Historia ya Wanyakyusa kufahamika zaidi kuliko Wasafwa ambao ni wazawa halisi wa Jiji la Mbeya

Historia ya Wanyakyusa kufahamika zaidi kuliko Wasafwa ambao ni wazawa halisi wa Jiji la Mbeya

Dah umezunguka mzee Hadi chimala. Kumi Bora unapakumbuka ?
Aise sana mbeya nimeizunguka sana maana nlipomaliza la saba nkatupwa mbeya...
Chimala nlisoma shule ya msingi pale
Nimakaa sana kwa mzee mmja maarufu wanamuita mjerumani alikuwa kama mzungu fulani
Nkarudi dar form 1 tena nkatupwa mbeya mjini kule nako nkakaa kwa mzee mmja tulimpa jina la gaddafi
Unajuwa zamani utotoni nlikuwa mtukutu sana,aise hizo familia nlizopelekwa ilikuwa si mchezo yaani kazi kazi
Ila mkoa wa mbeya ulinijenga sana aise.....
Kuzunguka mbeya nlizunguka maana mzee hyo alikuwa na chai maharage sasa kila jumamosi ilikuwa lazima na mm niingie mzigoni kama konda kuchukua hela za abiria
So mkoa ule nlitembea kiaina
Tulikuwa tunaenda mpaka santilia huko milimani

Ova
 
Huu uzi umenifanya niwakumbuke wababe wa zamani hapo mbeya mjini
Wakina dr zimwi na akina fike [emoji1]

Wanyakyusa,walikuwa wanapenda sana huu usemi" we dogo hebu njoo"

We dogo ,we dogo [emoji1]

Ova
 
WASAFWA NDIO WAZAWA HALISI WA WILAYA ZA JIJI LA MBEYA, KILITOKEA NINI MPAKA WANYAKYUSA WA WILAYA ZA NJE YA JIJI KUFAHAMIKA NDIO WENYEJI?

Yani hii Tanzania nzima ukiuliza jiji la Mbeya linakaliwa na kabila gani, fasta mtu anakujibu wanyakyusa lakini ukweli ni kwamba wasafwa ndio wenyeji na hata hili jina la Mbeya lina asili ya kisafwa. si ajabu mtu anaweza asijue kwamba waoambnaji wakuu na matajiri wengi wa mbeya wenye maduka mengi, mahoteli, viwanda na makampuni ni wakinga lakini ukimuuliza swali mwenyeji wa hapa mbeya ni nani, atakujibu fasta tu mnyakyusa, kilotokea nini hadi ikawa hivi?

ni kwamba nchi ilipopata uhuru kulikuwa kuna wanyakyusa wengi wazawa wa wilaya za rungwe na kyela walianza kuja na kuhamia wilaya ya Mbeya mjini (kwa sasa jiji) ambako ndio makao makuu ya mkoa wa Mbeya, wageni wengine nao pia walikuja kuhamia mjini kupata huduma za kijamii, kusoma, kufanya biashara, n.k.

Muda huo wakazi wa mbeya mjini wengi walikuwa ni wazawa ambao ni wasafwa kundi la wamalila, shida ikaja kwamba wasafwa wakiona wageni walikuwa hawataki kuchangamana nao walikuwa wanahamisha makazi kwenda sehem ambayo wapo peke yao, mji ulizidi kuchanganya na kufanya wanyakyusa na wageni wazidi kuja mjini na ikawa usumbufu kwa wasafwa kuhama hama mji unavyozidi kupanuka, ikafikia kipindi wengine wakaanza kukimbilia maeneo ya mbali zaidi hata milimani.

matokeo yake hapa mjini makabila ya ziada yaliyokuja kama wanyiha, wandali, wakinga, wahehe, wangoni, wabena, n.k. wao wakawa wanajua huu mji ni wa wanyakyusa maana wasafwa wengi walikimbilia milimani ikawa vigumu kuwajua wao ndio wenye mji.

Laiti wasafwa wangebaki kwenye huu mji huenda wangekuwa na maendeleo sana kuzidi hata wanyakyusa, mji huu ulikuwa ndio makao makuu ya mkoa wa Mbeya lakini hii bahati wakaichezea na ni ngumu kurudi tena. wasafwa waliletewa hivi vitu vizuri hapa mjini ila wakavikimbia.

-hapa mjini serikali ilijenga shule nyingi ila wasafwa walizikimbia

-ajira nzuri enzi hizo zinahitaji elimu hata za shule ya msingi au form 4 zilikuwepo mjini wao zikawa zinawapita

-mji ulianza kujaa na kukawa na fursa za biashara ambazo wasafwa wangeweza kupata pesa lakini kujitenga kwao kukaliacha soko wazi kwa wageni.

-madaraka, vyeo na teuzi serikalini za kuongoza mji huu wakawaachia wageni ambao nao walitumia bahati hii kuwekana maofisini na kupeana vyeo.

-viwanja vingi waliviacha ama kuviuza na kukimbilia milimani kusiko hata na huduma za jamii, n.k.

-baadhi ya wasafwa waliorudi hapa mjini ama waliobaki maeneo ya karibu wakaanza kujitambulisha ni wanyakyusa kwa kuogopa aibu na wengine kufikia hatua ya kufuta majina ya ukoo ili kuepukana na aibu, hii tabia hadi sasa inaendelea.

Ni historia yenye kusikitisha ila ina funzo kubwa sana, mkataa kwao hugeuka mtumwa.

Mwisho kwa kuhitimisha naweza kutoa ushauri kwa wasafwa kwamba historia haiwezi kubadilika itabaki kwajili ya kujifunza lakini mnachoweza kubadilisha ni muda wa mbele (future) kwa maamuzi mnayoweza kuanza kuyatekeleza sasa ili angalau mrudishe hadhi, mapendekezo yangu kwenu:

- wasafwa mzingatieni sana elimu pambanieni na ikibidi mjinyime watoto wasome.

- mjipanue na kutafuta fursa mpya za kibiashara na kujiajiri, Mbeya ni jiji lina watu wengi wenye mahitaji mengi muangalie ni sehemu zipi mnaweza kuchota pesa.

- muwe na bidii ya kugombea nafasi mbalimbali za kisiasa na uongozi kwenye huu mji wenu, mpambanie nafasi za kupaza sauti ya kero zetu wageni wa mbeya na zenu wazawa halisi wa mbeya.

-msaidiane na kubebana ili walio chini nao wawe na maendeleo, roho za umimi na ubinafsi haziwezi leta maendeleo.

-mjivunie asili yenu ya usafwa, kuna baadhi ya wasafwa hufuta majina yao ya ukoo na wengine kukana kabila lao, huu ni ujinga, jivunie kabila lako, nyumbani ni nyumbani kwa jirani sio kwako.

bila kufanya haya hakuna kitachobadilika..
Kwa sasa sisi Wanyakyusa na Wasafwa ni kitu kimoja, tunaoana na kuheshimiana. Tumekuwa ndugu na tunachangamana kila maeneo, milimani na mabondeni.
 
Aise sana mbeya nimeizunguka sana maana nlipomaliza la saba nkatupwa mbeya...
Chimala nlisoma shule ya msingi pale
Nimakaa sana kwa mzee mmja maarufu wanamuita mjerumani alikuwa kama mzungu fulani
Nkarudi dar form 1 tena nkatupwa mbeya mjini kule nako nkakaa kwa mzee mmja tulimpa jina la gaddafi
Unajuwa zamani utotoni nlikuwa mtukutu sana,aise hizo familia nlizopelekwa ilikuwa si mchezo yaani kazi kazi
Ila mkoa wa mbeya ulinijenga sana aise.....
Kuzunguka mbeya nlizunguka maana mzee hyo alikuwa na chai maharage sasa kila jumamosi ilikuwa lazima na mm niingie mzigoni kama konda kuchukua hela za abiria
So mkoa ule nlitembea kiaina
Tulikuwa tunaenda mpaka santilia huko milimani

Ova
Daah we mwenyeji. Mjerumani alishakufa na eneo lishauzwa kwa tajiri mmoja hivi amejenga Sana pale. Pia mji umeamia kule mlimani viwanja viliunzwa Kama njugu
 
Daah we mwenyeji. Mjerumani alishakufa na eneo lishauzwa kwa tajiri mmoja hivi amejenga Sana pale. Pia mji umeamia kule mlimani viwanja viliunzwa Kama njugu
Yah nlikaa pale,nakumbuka walikuwa wasabato kindakndaki aise
No soda no chai ,vyakula chemshachemsha....
Pale nlijifunza kazi nyingi sana kuanzia kilimo mpaka kuendesha vyombo vya moto
Sema sasa mjerumani aka mzee Charles kesi alizokuwa analetewa kila siku haziishi maana kila siku mm nlikuwa na misala
Sema licha ya kuwa na misala kazi pale nlikuwa napiga sana
Yah nlisikiaga paliuzwa
Ila kukaa mbeya kulinijenga sana sana

Ova
 
Yah nlikaa pale,nakumbuka walikuwa wasabato kindakndaki aise
No soda no chai ,vyakula chemshachemsha....
Pale nlijifunza kazi nyingi sana kuanzia kilimo mpaka kuendesha vyombo vya moto
Sema sasa mjerumani aka mzee Charles kesi alizokuwa analetewa kila siku haziishi maana kila siku mm nlikuwa na misala
Sema licha ya kuwa na misala kazi pale nlikuwa napiga sana
Yah nlisikiaga paliuzwa
Ila kukaa mbeya kulinijenga sana sana

Ova
Ndio ndio. Wasabato kanisa wamejenga kubwa Zaidi
 
Daah we mwenyeji. Mjerumani alishakufa na eneo lishauzwa kwa tajiri mmoja hivi amejenga Sana pale. Pia mji umeamia kule mlimani viwanja viliunzwa Kama njugu
Alafu Kyle kutoka nyumbani kwa mjerumani kama unakwenda mlimani
Alikuwopogi mama mmj mganga anaitwa hidaya,ilikuwa ukikaa usiku unasikia ngoma znapigwa watu wanaimba na kulia [emoji1]
Kuna siku nlijiuliza tukasema Acha twende usiku huko ilikuwa saa saba usiku,tulitoroka nyumbn pale kwenda kule...aise kufika tulikuta watuuu
Wakatustukia wacha watufukuze,kesi ikaletwa kwa mzee tena pale [emoji1]
Nlipokuja ondoka hapo chimala wazee wa kiburushi walifurahi sana
Maana walikuwa wanaona kama nawaharibu watoto zao....
Ila ilipopita kama mwaka hivi ahhh aise wenyewe wakaanza kunimiss
[emoji1] huko
Na pia nliishi pia kwenye zile kota za FAO igurusi,napo hko familia nliyokuwa nakaa nayo wakanitimua
[emoji1]
Ila mbeya nlipapenda sana

Ova
 
Wanyakyusa ni wavivu na wana kiburi na majivuno sio rahisi kukuza mji. Ila kuupaisha ujulikane hilo wanaweza sana tu.

Wasafwa mpaka kesho wanaogopa kuchangamana, huko ituha wako kibao waliohamia miaka hiyo wakidhani ni mbali na mji. Lakini sasa hivi lami imewafikia mpaka mlangoni. Wageni wanajazana hapo ituha, mijengo inaangushwa kila leo.
Wengine kama ilivyo kawaida wanahama wanakimbilia milimani zaidi, na akihama anauza kila kitu anaenda kuanza upya huko milimani .

Hawapendi kuchangamana, walau kizazi hiki cha sasa ila pia bado wasafwa kuchangamana ni tatizo kubwa. Bado wanakimbilia kujenga milimani wakae peke yao. So muda mrefu ituha itamilikiwa na wageni.
Hata viongozi wao tu sio wasafwa, aisee hili kabila.
 
wazawa watabaki kuwa wazawa mkuu, hata hili jina la Mbeya lina asili ya kisafwa, kule mteremko wa mbalizi na mlima wa nyoka, magari yanapopata sana ajali wanaofanya mila ni wasafwa, watu wakizama kule ziwa ngosi ni wasafwa ndio hufanya mila kuwapata, bila mila hamuwezi kuipata hio maiti. wasafwa walichokosea ni kukimbia maeneo wakiona wageni (hadi leo wanataniwa kwa jambo hili)

ila kwa idadi ya wakazi naweza kusema ni wanyakyusa japo nao wana kubarua kizito cha kujikwamua kiuchumi hasa kwenye utafutaji, wanyakyusa wengu ukifatilia wamejazana maeneo yenye maendeleo ya chini ama kawaida kama nzovwe, mamajoni, n.k. zile sehemu zenye maendeleo kama forest, block t, isyesye, n.k wamejazana wakinga pamoja na wageni wengine.

uzuri ni kwamba angalau wanyakyusa shule inawabeba wanapata ajira lakini sikuhizi kuna tatizi kubwa la ajira linalowalazimu vijana wageukie kujitafutia, ubaya ni kwamba kwenye utafutaji wa biashara na kujiajiri wanyakyus hapa wapo nyuma, ukifika sehemu kama mwanjelwa na kabwe maduka mengi yanamilikiwa na wakinga na wageni wengine.
Upo deep dogo ww ni wa soko matola, forest au isanga???
 
Niliwahi kuishi na Wasafwa 1996 kule Uporoto kwa muda wa mwezi 1 ila nilichojifunza toka kwa Wasafwa kuwa ni watu wapole na wasiojishughulisha na ufuatiliaji wa maisha ya mtu hata kidogo hii ni tofauti kwa Wanyakyusa wao......Ila naikumbuka Igoma,Simambwe,Isyonje,No_1 nk
Isyonje ya zamani kulikua na baridi makete isubiri, naona mabadiliko hali ya hewa saivi pa kawaida sana

Isyonje kwenye cabbage kama tako la kajala 🤠
 
Huu uzi umenifanya niwakumbuke wababe wa zamani hapo mbeya mjini
Wakina dr zimwi na akina fike [emoji1]

Wanyakyusa,walikuwa wanapenda sana huu usemi" we dogo hebu njoo"

We dogo ,we dogo [emoji1]

Ova
Hadi leo hadi kesho imekua tabia
 
Maana ya neno MBEYA unaipata kwenye lugha gani?


Namfahamu jamaa akiitwa Ngonde kwa jina la UKOO na ni msafwa, ana ndugu Malawi, anazungumzia NGONDE Empire mara nyingi nikikutana naye, anasema ilikuwa kubwa na hata sasa ipo kubwa isipokuwa kutokana na mambo ya lugha sijui Lahaja, Rejesta, jin linatoholewa, mara Gonde, Gondwe, Ngonde n.k

Historia inasemaje kuhusu wamisionari na mkoa wa Mbeya? Isije kuwa kama Wachaga, Wahaya na Umisionari, wameingilia huko, wakawapa madini wakwanza, basi wakajiona viiiiichwa, kumbe ni hali ya kutangulia tu.
Mkuu Ngonde hata leo ipo.
Ndonde area ni eneo la Unyskyusani linalotokea Kaskazini ya Malawi, Kyela yote na sehemu za Rungwe.
Ingawaje leo ukitamka mnyakyusa wa Ngonde utaeleweka kuwa unamaanisha mnyakyusa wa sehemu tambarare za Kyela na Malawi Kaskazini.
Wanyakyusa wa milimani Tukuyu, Busokelo na huko Mwakaleli wanajulikana kama ni wa Kumwamba(milimani).

Wanyakyusa wa Ngonde na wale wa Kumwamba, kitabia wako tofauti ingawaje lugha ni moja.
Wale wa Ngode ni wepesi kujidai, kujiamini na ni waongeaji sana.
Wanawake wa Kyela wengi ni "weupe" na wanapendeka.
Wanyakyusa wa Kumwamba wengi ni weusi na ni wakulima wa ndizi sana.
Wale walio mipakani na makbila ya wasafwa, wakinga, wapenja, waandali, wengi wamechanganya damu. Hawa kitabia ni watu wafanyakazi kweli kweli, hawana utani na akiamini kitu ambacho anaona ndiyo ukweli, si rahisi kumchanganya akili.

Kwa ujumla, wanyakyusa wote huamini ukweli na wako very loyal.
Ila kiujumla huwezi kumdharau mnyakyusa, hata kama ni masikini hana kitu.
Kwa ujumla, wanyakyusa nawa eneo lote la nyanda za juu kusini, ni wapambanaji na hawaogopi ku risk maisha yao.
Wakoloni waliwahi sema ,they are fierce fighters.
Kitu cha ziada, wanawake wa kinyakyusa ni wachakarikaji kuliko wanaume.
Na ukimzingua au kumdanganya katika mapenzi anaweza kukukung'uta.
 
Kwa ujumla, wanyakyusa wote huamini ukweli na wako very loyal.
Ila kiujumla huwezi kumdharau mnyakyusa, hata kama ni masikini hana kitu.
Kwa ujumla, wanyakyusa nawa eneo lote la nyanda za juu kusini, ni wapambanaji na hawaogopi ku risk maisha yao.
Wakoloni waliwahi sema ,they are fierce fighters.
Kitu cha ziada, wanawake wa kinyakyusa ni wachakarikaji kuliko wanaume.
Na ukimzingua au kumdanganya katika mapenzi anaweza kukukung'uta.
Hio sifa ya mnyakyusa hapendi dharau kwa kiasi flani kulingana na ninavyowajua wanyakyusa huwa inatumika sana na wanawake wa kinyakyusa kuficha ile tabia ambayo ni maarufu kwa baadhi yao kuwa na viburi na kutaka usawa na wengine hata ubabe mbele ya wanaume, hata wewe umekiri wazi hio point ya mwisho kwamba wapo wenye nguvu za kushushia vipigo wanaume. kwa upande wa wanaume umkute anasema hapendi dharau ni nadra sana maana mwanaume wa kinyaki huwa anacheza na mazingira tu, akiona sehem flan haifai anajiweka pembeni.

Kwenye elimu wanyakyusa wanaupiga mwingi tu na wapo maofisini wanakula mema ila kwenye suala la upambanaji kwenye biashara kwa wanyakyusa nikiwa kama mwenyeji niliyeishi hapa Mbeya bado wapo level za kawaida mno, wengi hata biashara wanafanya kwa nidhamu ndogo ya pesa hasa kwenye kushindwa kujibana, ni kawaida kumkuta mama wa kinyakyusa anauza maparachichi lakini ana wigi la bei na anakula chipsi mayai anashushia na pepsi yake, mambo ya kujibana bana wakati kipo kwao ni ngumu, Na hapa wote ni mashahidi hata Mwanjela tu hapo walio tawala na kukua (domainating and growth) ni wakinga na wageni, wanyakyusa wapo ndio lakini unakuta wapo pale pale (stagnant) biashara ile ile, na hii ni sababu kujibana kwao ni ngumu, hata wafanya biashara wengi hupambania watoto wao wasome kwa lengo la kuajiriwa, huko ndio wanaona kwenye uhuru.

wanawake wa kinyaki ni wachakalikaji kuliko wanaume, hii kwakweli nami nimeisikia ila sijathibitisha, maana nao wanaume wanapambana ila nao wanawake wanapambana pia, sijajua kigezo ni kipi hasa kilitumika ila naweza kusema labda ni kwamba kuna jamii nyingi hasa za huku kusini na pwani mwanamke anategemea zaidi kutafutiwa ila kwa wanyakyusa tunavyoona wanachakalika basi ndio watu wanashangaa na kukuza hii ishu sana hadi wengine wanaanza kusema kwamba wanawake wanapiga kazi sana kuzidi wanaume.

Kuhusu wanyakyusa hadi wapewe title ya fierce fighters bado sijajua hilo, Kwa wahehe mkwawa mziki wake ulikubalika, kwa wachaga mangimeli nae alileta resistance si haba, kina Mirambo nao wajerumani walipelekewa moto kimtindo, wakurya hao walitumika kwenye majeshi ya wakoloni, huko Singida nako naskia kuna sehem wakoloni walishindwa kabisa kutawala. Ila kwa wanyakyusa sijawai kusikia hilo, nachojua wajerumani waliingia unyakyusani kwa resistance ndogo waliweza kuwamudu ndani ya muda mfupi tu ila wamishenari walijenga shule, makanisa, mahospitali, n.k.
 
Acha maneno mengi weka bei ya kg moja ya kitimoto hapo mbeya!!
 
Inasemekana mwenye Hotel ya silver stone tunduma ni mswafwa

Kuhusu madon mbeya toka kitambo ni wakinga hata hapo block t walijaa sana

Hivi eland Hotel bado ipo hapo block t

Ova
Hata kama Wakinga ndiyo matajiri wa Mbeya mbona wanaishi maisha duni kuliko maskini Msafwa.

Yule mwenye Paradise Hotel pale Soweto anaitwa Kasisi, alikuwa anaishi nyumba ya tope kule Ilemi hata haikuwa na umeme.

Nashauri Wasafwa waishi kama Wasafwa kuliko kuishi kama matajiri lakini utajiri wa masharti
 
Elimu pia iliwapitia kushoto

Ova
Kwa taarifa yako Chief SECRETARY wa kwanza wa Tanzania huru baada ya Mwingereza kuondoka alikuwa anaitwa Dickson Nkembo, Msafwa kutoka Tarafa ya Iwindi. Utasemaje Wasafwa hawakusoma?
 
Back
Top Bottom