Hivi inakuwaje mtu unaendesha gari namba 'A' au 'B'

Inawezakana wewe ni mgeni sana kwa Habari xs magari ,mimi nimesha miliki magari kadhaa ngoja nikupe kidogo
Uchakavu wa Gari haupimwi kwa plate number kama number A,B,nk
Uchakuvu wa gari upsnde wa injini unapimwa kwa km ilizotembea
Uchakuvu wa vipuri vingine zinapimwa kwa life span yake
Ubora wa gari unazigatiwa maeneo 3
1- injini
2- body
3- vipuli kama shokapu ,na vingine vidogo vidogo
Baada ya kufanya utafiti mgari ya zamani na mpya nilichogudua tofauti ni technology iliyopo ndani ya gari
Kama kubana matumizi ya mafuta
Umeme kutumika zaidi katika ku control vitu mbalimbali kama kufungua milango ,buti nk
Upade wa body gari nyingi mpya ni soft body
Body zake ni mbovu zaidi ukilinganisha na gari za zamani
Ikiwa mtu kazi zake za shamba ni vizuri atumie gari za zanani
Kila kifaa kwenye gari kinaweza kufanyiwa matengenezo na kuwa bora kuliko jana

Inawezekana wewe gari yako ni ya kulia bata kaxini na mjini unaweza kwenda kigoma na gari yako number E isirudi salama body lote likawa tepetepe bampa zote zimepotea
Magari leo watu ufananisha na wanawake anaweza kuwa 20 age lakini amemshinda bibi yake ya km alizotembeza kitumbua
Tofauti na bibi yake ni body lake bado linaonekane zuri ila injini mbovu
 
 
Usikariri Maisha kwamba A na B zote ni mvivu...kuna nyingine ni za awamu hii
 
Ikiwa mtu alinunua gari ikiwa mpya 0km mwaka 2010 kwaiyo unataka kusema imechoka
Alafu ukitaka kkuangalia plate namba utapigwa kama ngoma kuna gari zinazotoka Zanzibar plate number E ila haitamaniki sembuse plate na A na B
 
Sawa tutaacha kutumia namba a na b lakini baba yako kule namabengo namba a bado kwake ni anasa.........yuko na baiskeli yake namba x phonex na anakata mitaa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Utunzaji tu wa kitu kuna watu wana gari namba E na zimechoka balaa. Hivi G wagon namba A unaanzaje kuikacha
 
Old is gold.
 
LEO NIMEIONA LAND LOVER 110 INA NAMBA E.
HIZI GARI ZINANUNULIWA KWA IDARA ZINAZOTUMIA NO ZAO, MFANO UMENUNUA GARI TOKA SHILIKA LA UMA UTSPEWA NO E KWA SASA.
 
Ubovu wa gari siyo Plate number mkuu acha kukariri
Sasa kama mtu alinunua zero Km gari miaka 2015 huko brand new na number labda A au B na aliyechukuwa mtumba jana number E ipi wewe unadhani ni gari mpya?
 
Gari za Tanzania zote 90% mitumba gari chache mpya unanunua KM 0 kuna harufu mfani very unique kama harufu hiyo hujawahi kusikia basi gari yako mtumba tu. Ile smell ni balaa
 

Ujinga mzigo.

Kwani manunuzi fasheni au mahitaji?

Au wewe ni dotto magari dalali uchwara?
 
Kama mashine inapwita vzr mwendo mdundo unakanyagia kimasihara
 
Wewe unaendesha no F? Mbona binafsi umechakaa ila hujauzwa skrepa?
 
Isanga family, huyu jamaa mleta uzi kazingua sana. Karusha jiwe porini limepiga mzinga wa nyuki, na wengi tumekimbia😂😂😂😂😂

Jamaa anayo hoja. 95% ya magari ya Tz ni mitumba pro max. Inaniuma lakini ukweli ni kwamba gari ya 10-15+ years emission yake ni kubwa sana. Ndo unaambiwa zile stories zetu pendwa kwamba gari za Europe zinazingua..hazina spare parts. You buy 15+ plus vehicle unataka isiwe na shida….

Ndo maana bongo gari ya 2015 au hata chini ya hapo tunaambiwa ni new model.

Mleta uzi umezingua sana. Unatusema wengi humu.

If you know, you know.
 
Wabongo wengi washamba, gari sio namba unakuta gari namb E ila body ni box engine hovyo kabsa tena gari za zamani nyingi body chuma na engine mashine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…