Hivi kwanini Hayati Magufuli aliamua tu kuwa katili bila sababu zozote?

Hivi kwanini Hayati Magufuli aliamua tu kuwa katili bila sababu zozote?

JPM yupi alikua mcha Mungu? Si ndio alikua anatembea nje ya ndoa kivipi Tena mcha Mungu? Si ndio huyo huyo alisema Maalim asipewe Hela za matibabu kisa kamnyima SheIn mkono!! Si ndio huyo huyo alitaka kumuua Lissu?? Mcha Mungu avuruge uchaguzi 2020?

Aiseee acheni kukufuru, sio Kila anayemtaja Mungu jukwaani ni mcha Mungu wengine ni unafiki tu kuonekana wema. Hivi si Majaliwa alidanganya msikitini kabisa yaani mtu anaongea uongo ndani ya msikiti alafu Bado mnadhani hao viongozi Wana hofu ya Mungu kweli?
Huyo baba yako ZITTO ndio mcha Mungu mchawi mkubwa huyo.alafu inaelekewa wewe ni hawala wa zitto
 
Na kama Chadema hatataka kushindwa bsi aende against Magufuli au amtukane uone
Kwahiyo watu watampigia kura Samia kisa Chadema wamemtukana JPM? Kwani kati ya Chadema na CCM ya Samia nani anaongozwa kwa kumchafua JPM?

Ni hivi 2025 Both CCM na Chadema ni anit JPM so labda useme watu wa JPM wasuse kupiga kura ila yeyote watakayempigia kati ya Samia au Chadema ni anti JPM so hakuna impact whether wapige au wasipige kura unless kungekua na chama Cha 3 ambacho mgombea ni Team JPM hapo kidogo mngekua labda mna kahoja.

2020 Lissu "kamtukana" sana JPM ila NEC wanadai alipata almost kura million 2 hivi ndio sembuse sahivi ambapo Samia hakubaliki so zitapanda tu whether or without "kumtukana" JPM.
 
Uchaguzi wa 2020 Magufuli aliuharibu vip.
Ivi ukikaa mwenyewe umetulia na akilizako zote ulidhani nani angeshinda uleuchaguzi 2020?.

Kwanini unasema 2020 uchaguzi uliharibiwa, vipi kuhusu 2015 uchaguzi ulikuwa halali??.
Uchaguzi wa 2020 kwenye kata yetu na Jimbo letu hatukupiga kura sababu wagombea wa CCM walipiga bila kupingwa yaani tulinyimwa haki ya kuchagua!! Sasa hayo mambo hayakuwepo huko zamani walau wangeiba ila sio kutufutia hadi uchaguzi kabisa.

Kingine serikali za mitaa hatukupiga kura pia maana mitaa na vitongoji wajumbe walipita bila kupingwa so uchaguzi ulipita juu juu hakuna Cha kampeni Wala kusikia sera za wagombea au kuchagua kiongozi. Sasa kwa style hiyo utasema uchaguzi haujaharibiwa??

Hata Kenya walisema Odinga lazima angeshinda ila matokeo yalikuwaje? Au Kuna aliyetegemea Biden amuangushe Trump? So Kuna vitu haviamuliwi kwa hisia ila kura zingeachwa kama zilivyo ungekua shocked mkuu. So acha assumptions otherwise kungekua hakuna haja ya kupiga kura maana tukituliza akili tu mshindi anajulikana!!
 
Huyo baba yako ZITTO ndio mcha Mungu mchawi mkubwa huyo.alafu inaelekewa wewe ni hawala wa zitto
Pole sana Sukuma Gang jamaa yenu ndio hivo Tena ameshaoza kaburini mnapoteza muda tu. Hakuna mcha Mungu atatuma watu wamuue binadamu mwenzie, hiko tu kinatosha kumpeleka kuzimu unless alitubu kwa wahusika na kwa Mungu wake Sasa sijui aliwezaje hayo ilihali Ali paralyse!!

Mwisho wa ubaya ni mauti
 
Hojazenu ni nyepesi na zakijinga sana.
Si uzijibu Sasa? JPM mwenyewe alishindwa kujibu hoja akatumia bunduki ndio sembuse wewe darasa la saba?? Hata ukiulizwa kwani JPM alituondoa kwenye Open Governance Initiative iliyotaka uwazi serikalini huna jibu? Hivi unajua sheria ya TEITI ilitaka mikataba ipelekwe bungeni kabla ya kusainiwa ila JPM alikataza Hilo ila watu Bado mnakomaa tu kumuita mzalendo.

Hii nchi wajinga wengi na ndio mtaji wa CCM.
 
Rais wa hovyo. Alizidiwa na Kenyatta alitoa misaada. Eti sikuleta tetemeko. Bull shit.
RAIS HAWEZI KUWA WA OVYO HATA KIDOGO , KWA SABABU KILA RAISI AU AWAMU HUA INAKUJA NA MAZURI YAKE KWA AJILI YA MANUFAA YA NCHI ILA KINACHOTAKIWA NI CC KUWA WATULIVU NA KUMWAMBIA KWA LUGHA YA STAHA KUA ANACHOFANYA KWAAJILI YETU KUA NI KIZURI AU KIBAYA BILA KUMLAZIMISHA AU KUMPIGIA KELELE , SHIDA WATU HUA WANAJIANDAA KUPAMBANA NA VIONGOZI BADALA YAKUTOA USHAURI NA NAMNA YAKUTEKELEZA ,VILE VILE KWA SUALA LA USHAURI NI HIYARI YA KIONGOZI KUFUATA AU KUTOUFUATA
 
Kwahiyo watu watampigia kura Samia kisa Chadema wamemtukana JPM? Kwani kati ya Chadema na CCM ya Samia nani anaongozwa kwa kumchafua JPM?

Ni hivi 2025 Both CCM na Chadema ni anit JPM so labda useme watu wa JPM wasuse kupiga kura ila yeyote watakayempigia kati ya Samia au Chadema ni anti JPM so hakuna impact whether wapige au wasipige kura unless kungekua na chama Cha 3 ambacho mgombea ni Team JPM hapo kidogo mngekua labda mna kahoja.

2020 Lissu "kamtukana" sana JPM ila NEC wanadai alipata almost kura million 2 hivi ndio sembuse sahivi ambapo Samia hakubaliki so zitapanda tu whether or without "kumtukana" JPM

Una matatizo gani? Mbona kama umedata?
Wewe ndio una matatizo ebu kaa ujifanyie tathimini vizuri kama upo sawa
 
Mafuriko ya Mbeya Rais Samia ametoa msaada wote wa kibinadamu.

Serikali imeweka full attention kusaidia wahanga. Nimefarijika sana.

Sasa nikakumbuka lile tetemeko la Kagera.. Magufuli alivyo wakashifu wahanga na kutosaidia chochote.. akasema 'kwani mimi ndo nimeleta tetemeko, fanyeni kazi...' na blabla kibaoo.

Sasa natafakari hapa ni kwanini Magufuli aliamua tu kuwa katili na kuweka ubinadamu pembeni kabisa. Why?

View attachment 2478896
kuongoza vichwa vya watz inataka akili ya ziada na bila kuwa katili mambo hayaendi.watz vichwa vyao ni vigumu na pia ni wagumu kuelewa.bila ubabe hii nchi haiendi.
 
We ndio hujitambui eti kisa shangwe, Ile ni appreciation sababu ule mradi ulifanyika awamu yake Wala Haina maana ndio approval ratings. Kama ni hivyo mara ngapi huyo Samia anampinga vijembe JPM na hao wananchi wanashangilia.
Endelea kujifariji na kujipa matumaini yasiyojengwa kwenye ukweli
 
Aisee mbona unakufuru sana MUNGU
Sijui ni dini gani lakini ni dhambi kubwa sana kumuhukumu wewe sio mungu. Hadi utoe hukumu binadamu hatujakamilika kila mtu ana madhaifu yake na mimi na wewe ni marehemu watarajiwa tunaosubili hukumu yetu hatujui itakuwaje.
Kwa hili uko sahihi, lakini kuna binadamu wanakuwa waovu mpaka mtu unajikuta umehukumu.
 
Magufuli alikuwa mropokaji na ingekuwa uraisi wake unapimwa kwa kauli zake za majukwaani; watanzania mtaani hakuna ambae anamkumbuka leo.

Unaacha legacy kwa kugusa watu directly positively ndani ya muda, kuacha alama za kazi watu wakiona wanasema huyu alikuwa Magufuli na kuwa na huruma na watu wako.

Sasa wewe unaweza jiongopea unavyotaka ila uhalisia ni kwamba huku kitaa mwamba bado anaishi kwenye vichwa vya watu kwa mazuri yake.
Vichwani mwa watu kama wewe
 
Ukila nyama ya mtu huwezi kuacha, kabla hajawa Rais alikuwa ana furaha kubwa sana kubomoa majengo ya watu ili apitishe barabara, akiona watu wanalia machozi na kuzimia, roho yake inasuuzika
Jamaa was a real sadist.
 
Back
Top Bottom