Jamani katika kitu kinachoniuzi ni kumuona mwanaume kavaa li bukta la kuchezea mpira ndani ya suruali yaani nakereka kuliko maelezo embu fikiria unakutana na mkaka kavaa kapendeza yaani yuko smart kuliko maelezo alafu kavaa libukta la mpira hivi wenzangu mnajisikiaje?
Kwanini mtu usivae boxer yako nzuri ya cotton uvae ndo utoke zako? Kuliko kuvaa hiyo mibukta inawafanya mtune utasema mmebeba mafurushi, hebu acheni hiyo tabiaaa bwana, huo ni uchafu, usmart wa mwanaume upo kwenye boxer na sio kuvaa mabukta kama mnaenda mpirani.
Alafu hamna kitu kizuri na kinachopendeza kama kumkuta bwana ako kavaaa boxer yaani unakuwa hata comfortable kumvuaa nguo sasa ukikuta mtu kavaa mipensi stimu zote zinakata.
Tatizo vijana mliozaliwa juzi ushuani hamuwezi kujua haya mambo,
Haya maneno unayafahamu,kupuna,ma play,sago,mkole,mnanda?
Kama huyafahamu Tanzania(Dar es salaam),umekuja baada ya Y2K(2000).
Hizo bukta ni silaha Incase ukikamatwa na njagu(,polisi)na kuwekwa ndani.
Vijana wanao hustle na deals zenye utata ilibidi wajihami.
Kipindi hicho vitendo vya sodomization vilikuwa vingi sana mahabusu,sasa ukiingizwa ndani Tena ni chalii,unakuta mijitu imeshiba inataka ikufanye hasusa,
Sasa kwenye purukushani basi uwe na bukta ndani,itakusaidia ku delay balaa lisikupate.
Vile vile,kipindi hicho ukitoka shule unaenda kucheza Mpira,au kuangalia muvi manzese kwa mfuga mbwa,sasa huwezi kucheza na uniform ya shule,bi mkora atakutia stiki ukirudi mchafu.
Vijana wa kileo,mnaoshinda kwenye luninga na DStv remote,hamyajuhi haya.
Kupiga bukta ndani ni mazoea tangu ujanani wetu,