Hivi huyu rafiki yangu anaweza kuwa mtu wa aina gani?

Hivi huyu rafiki yangu anaweza kuwa mtu wa aina gani?

Huyu nini mimi kabisa kila kitu ulichokitaja kinanihusu kasoro hapo hapo kwenye draft,mimi ni mchezaji mzuri wa hilo dubwasha
Unaweza kunifunga mimi ???
 
Mkuu kazi zetu sisi ni kujenga sasa msimu wa mvua umekuwa siyo msimu rafiki sana kwa shughuli zetu hizi basi ni wakati huu ndyo nilipokuja kulijua hilii juu ya rafiki yangu huyu wakati huu muda mrefu tumekuwa tukitumia akiba zetu kuweza kuishi kama ni kazi basi huwa moja moja sanaa
Huyo ni introvert, watu ambao hawapendi kujichanganya na wengine. Wanapenda kuwa wenyewe kufanya mambo yao kivyao bila kushirikiana na watu.
Wanajichanganya mara chache na wakiona hawakielewi mnachokifanya wanasepa kujitenga.

Huko kusikiliza nyimbo moja kunatokea kwa watu wengi tu hata mimi pia. Kuna siku naamka na mood flan nyimbo ni hiyo hiyo lakini sio kwa siku nyingi kama mwana huyo.
 
Aloo na ndyo maana mimi jamiiforum napapenda sanaa , hebu ongezea maelezo kidogo. Inaonekana unaozoefu mkubwa na hawa watuu , hapa nimeanza kupata mwanga jee hii tabia haina madhara kweli kama mtu labda atakapokuja kuoa maana kwangu mimi naona kama siyo tabia ya kawaida hii
Hiyo tabia hata mimi naifahamu mkuu.
Faida zake ni nyingi kuliko hasara kwa sababu kufanya hivyo hujiepusha na mambo mengi na ushawishi mbalimbali.
Watu wa aina hiyo huwa hawapendi makelele kutoka kwa watu wengine kwani huwa inawapa interference.
Faida nyingine ya watu wa hivi huwa wanafocus sana future/long term plans na huwa zinakuja imagination za success kichwani mwao jinsi itakavyotokea in future so kujichanganya na watu huwa wanahisi itamdisturb kisha itamtoa nje ya reli ya mipango yake.
Kutokana na hilo ili kupunguza athari ya upweke alionao ndio anatafuta kitu cha mbadala cha kumliwaza kama mziki ila aupendao ambao utagusa hisia zake na si kila mziki utamfaa,ukimbadilishia mziki usiogusa hisia zake pia atachukizwa na kuhisi makelele.

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Hii tabia wakati mwingine inachangiwa na malezi kwa kiasi kikubwa, kuna wazazi wasiopenda kabisa watoto wao wakacheze mbali na nyumbani, hawa muda mwingi wa makuzi yao wanakuwa kwenye mazingira ya nyumbani pekee.

Hivyo hawa hata wakikua, wakaanza kujitegemea, kwasababu walishazoea mazingira ya nyumbani, kutokwenda mbali, kuzungukwa na waliowazoea kila siku, inakuwa ngumu kwao kuja ku adopt ukubwani, japo baada ya muda wengine huanza kubadilika taratibu.

Wengi aina hii mara nyingi hata confidence huwa hawana, wanakuwa wenye aibu, wasioweza hata kukaa mbele ya wengine, mara nyingi hupenda palipo na wengi, wao wawe nyuma tena ikibidi hata uwepo wao usitambulike, pia huwa na maneno machache waliotawaliwa na tabasamu la muda mfupi wakiongea vichache vyao.
Uko sahihi mkuu

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Wakati mwingine ni vizuri kujipumzisha ndani kuliko kutoka kisha ukajikuta una tenda dhambi kwa kutazama hivyo vya Nje.

Imagine kumtazama Mwanamke kwa kumtamani umeshazini naye, kumbuka hapo Mjini Wadada wasivyopenda kuvaa nguo za ndani si utajikuta umezini na Dsm yote😜

Ndiyo maana jamaa ana epuka dhambi ndogo nndogo kwa kushinda ndani tu
 
Me naweza kukaa ndani kutwa nzima kila siku
Alafu muziki una hisia sana kama akili yako imetulia na kuusikiliza muziki vizuri utaenjoy sana unaweza kusikiliza tu beat na usizingatie yale maneno au kusikiliza tu maneno ukaachana na beat au pia ukawa unasikiliza feature mbalimbali zilizotengeneza hiyo beat na jinsi zilivyo unganishwa na kuwa beat kamili

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Sasa je hii hali ni kawaida ??.
Hali ya kawaida sana, Sikia huu wimbo, utaachaje kurudia kuusikiliza! ( japo kinachoimbwa hakieleweki)
"Todzungaira" is a traditional Zimbabwean song that has been performed by various artists. One such performance is by Hope Masike, featuring Abel Mafuleni, filmed Live Outside in Cahuita, Costa Rica. The song was performed to celebrate International Women’s Day ¹. Another performance of the song is by the marimba group Chapwititi from Kutsinhira Cultural Arts Center
 
Kweli watu na ulimwengu wenu
 
Aloo na ndyo maana mimi jamiiforum napapenda sanaa , hebu ongezea maelezo kidogo. Inaonekana unaozoefu mkubwa na hawa watuu , hapa nimeanza kupata mwanga jee hii tabia haina madhara kweli kama mtu labda atakapokuja kuoa maana kwangu mimi naona kama siyo tabia ya kawaida hii
Huyo naye ana watu wanaopenda watu wa hivyo, kwa hiyo kwenye kuoa, anaweza kupatana na mtu anayependa watu wa hivyo.

Hapo ni kama ataamua kuoa, maana anaweza kukataa kuoa, na hiyo ni haki yake pia.
 
Mi nadhani ni kawaida tu mfano mimi toka nimetoka kazini ijumaa nimetoka jana kuangalia mechi ya Manchester basi nimerudi hapa toka niamke sijagusa hata mlango, nimekunywa chai, napika, naangalia movie nalala.

Yani kifupi leo nje sigusi kabisa. Huwa kama sina ishu yoyote sitoki hata mlango sifungui[emoji2].
Labda tuna shida ila naonaga nakua na amani kuliko kutoka huna cha kufanya mkaishia kugombana au kurushiana maneno huko mtaani sipendi. So huwa nadownload movie zangu au series weekend namalizia ndani kama Manchester au simba haichezi sahau kuniona nje.
 
Wakati mwingine ni vizuri kujipumzisha ndani kuliko kutoka kisha ukajikuta una tenda dhambi kwa kutazama hivyo vya Nje.

Imagine kumtazama Mwanamke kwa kumtamani umeshazini naye, kumbuka hapo Mjini Wadada wasivyopenda kuvaa nguo za ndani si utajikuta umezini na Dsm yote😜

Ndiyo maana jamaa ana epuka dhambi ndogo nndogo kwa kushinda ndani tu
Katika mambo ya imani upo sahihi , ila kumbuka huyu ni mwanaume maisha ya kukaa kaka ndani awaachie wanawake , lakn pia katika mambo ya imani huko huko hakuna jambo (jaribu ) ambalo mwanadamu anakutana nalo likawa nje ya uwezo wake hivyo basi elewa hata hivi vishawishi vyote ulivyovisema au q
uvionavyo vipo ndani ya uwezo wetu katika kuvikwepa .
 
Uzoefu alionao katika jamii ndio chanzo Cha baadhi ya watu kubadilika na kuwa watu wasiopenda kujichanganya mfano,Unaweza Kuta watu wanaomzunguka hawathamini mawazo yake Hali kama hii inaweza kumbadilisha mtu akawa siyo mtu wa kuchanganyikana na watu.
 
Mi nadhani ni kawaida tu mfano mimi toka nimetoka kazini ijumaa nimetoka jana kuangalia mechi ya Manchester basi nimerudi hapa toka niamke sijagusa hata mlango, nimekunywa chai, napika, naangalia movie nalala.

Yani kifupi leo nje sigusi kabisa. Huwa kama sina ishu yoyote sitoki hata mlango sifungui[emoji2].
Labda tuna shida ila naonaga nakua na amani kuliko kutoka huna cha kufanya mkaishia kugombana au kurushiana maneno huko mtaani sipendi. So huwa nadownload movie zangu au series weekend namalizia ndani kama Manchester au simba haichezi sahau kuniona nje.
Sawa Lakini hebu niambie ungekuwa jobless kama huyu jamaa yangu niliyekusimulia hapo juu je kuishi namna hii uishio wewe ingefaa kweli ??
 
Back
Top Bottom