Hivi hii Tabia ya wanawake (wake zetu) kuacha simu ovyo ni ya wanawake wote ama mimi tu?

Hivi hii Tabia ya wanawake (wake zetu) kuacha simu ovyo ni ya wanawake wote ama mimi tu?

Hata mimi nishalala mika hadi basi.Kuna siku wageni walisubiri wafatwe barabarani kama masaa3 halafu wazazi sasa niliona kama kafanya makusudi.Mi nimekuja kuona simu yangu maana nilikuwa kwenye kikao simu nikaacha ofisini mzee kanitafut kama 4 yeye anajua nikiwa kazini juna muda akipiga nakata simu ila nitamrudia.

Hivyo ilibidi nipigie boda awapeleke japo ni mwendo wa kutembea kwa miguu kama dk saba tu
Ila mimi kama kuna taarifa ya wageni au maelekezo ya baba najitahidi nisipitwe na call yoyote.Ila kama hakuna maagizo yoyote hunipati ng'oo
 
dah hilo jambo linauma sana mkuu, mimi nimeshachoka mda tu sina la kufanya. Halafu wenyewe wanahisi ni normal situation kabisa hawahisi kama pana tatizo.
 
Muwekee bando la kutosha, pia mchatishe Mara kadhaa kwa siku.
Mkuu huko tumeshatoka kitambo sana ukiweka MB akiwa hana kazi atakaa na kuhakikisha hadi ziishe kabisa ndo anapata akili ya kufanya mambo mengine.Nadhani wewe na kwetu ni tofauti kwanza bando hawezi kukoswa maana ile pesa unayompa ya mahitaji ya familia ata balance hadi ibakie ya bando
 
Ni kweli ila mshukuru Mungu angalau changamoto yako ni hiyo. Kuna changamoto zinazovumilika na at least zina plan B (unaona kwamba unaweza kupiga simu kwa jirani na ukampata).

Wenzio wenye wake zao ambao kila siku wanatuletea visa vya kutuacha midomo wazi humu na kutoa points za kutosha kwa TEAM KATAA NDOA kwa % kubwa simu huwa zinahusika, hasa simu janja.

Sasa kama wa kwako hakuona uspesho wowote wa simu janja hadi ukamnyang'anya na kumpa kiswaswadu lakini nacho bado ni yaleyale ni jambo la wewe kumshukuru Mungu na kuvumilia changamoto zake. Siku akizoea simu atakuomba umpatie simu janja, na hapo itakuwa ni warning sign kuwa kabla hata hujakufa mambo yameanza kuharibika.

Zingatia pia bandiko lako limekuwa lalamiko pekee la ndoa hivi kwa kipindi kirefu humu ambalo halijatoa points kwa kataa ndoa😁
Simu janja nilimpa baada ya kuona hakuna badiliko maana kuna vitu kwa sasa lazima muwasiliane via whatsap hasa kwa picha ama video.Kwa sasa smart haina mbadala.
 
Mi nauza 120,000 tu
Kumbe tangaza.sasa saa yenyewe anavaa anapoenda kanisani au ana safiri. Nadhani kuna kitu ambacho ninyi mnakiona ni sawa tu lakini mngelikuwa mnafunua mioyo yetu kwa ndani tunavyo kereka mnapotoa sababu hizo mgeacha mara moja!

Kwani unapo pika au kufua huwezi kuiweka mezani au sehemu yoyote iliyo karibu nawe ili ukipigiwa usikie? Inakuaje simu inakuwa mbali kiasi cha kupigiwa hadi mara4 husikii?
 
Mhh sio wote yuko huyo shemeji yangu hujamaliza kuandika kisha jibu naona unaandika vipi tena yaani huyo mtumie hata msg saa 9 usiku anakujibu mpaka unashangaa hana kazi na mume wake yupo wapi. kwa ufupi anashida hakuna habari ikampita mpaka namuonea huruma sijui ndoa kama ataiweza. Nadhani bora ya huyo unayemuongelea.
Hili lina vumilika kwakweli na wengi tumesha kubalaiana nalo maana kila ujanja umegonga mwamba na sababu ni zilezile miaka miaka.
 
Nadhani asilimia 98 ya wanawake wapo hvo..mimi wakwangu hata pesa ukimpatia utakuta anaweka hovyo mara dirishani mara nje uwani kwenye mawe mara sebuleni kwenye masufuria..hii tabia vip wanawake wengine wanayo?Simu ndo usiseme anaweza weka juu ya paa akasahau,, nimeamua kuwa mpole tu.
Ulivyosema ni sahihi mkuu hata mimi kwenye hela ni hivyohivyo. Hela mara nyingi huwa nazikuta kwenye sofa na yeye anaendelea na shughuli zake na hana habari nilisema sana nikagonja labda atakuja kupoteza nipate sababu ya kumnyima lakini hajawahi mara nyingine unaingia uwani unakuta hela kwenye dirisha.


setensi yako ya mwisho "Nimeamua kuwa mpole tu " ndo jawabu mkuu hakuna namna hata mimi nilishanyanyua mikono juu nikiwa nashida nikipiga mara2 hapokei basi naangalia option nyingine ya kumpata.
 
Wengi wapo hivyo, unatakiwa umpe training na mafunzo maalumu ya kutumia simu. Usitegemee atakuwa nayo mkononi saa zote ila mzoeshe kuwa kuna muda fulani lazima utapiga na yeye ategemee simu yako hata kama hautapiga basi yeye akupigie hata kukusalimia.

Nilipata hii shida ila baada ya kutoa mafunzo maalumu na kumkazia kwasasa mimi nisipopiga nikiwa kimya huwa naulizwa why nipo kimya siku nzima why sijamtafuta au leo nipo busy na jambo gani.

Mjengee utamaduni labda ikifika kila kuanzia saa tatu hadi saa tano asubuhi lazima upige,then mida ya lunch kuanzia saa saba hadi saa tisa utapiga tena, then utampigia kabla haujatoka kwenye mishughuliko kuja home. Akizoea atakuwa anategemea simu zako then utaona anakuwa karibu na simu muda mwingi.
Senior njia hii bora nitaanza ifanyia kazi. Sema kazi zetu mara nyingine simu unaacha unaingia .........hadi jioni saa12 hujashika simu napo nichangamoto pia. but nitajihidi sana kuitumia hii njia Ahsante sana
 
Mwanamke asiepokea simu kwa wakati ni mwepesi sana ku deal nae.

Asubuhi ukiwa unatoka, tafuta sababu yoyote ile usimuachie hela ya matumizi, mwambie hata kuna mtu atakupigia simu akuletee, au unaeza kumwambia nitakupigia baadae nikuelekeze sehemu ukachukue.

Ikifika mida mpigie, piga mara moja tu, asipopokea usipige tena, sasa yeye ukifika muda wa uhitaji wake ataanza kukupigia, akipiga usipokee.

Kama anajuana na watu wengine ofisini kwako atawapigia, akipiga mjibu easy tu kama anavyokujibu yeye, nilisahau simu kwenye draw ofisini.

Kama hana contact za ofisini kwako, mkaushie mpaka kama saa kumi jioni hivi.

Hapa kama hujaacha hela ya kula utakua umemnyoosha vizuri, usihofu kuhusu watu wengine kwenye familia kushinda njaa, kwenye kuitaka heshima nyumbani kwako lazima waumie wanaohusika na wasiohusika.

Saa kumi flani ndio unampigia, unamwambia simu uliisahau kwenye kabati la ofisini.

Ukimchezea michezo hii mara tatu mara nne fulani, ataanza kukaa karibu na simu, maana ukimuahidi chochote, mida ikifika ni simu moja tu, asipopokea wewe ni mikausho.

Kuna time itafika, hata ukibeep kidogo mwenyewe anapiga fastaaaa.

Jifunze kutumia power uliyokua nayo kurahisisha mambo madogo kama hayo
Watu mna mbinu sana asee. Hii imekaa kibabe lakini ni ya kumnyoosha kabisa.Shukrani
 
Tuko wengi.Mwenyewe alishaongea Hadi basi.Kuna muda hata kama nipo nyumbani anaamua Tu kupiga kwenye kasimu Ka nyumbani kwa sababu muda wote yenyewe inakua sebleni.Yangu kuna muda naikuta kwenye vyombo jikoni."Utaskia dada em nipib"
 
Ulivyosema ni sahihi mkuu hata mimi kwenye hela ni hivyohivyo. Hela mara nyingi huwa nazikuta kwenye sofa na yeye anaendelea na shughuli zake na hana habari nilisema sana nikagonja labda atakuja kupoteza nipate sababu ya kumnyima lakini hajawahi mara nyingine unaingia uwani unakuta hela kwenye dirisha.


setensi yako ya mwisho "Nimeamua kuwa mpole tu " ndo jawabu mkuu hakuna namna hata mimi nilishanyanyua mikono juu nikiwa nashida nikipiga mara2 hapokei basi naangalia option nyingine ya kumpata.
duu hawa viumbe kumbe tabia zinafanana sipati presha tena.
 
Nadhani wanawake wengi tuko hivyo,mi kwakweli nikiwa nyumbani nakuwa bize sana kiasi kwamba habari za simu nakuwa sina.Mmewangu alianza kulalamika ila badae naona alizoea tu japo kuna mda najitahidi kupokea au kama niko bize bize namjulisha kwa sms.
Majukumu ya kulea yanapoteza sana mda
Tunajua sana majukumu yenu lakini hii haiwapi uhalali wa kutokupokea simu zetu kwa wakati jamani.Huwa tuna kasirika mno moyoni unatamani umeze mtu.
 
Back
Top Bottom