nasrimgambo
JF-Expert Member
- Jan 10, 2017
- 1,902
- 2,488
Wiki ina neno lake la Kiswahili, 'Juma'Zamani kabla ya baraza la kiswahili, wazee wetu walikuwa wanasikiliza wazungu wakisema cabbage wao wanasema kabichi.. wazungu wakisema week wao wiki.. ila hawa watu wa baraza kujua kwingi ukimuuliza decorder kwa kiswahili inaitwaje wanaenda ofisini kujitungia tu kisha wanarudi na kisimbusi!..
baadae haya maneno mapya yatageuka kigujerati lugha mpya kabisa.Propera Shafti kuitwa kipopojoka, aiseee
sawa tu dunia inajongea zaidi kuwa moja na huenda miaka mia ijayo lugha zitajielekeza kuwa moja.Kiswahili lugha adhimu kabisa.
Mapendekezo yako ni kwamba kiswahili "kisingekuwepo kabisa", maana kila neno la kiingereza umependekeza kiswahili chake kiwe ni "kiingereza kiswahili". Nadhani sio sawia.
Umependekeza hivi:
1. Tablet ingeitwa tableti.
2. Fridge ingeitwa friji
Kwa mtazamo huo kiswahili kama lugha itakua vipi endapo itajibanza kwenye kiingereza kwenye kila kitu mkuu ?
Neno KISHKWAMBI ni neno mujarab kabisa lisilo na tashwishwi yoyote. Na hiyo ndio ladha halisi ya lugha ya kiswahili.
Karibu
Tusubirisawa tu dunia inajongea zaidi kuwa moja na huenda miaka mia ijayo lugha zitajielekeza kuwa moja.
Drones huitwa ndege kipepeo[emoji1652]Wawe wanashirikisha wadau bana.
Na hata kama hawashirikishi wengine watunge basi majina ama maneno mazuri. Sasa kama hili kishkwambi Yani unaltamka huku umekunja uso. Angalau wangeita tu tableti.
Mengine yanayokera jokofu wangeacha tu friji. Smart phone Eti simu janja. Eti password nywila unabaki kushangaa WTF?! Angalau wangeita tu paswedi.
Nahisi ni wakenya Hawa kwasababu juice eti kinywaji tamu unabaki kukasirika tu afadhali bongo tumekomaa na juisi. Shirikisheni wadau mnapotunga nakuita vitu kwa majina ya ajabu ajabu.
Sijui drones wanaziitaje?
Mkuu nifanyie hisani ya maneno haya:Kiswahili lugha adhimu kabisa.
Mapendekezo yako ni kwamba kiswahili "kisingekuwepo kabisa", maana kila neno la kiingereza umependekeza kiswahili chake kiwe ni "kiingereza kiswahili". Nadhani sio sawia.
Umependekeza hivi:
1. Tablet ingeitwa tableti.
2. Fridge ingeitwa friji
Kwa mtazamo huo kiswahili kama lugha itakua vipi endapo itajibanza kwenye kiingereza kwenye kila kitu mkuu ?
Neno KISHKWAMBI ni neno mujarab kabisa lisilo na tashwishwi yoyote. Na hiyo ndio ladha halisi ya lugha ya kiswahili.
Karibu
Covid 19 = Corona Virus Disease-19.Hata hili jina UVIKO_19 nani alitafsiri kutoka COVID_19 yaani Corona Hadi kuita UVIKO_19 vigezo gani walitumia wakati ni gonjwa jipya
Ukiachana na hiyo uliugonjwa wa juzi uliotokea Kusini Lindi mwanzoni walikosa jina ila kwa Sasa wanaita MGUNDA[emoji23]
Mkuu nimefukunyua lakini sijafanikiwa kupata maana toshelezi ya maneno hayo.Mkuu nifanyie hisani ya maneno haya:
1> Ukuruba
2>Usufuba