ukweli uko wapi.
Faiza wewe unapiga makelele wala hujui kujenga hoja, tafadhari acha makelele yako na sifa za kijinga hapa jamvini, mzee Mohamedi Said aliliona bandiko langu akalijibu kabla ya wewe kuweka upupu wako hapa. Rudi usome jibu la mzee wako.Hao wazee unaowaorodhesha hapa na mchango wao hakuna anayeukataa, tunachokikataa hapa ni huo mtazamo finyu wa mzee wako kwamba wao ndio pekee walioleta ukombozi na kwamba Nyerere hakufanya chochote kuwaendeleza waislam.
 
Back
Top Bottom