Hivi haya ninayoyapitia na wanaume wengine mmeyapitia kwenye ujana wenu?

Hivi haya ninayoyapitia na wanaume wengine mmeyapitia kwenye ujana wenu?

Mimi ni kijana mwenye miaka 20 toka nizaliwe sijawahi kuyafurahia mapenz ngoja niwape historia yangu kidogo kwenye mapenz mwaka 2019 nilienda kufanya kazi kwa kaka yangu Morogoro wilaya ya Malinyi pale dukan tulikuwa wafanyakaz watatu halafu wote ndugu katika wote mi ndo nilikuwa mdogo japo mi ndo nilikuwa kiongozi wao

Tukaendelea kufanya kazi kuna bint mmoja nitamuita rehema(sio jina lake) alikuwa mteja pale dukan wale ndugu zangu wawil mmoja nitamuita zakayo mwingine John mi nitajiita Steve kwa upande wangu nilikuwa mpole Sana yule Rehema alizoeana Sana na zakayo Mimi na zakayo tulikuwa tunaelewana Sana yule rehema akawa anamwambia zakayo kuwa ananipenda zakayo nae akawa ananiambia siku zikazid kwema rehema akawa ananizoea taratibu ikafika kipindi Rehema akawa ananifuata Kila siku dukan il tuongozane wote maana tulikuwa majilani siku zikasonga jamaa zangu wakanishaul nimtongoze kwel nikamtongoza ilikuwa Kama nimemchelewesha na ndo alikuwa msichana wakwanza kutongoza.

Nilimpatia Kila alicho kitaka zilipita Kama wiki mbil nikamuomba game akanambia tarehe flani tukutane nyumbani kwao kulikuwa na sherehe baada ya kufika mda tuliopanga nikawa nampigia sim hapatikani nikaamua mimtimbie hukohuko maana nilikuwa na upwilu Sana japo nilikuwa sijui nitamfanya fanyaje ila niliamin naweza baada ya kufika kwao milimkuta anacheza kaloa jasho mwili mzima nilipo muuliza kwanin ulizima sim akasema iliisha chaji

Nikamuuliza mbona umelowa jasho akasema kazuiliwa kukaa bila kucheza ikabidi siku hiyo tuhairishe ikawa kila nikimwomba anakuwa na visingizio vingi baada ya wiki moja akanambia anasafil kwenda ifakala atakaa wiki mbil sikuwa na namna Zilipita wiki mbili hata hakuja nikazoea kuwa nimempoteza baada ya Kama miezi sita nikakutama na msichana mmoja anaitwa Sarah (jina halisi) Sarah alikuwa mtoto wa getkal alikuwa amakaa kwa shemeji yake (mme wa dada yake) nilisota Sana kupata namba yake kunajamaa alikuwa anafahamiana na Sarah yeye ndo alinipatia namba ya Sarah kwa kumpa pesa nilianza kumtongoza haikupita hata wik akanikubali nikawa nampa anachotaka tukazoeana ikawa kila nikimwomba penz visingizio vingi baada ya Kama mwez nikapoteza sim namba yake nikawa Sina baada ya kurinew lain nikasubil pengine atanipigia Wala hakunipigia

Nikajiuliza inamaana hanipend hata kidogo niliumia mno na sikujua nitampata wapi mungu si asuman siku moja nilikutana nae njian nilidhan ataniomba msamaha lakin hakuonekana kujal ikabidi Mimi ndo nijitetee nikamwelewesha hakutaka kunielewa akidai huwa ninamtafutaga nikiwa na haja zangu toka hapo hakunielewa tena tukawa tumeishia hapo nikakaa kama mwaka mmoja itaendelea.....
Wale wanaujilizaga kwanini biashara ngumu na wanafirisika jimu wamelipata imagine mtu anafanya kazi kwenye duka lakini anawapa mademu Kila kitu wanachotaka Sasa ukichanganya na hao wenzake wawili huo msingi utapona?
 
Tatizo wewe ni young Sana na huna hatia na hujui vingi kuhusu mapenzi.You are innocent.Ila hiyo ni kawaida Kwa wanawake ukionesha interest anakimbia.Shukuru umetoka na experience Fulani.Huo ndyo mwanzoo makubwa yanakusubiri.

Usiendekezee wanawake ambao huna malengo kuwaoa Zinaa ukianza kuacha ni ngumu.Tunza bikra Yako ya uanaume mapenzi yapo utafanya Hadi utachoka na kukimbia.
 
Huyu ananikumbusha binamu yangu mtoto wa shangazi nilimuweka kuuza dukani nilichoambulia ni Siri yangu kibaya zaidi alikuwa anahonga boyfriend zake.kuna siku alisema anaenda makambi ya kisabato nikapata taarifa amemghalamia mpenzi wake wameenda.sasa duka limeisha Mimi naendelea na kazi yangu yeye kazalishwa na kuachwa solemba.
vijana msikimbilie mapenzi mkipewa kazi fanyeni kwa uaminifu huku mkitarajia kuwa na biashara zenu.
 
Back
Top Bottom