Hivi kwanini mwendokasi huduma zinakuwa mbovu na wao ni monopoly?

Hivi kwanini mwendokasi huduma zinakuwa mbovu na wao ni monopoly?

Usimamizi mmbovu,jamaa wazembe,hawajali abiria wao

Yaani hawa wanapishana na hela Sana kwenye mradi huo

Huu usafiri ni wa ajabu na mateso kwa abiria

Ova
 
Basi moja inabeba watu si chini ya 350 during rush hours. Nauli ndogo ni 750. Per trip ni 262,500 hio ya kuishia Kimara tu. Chukulia basi kumi zifanye mzunguko huo mara 6 kuanzia saa 10 jioni hadi saa 3 usiku.

Roughly 262,500x10x6=15,750,000 hio ni Gerezani - Kimara one way hujahesabia kurudi. Ukiweka nenda rudi manaake unazungumzia 25M.

Kivukoni-Kimara nako upate 15,750,000 one way. Ukiweka nenda rudi maanake unazungumzia 30M kwa traffic ya ferry.

Hapo sijagusa ya mbezi mwisho ambayo ni 400x350=140,000
Ukiweka mabasi 10 yaende 6 trip kila moja ni 140,000x10x6 =8,400,000 hio ni one way Kimara-Mbezi tu during rush hours. Ukiweka 2 way maana yake inaweza gonga 12M.

Sijazungumzia less profitable routes kama Moroco, Muhimbili na Mwenge. Tuchukulie zote combined two ways zilete 23M tu during rush hours.

Twende kwenye hesabu ya jumla sasa.
Kwa masaa 5 tu ya jioni kuanzia saa 10.

Kimara-Gerezani: 25M
Kivukoni-Kimara: 30M
Kimara-Mbezi: 12M
Muhimbili-Morroco-Mwenge: 23M
SUB Totals================90M

Routes asubuhi: 70M
Routes jioni: 90M
TOTAL================160M

EXPENSES
FUEL. 20M
MISC. 5M (25)

NET==================135M

Humo una justify vipi kwamba umeshindwa nunua basi? Hio ni hesabu ya siku tu. Fanya kwa mwezi mzima utagundua kuwa hizo basi zinaweza generate 4.05B ukitoa mishahara ya kulipa staff wote, maintanance na vipuri utagundua the company makes around 2.5 Billions each month on average.

Basi moja la kichina sidhani kama linazidi 300M na hununui kila siku. Kwanini wanashindwa kununua gari hawa jamaa? Hivi wabongo ni nini tunaweza kusimamia wenyewe kikaenda bila ngendembwe? Ni aibu tupu!
Mawazo fikirishi yaliyoambatanishwa na ushuhuda wa takwimu. Wahusika tunaomba ufafanuzi.
 
mkuu madeni mkuu wangu wale wanadaiwa mafao ya wafanyakazi wa UDA toka zile ecarius bado madeni mengne ya UDA, bado madeni ya nmb, madeni yote ya UDA yalihamia UDA-RT mana kampuni mama ya UDA ni kama imeishakufa, hlf kampuni ya UDA-RT ni PLC maana yake ni ya serikali asilimia 85 halfu asilimia 15 ndio simon group wataacha kweli mradi wampe mtu binafsi kwa asilimia zaidi ya 50 wapigwe. maana pale karibia asilimia 90 ya mapato yanaenda serikalini

1. kuna salio linaenda TRA ukiangalie ile tiket utaona geresho la TRA
2. kuna salio linaenda DART tozo ya huduma maana UDART ni kama wamepangishwa kutumia barabara za BRT
3. mapato yanayobaki ya UDA-RT baada ya garam 85% yanenda hazina

half boss pale kuna aina 3 za mabasi
1.articulated ikizidi sana mwisho watu 250
2.rigid ikizid sana 150
3.feeder 100

note: mapato ya mwendokasi yanagawiwa sehemu nyingi ninkama hakibaki kitu TRA wanachao, DART wanachao tozo ya huduma, madeni ya UDA,nmb na mengne unafikiri kitabaki nn?


note: usilolijua ni kama usiku wa giza
Kama hali iko hivyo basi hamna namna lazmq kampuni iyumbe. Sema hata wale wakatisha tiketi watakuwa wanajikadiria sio kwa kiburi kile wako nacho.Hakuna anayetegemea mshahara wa laki 3 pale.
 
Mimi napandaga mwendokasi kama hiyo ruti hakuna daladala za kawaida.

Wale wakatisha tiketi nao ni wezi, ilishanitokea kuna siku kuna mdada alikuwa mbele yangu akatoa buku 2, wenyewe wakasema katoa buku. Baada ya kung'aka wakamrudishia chenji yake.

Zamu yangu na mimi nikatoa buku 2, akanirudishia 350 badala ya 1,350.
Sikutaka maneno mengi nikamwomba mgambo afungue mlango nimfundishe adabu huyo kibaka. Mgambo akasema kwani kuna nini? Nikasema we nifungulie tu.
Abiria tulioongozana wakaanza kusema huyo mkatisha tiketi ni mwizi, alitaka kumwibia yule dada (wanamwonesha yule dada ambaye ashaingia ndani, na yeye akasikia na akaja kutoa ushahidi alivyonusurika kuibiwa) kashindwa ndio anataka kumwibia huyu kaka.
Yule mgambo akataka kunipa buku yake ili kumaliza utata. Nikasema tatizo sio buku bali wizi, watu walipojazana pale ikabidi mhudumu anipe tu chenji kamili kumaliza utata.
Wana wizi wa kishamba sana yani, mtu anajisahaulisha chenchi makusudi kenge kabisa.
 
Sijui nikipi hua kina fanyika kwa usahihi wake hapa uswahilini, sijui labda nifahamishwe
Hapa Umatumbini nadhani ukiachia mdundiko ni vigoma vya misutano tu vile vinafanywa kwa ustadi wa hali ya juu.
 
Basi moja inabeba watu si chini ya 350 during rush hours. Nauli ndogo ni 750. Per trip ni 262,500 hio ya kuishia Kimara tu. Chukulia basi kumi zifanye mzunguko huo mara 6 kuanzia saa 10 jioni hadi saa 3 usiku.

Roughly 262,500x10x6=15,750,000 hio ni Gerezani - Kimara one way hujahesabia kurudi. Ukiweka nenda rudi manaake unazungumzia 25M.

Kivukoni-Kimara nako upate 15,750,000 one way. Ukiweka nenda rudi maanake unazungumzia 30M kwa traffic ya ferry.

Hapo sijagusa ya mbezi mwisho ambayo ni 400x350=140,000
Ukiweka mabasi 10 yaende 6 trip kila moja ni 140,000x10x6 =8,400,000 hio ni one way Kimara-Mbezi tu during rush hours. Ukiweka 2 way maana yake inaweza gonga 12M.

Sijazungumzia less profitable routes kama Moroco, Muhimbili na Mwenge. Tuchukulie zote combined two ways zilete 23M tu during rush hours.

Twende kwenye hesabu ya jumla sasa.
Kwa masaa 5 tu ya jioni kuanzia saa 10.

Kimara-Gerezani: 25M
Kivukoni-Kimara: 30M
Kimara-Mbezi: 12M
Muhimbili-Morroco-Mwenge: 23M
SUB Totals================90M

Routes asubuhi: 70M
Routes jioni: 90M
TOTAL================160M

EXPENSES
FUEL. 20M
MISC. 5M (25)

NET==================135M

Humo una justify vipi kwamba umeshindwa nunua basi? Hio ni hesabu ya siku tu. Fanya kwa mwezi mzima utagundua kuwa hizo basi zinaweza generate 4.05B ukitoa mishahara ya kulipa staff wote, maintanance na vipuri utagundua the company makes around 2.5 Billions each month on average.

Basi moja la kichina sidhani kama linazidi 300M na hununui kila siku. Kwanini wanashindwa kununua gari hawa jamaa? Hivi wabongo ni nini tunaweza kusimamia wenyewe kikaenda bila ngendembwe? Ni aibu tupu!
Mkuu, umeweka gharama za uendeshaji kama mafuta, maintenance, na kodi ya kutumia barabara BRT ili warejeshe mkopo wa WB.

Hata hivyo UDART huduma zao ni mbovu kwa kweli, njia ya Mbagala waipe kampuni tofauti ili tulinganishe ubora wa huduma.

Vv
 
Mkuu, umeweka gharama za uendeshaji kama mafuta, maintenance, na kodi ya kutumia barabara BRT ili warejeshe mkopo wa WB.

Hata hivyo UDART huduma zao ni mbovu kwa kweli, njia ya Mbagala waipe kampuni tofauti ili tulinganishe ubora wa huduma.

Vv
Itakuwa njema sana, sikujua kuna hizo gharama wanalipa ila still ukifanya assesment out of 135M kama faida still hela nyingi itabakia.Hakuna mfanyabiashara wa kukutengenezea million 100 halafu yeye akubali kupata 1M kwa siku!
 
Usimamizi mmbovu,jamaa wazembe,hawajali abiria wao

Yaani hawa wanapishana na hela Sana kwenye mradi huo

Huu usafiri ni wa ajabu na mateso kwa abiria

Ova
mkuu kwa kukudokeza mradi wa BRT phase I bado upo unasimamiwa na world bank na kuna muwakilishi wake hapa anatuma report mradi unavyokwenda na wb ndio mwenye maamuzi makubwa ya kufanya mradi uendeshwe vp maana pesa zao bado hazijarudi, zikirudi mradi unakua wa kwenu maamuzi mtafany nyie
 
Huyu mwendeshaji wa huu mradi aliyepo sasa Simon Group yuko ubia na serikali

Wamefeli ijapokuwa wenyewe wanasema alikuwa katika majaribio ya mradi huo kwa awamu ya kwanza

Ila mwaka jana mwishoni walisema wamepata mwekezaji kutoka UAE ambaye alishinda zabuni ya kuendesha huu mradi na ataleta mabasi 180 ndani ya miezi 6. Ngoja tuone

Katika mradi huu nafikiri serikali wasiingie ubia (joint venture) kama walivyofanya na Simon Group, wamwache mwekezaji auendeshe vile anaweza
Simon group ni kada mwenzao ndio maana wakampa shavu ...nepotism at its best
 
Jana nilikuwa napeleka mzigo pale kimara baruti nikasema Acha nipande mwendokasi kwakuwa faida yenyewe ni ndogo nitakomaa na mzigo wangu kuliko kuchoma mafuta Hadi sehemu husika Ila Ile adhabu niliyokutana nayo ya kubeba mzigo wangu kichwani Hadi nafika nilikoma aisee.
Mkono mmoja upo kichwani na mwingine nimeshikilia SITI maana chini hakuna nafasi ya kuweka mzigo Kwa kifupi huu usafiri ni unadhalilisha UTU wa MTU
Mwendokasi si kwa ajili ya kubebea mizigo ni kwa ajili ya abiria pekee.
 
Hahahah nilipoona tu wame ditch mfumo wa kadi nikajua tu ilikuwa itafutwa mbinu ya upigaji😀😀😀 kupitia mradi ule kuna vijana watajenga kupitia kukatisha tiketi tu pale 🤣🤣🤣
Nchi yetu sote Nkuu, acha nao walambe nkono maana hata zikikusanywa kwenda central government, wanaishia kulipana posho na kununua mashangingi
 
changamoto naona ni viongozi kampuni ya udart ipo chini ya msajili wa hazina(tresury) halfu DART ip chini ya Tamsemi .
DART wakitafuta mwekezaji lazima wahusishe wizara ya fedha namna mwekezaji atakavyolipa, sasa kumbuka sasa ivi wanaokusanya mapato ni hazina, wizara ya fedha ikiona mwekezaji alietafutwa hawezi kuleta pesa za kutosha kulipa mkopo wa BRT pamoja na garama zingine wanapiga chini wanaendelea kukusanya wao yaan ni kama kuna conflict of interest .
ndio maana kila muda utaona matangazo ya zabuni ya mtoa huduma BRT laki mchakato unaishia kwenye bomba
Wawape warabu coz huwa hawapendi longolongo watawalipa deni lao lote kwa sharti wawape njia zote za dar kwa miaka 50 ijayo.
 
Back
Top Bottom