Hivi kuna uhusiano gani kati ya 'gari' na 'mtoto wa kike?'

Hivi kuna uhusiano gani kati ya 'gari' na 'mtoto wa kike?'


Yani nashindwa kabisa kuelewa, ni kwanini watoto wengi wa kike wanashobokea sana magari? Yani hata ajue sio lako, ili mradi kakuona tu unaendesha basi ukimgusia tu anajaa!!! Wengine kwao yapo, tena mengi tu ya kifahari, lkn bado akimuona kidume "anatembelea ------" yaani anadrive lazima ashoboke! Duh..


Uhusiano kama wa mbwa na chatu.
 
Tized hahaha...nnavyojua mm kwenye equation kama hiyo lazima uwe na "unknown" moja tu, sasa nashangaa kwenye eqn yako kuna unknown zaidi ya tatu!!! nakokotoaje sasa hao...hahaha
 
Masela kuwashobokea madem wenye magari ni very rare, ila madem kwa masela wenye magari ni worse!!!
 
Binti.com hahaha umenichekesha sana! Lara 1 u are genious!
 
Kifupi wanaume pia huchukulia kama gari ni kifaa cha kutongozea, ndo maana mimi nilipopata hela nikaona bora ninunue langu sipendi ile idea ya mtu kuona nimempendea gari lake bora na mi niendeshe ili mtu anipe heshma yangu. Spendi dharau kisa kidume kina gari
 
Wanawake kiasili wanavutiwa na watu wenye hadhi ya aina flani mbele ya jamii. Kitu gani kinapima hadhi ya mtu inategemea na wakati na mazingira. Zamani mtu mwenye mashamba mengi na chakula cha kutosha ndio ilikuwa kipimo cha hadhi ya mtu. Ukiwa huna hivi vitu utakosa au utapata wanawake wa ajabu ajabu wasiotakwa na wenye uwezo.

Na mazingira yana matter, kwa waliosoma shule mtakuwa mnakumbuka wanamichezo mahiri mashuleni walivyokuwa wanang'ang'aniwa na mabinti. Kwenye mazingira ya shule, ukiwa good on the field inakupa hadhi flani ambayo wengine hawana.

The same applies to modern life and cars. Kwa kiasi gari limekuwa kipimo cha hadhi ya mtu kwenye maisha yetu. Ukishakuwa na gari, jamii inakupandisha status yako, na wanawake wengi watakupenda tu.

Kwa wanaopenda STK, hao sijui huwa wanafikiria nini!?
 
Back
Top Bottom