Hivi kwanini Mabasi kutoka Dar kwenda Mpanda, Katavi yanazuiwa kuendelea na safari yakifika Sikonge, Tabora?

Hivi kwanini Mabasi kutoka Dar kwenda Mpanda, Katavi yanazuiwa kuendelea na safari yakifika Sikonge, Tabora?

Tunayo majeshi mengine mkuu, na nimeshaona JW TZ wakisaidia kwenye mambo mbalimbali nchini, sembuse hili la kuwadhibiti hawa vibaka kwenye mapori?
Umeshakaa Tabora vijini? Kuna wanajeshi hao wakimbizi unatakiwa ujipange kuwadhibiti sio wakuwaendea kindezi unadhani hao polisi hawana hizo habari ama jeshi unajua kama kuna kikosi hapo cha 25KJ.

Achana na maisha ya barabara za mapori makubwa ama usiombee sakata la kutekwa unaweza kushangaa mzee wako anapigwa mjengo mbele yako. Kulaza gari Sikonge siungi Mkono bora hata Tabora mjini.
 
Miaka 60 baada ya uhuru bado tunayaogopa mapori yetu wenyewe kweli? Kwa nini kusiwe na network hicho kipande wakati hiyo ni highway? Sina lengo la kukushambulia wewe personally but nataka hoja zangu ziwafikie wahusika kwa sababu hatuwezi kupiga maendeleo kwa staili hii.
Nadhani hata kipande cha Manyoni Tabora maeneo karibu na Kazikazi au Gang 48 kuna sehemu umetembea mtandao ukawa haupatikani kabisa
 
Shukuru sana kwa jambo hilo kuna mapori makubwa sana hiyo baranara nakumbuka tulitaka kutekwa na BUS la SABENA sijui kama lipo. Kuna wahuni sana wa Kirundi na Kinyarwanda hasa pori la Inyonga. Polisi hawa wazembe hawana uwezo wa kuwadhibiti hao wahuni na Wakorofi. Sehemu zote za maporini ukiona kuna Waarabu wanakaa hapo muda mrf tia akili. Tulia kupambazuke mbelembele ya Sikonge jiandae na Nzi pori Mbung'o.
Mkuu unazungumzia mambo ya zamani sana hayo!!sio kwa sasa,kwanza barabara ni lami tupu,ni hiyo sheria itakuwa imeanza hivi karibuni tu,mimi nimepita sana hilo poli la IPOLE na INYONGA,mala nyingi sana usiku mnene kwa basi.

hivi kweli serikali inashindwa nini kuweka barriers kila baada ya kilomita kadhaa humo?tena wakakaa jwtz.kuliko hii ya kulaza watu sikonge.



gjj
 
Kwanza kabisa mimi sio na sifanyi kazi LATRA.

Pili kwa experience yangu hayo mapori wanayoyasema ni kweli yapo lakini mbaya zaidi humo maporini hakuna network ya mtandao wowote inakamata na hakuna makazi so kwa usiku emergency ikitokea like gari imepata breakdown humo it's you on your own hakuna msaada mtapata labda itokee kuna gari nyingine ipite iwape msaada ila there is no way mtafanya mawasiliano hasa ya simu so possibly wanazuia kwa sababu hio maana pia kuna wanyama pori humo.
Ni kukurupuka tu mbona siku zote utaratibu huo haukuwepo?hata mwaka jana mwanzoni nimetoka dar asubuhi nimefika mpanda saa 11 alfajiri na MAJINJA BUS?!!
 
Umeshakaa Tabora vijini? Kuna wanajeshi hao wakimbizi unatakiwa ujipange kuwadhibiti sio wakuwaendea kindezi unadhani hao polisi hawana hizo habari ama jeshi unajua kama kuna kikosi hapo cha 25KJ.

Achana na maisha ya barabara za mapori makubwa ama usiombee sakata la kutekwa unaweza kushangaa mzee wako anapigwa mjengo mbele yako. Kulaza gari Sikonge siungi Mkono bora hata Tabora mjini.
Hoja yako ni nini hasa??
 
Kama ulikua na akili timamu 2000,hiyo njia hapo sikonge ndipo walupotekwa na kuimbishwa mtaji wa masikini,walivuliwa nguo na kuamuriwa kucheza
Unaleta habari za 2000 leo 2023 na barabara yote ni mkeka? Acheni kuishi kwa kukariri.
 
Ni kukurupuka tu mbona siku zote utaratibu huo haukuwepo?hata mwaka jana mwanzoni nimetoka dar asubuhi nimefika mpanda saa 11 alfajiri na MAJINJA BUS?!!
Nakubaliana na wewe huu utaratibu ni wa kukurupuka tuu na kusalimu amri kwa vibaka...Miaka ya 1980 Ma Bus njia za Dar to Mbeya, Dar to Arusha na kwingineko yalikuwa yanasafiri mpaka usiku, yaani saa 10 jioni unaenda Kisutu au pale Mnazi mmoja na alfajiri uko mkoani. Kumbuka kipindi hicho barabara zilikuwa mbaya sana na hakuna simu za mkononi kama sasa. Je tunaenda mbele au tunarudi nyuma kimaisha na kimaendeleo?
 
Unaleta habari za 2000 leo 2023 na barabara yote ni mkeka? Acheni kuishi kwa kukariri.
Polisi nao wanakariri!?..unajua gari zinavyotekwa!?..acha ujinga,wanaolinda usalama wanakuambia hatari,wewe unang'ang'ana,nenda kwa miguu Kama una harak
 
Kwamba 2023 mapori yameondoka? Kama bado yapo basi jua jamaa nao bado wapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hiyo vibaka sasa wanadictate maisha ya raia siyo? Kwa hiyo Mungu kutubariki haya mapori na misitu mikubwa ndo imekuwa kama nuksi kwetu au laana kwetu?? [emoji12] Mungu angetupa jangwa tungelalamika pia.
 
Badala ya kulalamika, ungekua mjanja, ungetumia hiyo fursa kula tunda kimasihara [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Daaah vijana mnawaza utelezi tuu aiseeee... Leta mawazo Chanya ya kuondokana na hili tatizo kijana..
 
Polisi nao wanakariri!?..unajua gari zinavyotekwa!?..acha ujinga,wanaolinda usalama wanakuambia hatari,wewe unang'ang'ana,nenda kwa miguu Kama una harak
Hapana siyo ujinga ila tatizo ni wewe una mawazo ya kizamani sanaa wakati dunia inaenda kasi sana. Narudia hatuwezi kuendelea kwa kupoteza 8 to 10 hours kwa kisingizio cha usalama wakati kama nchi tuna majeshi ya kutosha kiasi kwamba wakati mwingine huwa tunaenda Congo DRC na kwengineko kuwasaidia wenzetu.

Nitakupa mfano kuna mikoa ya ukanda wa magharibi (ziwa Tanganyika huko) ambako kuna changamoto ya uvamizi na uharibifu wa misitu ya hifadhi wamekuwa wanaungana Police, JW TZ, TANAPA nk kufanya doria kubwa kubwa ambapo wameweza kuwadhibiti wahalifu.
 
Daaah vijana mnawaza utelezi tuu aiseeee... Leta mawazo Chanya ya kuondokana na hili tatizo kijana..
Mawazo chanya tuliyoleta ndio yalifanya hiyo bara bara ikawekwa lami. Enzi izo nyie mlikuwa mnawaza utelezi tu...
 
Hapana siyo ujinga ila tatizo ni wewe una mawazo ya kizamani sanaa wakati dunia inaenda kasi sana. Narudia hatuwezi kuendelea kwa kupoteza 8 to 10 hours kwa kisingizio cha usalama wakati kama nchi tuna majeshi ya kutosha kiasi kwamba wakati mwingine huwa tunaenda Congo DRC na kwengineko kuwasaidia wenzetu. Nitakupa mfano kuna mikoa ya ukanda wa magharibi (ziwa Tanganyika huko) ambako kuna changamoto ya uvamizi na uharibifu wa misitu ya hifadhi wamekuwa wanaungana Police, JW TZ, TANAPA nk kufanya doria kubwa kubwa ambapo wameweza kuwadhibiti wahalifu.
Urefu wa Hilo pori kufuata hiyo barabara ni kilomita ngapi!?..panatakiwa vituo vingapi vya ulinzi vya kuweka Askari!?..au escorts wangapi kwa kila gari!?..unajua kwamba polisi Haina Askari wa kutosha!?..ipi cheap kati ya kuzuwia usafiri usiku na kujaza Askari kwenye Hilo pori!?
 
Back
Top Bottom