Hivi kuna ndege imeshatua Chato tangu baada ya mazishi?

Hivi kuna ndege imeshatua Chato tangu baada ya mazishi?

Mkuu watalii watakao nje wanafanya booking zao kupitia makampuni makubwa ya Utalii mfano TripAdvisor. Hizi kampuni zipo kwenye mitandao ya kimataifa ya utalii inayomwezesha mtalii kupata package yenye vitu kama Hotel, usafiri wa ndege na ground transport. Sasa kama nyie hamna ndege wenzenu Kenya wanazo unadhani booking nyingi zitaenda wapi? Mbona hii haihitaji kichwa laini sana kuelewa. Utamtoaje Mtalii toka Zanzibar kwenda Kia mpaka Seronera? Basi la Esther?
Hayo ya Dreamliner na Chato sijayaandika mimi.
Wakati hatuna hizo ndege kama zilivyo sasa yaani wakati ule shirika letu la ndege linasuasua, tuliwahi kufanya utafiti tukagundua kwamba watalii wamepungua ni kwasababu shirika letu la ndege halifanyi vizuri!? Yaani shirika kama shirika kusuasua kwake kulikuwa ni chanzo cha utalii pia kusuasua!?
 
Kwa abiria wangapi kila trip??
Wapo wengi maana mkoa wa Geita, Kigoma, Kagera na maeneo ya Shinyanga jirani na Geita kama vile Kahama wanategemea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Chato
 
Chatoo!!😂😁
Yule Mwenetu Anaitwa Nani Vile........
 
"Hivi hapa wapi vile? Angekuwepo Siti karibu hapa angenitajia!" ananong'onezwa na kukumbushwa panaitwa Chato - anaitikia kwa nguvu "CHATOOO!"

Eti jamani hivi kuna ndege ambayo ishatua Uwanja wa Kimataifa wa Chato tangu baada ya msiba? Na kama ipo ilipeleka huduma gani?

Inasemakana pia hata wale twiga waliopelekwa kule Hifadhi ya Burigi na baadhi ya wanyama kama hao wengi wao wamekufa kutokana na kutoendena na ikolojia!
Tupia kapicha mkuu
 
Wakati hatuna hizo ndege kama zilivyo sasa yaani wakati ule shirika letu la ndege linasuasua,tuliwahi kufanya utafiti tukagundua kwamba watalii wamepungua ni kwasababu shirika letu la ndege halifanyi vizuri!?yaani shirika kama shirika kusuasua kwake kulikuwa ni chanzo cha utalii pia kusuasua!?
Inawezekana labda mimi ndio mwenye kichwa kigumu. Nashauri utumie vyanzo vingine vya taarifa vya mitandaoni kupata majibu ya maswali yako. Unaweza kutumia hata google tu .. Impact of aviation on tourism.
Maandiko na data vipo.
 
"Hivi hapa wapi vile? Angekuwepo Siti karibu hapa angenitajia!" ananong'onezwa na kukumbushwa panaitwa Chato - anaitikia kwa nguvu "CHATOOO!"

Eti jamani hivi kuna ndege ambayo ishatua Uwanja wa Kimataifa wa Chato tangu baada ya msiba? Na kama ipo ilipeleka huduma gani?

Inasemakana pia hata wale twiga waliopelekwa kule Hifadhi ya Burigi na baadhi ya wanyama kama hao wengi wao wamekufa kutokana na kutoendena na ikolojia!
Labda kama unamaanisha Ndege hawa wanaotaga mayai
 
Umeandika kama vile sijaelewa kabisa kama kuna hasara inapatikana, anyway tayaache hayo. Kweli hii ni mada pana sana na ndio maana hata ule mfano wako wa Fastjet haukuwa sahihi kwani ile ni airline ambayo ni LCC. Na pia inatoka nje ya nchi na ni rahisi kwao ku-target kaeneo/ route moja yenye faida bila kujali mengine.
Nisikuchoshe sana, msingi wa hoja yangu ni hivi, solution sio kutowekeza kwenye airline business na kuwanyima watu huduma hiyo kabisa, bali kuangalia maeneo ambayo ni vyanzo vya hasara ya biashara. Nilitaja machache, aina za ndege ziendane na operations husika/( mfano huwezi kupata hasara kwa kwenda Iringa kwa kutumia Bombardier Q 300) au kuangali suala la kuwa na Dreamliner kama haina route, gharama na maintenance kwa kuwekeza kuwa na wataalamu wa ndani na effective management kwa ujumla. Hivi vyote viwe kwenye mpango wa biashara.
Lengo iwe pia kutumia Airline kuwezesha sector nyingine za kiuchumi, i.e tourism. Fastjet hawawezi kuwa na malengo kama hayo.
Mwisho wa siku kila anayefanya biashara hii anajua ni biashara yenye faida ndogo ( small marginal profit).
Hatahivyo, mbona wenzetu wanawekeza kwenye hicho kilimo na wana ndege?!?
Hayo yanaweza kuwa achieved by phased approach Ila siyo Kama Marehemu alivyokuwa ananunua madege bila plan utadhani ananunua midoli ya kuchezea wanaye
 
Unasema kweli Fast Jet walikatisha safari ya Shinyanga abiria wakawa wanaenda wanapandia Mwanza wanaorudi Shinyanga wanaletwa na basi Lao maalumu toka Mwanza. Ndege inatua na kuchukua au kuleta watu wawili. Hiyo ni biashara au bangi?.
Asante mama kubwa kwa kunisaidia kwa mfano hai.

Sisi tunataka tuiendeshe ATCL Kama mwenge wa uhuru. INSANE
 
Iringa utawaonea aisee kuna mbuga kubwa sana ya Ruaha Ina wanyama wote ambao wapo kwenye group la big five. Ukiacha hiyo kuna mashamba ya chai makubwa ya Brookings na Msitu mkubwa wa kuzalisha mbao na karatasi ambao nadhani unasupply mbao kwa asilimia kubwa Tanzania. Ukiacha hayo pia kuna mashamba ya tumbaku makubwa sana hii ni uchumi wa kutosha sana kuweka airport yenye hadhi pia ni karibu na Dodoma mji mkuu.
Hizo activities kweli zipo Iringa je vipi ukiangalia na usafiri mbadala wa kwenda Iringa? Yaani Iringa ni kati ya mikoa inayofikika kirahisi kwa usafiri wa barabara kutoka Dar na Dodoma. Kiasi kwamba hata mabasi yanakuwa competitor wa ATCL.

At the end of the day unaangalia Je kuna abiria 24 wa kwenda Iringa ambao ni 40% ya uwezo wa Bombardier watakaokupa break even revenue??

Kinyume cha hapo ATCL itakuwa charity airline
 
Hayo yanaweza kuwa achieved by phased approach Ila siyo Kama Marehemu alivyokuwa ananunua madege bila plan utadhani ananunua midoli ya kuchezea wanaye
Hatua kwa hatua ingekuwa jambo jema zaidi.
 
Back
Top Bottom