Hivi kuna uhusiano wa kwenda Ulaya na kufeli maisha?

Hivi kuna uhusiano wa kwenda Ulaya na kufeli maisha?

Duuu! Sasa tutafanyaje mbona Mie nipo Ulaya Saizi. Ila connection na wadau kibao bongo, wameniaidi Kuwa siku nikirudi tu,watanipa Dili ya maama.
Masuala kama connections kwa shughuli za maana zenye kuleta tija kwa jamii na taifa hayana shida.

Dili likiwa kwenye mstari mmoja na connections kama nilivyosema hapo juu pia hakuna shida ila ikiingiza masuala kama dili za akina Seth basi hayo ni maisha ya kubahatisha.
 
3.Utamaduni wetu sio wa huko--vise versa is also true----kwenda nje ukasomea degree ya mambo ya fashion sijui interior design sijui upholstery---ulaya ni kazi zenye hela---unaenda UK kusomea kushona masofa---kazi ambayo bongo haihitaji degree---ni nyundo yako na kigodoro baas..

usinichekeshe,kuna mmoja alirudi bongo na bsc in motorsport engineering.

nilipomuuliza degree yake inahusu nini, akaniambia ni uhandisi wa magari ya michezo kama yale yanayotumika kwenye formula one.

sasa issue ikawa kwenye kutafuta kazi, alisota sana.

ashukuru Mungu familia yake kidogo ilikuwa inajiweza, wakampa mtaji afungue gereji. kwa sasa ana miliki gereji yake na car wash maeneo ya kirumba, mwanza.
 
KABISA KABISA WENYE MALENGO NA NIDHAMU WANA TUSUA SEMA KWA JASHO SANA SANA SIYO LELEMA , UJANJA , WIZI NA RUSHWA KAMA BONGO,
ILA KATIKA KUMI NI WAWILI TU!!!!!!!!!!!!!!!
Katika 10 wawili...kunahitajika nguvu za ziada
 
usinichekeshe,kuna mmoja alirudi bongo n bsc in motorsport engineering.

nilipomuuliza degree yake inahusu nini, akaniambia ni uhandisi wa magari ya michezo kama yale yanayotumika kwenye formula one.

sasa issue ikawa kwenye kutafuta kazi, alisota sana.

ashukuru Mungu familia yake kidogo ilikuwa inajiweza, wakampa mtaji afungue gereji. kwa sasa ana miliki gereji yake na car wash maeneo ya kirumba, mwanza.
Vijana wa Kitanzania na Afrika kwa ujumla waanze kula samaki khasa yule Goldfish.

Huyu samaki ana madini muhimu sana kuimarisha ufanisi wa ubongo wa binadamu.
 
Mimi Niko bongo hapahapa ila Mwanaume ambae anatafuta maisha kiasi Cha kuizunguka dunia hawezi kuitwa amefeli hata kama bado hajapata/hajafanikiwa huyo anaitwa mpambanaji, ndo maana askari anaefia vitani bado anazikwa kwa heshima hata kama hakushinda vita ila ujasiri wake wa kusimama katkat ya njia za risasi unatosha kupewa heshima.

Bali mwanamke asie na mapenzi ya dhati ambae anaingia kwenye mahusiano na mtu asiempenda ila anautoa mwili wake kingono kwa mategemeo na nia ya kupata hafadhali ya kimaisha kupitia mgongo wa mwanaume mtafutaji mwanamke huyo ndo amefeli maisha, maana utatumika sana na wanaume wanaoigiza maisha Hadi utachakaa
Aisee tuko tofauti Sana,Kama Mambo yenyewe ndio hivyo nimekubali kweli Sina mapenzi ya dhati, siwezi kaa na mwanaume asiye na malengo Wala mwelekeo kisa penzi la dhati Hapana, NO!..Mimi binafsi naumiza kichwa mchana na usiku nalala masaa machache ili nitoboe maisha eti nikae nampenda mtoto wa mtu asiyeshughulisha kichwa chake...Hapana dada...Imani yangu yenyewe ya kiroho inamtaka mwanaume atafute kwa jasho mimi ni nani sasa nikae namvumilia mwanaume asiyetafuta.....we endelea na wapambanaji wanaozunguka duniani na kurudi na cheni na laptop ukiwaita mashujaa.
 
Yupo jamaa yetu mmoja aliishi UK miaka 10 bila kurudi home.
Siku amerudi kwao Choo cha nyumba ya uswahilini.
Haingii bila kupuliza air freshener kopo zima.
,na haogi maji ya bomba anasema mavumbi.
Ananunuwa chupa kubwa la litres 15.

Kibunda cha noti kilipokwisha mbwembwe zote ziliyeyuka.[emoji3][emoji3][emoji3].
Watu wa Ng",ambo,,vituko vitupu.
 
usinichekeshe,kuna mmoja alirudi bongo na bsc in motorsport engineering.

nilipomuuliza degree yake inahusu nini, akaniambia ni uhandisi wa magari ya michezo kama yale yanayotumika kwenye formula one.

sasa issue ikawa kwenye kutafuta kazi, alisota sana.

ashukuru Mungu familia yake kidogo ilikuwa inajiweza, wakampa mtaji afungue gereji. kwa sasa ana miliki gereji yake na car wash maeneo ya kirumba, mwanza.
🤣🤣🤣🤣Ila Bora hata alirudi na ujuzi
 
Yupo jamaa yetu mmoja aliishi UK miaka 10 bila kurudi home.
Siku amerudi kwao Choo cha nyumba ya uswahilini.
Haingii bila kupuliza air freshener kopo zima.
,na haogi maji ya bomba anasema mavumbi.
Ananunuwa chupa kubwa la litres 15.

Kibunda cha noti kilipokwisha mbwembwe zote ziliyeyuka.[emoji3][emoji3][emoji3].
Watu wa Ng",ambo,,vituko vitupu.
Unaona Mambo yao ya ajabu hayo!kilichomfanya asijenge akiwa huko nje Ni nini?wakiambiwa ukweli Ni wakali kwelikweli
 
Mtu yoyote ambae amekwenda Marekani, UK au kwingine madhali ni ughaibuni na akasoma uzuri na kupata kazi za maana hukuhuko, hawezi kuwa na maisha ambayo umeyaeleza ya hao jamaa watatu.

Pili, kama ulikwenda huko kati ya 1995-2010 basi wewe utakuwa umetulia kimaisha yaani una nyumba hukohuko na una nyumba Tanzania lakini huiishi bali waipangisha na nyumba nyingine ndo wazazi wanaishi.

Tatu yaunga mkono namba 2 kwamba pia kama wazazi walikupeleka kule na wakahakikisha warejea bongo na wapata kazi nzuri, nyumba na baadae waanza familia, basi weye Ughaibuni ni kwa vekesheni tu.

Nne, yote niloeleza hapo juu yanataka plan, msaada wa wa wazazi kama walikuwa wajiweza uzuri ma kisawasawa.

Kwa mfano wapo vijana ambao wengi wapo nafasi za juu sasa hivi serikalini na nawafahamu wengine walikwenda huko na wakasoma uzuri na kisha wakarudi na sasa wapo wadunda.

Sasa ukitoka familia maskini au ya kipato cha kati lakini ikajikamua kukutafutia angalau nauli uende kule, lakini wakasahau kuwa wewe kichwani una yako na ukifika kule waanza vurugu basi utaishia kama hao ulowataja.

Hivyo uhusiano wa kwenda Ulaya na kufeli maisha kunategemea zaidi na business plan, strategy yako na mwono.

Kama huna hivyo basi weye ni failure.
Hao ndo wenye nidhamu na kujielewa...wengi wao ulimbukeni tu
 
Nina washkaji zangu kama 11 hivi, Mmoja yuko JAPAN, Kyoto, Mmoja yuko UK, Brmingham, Mmoja yuko CANADA, Toronto, Mmoja yuko Denmark, Oslo, m1 yuko Namibia, Windhoek, Wa3 wako USA, Texas, California na Las Vegas Nevada, mwingine yuko zake South Africa, Cape town na mwingine anaishi TURKEY, Instanbul na wa Mwisho yuko Sehemu matata sana ARGENTINA, Iruya (Andes). Wote wana maisha mazuri tena sana wanasaidia sana ndugu zao. Ikumbukwe hawa wametokea maisha magumu tu, walikwenda huko kimasomo lkn wakabahatika kupata kazi.
Nilipata bahati ya kufika nchi 7 kati ya hizo, na niseme wazi anayeishi ARGENTINA yuko njema zaidi, yeye anafanya kazi kwenye hotel za hapo IRUYA, ana mke na watoto wa3 wazungu as You know Argentina haina wazawa weusi.

Wengi wanaotoka maisha safi kwenda nje kusoma wakirudi home wanakuwa tegemezi mifano iko mingi sana JUX ni mfano hai kabisa.

Wengi hawajitumi kwakuwa wanajua home kwao kuko njema.

Kuna jamaa tulikuwa nae Chuoni yeye Degree alichukulia Copenhagen Norway yaan hajielewi na sijui shida nini, na mwingine alitokaga kitambo ni kama bro kwangu alienda URUSI kusoma Udaktari ni mlevi sana, na ajabu anaijua dini (Muslim) ambapo aliwahi tuambia kuwa Russia kuna waislam wengi kuliko wakristo RC.

Kikubwa ni kujitambua tu. Mimi ni familia tu ila niliwahi kukaa Brazil miezi 6, nchi iko njema sana kazi nyingi nk sema changamoto ni kwamba mimi ni Muislam hivyo nililazimika kuhamia mji wa Rio de Janeiro ambako kidogo kuna misikiti angalua niweze kula chakula halali kwangu.

Vijana mupatapo fursa nje ya nchi ni muhimu sana kukumbuka shida za nyumbani na kujisevia kihela kidogo. Trick nzuri ni kutafuta demu wa kizungu afu unakuwa mwaminifu kwake maisha utayaona mtelezooooooo. Ref, MAD ICE yuko zake FINLAND, RAMA DEE Australia wanakula shushu kisa mbunye za kizungu.

Kuwa na maisha mabovu ni kujitakia.
Wewe ni global citizen...Hali yako kwa Sasa niaje lakini?
 
Kuna mwamba mmoja alitoka bongo 2000 hadi leo hajarudi haijulikani kama mzima au kafa

Mama na dada yake walishakufa kitambo sana yeye hata simu hapigi duuuh sijui kama mzima au alishakufa kitambo
Ukute Hana hata hela ya voucher🤔🤔🤔
 
The diaspora is not monolithic.

If you associate with people who failed economically, that is a reflection of your poor judjement, small network and its poor reach.

We are out here making big moves.

Na siku hizi hata likizo tunaishia Turks and Caicos, au tukijq Bongo ni kifqmilia zaidi, kwa sababu ya umbeya wa wabongo.

Kama kuna lawama, laumu watu wako specifically, usipakazie diaspora.
Kiranga mbona Kama umeamka na hasira?relax mkuu.hayo maneno ya umbeya wanatupa wenzenu wanaorudi na kutupiga virungu sisi na kutumia vizungu vigumuuu ili tuwaamini 🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom