Hivi kuna mtu aliwahi kufanya ligi na Brevis AI 300 na akaishinda kweli? Mbona vigari vinakuwa uji sana mbele ya huyu mnyama?

Hii ni habari nyingine mkuu, hii uzao wa Subaru Impreza wrx sti na ni toleo la kisasa kuanzia 2014.Hii imetengenezwa special kwa mbio mwenzake ni Subaru VAB.

Hii inatakiwa ifanye ligi na Mitsubishi Evolution,Nissan Skyline GT-R na Toyota Supra.

Napendelea body ya imprezza wrx sti 2004 facelifted,2008 model kwenda juu hazivutii kabisa.
 
Nissan Navara, ni gari inayochanfanya haraka sana na inafika 180 km/ h kiulaini bila engine kulalamika.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nissan Navara, ni gari inayochanfanya haraka sana na inafika 180 km/ h kiulaini bila engine kulalamika.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Nissan Navarra ya Petrol au Diesel?
Maana kwa engine za diesel za TD25,YD25 na QD25 zina mbio kawaida.

Kwa Petrol ambazo ni V6 VQ40 na VQ38 ndio zina balaa Kwa upande wa pickup.
Hiyo pickup kumshinda sedan ni kazi.
 
Nissan Navara, ni gari inayochanfanya haraka sana na inafika 180 km/ h kiulaini bila engine kulalamika.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa Navarra ya kumzingua Brevis au Mark X labda ile Second Generation yenye engine yenye Supercharger VG33 na zipo chache Tanzania na tena dereva anayeikanyaga haswaa. Navarra itabebwa na engine ila body weight na aerodynamic itamtesa ndio maana nimesema impate dereva mtata.
 
Mkuu hatari sana burudani ya kibabe. Hao ni wasauzi wanafanya spinning za kutisha.

Kama ni mdau cheki na video za King of Spinning in South Africa anaitwa Magesh Ndaba huyu ana balaa mpaka makaburu wamemnyoshea mikono.

Pia kuna huyu dada ambaye ni Queen of Smoke kinara wa spinning kwa wanawake naye ni msouth anaitwa Stacey Lee May ana ichezea BMW series 3 Kama kazaliwa nayo.

Kwa michezo hii Magesh Ndaba ndio Lionel Messi. Ukipata muda wacheki YouTube uone burudani isiyochosha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…