Uchaguzi 2020 Hivi kwanini baadhi ya watu wanataka Aidah Khenan wa CHADEMA ajiuzulu Ubunge alioshinda?

Mkuu mimi sioni mkanganyiko wowote Mkuu. Huu uchaguzi ni BATILI na kuna ushahidi chungu nzima wa kuthibitisha hilo. Boniface hakutaka awe mshindi katika uchaguzi ambao ulijaa udhalimu wa kila aina mwanzo mwisho. Na huyo dada hana furaha pamoja na kuwa kashinda. Sijui atachukua maamuzi gani baada ya kushauriana na viongozi wa Chadema, ngoja tusubiri.
Bado mkangamyiko upo Mr BAK.
Jacob kasema anashukuru katangazwa ameshindwa, sasa hii hali inamueka huyu Mama matatani bure.
View attachment 1616107
Mama aende bungeni, pamoja na kwamba vyama vipo ila kila mtu ana maisha yake na anatafuta maisha.
 
Mkuu ule uliofanyika ulikua uchaguzi na mshindi lazima atangazwe. Sasa katangazwa Aidah kashinda dhidi ya Kess wa CCM, kumyima haki yake ya kufanya kazi kuwakilisha wananchi kupitia alichokua anapigania siyo sahihi.
Na wale walioteuliwa na NEC wakati wananchi hawakuwachagua unasemaje na hapo?. Wananchi wamenyimwa haki yao ya kuchagua.
 
Chadema hawana nia ya kutetea nchi bali ubishi na utovu wa nidhamu na kashfa kwa serikali.
Mbaya zaidi wanajiunga na jumuiya za kimataifa kuisema nchi.
Hawafai kabisa
 
Ina maana hata nafasi za Viti Maalumu CHADEMA hawatawarusu akina mama wale kwenda bungeni?

Tulizeni akili kwanza na mfikirie kwa mapana kwa maslahi ya Taifa. Mh. Aidah Khenan aachwe aende Bungeni akachape kazi na aungane na wenzie kutoka viti maalumu.
 
Uko sahihi ni vyema wamwache na yeye alambe posho kama wao walivyokula kwa miaka 10.
Na yy alikuwa mbunge wa vitu maalum chadema. Siyo mara yake ya kwanza kuwa mbunge
 
Keshasem anaweza asiende ili ccm wawe 101% kazi iendeleee
 
Ale pesa yake ya ubunge taratibu tu hana sababu ya kupiga chini.
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa chagueni kiongozi mpinga Ruswa na udini na msipofanya hivyo wananchi watamtafuta mtu kutoka nje ya CCM, hivyo mwaka 2015 wakafanya kweli wakamchagua mtu mpinga Rushwa Magufuli na hatimaye yake mmeona. Magufuli mwaka 2015 alipata kura asimilia 58 lakini mwaka huu nafikiri asilimia itakuwa kati ya 80 na 90. Ndio maana mtu akitaka kuwa mbuge anapigana juu chini apitishwe na CCM. Hivyo muacheni Aidah aende bungeni ili awakilishe wananchi wake.
 
Keshasem anaweza asiende ili ccm wawe 101% kazi iendeleee
Hizi hasira hazijengi. CCM wasiachwe peke yao kule ndani. Huu ususaji hautawazuia CCM kuendelea na Bunge lao

CHADEMA ipeleke hao viti maalumu angalau wakaobserve na kuchallenge vitu vya kipuuzi. Hata kama watashindwa, which is obvious, lakini raia watapata taarifa
 
Akikubali kwenda bungeni atakuwa kawasaliti Watanzania waliomuamini na kukubali kuhalalisha matokeo haramu yaliotendwa na watendaji...
 
Walioshinda kihalali ni wengi tu, ila mamlaka imeamua kuchafua. Na huyo waliye mtangaza wamefanya hivyo ili kuweka kumbukumbu ya kutetea uovu wao kwamba haki imefanyika. Kama aligombea kwa ajili ya maslahi yake binafsi ni sawa mwacheni aende mjengoni akabembee kwenye vile viti vyao ili mradi posho iingie atimize malengo yake. Lakini kama aligombea kwa maslahi mapana ya wananchi wenzake na taifa kwa ujumla basi ni bora awaachie hao waliojimilikisha hati miliki ya taifa ili.
 
La muhimu tusubir tamko la chama hapo kesho tuone itakuaje.

Lakini huyu dada haki yake ya msingi ya kua na ubunge mkononi ibaki palepale.
 
Hilo ndilo la kufanyia kazi na siyo figisu.
Ambaye hajapita basi harakati afanyie nje ya bunge, aliyepita aende bungeni.

Kwani ni wagombea wote wa chadema walishinda chaguzi za nyuma? Mbn hawakususa na figisu zilikuwepo?
 
ajiuzulu tu,halafu ajiunge kule kwa wale wengi kisha agombee kwa chama cha wengi,ulaji wake utakuwa palepale,haina maana kwenda mjengoni wakati wenzako wengi wamefanyiwa uhuni
Ya nini sasa afanye hivyo?

Hivi hizi ideas ni za nini?

Kashinda, aachwe aende bungen..shit!!!
 
Naam hiyo ni haki yake ya msingi lakini pia kama akiwa haoni umuhimu wa kwenda mjengoni pia hiyo ni haki yake, tusimlazimishe. Na kwa kauli yake hii ya leo sioni kama ana mpango wa kujiunga na maccm.
La muhimu tusubir tamko la chama hapo kesho tuone itakuaje.

Lakini huyu dada haki yake ya msingi ya kua na ubunge mkononi ibaki palepale.
 
Na utaratibu/kanuni inasemaje juu ya kumvua mtu uanachama bila kutumia hisia binafsi?
Wanasema tu amekiuka maazimio ya kamati kuu basi bunge linapelekewa minutes za kumvua huyo mtu uanachama.
Kisheria wanakua wamejustify kumvua uanachama mpka hapo
 
Ahsante..
Hlf wanainuka watu wanapinga asiende bungeni.

Tamko la chama likitoka na likiminya haki yake, itakua si halali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…