Hivi kwanini tunawabadilisha watoto wetu majina asilia baada ya ubatizo au kubadili dini?

Hivi kwanini tunawabadilisha watoto wetu majina asilia baada ya ubatizo au kubadili dini?

Wasalaam,
Hivi kwanini mtoto alizaliwa anaitwa Mkwavinyika lakini baada ya kufanyiwa ubatizo anaanza kuitwa Paulo.

Au mtu alizaliwa anaitwa Mushaija lakini baada ya kutaka kumuoa Maiumuna anasilimu na kuanza kuitwa Juma.

Sasa nataka kufahamu haya yote yanatokana na nini:
Je, majina yetu asilia yanakuwa na walakini au yanabeba nuksi fulani hivi kwa mtoto ?

Au, hayo majina hutumika kama utambulisho wa dini ya mtu fulani kama ilivyo kwa kabila ?
Tumeaminishwa kuwa majina ya kizungu/kiarabu ni bora zaidi kuliko majina yetu ya asili na pia tumeaminishwa kuwa kutumia majina haya mapya ni aina fulani ya ustaarabu au kuelimika.

Lakini pia tumedanganywa kuwa baadhi ya majina yetu ukimpa mwanao atarithi tabia za jina hilo kama liliwahi pengine kutumiwa na wazee wa zamani katika ukoo wenu, hivyo majina yetu tunaya-associate na urithi wa mizimu, hivyo ili kuepuka chain ya mizimu ya kiukoo ni bora eti utumie jina la kizungu/kiarabu. Hapa napo ndipo tumedanganywa na tukadanganyika kweli kweli.

Binafsi nilipokuwa mdogo nikiwa na miaka kama 14 hivi nilibatizwa nikachagua jina la kizungu. Nilikuja kutafakari kwa kina nikiwa na miaka 25 hivi nikaona hiki tulichoaminishwa ni ujinga kabisa. Maana tumedanganywa na tukaamini kuwa ni kweli eti majina ya kizungu/kiarabu ni bora zaidi na wengi huwa tunaamini kuwa ni lazima utumie jina la kizungu/kiarabu unapobatizwa/kusilimu.

Baada ya tafakari yangu ya kina niliamua kubatizwa upya ili nizaliwe upya kwa kutumia jina langu la asili na sio lile la awali nililojipa kipindi nabatizwa mara kwanza. (Nashukuru Mungu baba alipokuwa anaenda kutuandikisha shuleni alikuwa anatuandikisha majina ya asili na pia hata la kwake alikuwa anatumia la asili. Hivyo shuleni nimekuwa nikitambulika kwa majina ya asili ie first name na surname ni ya asili).

Siku ya ubatizo ya nilipoamua kubatizwa mara pili ili kufuta lile jina kizungu nitumie majina yangu ya asili, mbatizaji aliponiuliza jina langu nilimtajia majina matatu yote ya asili, nashukuru Mungu hakuwa na pingamizi juu ya majina hayo hivyo alinibatiza kwa majina yangu ya asili ie jina langu ni la asili, baba naye jina lake ni la asili (japokuwa yeye ana jina la ubatizo la kizungu), jina la babu pia ni asili. Hivyo hayo ndio majina yangu kila mahali kuanzia mtaani, kazini, na kanisani.

Na nimeazimia kuwa wanangu wote lazima watumie majina ya asili. Labda waje waamue kujipa wenyewe hayo ya kizungu/kiarabu wakiwa wakubwa.
 
Afrika Magharibi wana enzi sana majina yao ya asili. Unamkuta Adebayo Ankunle hata huwezi kujua ni dini gani lakini utajua ni Mwafrika.
Shukuru Mungu kam ukoo wako siyo wachawi!!! hasa wivu wa mashangazi!! au labda nyota yako haiwaki ktk ulimwengu wa Roho! majina ya kienyeji usipo badili hutakaa utoke kijijini kwenu mpaka kifo kikukute!!

Kijijini Mtoto wa flani akifaulu kimaisha km shule hivi!! chupi zinawabana hawali wala hawanywi!! fikiria tu unajenga kajumba ka bati wazee wako wanaogopa kulala au wanakukataza kabisa!! haya hapo kazini kwako unawindwa uwe mfanyakazi hewa!

Hata wale wana ukoo wa kusaidiwa sana kimaisha, wanakaa na kula kwenu wewe ukiwa mtoto wa boss mfadhili wao, watu wa hivi wabaya sana jichunge nao, hawapendi mtoto wa mtoa misaada awe juu kielimu!!! kifedha! na kutoka kimaisha, safari!

Waafrica wengi ndivo mlivyo mpaka Mama mtu afanye kazi ya ziada!! ya kuganga na kugangua! na utambuzi wa hali ya juu! ili watoto mtoboe!! tena mengine haya jifichi mfano ukifiwa, uki fail kimaisha wanapataga nafuu sana ya afya zao tena waziwazi!

yaani hao hao! waweza kukukebehi wazi wazi, mbele yako! bila hata chembe ya aibu, wala kificho! yaani wanumia km wanakatwa na kisu rohoni!! cha msingi ficha jina lako, lisijulikane huko mbele ya safari!! ili wakitupa kombora lisikufikie!!

Fikiria kimdada umekutana nacho tu mtaani! umepiga mashine mara moja imekubali!!! au unataka kukioa, mtu una Elimu na kazi yako safi ambayo richa ya kuitolea jasho!! pia huyu mdada haijui!!! then umenunua kigari, cha kutanulia jamani eti ana jitahidi kukuroga jamani mwee!,

Eti mimi muoaji nisifanikiwe kimaisha kabisaaa anazuia riziki! jamani!!! hakujui asili yako, wala humujui!! mmekutana tu ktk harakati za maisha hata kwao hujawahi fika kujitambulisha... mfano mzuri ni dada Jack wote mnamjua humu alivo taka niroga.

kosa hakujua mimi ni jichawi nilie roga hasa, mpaka nika hasi kikundi na bado hawakunifanya kitu!! kubadili badili jina kwa wakati hasa hutokana sababu za kiusalama katika ulimwengu wa giza na ni muhimu kwa wano jua km mimi.

Na wale wenye nyota zao zinazo waka, nguvu za giza zipo sana si kitoto! ukizubaa wewe ni fursa kwa wachawi, Nyota hilo lina chukuliwa kiulainiii! kwani Biblia kitabu cha Mungu mwenyewe si imetamka wazi, Yesu tu alifanyiziwa sembuse wewe!!!

Sky Eclat jaribu tu kubadili jina uone utakavo piga hatua kimasihara, kinyume na hapo utashangaa tu kwa nini hufanikiwi, sometimes usijue kilele cha mafanikio yako milele kabisaaa!!! na ukaona ndo maisha yako usivo fanikiwa ktk ulimwengu huu!

Kma mimi muongo tumia majina tofauti tofauti, siku na wakati tofauti! uone utakavo tusua!! then baada ya muda rudia jina lako la asili uone kimavi kitakavo kusonga! utauza magari yooote hayo!

Ndo maana unaona Mabasi yaendayo Moshi/Arusha yana badili majina mara kwa mara! na hawafilisiki hovyo wale! wanabadili mabiashara tu!! kuzuga wachawi! na hakuna kabila Tanzania au watu wanaojua kutambika km nyie wachaga/wapare!
haya wee! mie naenda...
 
Unajua sielewi mfano Ghana SA, wanatumia majina ya asili na wanaenda church na misikitini, sasa sisi sijui kwann hatuitani majina ya kiasili wenye vyeti vya ubatizo au, Uislam.

Tunaambiwa yanabeba maroho na mapepo wachafu! Inasikitisha mno!

Everyday is Saturday............................. 😎
siku hizi yametamalaki majina ya wachezaji bila aibu mtu mzima anajiita cortino,mbappe,beckham
 
Yesu mwenyewe pamoja na uwezo na jeuri yake yooote!! alienda ishi uhamishoni kwa jina tofauti msilolijua wengi, na mahali tusipo pajua!!! hakurudi kwao ng'ooo! mpaka mbaya wake aliye taka kumuua huyo Yesu yaani Herode de Great alipo kufa kabisa!

Sasa kama Yesu Mungu Mwana alificha identity yake!! wewe kibaka mweusi tii! mbongo mwenda wazimu, Maskini, nusu jini mchawi, mwenye husda, ambae hata sometimes Malaika hawakujui kwa nini uliweke jina lako peupe? weka ufe!

Upigwe mikosi mpaka utembee kinyume nyume! na huchomoki na Dini zenu fake hizo! kwani unadhani shetani ana huruma? hata ukiwa wake ni twende tu!! msiige wa-congo kichwa kichwa! wale wana vidhibiti mwendo vya kichawi si kitoto na hawaachi!!!

Ujue kuwa Mariam kwa siri Yamkini pia walibadili jina la Yesu wakati wa ku cross Border la nyumbani kwao!! wasije wakarudishwa kwa Mfalme Herode sababu ya kumkimbia! ni wazi wangekufa wote!!! tena vibaya kwa kitendo cha kumtorosha mtoto mlengwa kwa siri!!!

Hebu mleta mada fikiri tu kidogo wale askari wa Herode wangejua ka Yesu kanakotafutwa kaleee!! kanatoroshwa kwenda Misri ingekuwaje? Km askari wa jiwe tu wanatafuta sifa za kuiba kura dhidi ya Lisu! je hao wa Herode?

Hata ivo Mungu alikuwa na uweza wa kumuua Herode palepale! au kumpa gonjwa/ kigugumizi tu! asimuone mtoto wake pendwa! lkn alitaka toa fundisho kwetu sisi namna ya kuukabili uovu wa mwanadamu kirahisi bila jasho!!

Sasa mfano rahisi tu wewe weka Avatar yako wazi halafu itukane serikali km utachukua siku mbili tu humu! Si unaona Max Mello alivo pata msukosuko! kwa ajili yetu!!! hatasahau na ameshika adabu! Muheshimiwa Mello upo>>>..

Kama tungeweka avatar za ukweli humu yaani wenye midomo km sisi ni mmoja baada ya mwingine unawekwa sehemu salama hatutakuona tena na wengi mngekimbia, lkn bado tumo!! wengine km Kigogo wanatafutwa!!

Jina jipya unaficha identity yako dhidi ya ulimwengu wa Giza! wengine mmesemewa vibaya na vichawi vya kijijini kwenu! ukiitwa humu '' flani'' kuzimu kunaitika ''Bee'' wee tayari yako hayasongi!....

Ni wazi Malaika wa Mungu alisema in advance '' Mariamu ondokeni mwende Uhamishoni Misri !!! wala siyo mbali na Bongo ni hapo tu .....sawa




ngoja ninywe maji ntakuja!!
 
Wasalaam,
Hivi kwanini mtoto alizaliwa anaitwa Mkwavinyika lakini baada ya kufanyiwa ubatizo anaanza kuitwa Paulo.

Au mtu alizaliwa anaitwa Mushaija lakini baada ya kutaka kumuoa Maiumuna anasilimu na kuanza kuitwa Juma.

Sasa nataka kufahamu haya yote yanatokana na nini:
Je, majina yetu asilia yanakuwa na walakini au yanabeba nuksi fulani hivi kwa mtoto ?

Au, hayo majina hutumika kama utambulisho wa dini ya mtu fulani kama ilivyo kwa kabila ?
Historia isiyofundishwa darasani inaeleza...!
Baada ya uvamizi wa mtu mweupe afrika ya kale had enzi za utumwani watu weupe walipojifunza ukuu wa uafrika uwalingundua haya majina yana nguvu kiasili...mfano kiafrika inaminka mtu akifa anaweza kuzaliwa tena kwa majina ya watoto ambayo walikuwa wanaridthi kupotia kwa mababu zao hvyo mtu kama kinjekitile ngwale angeweza kuzaliwa tena kupitia mjukuu au kituu chake na akawa na tabia km za kijekitile. Kumbuka hawa viongozi kama kinjekitile, malikia liti ni viongozi ambao walipiga watu weupe kupitia miujiza ya mila za kiafrika mfno huyo mama anayeitwa malki liti ambaye alikuwa pale singinda aliwashinda vita wajerumani kwa kutumia nyuki. Sasa hawa mashujaa walikuwa wengi afrika kwa tanzania kila mkoa ukichimba historia ambayo inafichwa utawakuta hawa machiefu ambao walikuwa ni mashujaa lkn pia kwa upande mwingine yalikuwa ni ngumu kwa kuyatamika.

Sasa wazungu na waarabu walipojifunza hilo wakaji na huyo ufumo wa kuwabatiza watu majina ili kuukataa utu wao uwafrika wa wao desturi zao mila zao na kila kitu chao kwa kuwaaminisha majina yetu sio matakatifu bali majina yao ndio matakatifu hasa wakitumia kipinge cha watu wanaoitwa mitume kutumia hvyo vitabu vya dini waliopambwa kwa sifa njema. Ambazo hata hao wazungu wenyewe pamoja na kujiita hayo majina walishindwa kuwa nazo kipind cha utumwa. Lkn kipind cha utumwa ilikuwa ni lazma kutumia jina la kikoloni ili iwe rahc pia wao kukufahamu kwa sbb wao ilikuwa inawapa tabu kuyatamka sasa ilikuwa mzungu au mwarabu anakuja anakwambia ww utaitwa petro kipindi hicho labda ww ulikuwa unaitwa andungulile sasa ili lazmika jina la andungulile uachane nalo utumie jina la petro.

Kimsingi dini ili andaliwa kuja kutumika km nyenzo ya kucontrol watu na kufuta asili yao kwa ilivyo sasa majina ya mohammed, said, rashid, james, peter ni majina yaliokuja kupoteza asili yetu.

Nb: hii ni elimu isiyofundishwa darasa kwahyo sio lazma kufungamana na mm
 
Sababu yao RC kubatiza jina la mtakatifu ni nini?? Kutokuthamini jina asilia,
Sauzi, Sibongile ni Sibongile, Ghana Nana ni Nana, Nigeria Adebayor ni Adebayor, hao watakatifu RC wanajulikana Bongo tu??

Everyday is Saturday................................😎
Ni ufala tu na uzuzu wetu waafrika hasa wa Tz..kwanza ni dharau kubwa sana kwa wazee wetu walio tufanya leo tupo duniani.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom