Hivi kwanini Tundu Lissu hakuwa Rais baada ya kifo cha Hayati Magufuli kwa kipengele cha kuwa namba 2 katika kura za Wananchi

Maan

Member
Joined
Sep 11, 2023
Posts
50
Reaction score
76
Ili kuepuka kuwa na Rais ambae hakutokana na kuchaguliwa na wananchi ilipaswa kupewa nafasi yule aliye shika nafasi ya pili.

Alafu Rais Samia angetumika kuongoza nchi kwa kipindi kifupi hadi pale Rais atakapo tawazwa kisha aachie nafasi ya Urais ambayo alishikili baada ya Rais aliye madarakani kututoka.

Hii itasaidi kuondokana na masononeka kwa watanzani kuongozwa na Rais ambae hakutokana na kuchaguliwa kwa kura
 
Ili kuepuka kuwa na Rais ambae hakutokana na kuchaguliwa na wananchi ilipaswa kupewa nafasi yule aliye shika nafasi ya pili.
Japo mfumo wetu wa utawala ni Westminster style kama wa Uingereza, tulidumu nao just for one year, 9 December, 1962 tukawa Jamhuri na kuadopt American style, tukaanza presidential system. VP anapigiwa kura na rais hivyo kura zote za Magufuli, pia ni za Samia!.
Hii itasaidi kuondokana na masononeka kwa watanzani kuongozwa na Rais ambae hakutokana na kuchaguliwa kwa kura
Samia amechaguliwa na wananchi by proxy, kila kura ya Magufuli ni kura ya Samia!.
P
 
Hili ni moja ya mapungufu makubwa ya katiba ya sasa
Tunalazimishwa kuongozwa na rais asiyechaguliwa maana awamu ya sita haujafanyika uchaguzi.
Swali: 2025-2035 ni awamu ya saba?
 
Katiba




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha kukufuru watanzania. Utakufa ukiwa umejibebea laana za maskini wa Tanzania wanaonyanyaswa na utawala huu haramu. Endapo tungekuwa na mfumo bora wa kikatiba basi Alipaswa ashikilie hiyo nafasi siku 90 tuchague mwingine tuepukane na haya mambo ya mabadiliko ya sera kwa malengo ya kuhujumu taifa. Katiba mpya tuliangalie hili. Binafsi wakati napiga kura sikuwaza kabisa kuongozwa na Rais muuza nchi kinyume kabisa na sera za niliyemchagua.
 
Hili ni moja ya mapungufu makubwa ya katiba ya sasa
Tunalazimishwa kuongozwa na rais asiyechaguliwa maana awamu ya sita haujafanyika uchaguzi.
Swali: 2025-2035 ni awamu ya saba?
2025 - 2030 ni kipindi cha pili cha awamu ya 6!.
P
 
Kwa hiyo umeuzwa wewe!
Hapo ulipo ni mtumwa tu!
Haya hebu tuambie hii nchi imeuzwa kwa bei gani vile
 
soma katiba yako ndugu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…