Hivi hii harufu ya baadhi ya mitaa ya jijini Dar naisikia peke yangu tu?

Hivi hii harufu ya baadhi ya mitaa ya jijini Dar naisikia peke yangu tu?

Ni kweli kunanuka sana,
Mama Ntilie wanazalisha taka za maji machafu na mabaki ya vyakula kila kona ya jiji.
Hizi zote zinamwagwa njiani na kwenye mitaro isiyotiririsha maji kila siku.

Hii imepelekea harufu mbaya sana na hatari ya magonjwa ya mlipuko.

Hakika kuna Jambo la kufanya
 
Wakuu Kwema!

Aisee! Baada ya kutoka kuzurura huko Duniani, sitaki kupataja nisijeonekana najikosha hapa, na wenye nongwa zao na vijiba vya roho wasije nitolea mvuke wa ushubwada. Ila ifahamike tuu nimetoka huko Dunia ilipo.

Kwa kweli Dar inanuka vibaya mno. Inanuka vitu mfano wa mavi, sijasema ni mavi jamani Ila ni Kama hivyo.

Yaani Asilimia kubwa ya Maeneo yananuka chemba za maji taka. Nashindwa Kueleza hapa. Sitaki kugombana na wenye DAR Yao, sitaki kabisa. Maana najua wapo wanayoipenda, ikumbukwe siiongelei Jambo hili Kwa ni mbaya lakini naongea ili Jambo Fulani lifanyike.

Alafu ukiwaona wakazi wa Dar ni Kana kwamba hawaisikii hiyo harufu, pengine wamekuwa sehemu ya harufu yenyewe, sijasema watu wa DAR mnanuka chemba za maji taka 😃😃😃. Maana wenye hasira hamkosekani.

Hata hivyo akili yangu ikanambia sio rahisi watu WA DAR kuisikia hiyo harufu mbaya ya mavi Kwa maana maisha yao ni yataabu Sana. Taabu zimeua mishipa ya Nostril ndani ya pua. Hawezi kunususa tena.

Hasa watu masikini wapanda Daladala, hawa ndio wanaoonja joto ya jiwe,hata hivyo wenyewe ni Kama joto Hilo hawalisikii kwani taabu imewafubaza na kuwafanya waone kila kitu Kama kipo Sawa.

Kipindi nasoma pale Udsm wala sikuwa najua DAR inanuka, nimekaa zaidi ya miaka mitano Kama sio sita sikuwa naona hizo harufu. Labda Maeneo ya Tandale huko na viunga vya makazi ya WALIA NA MUNGU watu fukara apeche Alolo.

Najiuliza niliwezaje kuishi miaka mitano kipindi kile?

Nafikiri serikali ipitie tena miundombinu ya taka hasa mitaro ya maji taka ili mji usiwe jiji la harufu mbaya.

Wananchi wa Dar nanyi mjitahidi kuwa wasafi hata Kama mmezoea harufu yenu mbaya kumbukeni wageni Kama Sisi tunaotoka Duniani tunakujaga pia kuwasalimu.

Muwe na Haya hata kidogo.

Taikon nitakuwa DAR Kwa wiki tatu mfululizo kabla sijaenda kudhuru Zanzibar nikielekea kuchumbia Visiwa vya Comoro.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Nenda Dodoma ndio utashangaa,yaani mitaro ya maji machafu inatoa balaa halafu kama vile kila kitu kipo sawa,hakuna Mamlaka inayojishughulisha kuondoa hali hiyo,hayo ni baadhi ya maeneo machache tu huenda asilimia kubwa ya mikoa mingine nayo ipo hivyo hivyo pia,nchi yetu kwa kweli bado sana
 
Ni kweli haujaongopa. Dar inanuka hasa mchana muda wa jua kali. Usiku ni kawaida sana kukuta vifurushi vya "nnya" na chupa za mikojo zimetupwa pembezoni mwa mitaro.
 
Wakuu Kwema!

Aisee! Baada ya kutoka kuzurura huko Duniani, sitaki kupataja nisijeonekana najikosha hapa, na wenye nongwa zao na vijiba vya roho wasije nitolea mvuke wa ushubwada. Ila ifahamike tuu nimetoka huko Dunia ilipo.

Kwa kweli Dar inanuka vibaya mno. Inanuka vitu mfano wa mavi, sijasema ni mavi jamani Ila ni Kama hivyo.

Yaani Asilimia kubwa ya Maeneo yananuka chemba za maji taka. Nashindwa Kueleza hapa. Sitaki kugombana na wenye DAR Yao, sitaki kabisa. Maana najua wapo wanayoipenda, ikumbukwe siiongelei Jambo hili Kwa ni mbaya lakini naongea ili Jambo Fulani lifanyike.

Alafu ukiwaona wakazi wa Dar ni Kana kwamba hawaisikii hiyo harufu, pengine wamekuwa sehemu ya harufu yenyewe, sijasema watu wa DAR mnanuka chemba za maji taka 😃😃😃. Maana wenye hasira hamkosekani.

Hata hivyo akili yangu ikanambia sio rahisi watu WA DAR kuisikia hiyo harufu mbaya ya mavi Kwa maana maisha yao ni yataabu Sana. Taabu zimeua mishipa ya Nostril ndani ya pua. Hawezi kunususa tena.

Hasa watu masikini wapanda Daladala, hawa ndio wanaoonja joto ya jiwe,hata hivyo wenyewe ni Kama joto Hilo hawalisikii kwani taabu imewafubaza na kuwafanya waone kila kitu Kama kipo Sawa.

Kipindi nasoma pale Udsm wala sikuwa najua DAR inanuka, nimekaa zaidi ya miaka mitano Kama sio sita sikuwa naona hizo harufu. Labda Maeneo ya Tandale huko na viunga vya makazi ya WALIA NA MUNGU watu fukara apeche Alolo.

Najiuliza niliwezaje kuishi miaka mitano kipindi kile?

Nafikiri serikali ipitie tena miundombinu ya taka hasa mitaro ya maji taka ili mji usiwe jiji la harufu mbaya.

Wananchi wa Dar nanyi mjitahidi kuwa wasafi hata Kama mmezoea harufu yenu mbaya kumbukeni wageni Kama Sisi tunaotoka Duniani tunakujaga pia kuwasalimu.

Muwe na Haya hata kidogo.

Taikon nitakuwa DAR Kwa wiki tatu mfululizo kabla sijaenda kudhuru Zanzibar nikielekea kuchumbia Visiwa vya Comoro.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kuna siku Dar iliwahi kuacha kunuka? Ni moja ya Miji ya hovyo kuishi.

Mkiambiwa dhibitini ujenzi holela na kuzaana hovyo hamtaki,komaeni
 
Wivu tu unakusumbua, au umetumwa na mabeberu, Macdm bwana!
 
zamani marehemu Ephraim Kibonde kwenye kipindi cha jahazi alikuwa ana utani wake anaita Dar "jiji kunuka"
 
Wahuni huku wanatembea na kiberiti kimejazwa nyaa(Kama ambavyo ulikua Zamani ukienda hosp. kupima choo unaenda umekiweka kwny kiberiti), kila akisikika handasi anakifunua ananusa full kudindisha,hii harufu ya nyaa itakuja kuwakera lini huko road?
Dah! Wahuni hamuwezekani, nakuona katika uborabwako.
 
Kiduku lilo alioongea sana humu kwamba watu wa Dar wamebanana sijui wanapumuaje watu walimcheka.

Ukikaa nje kwa mda siku unafika Dar utashangaa makelele,wenzetu ukienda sokoni pako na utulivu ,ukiingia zile malls na supermarket kubwa kubwa unakuta mziki tulivu watu wanafanya shopping. Siku ukiingia dar upo kama club inayopigwa miziki zaidi ya 100 tofauti ,hapa mwuza sumu ya mende spika inapiga kelele ,mbele mwuza CD anapiga mziki wake kwa nguvu ,hapa mwuza nyama anapasua mifupa ,kule mwuza sim card anatangaza ,pembeni gari ya promotion ya tigo inapiga mziki ,makonda wanapiga debe ,piki piki na bajazi zinapiga honi na mziki, mno visu naye anachanganya baiskeli. Mwinjilisti naye kashika bible na mic pembeni ya barabara anahubiri . Ili mradi vurugu mtindo mmoja.
 
Back
Top Bottom