Ukiacha kufanya majukumu ya mtoto wa kwanza kuna atakaye ichukua nafasi yako. Utagundua hilo wakati wa vikao vya familia.
Yule anayebeba majukumu ndiye anayesikilizwa, ndiye anayeheshimiwa, ndiye mwenye sauti pengine kuliko ya baba sema heshima hufata mkondo wake, ndiye anayeamua wawe na familia ya aina gani. Ndiye anayeamua identity na heshima ya familia kwenye jamii inayomzunguka.
Unaposikia familia ya Mengi au Familia ya Ongala, au Familia ya Kikwete, au Familia ya Osea, ile heshima ni matokeo ya kazi zilizofanywa na wazazi na uzao wao.