Hivi hii ya mtoto wa kwanza kuwa makamu wa wazazi ni Tanzania pekee au kote?

Kina
Ndio kawaida huku, mara nyingine tunaonekana tunaringa kumbe watu tunaona majukumu yaliyopo yanatosha
Kinachouma hao ndugu wa pembezoni wakijipata hata kupitia wewe wanahangaikaga na familia zao sio wewe tena .
Ni bora usaidie nduguzo wa kuzaliwa nao hata wakikutupa haiumi sana maana unajua ulihangaikia damu yako hivyo mungu ni mwema watakukumbuka siku
 
Kwani lazima kwenda kwenye hivo vikao vya familia?
 
Haka ni kautaratibu ka watanzania tu bila shaka😂
 
Kwani lazima kwenda kwenye hivo vikao vya familia?
Hapana. Unaweza pia usiende. Mfumo wa maisha ni maamuzi binafsi. Ni wewe tu kupima, familia yako ina watu wa aina gani? Nisipojihusisha nao napoteza nini? Nina mbadala wa uwepo wao?
 
Ujue mtoto wa kwanza wazazi wanakuwa wageni wa suala la kuwa na watoto kwahiyo wanamjengea matarajio lukuki ya kutaka aje kuwa hivi au vile.

Vilevile wazazi wanakuwa bado wamoto wamoto, ni kama askari waliotoka tu deppo wakienda kutuliza ghasia sehemu usikae hapo kimbia mbio zako zooote vinginevyo wanakuua kama sio kukupa ulemavu
 
Na kama kuna mdogo wako mwenye kibunda cha kutosha hiyo nafasi ya "Makamu Mzazi" anaichukua kibabe. Ifike sehemu sisi wazazi wapya tuwalee watoto wetu kwa namna ya kuja kujisaidia wao na sio kutusaidia sisi. Hii kuzaa mtoto ili aje kuwa kitega uchumi baadae sio sawa. Wazazi wengi pia wanafanya kosa la ubaguzi kwa watoto wao kwasababu ya hali zao za kiuchumi.
 
Na tabia nyingine inayokera umeshakua mkubwa una maisha yako ila mzazi wako anakushikiria kutaka kukupangia kila kitu hasa wazee waliozaliwa kabla ya utawala wa Hayati Mwinyi.
 
Ili ufanikiwe kwenye maisha jitoe ufaham tu. Potea miaka miwili hiv uone
 
B
Na tabia nyingine inayokera umeshakua mkubwa una maisha yako ila mzazi wako anakushikiria kutaka kukupangia kila kitu hasa wazee waliozaliwa kabla ya utawala wa Hayati Mwinyi.
Bro mbona mzee wa hivyo ni mbabu sana atakushauri nini huyo maana hata smart phone sidhani kama anaijua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…