Hivi inakuwaje mtu unaendesha gari namba 'A' au 'B'

Ume
A,B na C ukisafiri umbali mrefu highway Ni nadra Sana kuzikuta zimepakiwa pembezoni mwa barabara zimefunguliwa boneti,kuashiria changamoto.Hayo unayoyasifia kibao kila baada ya km kadhaa tunaziona boneti juu hali tete.
 
Waambieni TRA kodi inatakiwa iwe fixed around 10% of the CIF Value. Hio iwe kwa gari zote halafu uone nani ataendesha hata namba D tu.
Huu ushamba wa plate no niliupata wakati natakankununua gari ya pili...kila nikipita barabara I naangalia plate no...baada ya ushamba kunitoka nimenunua no dgp show room GARI ya 1993...na Kuna namba a mtaani au b ya mwaka 1996 na imesimama ...hoja ya magari chakavu siipingi Ila sio plate no...ukiongelea plate no wajuvi wanamuona una walakini
 

Kuna rafiki yangu Mzee Said Roka ...Iringa ...... Peugeot 404 na bado nzima ...ni Taxi namba 14 ubavuni...safari popote,,,,
Gari ni matunzo tu.
 
Wenye uwezo wa vintage wana customize engine kuwa ya kisasa kwa muundo wa zamani na hiyo wanafanya huko USA na Dubai plus UAE wenye uchumi mkubwa maana gharama ya ku customize vintage ni sawa au zaidi ya kuinunua super car...acha magari mabovu mkuu
Tanzania hii hii watu wanatengeneza Magari. Ulifuatilia Landrover festival ya makonda kunachuma za 1950 ilikiwepo pale.
 
Brother Tanzania tunaendesha magari machakavu kweli ila jamaa katumia lugha ya kutukejeri ila ndio ukweli Wazambia na Wamalawi wanaopitisha gari Tanzania wana gari nzuri kuliko sisi huo ndio ukweli pia 2010 ni chakavu tu sio latest kama ulivyosema na pia hauwezi kununua gari yenye 10km kwenye dashboard ukapewa namba B hicho kitu hakipo maana namba zinatoka kwa series labda ukwepe kodi..eti mtu anunue gari mpya atumie namba A akipenda unajua mchakato wa kuingiza gari Tanzania au umeamua kuongea tu mkuu wangu usitumie matusi kwenye mambo ya msingi tukubali tunatumia magari machakavu ila sio kwa kupenda tumelazimishwa na mfumo.
 
99% ya magari yaliyo barabarani yana miaka 10 na zaidi.
Mimi ni aaa napiga route za dar -arusha kama sina akili nzuri.
Upo sahihi magari huku sokoni yapo bei ndogo sema mfumo ndio unatufanya tubaki na hizo Aaa harafu jamaa anatucheka gari ina kodi ya 79m wakati kwenye manunuzi ni nusu yake ya bei utaachaje kutumia Triple A Moshi zipo Stout kama mpya..
 
Kwa polution iliyoko hapo kipawa mtakufa sana tu hata uendeshe gari Z.
Tena we bonge la wakuja hizo namba zinaweza kupangwa na dalali tu kupunguza kodi.
Angalieni mburula hili, linahesabu herufi halijui kuna magari yanatupwa huko kwa wenzetu na likifika litaandikwa E unayotaka we lofa.
 
Ukitaka ujue Watanzania tunaburuza matakataka nenda Lusaka hapo Ford ranger,GD 6,Rover za kumwaga maana wao kodi ni kwa Gvm sio sisi tunakomoana saana..
 
Kuna magari yenye hizo namba ni mazuri na magumu kuliko hayo yenye C, D na E jambo muhimu ni servicing the car at the right time
 
Kama hashiki bomba kwenye daladala wala kupigana vikumbo kwenye mwendo kasi wacha atambe nayo namba A yake au B.
 
Sawa tutaacha kutumia namba a na b lakini baba yako kule namabengo namba a bado kwake ni anasa.........yuko na baiskeli yake namba x phonex na anakata mitaa
 
Number T.....AAA, T....BBB, T.....CCC Zipo Tele Kilimanjaro
 
We nae chizi tu.

Nmesema endapo mwaka 2010 mtu alinunua hilux zero km kutoka toyota akapewa namba B au C (series ilikua hapo), na huuhuu mwaka 2025 mtu mwingine akaja kununua hilux ya 2009 used from japan akapewa E sabab series imefikia hapo. Je gari ya nani ni chakavu zaidi? Tatizo mnatumia matako kufikiri, na vijambio kuongea
 
Walimu mkikopa gari mnasumbua sana!!! Ongezeko la gari namba E ni kutokana na walimu wengi kupata mikopo ya magari.
 
Usikariri! Nina gari B ambalo lilitengenezwa mwaka 2008 nikalinunua 2009 lina km 3,000 tu. Mpaka sasa lina km 51,000! Unasemaje kuhusu hilo na lilikuwa na grantee ya kutokuwa na rust kwa miaka 12 na Mpaka sasa hakuna chembe ya kutu. Niiwache
Likewise haya magari ya IST yanayopendwa unajua yalitengenezwa mwaka gani? Ni 2003-06 na unakuta ni namba E na kilometre zaidi ya 120,000 lipi bora.

Umuhimu wa gari ni mwaka gari lilopotengenezwa na matumizi yake. Si namba plate.
 
Daah mbona unatukana sana mkuu yaani unanitukana kwa sababu ya huu uchafu wa magari au una matatizo yako binafsi..
 
Wewe mbona akili zako ni za zamani kuliko namba A mbona huzibadilishi ziendane na namba E
 
For as long as aslimia 98 ya gari za TZ zinakuwa imported used basi kuwa na hakika hata wewe wa namba E bado unaendesha namba A tu.

Halafu usipende kukariri kuwa ubora wa gari ni registration number.

Kuna Corolla AE100 ya muhindi ni namba A aliiagiza 0 mileage, hiyo gari ukitoa plate number ukaweka E hakuna atakaehoji. Huyo mzee anakaa mtaa Mindu Upanga na duka lake lipo Mt. Mazengo, miaka yote anaitumia kwenda dukani na kurudi kwake tu. Inafanyiwa full service, well maintained. Gari ni kama imetoka leo Japan.

Sasa na wewe unaekaa kwa mabonde ya Bonyokwa kanunue AE100 yako leo iweke namba E, kipindi hicho ishapigizwa Japan huko halafu uje ulinganishe na ya muhindi iliyotunzwa vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…