Historia ya Wanyakyusa kufahamika zaidi kuliko Wasafwa ambao ni wazawa halisi wa Jiji la Mbeya

Hakuna kilichoharibika wakae wanyakyusa ama wasafya yote ni sawa,hakuna aliyewafukuza wasafya ni wao wenyewe na ubinafsi wao .by the Way "survival for the fittest"
 
Mimi nikajua unataka kutuambia kuwa wanyakyusa ni watu wa Zimbabwe. Au nikajua unataka kusema kuwa Yale maendeleo makubwa ya mkoa mbeya yameletwa na Wasafwa na siyo Wanyakyusa kama tujuavyo. Kumbe ni historia ya machifu na uhuru
 
Ni sawasawa na mji wa mbalizi na kabila la Wamalila.

Ila Wamalila nao hawajulikani kisa ni uchache wao
 
Mbeya n mkoa wenye makabila mengi kuna wamalila pia wamesaulika kabisa
 
Maana ya neno MBEYA unaipata kwenye lugha gani?

Ha ha ha!
Kuna wanyakyusa Malawi-wanaitwa wa Ngonde, Zambia na hata Zimbabwe.
Namfahamu jamaa akiitwa Ngonde kwa jina la UKOO na ni msafwa, ana ndugu Malawi, anazungumzia NGONDE Empire mara nyingi nikikutana naye, anasema ilikuwa kubwa na hata sasa ipo kubwa isipokuwa kutokana na mambo ya lugha sijui Lahaja, Rejesta, jin linatoholewa, mara Gonde, Gondwe, Ngonde n.k

Historia inasemaje kuhusu wamisionari na mkoa wa Mbeya? Isije kuwa kama Wachaga, Wahaya na Umisionari, wameingilia huko, wakawapa madini wakwanza, basi wakajiona viiiiichwa, kumbe ni hali ya kutangulia tu.
 
Wasafwa wazee wa kulima viazi.
Sema wasafwa wa hapo karibu na Kiwira (Mbeye 1, Ntokela n.k ) wanapwaya sana kwenye usafi na wamama wana bass nzito kama wanaume! Ila wana roho nzuri sana kwa wageni!
 
Wasafwa nao wajitutumue kujitangaza tamaduni zao.

Wasitegemee watu kutoka nasaba nyingine kuwabeba. Wajibebe
 
Inasemekana mwenye Hotel ya silver stone tunduma ni mswafwa

Kuhusu madon mbeya toka kitambo ni wakinga hata hapo block t walijaa sana

Hivi eland Hotel bado ipo hapo block t

Ova
Naona ni wazi kabisa Mbeya hujaenda miaka, Mbeya imebadilika sana mkuu, hio erland hotel ilishakufa walijenga tawi la karibu la chuo kinaitwa teku. kwa sasa hapa Mbeya kuna hoteli kama Tughimbe, Desderia (ya sugu), Mdope, usungilo, n. k hizi zote nilizotaja wamiliki ni wakinga.

hotel hio ya silver stone sijajua maana ipo mkoa mpya wa Songwe, mambo yalivyobadilika kwa sasa siwezi shangaa nayo ikawa ni tbt zilizopendwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…